11 Jan 2011



Pengine wakati uongozi wa Chadema mkoani Pwani ulipochukua uamuzi wa kuahirisha mkutano wao wa hadhara-baada ya "intelijensia yao kubainisha kuwa jeshi la polisi lilikuwa na njama za kuzusha zahma kama ile ya Arusha-hawakufahamu kuwa actually wanavumbua mbinu inayoweza kuwatwanga misumari wadhalimu pale inapouma zaidi (hitting where it hurts most).

Ofkozi,yayumkinika kuamini kuwa Chadema mkoani Pwani waliingia gharama kuandaa mkutano huo,na kuuahirisha kumewatia hasara.Lakini ni dhahiri kuwa upande uliopata hasara kubwa ni Serikali iliyoamua kutuma rundo la askari kwenda "kutoa kipigo" kwa wananchi wasio na hatia,lakini target ikayeyuka.

Mbinu hii inaweza kuwa na ufanisi mkubwa.Kutangaza maandamano au mkutano mkubwa,kisha kama kawaida Serikali inaingia gharama za kuandaa operesheni ya kwenda kuangamiza watakaohudhuria maandamano/mkutano husika,lakini hatimaye nguvu ya tembo kukanyaga sisimizi inaishia kukanyaga hewa tupu.

Ili mpango huu ufanikiwe kunahitajika intelijensia bora zaidi ya vyombo vyetu vya usalama vilivyosheheni vihiyo wa taaluma ya usalama.Intelijensia inayohitajika ni ya kuhakikisha ujumbe kuwa kutakuwa na maandamano au mkutano umefika kwa wakandamizaji hao wa haki za binadamu.Ujumbe ukifika,raslimali na nguvu kazi ya kukandamiza jamii itaandaliwa chapchap,only for them kuishia kukandamiza hewa (uwanja au ukumbi mtupu).

Good news is,viongozi wengi-kama sio wote- wa vyombo vyetu vya usalama ni vihiyo wa taaluma ya usalama.Kwao,usalama ni kwa vigogo na mafisadi tu ilhali kinachowezesha wanausalama hao kulipwa mishahara na marupurupu lukuki ni fedha zinazotokana na kodi za walalahoi (vigogo na mafisadi wakilipa kodi ni kwa hisani tu,si lazima kwa vile hakuna sheria dhidi yao).Ukihiyo wa viongozi hao ni muhimu katika mkakati huu kwani,kama ilivyothibitika katika intelijensia yao ya kiwendawazimu kabla ya mauaji ya Arusha,wakishaskia kuna maandamano au mkutano basi badala ya kufanya analysis makini ya kiusalama za kuwawezesha kubashiri matishio la usalama na namna ya kuyadhibiti,wao wanakimbilia kuamrisha askari polisi wajiandae kwa vita huku magari ya mapambano na yale yenye maji ya upupu yakijazwa mafuta tayari kwa "vita".

Sasa kama kila baada ya wiki mbili wanyanyasaji hawa wanaingia mkenge na kujitwisha gharama za kudhibiti maandamano au mikutano hewa,ni dhahiri kuwa sio tu itavunja morali wa polisi wanaomtumikia kafiri ili mkono uende kinywani bali pia itaikamua serikali ambayo imeshatumia mabilioni kuchakachua uchaguzi uliopita,let alone gharama za kumudu lifestyles za kifahari za watawala wetu.

Wito wa blogu hii kwa Chadema ni simple: moto mlioanzisha haupaswi kuzimika mpaka kieleweke.Kwa upande mmoja,kuuzima moto huo kutamaanisha kusalimu amri kwa utawala wa kidikteta wa Kikwete.Na kwa upande mwingine,kuzima moto huo kutamaanisha uhai wa wazalendo waliouawa na polisi umepotea bure.Sio tu kwamba vuguvugu lililoanzishwa likiendelea kwa muda mrefu litapelekea Serikali kuishiwa nguvu ya kupiga na kuua kila kunapokuwa na mkutano au maandamano bali pia linaweza kuwafanya polisi wanaotumwa kuua Watanzania wenzao kupatwa na akili ya kutambua kuwa wanatumika vibaya kukandamiza raia wasio na hatia.Unaweza kudhani polisi hawa katili hawawezi kupatwa na roho ya kibinadamu.Hilo linawezekana,na dalili kuwa mwenye nguvu anaweza kutalikiwa na mnyonge kukumbatiwa inaonekana katika uamuzi wa diwani wa CCM huko Arusha aliyeamua kukitosa chama hicho tawala na kujiunga na Chadema.Uthibitisho mwingine ni kitendo cha Naibu Meya wa Arusha aliyeamua kubwaga manyanga kwa vile hayuko tayari kuwasaliti Watanzania wenzie.Trust me,vuguvugu hili likiendelea tunaweza kusikia stori kwamba polisi kadhaa wameamua kubwaga silaha kukwepa kwenda kuwaadhibu Watanzania wenzao wasio na hatia.

Kama alivyoandika mwanahabari mahiri Ansbert Ngurumo katika safu yake ya "Maswali Magumu" katika toleo la juzi la gazeti la Tanzania Daima,uamuzi wa Rais Kikwete na IGP wake Said Mwema kukandamiza wananchi kwa kipigo na risasi kitasaidia kuchochea hamasa kwa Watanzania wengi zaidi,na-kama alivyobainisha mwanahabari mwingine mkongwe Padri Privatus Karugendo- polisi hawana uwezo wala raslimali za kupiga risasi kila Mtanzania.Tupo wengi kuliko wao,na pia kama sera ya chinja chinja itaendelea basi mwishowe polisi hao watajikuta wanaua wazazi wao kama sio memba wengine wa familia zao.

Naanza kuhisi joto la ukombozi wa pili ikijongea kwa kasi.Na kichocheo cha joto hilo si kingine bali damu za wazalendo na mashujaa zilizomwagwa na askari waliotumwa na Kikwete kudhibiti raia wema huku mafisadi wakipewa hifadhi na fidia (rejea mabilioni kwa Dowans).

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.