18 Sept 2010

Nimetumiwa ujumbe huu jamani, sifahamu ikiwa ni kweli ama sivyo.
Subi

Wafungwa wa gereza la IBUKONI, wilaya ya ROMBO tarehe 13/09/2010, walitumika kujenga jukwaa alilotumia JK jana wakati akifanya mkutano 15/09/2010, katika shule ya msingi mbomai kati, TARAKEA, ROMBO MKOANI KILIMANJARO. Hii ilisababisha wakazi wa Tarakea wabaki na mshangao kwani siku hiyo Tarakea ilikuwa siku ya soko, na watu wengi walishuhudia tukio hili.
MAPENDEKEZO
Wanasheria wa CHADEMA, angalieni jinsi mtakavyoshughulikia hili.
CCM tafuteni risiti nyingine za kufoji , ambazo zinaonyesha, mmewalipa MAGEREZA WILAYA YA ROMBO, au MAGEREZA MKOA WA KILIMANJARO kwa ajili ya kazi hii ya kujenga jukwaa.

BLOGU HII PIA INAWASHAURI CHADEMA KUANGALIA NAMNA YA KUSHUGHULIKIA UHUNI HUU

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.