10 Sept 2008

Matatizo ya kidunia yalinifanya nishindwe ku-update blog hii kwa takriban miezi miwili hivi.Kupoteza mzazi inaweza kuwa tukio la kawaida iwapo litatokea kwa mtu mwingine.Lakini ukweli mchungu ni kwamba once ikitokea kwako ni vigumu mno kuhimili matokeo yake.Inaumiza zaidi pale mmoja wa watu aliyekuwa inspirational katika kufikia malengo yake flani (kwa upande wangu,suala la shule) anapoondoka duniani miezi michache kabla ya wewe kufikia lengo hilo.Lakini kwa sie tunaoamini katika mapenzi ya Mungu na usahihi wa maamuzi yake inalazimu kufika mahala kukubali kuwa yote,hata kama machungu kiasi gani,ni MAPENZI YA BWANA.

Blogu hii itaendelea kuwaletea uchambuzi wa masuala mbalimbali,hususan ya kisiasa.Kwa vile tunaelekea kwenye uchaguzi wa rais huko U.S.A,blogu hii itajitahidi kuleta mkusanyiko wa habari mbalimbali.Pamoja na hayo ni picha mbalimbali kutoka Tanzania zilizopigwa katika kipindi cha takriban miezi mitano niliyokuwa huko.

Karibuni tena

Kwa kuanza,kuna hapa chini ni picha kadhaa kutoka angani.Picha ya kwanza ni Addis Ababa kutoka angani,ya pili ni Dar kutoka angani,ya tatu ni Schiphol Airport,Amsterdam na ya mwisho ni Aberdeen Airport.









0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.