6 Jan 2009

Picha kwa hisani ya Mjengwa.

Habari hiyo ni kwa mujibu wa gazeti la  Sunday Citizen.Pia,mwanablogu BWAYA ameichambua kwa undani habari hiyo ya kusikitisha.Makala za Padre Karugendo ni miongoni mwa maandiko yaliyonishawishi nami njiingize kwenye fani ya uandishi wa makala.Nahisi Kanisa Katoliki limechukua hatua hiyo kutokana na msimamo makini na wa uwazi wa Padre Karugendo kuhusiana na mambo mbalimbali ya Kanisa hilo.Japo mie ni Mkatoliki pia,lakini sipendezwi na namna Kanisa hili lisivyopenda kukosolewa.Nalinganisha tukio hili na lie la Father Nkwera (na wanamaombi) ambaye kimsingi kosa lake kubwa ni kutumia karama kama ile aloyokuwanayo Bwana Yesu ya kuponyesha wagonjwa.Yayumkinika kubashiri kwamba hatma ya Kanisa letu sio ya kuleta matumaini sana kama litaendeleza UKALE na kujifanya halitambua dunia inavyobadilika.

1 comment:

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.