Kabwe ZuberiZitto, Mb



WaziriKivuli wa Fedha na Uchumi



TAARIFA KWAVYOMBO VYA HABARI



Waziri wa Fedha ndugu Mustafa Mkulo akae pembeni kupishauchunguzi dhidi yake kuhusu Shirika la CHC.

Katika Mkutano wa Nne wa Bunge la Kumi kulitokea malumbano makali kati ya Serikali na Wabunge wajumbe wa Kamati yaHesabu za Mashirika ya Umma kuhusu kuongezwa muda wa Shirika la CHC. WakatiWaziri wa Fedha alileta Azimio la kulivunja Shirika hili lenye taarifa nyingina nyeti kuhusu zoezi la Ubinafsishaji, Kamati ya Bunge ya POAC kutokana nauzoefu wake wa kukagua mahesabu ya Mashirika ya Umma na kufuatilia zoezi laUbinafsishaji wa Mashirika ya Umma, ilipinga hatua hii na kulitaka Bungekukataa Azimio la Serikali na kulifanyia marekebisho makubwa.

Hatimaye Bunge liliridhia kufanya mabadiliko makubwa katika Azimio la CHC, kwa kuamuru Shirikalipewe uhai wa miaka 3 na kuagiza uchunguzi wa namna bora ya kuendesha shughuliza Shirika la Consolidated Holdings. Mapendekezo ya Kamati ya POAC ni kulifanyaShirika hili kuwa la kudumu na kulipa jukumu la kumiliki na kusimamia uwekezajiwa Serikali kwenye kampuni binafsi (National Investment Agency) kama ilivyo Shirikala Tamasek ya Singapore na Shirika la Khazana ya Malaysia. Kwa sasa Uwekezajiwa Serikali katika Kampuni binafsi unasimamiwa na Hazina na usimamizi wake nimbovu na hauleti tija kwa Taifa.

Kitendo cha kushindwa kwahoja Bungeni kiliifedhesha Serikali na hivyo kwa kupitia Wizara ya Fedha kuamuakulihujumu Shirika kwa kumsimamisha Mkurugenzi wake Mkuu kwa makosa ya kimajungumajunguna kwa kuzusha kwamba CHC iliwahonga wabunge ili kuitetea. Waziri wa Fedha ndugu Mustafa Mkulo alilitaarifuBunge kuwa Bodi ya CHC imeomba ukaguzi maalumu kuhusu tuhuma za ubadhirifundani ya Shirika hilo. Niliitaka Serikali ichunguze pia tuhuma kwamba Kamati yaPOAC ilihongwa na kuahidi kuahidi kujiuzulu nyadhifa zangu zote ikithibitika.

Katika Uchunguzi wakeMdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Heabu za Serikali kwa kupitia Kampuni ya Ernest andYoung walitaka kufanya mahojiano na Waziri wa Fedha juu ya tuhuma mbalimbalizinazomkabili ndani ya CHC. Waziri Mkulo alikataa kuhojiwa na wakaguzi nabadala yake akaandika barua (kumb TYC/B/70/2/03 ya Oktoba 8, 2011) yenye kujibutuhuma moja, tena kwa juu juu, kuhusu yeye kuliamuru Shirika kuuza kiwanja cha Shirikabila kufuata taratibu za sheria.

Wakati Waziri anakanusha kuliagiza Shirikakuuza kiwanja kwa mtu aliyemtaka yeye, mimi nina ushahidi tosha wa Nyarakakutoka Hazina, kwa mfano barua TYC/A/290/13/4 ya Machi 9, 2011 ambayo inawagizaCHC kutekeleza agizo la Waziri la Fedha kuhusu kiwanja na. 10 barabara yaNyerere. Vilevile, nina ushahidi wa mkutano uliofanyika huko Morogoro Hotelkati ya Waziri wa Fedha na Mwenyekiti wa Bodi ya CHC kuhusu jambo hilo.

Siku mbili baada yakumjibu CAG, Waziri wa Fedha ndugu Mustafa Mkulo aliamua kutengua uamuzi wakewa kuongeza muda wa Bodi ya Shirika la CHC mpaka mwezi Disemba 2011 na hivyokuivunja. Uamuzi huu wa Waziri una lengo la kuficha ukweli kwani CHC bila Bodiya Wakurugenzi inaendeshwa na Hazina na hivyo taarifa ya ukaguzi itabidiipelekwe Hazina ambayo Waziri wake ni mtuhumiwa.

Uchunguzi wa kina
Ninapendekeza uchunguzi wakina ufanyike kwa kutumia vyombo vya dola na hasa TAKUKURU kuhusu tuhuma hizidhidi ya Waziri wa Fedha na alazimishwe kisheria kujibu maswali ya wakaguzi (Auditors) kuhusu tuhuma dhidi yake.

Wakati uchunguziunaendelea ndugu Mustafa Mkuloasimamishwe kazi ya Uwaziri wa Fedha hadi hapo uchunguzi utakapokamilika.Kitendo chake cha kuiamuru Bodi kumsimamisha kazi aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu kwatuhuma za kutunga na majungu na baadaye kuvunja Bodi ya CHC wakati inasubiritaarifa ya uchunguzi kutoka kwa CAG ni kuingilia uchunguzi na pia ni matumizimabaya ya Ofisi ya Umma ili kulinda maslahi binafsi. Ni dhahiri akiendelea kuwaWaziri wa Fedha ataharibu uchunguzi.Vilevile, Rais wa Jamhuriya Muungano wa Tanzania ndugu Jakaya Kikwete aangalie kama anaitendea haki nchina Uchumi wa nchi kwa kuwa na Waziri wa Fedha ambaye anasema uwongo Bungenibila kuogopa na mwenye kutumia Ofisi yake vibaya kwa kuchukua maamuziyanayoingilia uchunguzi unaomhusu ili kujilinda.

Taarifa ya Uchunguzi ikabidhiwe kwa Spika
Kutokana na ukweli kwambasuala la CHC lilianzia Bungeni na hata Waziri mwenyewe kukiri kuwa taarifa yauchunguzi inapaswa kuwekwa wazi. Kutokana na matokeo ya sasa ambapo Waziri waFedha mwenyewe ana tuhuma za kujibu na kwamba hivi sasa hakuna Bodi yaWakurugenzi ya Shirika na hata itakayoundwa itateuliwa na Waziri mtuhumiwaninashauri kuwa taarifa ya uchunguzi wa Shirika la CHC sasa ipelekwe kwa Spikawa Bunge kwa hatua zaidi.

KZZ
Dar es Salaam, 13 Oktoba,2011.