1 Apr 2011



Hivi msomaji mpendwa umeshwahi kujiuliza ungekuwa unafanya shughuli gani kama sio hiyo unayofanya sasa?Binafsi,ukiweka kando ndoto zangu za kitaaluma,nilikuwa na ndoto nyingine mbili.Moja ni kuwa daktari,ndoto iliyoyeyuka baada ya kupata F kwenye Fizikia na D kwenye Hisabati,japo nilikuwa na A ya Kemia na C ya Bailojia.Nilipofaulu kujiunga na Kidato cha Tano nikaamua kuchukua mchepuo wa Historia,Jiografia na Kiingereza (HGL).

Ndoto ya pili ilikuwa kuwa mtengeneza muziki au prodyuza.Msanii aliyenivutia sana (na anayeendelea kunivutia hadi leo) ni Dr Dre.Bahati mbaya,masuala ya shule yakanielemea zaidi na ndoto hiyo pia ikaenda na maji.Hata hivyo,tangu wakati huo nimekuwa nikiwathamini sana watu wanaofanya kazi kubwa japo haionekani waziwazi na pengine hawafahamiki zaidi ya wanaoonekana.

Chukulia mfano wa prodyuza wa muziki.Wakati takriban dunia nzima inawajua akina Lady Gaga,Beyonce na wengineo,ni watu wangapi wanaowafahamu wanaotunga nyimbo za wasanii hao?Au wataalamu wanao-prodyuzi miziki yao?

Mfano mwingine ni kwenye filamu.Wakati majina yanayovuma ni ya actors na actresses,watengeneza filamu-kwa maana ya waandishi wa script,waongozaji,nk wanabaki kuonekana kwenye shukrani za mwisho wa filamu tu japo wao ndio hasa wanaowawezesha actors na actresses kupata majina na kufanya movies zivunje rekodi za mauzo.

Na unapoangalia runinga,unapata wasaa wa kujiuliza kuhusu watu walio nyuma ya kamera,waandaaji wa kipindi,na wengineo wanaofanya mtangazaji unayemowna kwenye runinga afanye kile unachotarajia kama mtizamaji?

Hizi ndizo sababu zilizopelekea tovuti hii kumsaka Sophia Mwanauta,binti wa Kitanzania anayeishia hapa Uingereza,ambaye ni "moyo" wa utengenezaji wa kipindi maarufu cha Sporah Show,kinachoandaliwa hapa na kurushwa hewani na vituo vya BEN TV ya Uingereza na Star TV ya huko nyumbani.

Historia ya maisha ya Sophia,na namna alivyoingia kwenye fani ya kutengeneza vipindi vya televisheni kwa kamera,na hadi kuimudu fani hiyo,sio tu ya kuvutia bali inatia moyo na kutoa changamoto kubwa kwa Watanzania wengine,hususan akina dada.

Basi nisiongee kwa niaba yake bali nikuachie msomaji mpendwa usome mwenyewe historia ya maisha ya mwanadada huyu kwa maelezo yake mwenyewe.

Kwa jina naitwa Sophia Mwanauta ni mtoto wa kwanza katika familia ya watoto watatu ya Mr & Mrs Mwanauta. Nilizaliwa Arusha, Nimesoma Primary Arusha international school liliyopo Arusha, Secondary nimesoma Arusha Day Secondary school mpaka form four na A-level nilitoka nje ya nyumbani kidogo na kwenda Kampala Uganda katika shule ya St.Marys Kitende. Safari haikuishia hapo nilipomaliza A-level nilirudi nyumbani na kujiunga na Chuo cha Uhasibu Arusha (Arusha School of Accountant) ambapo nilitunikiwa cheti cha Certificate ya Accounting and Finance na baada ya hapo ndio nilikuja London na kufanya Joint Degree ya Accounting and Business of which I finished last year June.


Nini kilimvutia Sophia hadi akaingia kwenye fani yake anayoimudu vilivyo?
Ni swali ambalo nalipata kilaniendapo kufanya kazi. Being behind the camera nikazi amboyo niliipenda sana tangu mdogo i really enjoy it. Nakumbuka wakati na maliza darasa la saba mama yangu aliniandalia mtu wa kuchukaa video katika graduation yangu! Alie kuja kufanya hiyo video alikuwa ni mwanamke alinivutia sana, since nilijiambia ningependa kufanya kazi hiyo nikiwa mkubwa japo wakati huo kazi za camera, haikua kazi ambazo wanawake wengi waliifanya hivyo sikuweza kujitoa directly kwamba hii ndio kazi nataka kuifanya in future ndio maana nilienda kusoma course tofauti kabisa.
Wakati nilipofika London kufanya Degree yangu, sikumoja tulikaa na ndugu yangu Sporah na katika maongezi yetu tulikutana na interest zinazofanana yeye alipenda kuwa Talk Show Host na mimi nilipenda kufanya kazi ya Camera hivyo tukaungana na kuamua kufanya tunachofanya sasa ( THE SPORAH TV SHOW) Kusema kweli at that point sikuwa na any knowledge ya camera so nilichokuwa nafanya nikuwa nyuma ya Ma camera men walipokuja kufanya filming kwenye SPORAH SHOW. Niliendelea hivyo hivyo bila kuchoka mpaka nikajua atleast the basic things to do on a camera, believe me nilikuwa so determines baada ya muda mfupi tu nilijua kipi kinafanya nini kwenye camera. Mwisho nikaamua kwenda kufanya training ndogondogo ilikuelewa kazi vizuri zaidi.
Kwakweli mwanzo ilikua ni ngumu sana maana wote mimi na SPORAH tulikuwa bado tupo University na tulikuwa tunasoma course tofauti kabisa na kazi tunazozifanya lakini kwasababu tulikuwa determided tuliweza.


Sote tunafahamu kuwa kila safari ya maisha ya mwanadamu ni mchanganyiko wa milima na mabonde,vihunzi na tambarare.Je safari ya mwanadada Sophia ilikuwaje?
It was not an easy journey, kwani ilibidi tuachane na mambo yoote ili kufanya kazi, tulipoteza marafiki zetu wakaribu wakati mwingine hata familia zilikua hazituelewi maana hata kupiga simu nyumbani haikua sana kama mwanzo, na hii ilikua napale tulipokua tunakimbizana na shule na hapo hapo kurun a TV SHOW Every Week.
NO, IT WAS NOT EASY AT ALL!! , lakini namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwani tumefika tulipo leo inaonyesha matumaini.


Maisha ni changamoto.Ukipiga hatua moja unapata changamoto ya kupiga hatua zaidi.Lakini kuna changamoto nyingine zinatokana na jinsia,hususan mfumo dume unaopendelea kuangalia fani flani kama ni za kiume pekee.Je ni changamoto zipi anazokabiliana nazo Sophia?

Kwa mimi binafsi kwanza kabisa ni kuwa Mwanamke katika field hii, watu wengi wakikuona umevaa umependeza basi wanaona huwezi kushika Camera. Wakati mwingine nakutana na wanaume ambao wana just basic knowledge kuhusu Filming, lakini mara tu wakikuona we ni mwanamke then wanaona kama huwezi kazi, "Wakati mwingine inauzi sana"
So am always on computer and reading alot of books ili tu kujua mengi kuhusu Filming. Naipenda sana kazi yangu.


Maisha ni malengo.Mtu asiye na malengo ni sawa na mtu asiyejua kwanini yupo duniani.Je Sophia ana malengo gani ya baadaye?

My future plan is to have my own production company one day and be successful in what am doing ,i would love to be recognise internationally.

Je ana ushauri gani kwa akina dada wenzake-hususan wanaokubali dhana potofu kuwa fani flani ni kwa wanaume tu?
Kwanza kabisa ningependa kuwaambia wakinadada waondoe wazo la kuona wanamke ana tofauti na wanaume kwenye kazi kwani binadamu wote nisawa anachoweza kufanya mwanaume ,mwanamke pia anaweza kukifanya. Pia kama ukiweka nia, dhamira na juhudi katika kitu hicho utafanikiwa. (“Think like a queen. A queen is not afraid to fail. Failure is another stepping stone to greatness
The big secret in life is, Whatever your goal, you can get there if you're willing to work.

Tovuti hii inampongeza sana mwanadada Sophia Mwanauta kwa bidii na jitihada zake zinazostahili kuwa mfano wa kuigwa.Pia inamshakuru kwa mahojiano haya.Lakini kabla ya kumaliza,aliulizwa kama ana ujumbe wowote kwa jamii,hususan wapenzi wa Sporah Show,na alikuwa na haya kusema


Asante sana na Msikose kuangalia THE SPORAH SHOW, kila IJUMAA SAA KUMI NA MBILI Jioni na JUMAMOSI SAA SABA Mchana STAR TV IN TANZANIA.
And in EUROPE EVERY MONDAY 9:30PM BEN TV SKY 184.
Pia tembelea tovuti yetu inayopatikana www.sporah.com na www.sporahshow.com.Pia karibuni sana kutembelea blogu yetu inayopatikana www.thesporahshow.blogspot.com.

Join Us On Face Book at:

Check Our Video's on Youtube http://www.youtube.com/user/sporahshow
Asanteni



2 comments:

  1. Hongera sana mwanakwetu!maisha ni safari ndefu,tutafika tuu kama tutajitahidi kutembea bila kuchoka!.

    ReplyDelete
  2. Ustadhi Bonge hongera kwa kazi nzuri unazofanya kama hizi!Nimefurahi kupata history ya huyu dada na kipindi cha The sporah show, huwa nakifuatilia huku nyumbani

    ReplyDelete

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.