10 Apr 2008

Huduma za afya hapa nyumbani ni duni na hazileti matumaini ya Maisha Bora kwa Kila Mtanzania (by the way,tangu nifike hapa sijaona ile hamasa niliyoikuta 2005 kuhusiana na kauli-mbiu hiyo.Sijui imekufa kifo cha asili au imepotea kama Gavana Daudi Ballali!).Hospitali za umma zinaweza kujitetea kuhusu huduma zao mbovu,na utetezi unaweza kuwa ule uliozoeleka:serikali haitengi fungu la kutosha kwenye sekta ya afya,mishahara ya watumishi ni midogo,na mlolongo wa sababu ambapo mlengwa mkuu ni serikali.Lakini haitarajiwi hospitali binafsi,ambazo gharama zake ni za juu sana,zitoe huduma ya chini ya kiwango.Nimeelezea kwa kirefu kuhusu suala hilo katika makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema.Pamoja na makala nyingine na habari motomoto,bingirika na vyote hivyo kwa KUBONYEZA HAPA

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.