22 Jun 2009


Katika MAKALA HII nilionyesha wasiwasi wangu kuhusu hatua ya Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo kutangaza kufutwa kwa misamaha ya kodi kwa taasisi za dini.Katika makala hiyo,nilieleza hivi (najinukuu)

Lakini binafsi natafsiri kuwa hatua hii ina ajenda mbalimbali zilizofichika
ikiwa ni pamoja na kuonyeshana nani mwenye nguvu zaidi: mamlaka za kidunia au za kiroho.Usisahau kauli za hivi karibuni kutoka kwa madhehebu mbalimbali ya Kikristo kwamba mafisadi wameteka nchi....na kuandaa mkakati wa kupata viongozi bora katika uchaguzi mkuu wa 2010.
Toleo la leo la gazeti la Majira lina habari inayothibitisha hypothesis hiyo.Kwa mujibu wa gazeti hilo,kauli zilizoikera Serikali hadi kufikia hatua ya kutoa "kibano" hicho ni pamoja na ile ya Kanisa Katoliki kuanzisha program maalum ya kuelimisha waumini wake kuhusu masuala mbalimbali ya demokrasiapamoja na namna ya kuchagua viongozi bora.

Kwa mujibu wa Majira,kauli nyingine ni ile iliyotolewa na na Jumuiya ya Kikristo Tanzania kwenye Mkutano wake mjini Dodoma ambapo ulitolewa wito kwa waumini wa madhehebu hayo kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu hapo mwakani.




Picha ya gazeti la Majira kwa Hisani ya KENNEDY.

Najiuliza,hivi hapa nimejisifu au nimejipongeza?


1 comment:

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.