7 Jan 2009

Padre Privatus Karugendo amekuwa akisimulia mkasa ulisababisha yeye kusimamishwa,na hatimaye kuvuliwa,daraja la upadre.Kma nilivyoeleza katika post hii,japo sifahamiani personally na Mtumishi huyu wa Bwana,alikuwa columnist mwenzangu katika jarida la Raia Mwema hadi nilipolazimika kuchukua "sabbatical leave" ya uandishi wa makala.Pia,maandiko mbalimbali ya Padre Karugendo yalinipa changamoto kubwa hadi nikaamua kujiingiza katika anga za uandishi wa makala kwenye magazeti mbalimbali huko nyumbani.

Unaweza kusoma SIMULIZI kuhusu chanzo cha mkasa uliopelekea Padre huyo kusimamishwa na hatimaye kuvuliwa upadre kwa KUBONYEZA HAPA (Sehemu ya Kwanza) na HAPA (Sehemu ya Pili) na HAPA (latest).Blogu hii itaendelea kuwaletea simulizi hizo kadri zinavyochapishwa gazetini.Mkasa uliomkumba Padre huyu unanigusa sio tu kwa vile napenda makala zake au kwa sababu tuliwahi kuandikia gazeti moja,bali pia kwa vile kwa namna flani yeye,kama mie,ni majiruhi wa mfumo uliozowea kupongezwa na kunyenyekewa lakini usiotaka kusikia criticism au mawazo mbadala.
NYONGEZA: Nimekutana na post katika blogu ya Pambazuko ambapo Askofu (anayetajwa kwenye Simulizi za Karugendo) ANADAIWA KUWA NA MTOTO NA ANATAKIWA AKAMCHUKUE. (Bonyeza link kuisoma)

3 comments:

  1. Dah!! Haya. Mimi ntasoma tuu na wenyewe watamalizana. Kali kwelikweli.
    Asante Kaka Evarist

    ReplyDelete
  2. kak Evarist, nimepita kukusabahi.
    Ahsante kwa kunitembelea na kunipa changamoto.
    Najifunza mengi kupitia kwenu wanblog wenzangu.

    ReplyDelete
  3. Hii ni habari ya kusikitisha sana.

    Nimesoma maoni ya wasomaji mbali mbali katika blog ya kaka Bwaya, imenisikitisha sana.

    kwa leo sitasema mengi lakini napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza kwa ujasiri wake.

    Ahsante sana kaka Evarist kwa kutuhabarisha.

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.