22 Aug 2011



BENDI ya mziki ya msondo ngoma imepata TUZO ya the Best Rhumba Group katika East Africa Music Awards mashindano yariyofanyika Nairobi Kenya na kukusanyika kwa bendi za Afrika Mashariki na bendi ya msondo kuibuka Kidedea katika mashindano hayo akisibitisha ushindi uho meneja wa bendi Saidi KIbiriti alipokuwa akiongea na Msemaji wa Bendi hiyo, Rajabu Mhamila , Super D (pichani)

Alisema wameshinda tuzo hiyo na watahakikisha wanaionesha kwa mashabiki wa bendi hiyo ili kudhirisha kuwa bendi ipo ng'ang'ari popote duniani mana bendi imekamilika kila idara alisema Super D
(pichani)

Bendi hiyo itanza mazoezi siku ya jumatatu kwa ajili ya kujiandaa na sikukuu ya Iddi inayotarajia kufanyika wiki ijayo ambapo wanaingia kambini kusuka vibao vipya ikiwemo na kuvifanyia kazi vile vya Zamani

Super D alisema bendi hiyo siku ya Iddi Mosi itapiga katika viwanja vya TTC Chang'ombe ambapo mashabiki watapata kuona tuzo hiyo ya Afrika Mashariki walioitwaa hivi karibuni na kupata fursa ya kupiga nayo picha katika viwanja hivyo

Bendi hiyo inayotamba na vibao vyake vipya vya Suluu uliotungwa na Shabani Dede na Nadhili ya Mapenzi uliotungwa na Juma Katundu

Rajabu Mhamila 'Super D'
Photojournalist at Majira, Business Times [email protected] www.burudan.blogspot.com
 Mob;+255787 406930
        +255774406938
        Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.