24 May 2010


Hatimaye kesi inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Benki Kuu,Amatus Liyumba,inafikia ukingoni leo ambapo atasomewa hukumu.Japo zamani hizoo nilishawahi kuwa 'mnajimu/mtabiri wa kizushi' nilipoandikia magazeti ya Sanifu,Kasheshe na Komesha huku nikijiita 'Ustaadh Bonge' (na baadhi ya watu walikuwa wakiamini 'unajimu' huo),siwezi kwa hakika kubashiri lolote kuhusu hukumu hiyo.Kibaya zaidi,upeo wangu wa taaluma ya sheria ni dhaifu kama uchumi wa Somalia.

Lakini kabla ya kuzungumzia kwa undani kuhusu hukumu hiyo,pengine ni muhimu kuangalia kidogo mwenendo wa kesi hiyo inayogusa hisia za wengi (na wengine wakiwa na sababu zao binafsi).Hadi sasa sielewi mantiki iliyotumika katika kumweka Liyumba gerezani muda wote huu ilhali kisheria yeye anabaki kuwa mtuhumiwa hadi itakapoamuliwa vinginevyo na mahakama.Naomba ieleweke kuwa simtetei Liyumba japo ni 'mwana wa pakaya' kwangu.Ninachohoji hapa ni uhalali wa kumweka mtuhumiwa rumande kwa zaidi ya mwaka mzima pasipo kumpatia dhamana.Hii ni mithili ya kuwa na kiji-Guantanamo chetu ndani ya jamii inayodai kuzingatia utawala wa sheria.Hatari iliyopo ni kwamba kama akishinda kesi,Liyumba anaweza kudai fidia kubwa zaidi ya kiwango anachotuhumiwa kukifanyia ubadhirifu.Afungwe au aachiwe huru,kwa kuwekwa gerezani muda wote huo pasipo kupewa dhamana ni kama alishakuhukumiwa kabla ya hukumu ya leo.Badala ya kuwa 'innocent until proven guilty',hii imekuwa 'guilty until proven innocent'.

Tuje kwenye mwenendo wa kesi yenyewe.Kulikuwa na mikanganyiko kadhaa kwa upande wa mashtaka huku baadhi ya mashahidi wake wakimtetea mshtakiwa waziwazi.Pigo jingine kwa upande wa mashtaka ni kutokuwepo kwa mtu ambaye wangeweza kumfanya 'shahidi nyota' (star witness),aliyekuwa Gavana wa BOT,hayati Daudi Ballali (huyu nae alikuwa 'mwana wa pakaya' just like alivyo 'mrithi' wake,Prof Benno Ndulu).Kwa vile haingekuwa rahisi kwa Liyumba kufanya ubadhirifu huo pasipo Gavana kufahamu kinachoendelea kwa kipindi chote hicho,yayumkinika kusema kuwa marehemu Ballali angekuwa na umuhimu wa kipekee katika kesi hiyo.Na japo 'star witness' huyo hakuwepo,ushahidi ulotolewa na Naibu Gavana na watendaji wengine wa BOT unaweza kutafsiriwa kama 'habari njema' kwake badala ya kumkandamiza.

Halafu kuna tatizo jingine,nalo ni udhaifu wa wanasheria wa serikali/ waendesha mashtaka.Mjuzi mmoja wa masuala ya mahakamani aliwahi kuniambia kwamba wahitimu wa sheria waliofanya vizuri kwenye masomo yao hukimbiliwa na kampuni binafsi za sheria,na hivyo kuwaacha 'wale wa kawaida' wakitarajia ajira kutoka serikalini au vyombo vya sheria vya umma.Sote twaweza kubashiri nini kitajiri pindi wahitimu hawa wanapokutana mahakamani,huku wale wa 'daraja la kwanza' wakiwa upande wa washtakiwa au washtaki dhidi ya serikali.Inaelezwa pia kuwa kipato cha mawakili binafsi kipo juu zaidi ya cha wenzao wa serikalini/taasisi za umma.Ni dhahiri mwanasheria anayelipwa kwa saa au mwenye maslahi bora atakuwa katika nafasi nzuri dhidi ya mwenzie ambaye si ajabu wakati akiwa mahakamani atakuwa bize zaidi kupiga mahesabu ya namna ya kumudu maisha hadi siku ya mshahara wake kijungujiko kuliko kutimiza wajibu wake sawasawa.

Kwa wengi tunaofahamu ugumu kwa mtu wa tabaka la juu kama Liyumba kuhukumiwa kifungo,let alone kufunguliwa mashtaka (akina Chenge 'wanapeta' tu huku kesi ya Pro Mahalu ikisuasua na mafisadi wa Kagoda wakiendelea 'kula bata'),kuna hisia kuwa Liyumba 'anafanyiziwa' tu.Yani,si kwamba anachotuhumiwa kufanya hakikupaswa kumfikisha mahakamani bali ni imani inayozidi kushamiri katika Tanzania yetu kuwa mashtaka na vifungo ni kwa wanyonge na wasio na uwezo wa 'kununua au kutetea haki zao.'Wambeya' wanadai kuwa ishu ya Liyumba inaweza kuwa kama ya 'Babu Seya' ambapo inadaiwa kuwa kesi zao ni matokeo ya 'kuingilia maslahi ya watu'.By 'watu' haimaanishi mie na wewe bali vigogo ambao 'kugusa mali zao' ni zaidi ya kosa la jinai.Inadaiwa kuwa mtu anaweza kufisadi atakavyo na asichukuliwe hatua alimradi hagusi 'mali' za 'wenye nchi'.Na kama hujaelewa by 'mali' namaanisha nini,well,huijui vema Tanzania unayoishi au unayotoka.

Ok,tusubirie hukumu lakini kama umesoma vema between lines katika nilichoandika hapo juu basi utakuwa unafahamu bet yangu ikoje.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.