20 May 2010

Nadhani unamfahamu Christina Aguillera,na kama unamfahamu basi ni dhahiri utakuwa unakumbuka 'singo' yake ya kwanza kabisa Genie in a Bottle (Kama huukumbuki basi cheki video hii hapa).

Ushaikumbuka?Well,lengo la makala hii si kumjadili mwanamuziki huyo au wimbo huo uliovuma sana.Nacho-focus hapa ni hiyo ishu ya 'jini kwenye chupa'.

Lakini kabla sijainyambua,ngoja nikupe stori moja fupi.Mwaka 2005 nilipokwenda nyumbani kwenye fieldwork,nilikutana na rafiki yangu mmoja wa zamani ambaye ni mtoto wa Sharifu huko Tanga.Baada ya mahojiano yetu nilimdadisi kuhusu suala la majini.Nae bila hiana akanipa darasa kutoka A mpaka Z.Actually,alikwenda mbali zaidi hadi kunionyesha namna jini linavyotengenezwa.Bila kuingia kwa undani sana,alichovya maandishi flani kwenye chupa na kutengeneza kitu alichokiita kombe,kisha akafunga hiyo chupa.Akaeleza kuwa katika muda aliokusudia,jini litatoka katika hiyo chupa na 'kufanya vitu vyake' (kwa mujibu wa manuizo/dua.Bado nakumbuka jinsi nilivyosisimka baada ya 'kuonyeshwa jini mtarajiwa'

Naamini usemi 'jini ndani/kwenye chupa' unaendana na mantiki ya utengenezaji jini (yaani linawekwa kwenye chupa kisha 'linalipuka' katika muda ulokusudiwa).Kwa mujibu wa yule mtoto wa Sharifu ni kwamba jini likishatengenezwa na kuhifhadhiwa ndani ya chupa tayari kwa 'maangamizi' haliwezi kurejeshwa.Na la zaidi ni kwamba jini likishatoka kwenye chupa haliwezi kurudisha.Kwahiyo basi,usemi 'jini kwenye/ndani ya chupa' unamaanisha kitu ambacho 'kikitoka kimetoka',yaani ni kama maji yakimwagwa ardhini,hayawezi kuzoleka.

Kwanini basi nimeamua kutumia msemo huu katika makala hii?Well,katika uchambuzi wangu kuhusu kauli za/matendo ya Rais wetu (Chaguo la Mungu) Jakaya Kikwete,naanza kupatwa na wasiwasi huohuo wa 'jini ndani/kwenye chupa'.Simaanishi kuwa JK ndio jini.Hapana.Nazungumzia kauli na matendo yake ya hivi karibuni.

Sijawahi kuzungumzia lolote kuhusu hotuba yake kali alotoa kwa wafanyakazi wa serikali waliokuwa wametishia kugoma.Kwa kifupi,baadhi ya kauli zake hazikupaswa kutolewa na kiongozi anayejali utawala wa sheria.Kwa kutaja maneno kama risasi za moto au namna wafanyakazi wangeweza kukumbana na nguvu za polisi ilikuwa ni mithili ya kubariki ukatili.Hata kama wafanyakazi wangegoma bado isingehalalisha matumizi ya nguvu 'to an extent baadhi yao wangeweza kukumbana na makali ya risasi za polisi'.Hivi sio JK huyuhuyu alosema kuwa yeye anathamini haki za binadamu ikiwa ni pamoja na za mafisadi?Tuliache hilo kwa sasa.

Juzijuzi akaibuka tena na kudai suala la takrima ni gumu kukwepeka.Mkuu wa nchi anaposema hivyo ni sawa na kubariki matumizi ya rushwa kwa jina la takrima.Kauli kama hiyo haipaswi kutolewa hata na katibu kata,let alone Mkuu wa nchi.Ugumu wa jambo haumaanishi liachwe kama lilivyo.Yaani kwa vile mapambano dhidi ya ukimwi ni magumu kwahiyo tuache watu 'watembee pekupeku'?Au kwa vile ugonjwa wa malaria umekuwa ukitusumbua miaka nenda miaka rudi basi tuuache kwa vile ni vigumu kupambana nao?Sasa alipohamasisha kampeni ya ZINDUKA na wapambe wake wa bongoflava alikuwa anamaanisha nini?Rais alipaswa kuelewa kuwa kwenye mapambano dhidi ya udhalimu,giving up is not an option.Laiti Nyerere na wapigania uhuru wengine wangekuwa na mtizamo finyu kama huo wa 'jambo hili gumu kwahiyo tuliache kama lilivyo' basi hadi leo tungekuwa bado koloni la Mwingereza.

Kilichonishtua zaidi hadi kufikia hatua hii ya kuleta ulinganifu na 'jini kwenye/ndani ya chupa' ni mkanganyiko uliojitokeza katika sakata la Jumuiya ya Vijana wa CCM (UVCCM).Awali ilielezwa kuwa kuna vipeperushi vilivyosambazwa kumtuhumu aliyekuwa Mwenyekiti ya jumuiya hiyo,Hamad Yusuph Masauni.Baadaye gazeti moja likabainisha kuwa mtoto wa JK,Ridhiwani,anatuhumiwa kuivuruga jumuiya hiyo na kuchochea suala hilo la Masauni.Lakini,akihutubia mkutano wa Jumuiya hiyo huko Iringa,JK aliweka bayana kuwa (namnukuu) "Tulipochunguza ilibainika ni kweli alighushi, wakati wa uchaguzi alisema alizaliwa mwaka 1979, lakini ukweli alizaliwa mwaka 1973 na alianza darasa la kwanza mwaka 1979".Je hii haimaanishi kuwa hata vipeperushi vilivyosambazwa kumhusu Masauni vilikuwa na uhusiano na 'uchunguzi' huo anaozungumzia JK?Kama ni hivyo,je si hatari inapotokea kiongozi wa nchi anaporuhusu michezo michafu kama hiyo kwa minajili tu ya kukidhi matakwa flani?

Kinachokasirisha ni kauli yake kuwa  "kijana huyo (Masauni) mpole na mzito kufanya maamuzi magumu na haraka...ni mkakamavu na mchapakazi atapangiwa kazi nyingine hapo baadaye".Yaleyale ya Mwilima.Mtu anaboronga huku kisha anazawadiwa uongozi.Kama ni kweli Masauni alifoji umri wake,hivi hiyo haimpotezei sifa za kuwa kiongozi mahala kwingine?Sasa JK anapotuambia kuwa aatapangiwa kazi kwingine anamaanisha nini?Au huko atakapopangiwa hakuhitaji uadilifu?Na kama 'kudanganya umri' si big deal kwanini basi wameshinikiza aondolewe UVCCM?Nauliza hiyo kwa vile,kwa mujibu wa 'Chaguo la Mungu',kufoji umri kulikopelekea Masauni kujiuzulu sio big deal ndio maana 'atapewa kazi nyingine baadaye'.

Habari nyingine zinazoweza kuashiria kuwa 'jini lililo ndani/kwenye chupa linaweza kutoka muda wowote ule' ni katika jarida la Raia Mwema kwamba Mawaziri Wakuu wastaafu wanafuatiliwa.Ukisoma habari hiyo utabaini kuwa kwa vyovyovte vile,Mkuu wa Nchi anafahamu kuhusu suala hilo.Lakini sidhani kama tunapaswa kushangaa sana kwa vile kama Masauni alichunguzwa (which is equivalent to kufuatiliwa kwa ex-PMs hao) na hatimaye vipeperushi vikasambazwa,basi katika utawala huu lolote linawezekana,hususan uzandiki na character assassination.

Na hili suala la promotion ya familia kwenye uongozi,japo si kosa,linaweza kutafsiriwa kwa namna ya maandalizi ya udikteta.Baba/mume rais,mama/mke naye mwanasiasa 'kiaina',kaka wa rais naye mwanasiasa,mtoto naye mwanasiasa,na hadi kitinda mimba naye kaingizwa kwenye siasa.Na hapa sizungumzii siasa kwa maana ya hamasa tu bali siasa za mizengwe na kugombea kwa kutumia jina.Hapa tunazalisha mfalme au dikteta?

Kwa Watanzania wengi ni business as usual.Lakini kwa wanaoangalia ishu na kukumbuka kuweka alama za kuuliza,yayumkinika kufananisha suala hili na ' jini ndani/kwenye chupa'.LIKITOKA LIMETOKA,hakutokuwa na jinsi ya kulirejesha kwenye chupa.

Kwa atakayechukizwa na uchambuzi huu (kama yule mjinga alontumia comment ya matusi) all I could tell them is SUCK IT UP!


2 comments:

  1. Listening to part of Kikwete's speech with Wazee of Dar i could not believe words coming from his mouth. He threatened people with the use of violence not to perform their democraric rights. I was also amazed by the people sitting along side kikwete,Shein, Kapuya, Lukuvi listening to him as a dictator without any disgust for the threats coming from his mouth,the people in the audience even applauding him was shameful. Are we leaving in the same world. People must wake up and say no more! CCM are taking people's patience for granted as they know they are capable of rigging the election and rule for years to come.

    Thanks Phil for bringing to attention news and views which most blogs in TZ are afraid of printing. We need more people like you, not afraid of standing up to CCM and say the truth. What i dont understand is how come the ministers, leaders they travel to the west but they do not want to adopt the way their counterparts behave to the people who put them to power by electing them.

    Keep up the good work phil!!

    ReplyDelete
  2. Dr Chahali endelea kuwakilishi mawazo yako binafsi na sisi watanzania wachache ambao tunapigana na hii vita ya mafisadi, tunayakubali kwa mikono miwili hao vichaa wawakilishi wa mafisadi wanaokutumia hizo meseji za kifisadi...huyo mtu anatakiwa kwenda tena Hospitali akadungwe sindano nyingine ya chanjo na CCM yakummaliza kabisa na kumpofua macho awe kipofu na masikio awe kiziwi...

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.