17 Sept 2008

Chama cha siasa huzaliwa,hukua na kinaweza kufa pengine hata kabla hakijakua.Tofauti nachama nchi ikishazaliwa ni lazima iishi milele,tena kwa gharama yoyote ile.Lakini kuna wenzetu wengine hawataki kuelewa ukweli huo.Kwao,chama cha siasa ni kila kitu hata kama kinaipeleka nchi ahera.Angalia mfano huu mwepesi: chama kinapewa dhamana ya kuongoza nchi,lakini kinaendesha mambo yake kihuni na kupeleka nchi mrama.Ni dhahiri kwamba chama cha aina hiyo kinaamsha vurugu ambazo zitalekea mmomonyoko wa amani katika nchi husika.Kwa bahati mbaya au makusudi,kuna wenzetu hawataki kuamini kwamba ni vigumu kujenga na kudumisha amani kuliko kuivunja.Sote tunawajibika kuhakikisha nchi yetu haipelekwi kusikofaa badala ya kunyoosheana vidole tunapotofautiana namna ya kuboresha ustawi wa Tanzania yetu.

Katika toleo la wiki hii la gazeti mahiri la Raia Mwema,pamoja na mkusanyiko wa habari na makala motomoto,kuna hababari kuhusu the man of the moment,Nape Nnauye.Kuna wanaodai kuwa huyu jamaa aanashupalia ishu za ufisadi ndani ya UVCCM kwa minajili ya kutafuta umaarufu utakaopelekea apate nafasi ya juu kwenye jumuiya hiyo.Sina uhakika kuhusu hilo lakini binafsi naamini kwamba hata kama malengo yake ya ni kupata umaarufu au uongozi,jitihada zake kuushikia bango ufisadi ndilo lililo muhimu zaidi kuliko motives zake.Na wanaokemea ufisadi,hata kama kwa njia zisizo sahihi,wanapaswa kuungwa mkono badala ya kunyanyaswa.Enewei,habari ya Nape ni hii HAPA na mambo mengine motomoto yanapatikana ndani ya gazeti hili la RAIA MWEMA.


0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.