27 May 2012



Ama kweli dunia haiishiwi vituko.Katika mazingira ya kawaida haingii akilini kusikia mganga wa kienyeji kalazwa hospitali "ya kawaida" (yaani inayotibu kwa kutumia dawa za kisasa badala ya mitishamba).Hivi,kama mganga anaweza kutibu wagongwa pasipo kutumia dawa za kisasa,iweje yeye akiugua anaenda hospitali kutumia dawa hizo badala ya mitishamba yake?

Hili linapaswa kuwa fundisho kubwa kwa wanaotegemea tiba za kienyeji.Ukiona waganga wanaotibu kwa ndumba wanakimbilia hospitali huhitaji kujiuliza mara mbili kuhusu ufanisi wa dumba hizo.

Pichani juu ni Mbunge wa Korogwe Vijijini kwa tiketi ya CCM, 'Profesa' Maji Marefu,ambaye imeripotiwa kuwa amelazwa nchini India kwa matibabu ya ugonjwa ambao haujafahamika.

Hata hivyo,blogu hii inamtakia mganga huyo apate nafuu katika matibabu anayopatiwa ili arejee nchini kuutumikia umma kisiasa na katika tiba zake za asili.

0 comments:

Post a Comment

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.