Showing posts with label ADELINA MAPANGO. Show all posts
Showing posts with label ADELINA MAPANGO. Show all posts

29 May 2017



Mama mpendwa,ilikuwa siku kama yale leo,miaka tisa iliyopita,uliondoka hapa duniani wakati tunakuhitaji sana. Japo miaka tisa inaweza kuonekana ni muda mrefu kusahau machungu,kwangu mwanao imeshindikana. Kila siku ya Mungu ninaposali kukuombea pumziko na raha ya milele huko ulipo,hujikuta napatwa na uchungu usioelezeka. Kwa kifupi, mama mpendwa, kila siku baada ya kifo chako-siku kama ya leo miaka minane iliyopita,imeendelea kuwa ni hudhuni na majonzi yasiyoelezeka.

Mama mpendwa, ulikuwa ni zaidi ya mama kwangu, kwa mumeo marehemu Baba Mzee Chahali (aliyeungana nawe huko peponi mwaka juzi) na kwa wanao wote na ndugu na jamaa. Nakumbuka mwaka 2005 nilipokuja likizo nyumbani, ulirukaruka kwa furaha, ukanikumbatia na kunipakata mwanao, ukaniandalia maji ya kuoga, ukanifanya nijsikie kama mtoto mchanga. Sikujua kuwa furaha ile ya mzazi kumwona mwanae waliopoteana kitambo kidogo sintoipata tena maishani. Inaniuma sana.
Marehemu mama akicheza siku ya harusi ya mwanae wa nne. Yeye na marehemu baba walijaliwa kupata watoto tisa, mmojaalifariki  na tukabaki wanane, wanaume sita na wanawake wawili.
Nakumbuka wakati huo ambapo wewe na marehemu Baba mlikuwa mnasherehekea miaka 50 ya ndoa yenu, ulinipa mafundisho mengi kuhusu maisha, ndoa, upendo na zaidi ni kumweka mbele Mungu katika kila ninalofanya. Kabla ya kifo chako, nilikuwa nauangalia mkanda niliowarekodi wewe na  marehemu Baba, na kila nilipofanya hivyo niligundua kuwa nina bahati ya pekee kuwa na wazazi wanaonipenda kiasi hicho. Sikujua kuwa mahojiano yale ndio ulikuwa wosia wako na marehemu baba kwangu mwanenu. Kwa sasa sina nguvu ya kuangalia video hiyo, kwani kila nikijaribu naishia kububujikwa na machozi.

Nakumbua nilipokwenda chumba cha maiti na kukuona umelazwa kwenye zile friji wanzohifadhia maiti. Nilikugusa mama, nilitaraji muujiza kwamba ungeamka na ndoto ile mbaya ingeisha. Hukuamka hadi leo hii.
Hospitali Teule ya Mtakatifu Fransisko ambapo marehemu mama alilazwa akiwa amepoteza fahamu kwa zaidi ya miezi mitatu hadi alipofariki siku kama ya leo miaka minane iliyopita
Mama,inaniuma sana kwani nilipokuja kukuuguza Februari 2008 ulikuwa umeshapoteza fahamu. Ulipokuwa Muhimbili na baadaye St Francis, Ifakara,nilikuwa najaribu kukusemesha. Kama vile ulifahamu mwanao nimekuja kukuuguza, kuna nyakati ulikuwa unatoa tabasamu lako lenye mwanya ulionirithisha. Nikategemea ungemka na kunieleza japo neno moja. Kwa bahati mbaya hadi unafariki hukuweza kuniambia chochote. Iliniuma sana, inaniuma sana na itaendelea kuniuma sana, mama.

Kabla marehemu baba hajaungana nawe huko uliko, nilikuwa na wakati mgumu sana kila nilipopiga simu nyumbani kwa wakati wa uhai wako, nilizowea kuwa nikimaliza kuongea na Baba anakupa simu wewe tupige stori. Na kila nilipoongea nawe nilijisikia kudeka kutokana na upendo wako usiomithilika. Baada ya kifo chako, na kabla marehemu baba hajafariki, kila nilipompigia simu mzee huwa nilijikuta najisahau na nataka kumwambia Mzee akupe simu niongee nawe,kisha nakumbuka kuwa hauko nasi. Sasa ndio imekuwa uchungu maradufu kwani kila nikipiga simu nyumbani, ninatamani kuongea nawe na marehemu baba kisha nakumbuka kuwa hampo nasi.

Nyakati nyingine baadhi ya watu wangu wa karibu (ninao wengi kutokana na malezi bora uliyonipatia) huwa wananiona kama dhaifu ninapowaeleza uchungu nnilio nao takriban kila siku tangu ufariki wewe na baadaye marehemu baba. Siwalaumu, kwani wanachojitahidi kufanya ni kunishawishi nikubali ukweli kuwa hampo nasi na haiwezekani kuwarejesha. Kuna wakati wananichukiza kwani najihisi kama hawaelewi jinsi kifo chako na cha baba vinavyoniathiri.Lakini baadaye akili hunirejea na kutambua wanachofanya ni kujaribu kunisaidia tu.


Mama mpendwa, sijui nisemeje. Rafiki zako wakubwa, wanao vitinda-mimba, Kulwa na Doto, ndio wananitia uchungu zaidi, Wanawa-miss mno wewe na marehemu baba kwa sababu ndio uhusiano wenu ulikuwa zaidi ya kati ya wazazi na vitinda-mimba wao. Nakumbuka siku zile nawapigia simu na kuwasikia mnacheka, mnataniana na kunipa kila aina ya faraja. Kwa sasa imebaki kumbukumbu tu.

Mama mpendwa,siku ya mazishi yako Padre alituambia maneno haya: "Mama Adelina alikuwa mtu wa watu, na kila anayemjua anafahamu hilo. Japo mnaomboleza kifo chake, lakini mnapaswa kupata faraja kuwa kutokana na matendo yake mema, Baba Yake wa Mbinguni Ameamua kumchukua. Sote tulimpenda lakini Mungu alimpenda zaidi, na ndio maana amemchukua." Maneno hayo ndio nguvu pekee inayonisaidia kumudu kufanya mambo mengine maishani. Nguvu nyingine niliyonanyo ni imani kuwa wewe na marehemu baba mnaendelea kutuombea huko mlipo.

Nyumba ya milele ya marehemu Adelina 

Basi naomba nikuage tena mama kwa kumwomba BWANA AKUPATIE WEWE NA MAREHEMU BABA PUMZIKO LA MILELE NA MWANGA WA MILELE AWAANGAZIE, MPUMZIKE KWA AMANI AMEEN.


29 May 2016

Mama mpendwa,ilikuwa siku kama yale leo,miaka minane iliyopita,uliondoka hapa duniani wakati tunakuhitaji sana.Japo miaka minne inaweza kuonekana ni muda mrefu kusahau machungu,kwangu mwanao imeshindikana.Kila siku ya Mungu ninaposali kukuombea pumziko na raha ya milele huko ulipo,hujikuta napatwa na uchungu usioelezeka.Kwa kifupi,mama mpendwa,kila siku baada ya kifo chako-siku kama ya leo miaka minane iliyopita,imeendelea kuwa ni hudhuni na majonzi yasiyoelezeka.

Mama mpendwa,ulikuwa ni zaidi ya mama kwangu,kwa mumeo marehemu Baba Mzee Chahali (aliyeungana nawe huko peponi mwaka jana),na kwa wanao wote na ndugu na jamaa.Nakumbuka mwaka 2005 nilipokuja likizo nyumbani,ulirukaruka kwa furaha,ukanikumbatia na kunipakata mwanao,ukaniandalia maji ya kuoga,ukanifanya nijsikie kama mtoto mchanga. Sikujua kuwa furaha ile ya mzazi kumwona mwanae waliopoteana kitambo kidogo sintoipata tena maishani.Inaniuma sana.
Marehemu mama akicheza siku ya harusi ya mwanae wa nne. Yeye na marehemu baba walijaliwa kupata watoto tisa, mmojaalifariki  na tukabaki wanane, wanaume sita na wanawake wawili.
Nakumbuka wakati huo ambapo wewe na marehemu Baba mlikuwa mnasherehekea miaka 50 ya ndoa yenu,ulinipa mafundisho mengi kuhusu maisha,ndoa, upendo na zaidi ni kumweka mbele Mungu katika kila ninalofanya. Kabla ya kifo chako, nilikuwa nauangalia mkanda niliowarekodi wewe na  marehemu Baba,na kila nilipofanya hivyo niligundua kuwa nina bahati ya pekee kuwa na wazazi wanaonipenda kiasi hicho. Sikujua kuwa mahojiano yale ndio ulikuwa wosia wako na marehemu baba kwangu mwanenu. Kwa sasa sina nguvu ya kuangalia video hiyo, kwani kila nikijaribu naishia kububujikwa na machozi.

Nakumbua nilipokwenda chumba cha maiti na kukuona umelazwa kwenye zile friji wanzohifadhia maiti. Nilikugusa mama,nilitaraji muujiza kwamba ungeamka na ndoto ile mbaya ingeisha. Hukuamka hadi leo hii.

Hospitali Teule ya Mtakatifu Fransisko ambapo marehemu mama alilazwa akiwa amepoteza fahamu kwa zaidi ya miezi mitatu hadi alipofariki siku kama ya leo miaka minane iliyopita

Mama,inaniuma sana kwani nilipokuja kukuuguza Februari 2008 ulikuwa umeshapoteza fahamu. Ulipokuwa Muhimbili na baadaye St Francis, Ifakara,nilikuwa najaribu kukusemesha.Kama vile ulifahamu mwanao nimekuja kukuuguza,kuna nyakati ulikuwa unatoa tabasamu lako lenye mwanya ulionirithisha. Nikategemea ungemka na kunieleza japo neno moja.Kwa bahati mbaya hadi unafariki hukuweza kuniambia chochote. Iliniuma sana, inaniuma sana na itaendelea kuniuma sana, mama.

Kabla marehemu baba hajaungana nawe huko uliko, nilikuwa na wakati mgumu sana kila nilipopiga simu nyumbani kwa wakati wa uhai wako, nilizowea kuwa nikimaliza kuongea na Baba anakupa simu wewe tupige stori. Na kila nilipoongea nawe nilijisikia kudeka kutokana na upendo wako usiomithilika. Baada ya kifo chako, na kabla marehemu baba hajafariki, kila nilipompigia simu mzee huwa nilijikuta najisahau na nataka kumwambia Mzee akupe simu niongee nawe,kisha nakumbuka kuwa hauko nasi. Sasa ndio imekuwa uchungu maradufu kwani kila nikipiga simu nyumbani, ninatamani kuongea nawe na marehemu baba kisha nakumbuka kuwa hampo nasi.

Nyakati nyingine baadhi ya watu wangu wa karibu (ninao wengi kutokana na malezi bora uliyonipatia) huwa wananiona kama dhaifu ninapowaeleza uchungu nnilio nao takriban kila siku tangu ufariki wewe na baadaye marehemu baba.Siwalaumu,kwani wanachojitahidi kufanya ni kunishawishi nikubali ukweli kuwa hampo nasi na haiwezekani kuwarejesha. Kuna wakati wananichukiza kwani najihisi kama hawaelewi jinsi kifo chako kinavyoniathiri.Lakini baadaye akili hunirejea na kutambua wanachofanya ni kujaribu kunisaidia tu.


Mama mpendwa, sijui nisemeje. Rafiki zako wakubwa, wanao vitinda-mimba,Kulwa na Doto, ndio wananitia uchungu zaidi, Wanawa-miss mno wewe na marehemu baba kwa sababu ndio uhusiano wenu ulikuwa zaidi ya kati ya wazazi na vitinda-mimba wao. Nakumbuka siku zile nawapigia simu na kuwasikia mnacheka,mnataniana na kunipa kila aina ya faraja. Kwa sasa imebaki kumbukumbu tu.

Mama mpendwa,siku ya mazishi yako Padre alituambia maneno haya: "Mama Adelina alikuwa mtu wa watu, na kila anayemjua anafahamu hilo. Japo mnaomboleza kifo chake, lakini mnapaswa kupata faraja kuwa kutokana na matendo yake mema, Baba Yake wa Mbinguni Ameamua kumchukua.Sote tulimpenda lakini Mungu alimpenda zaidi,na ndio maana amemchukua." Maneno hayo ndio nguvu pekee inayonisaidia kumudu kufanya mambo mengine maishani. Nguvu nyingine niliyonanyo ni imani kuwa wewe na marehemu baba mnaendelea kutuombea huko mlipo.

Nyumba ya milele ya marehemu Adelina 

Basi naomba nikuage tena mama kwa kumwomba BWANA AKUPATIE NA MAREHEMU BABA PUMZIKO LA MILELE NA MWANGA WA MILELE AWAANGAZIE, MPUMZIKE KWA AMANI AMEEN.


29 May 2015

Tarehe kama ya leo miaka 7 iliyopita (29/05/2008), mama yangu mzazi Adelina Mapango (Mama Chahali) alifariki. Kifo chake kimeacha pengo kubwa lisilozibika-kwa mumewe (yaani baba) walodumu katika ndoa kwa miaka 53, kwa sie wanawe wanane, na hasa kwa vitinda mimba Kulwa na Doto ambao kwao marehemu alikuwa ni zaidi ya mzazi kwao bali rafiki pia. Miaka 6 imepita lakini uchungu moyoni ni kama kifo hicho kimetokea leo. We miss you so much mama. We stiĺl and will always love you. May your soul rest in eternal peace. Amen!




29 May 2013


Tarehe kama hii, miaka mitano uliyopita,mama mpendwa Adelina Mapango, uliagana nasi. Nikisema 'uliagana nasi' inaweza kutafsiriwa kana kwamba ulipata nafasi ya kutuaga.Nilikuja huko nyumbani kukuuguza Februari 2008, lakini tangu nilipokuona pale Muhimbili hadi tarehe 29 Mei 2008 hukuwahi japo kuniambia neno moja la mwisho.Nakumbuka ulivyokuwa ukiniangalia kwa upendo wako mkubwa,nakumbuka pia tabasamu lako licha ya maumivu makubwa uliyokuwa nayo.Lakini kila nilipojaribu angalau kusikia neno lako moja tu,haikuwezekana hadi siku unafariki.

Mama mpendwa, kabla ya kifo chako sikuwahi kuelewa maana ya kufiwa na mzazi au mtu wa karibu.Sasa sio tu naelewa bali kila siku ya Mungu tangu siku ulipotutoka imekuwa kama ndoto mbaya ambayo natamani iishe ili hali irejee kuwa kama zamani.Kwa bahati mbaya, ndoto hiyo mbaya ni ukweli (hali halisi), na hadi sasa matarajio kuwa kuna siku nitaamka na kukuona au kukusikia ukiwa hai yanazidi kufifia.Kwa kifupi,mama mpendwa,hadi leo bado napata shida kuamini na kukubali kuwa haupo nasi.

Nyakati mbili ngumu zaidi kwangu ni wakati ninapofanya sala kabla ya kulala ambapo wakati wa uhai wako nilikuwa nikisali "Ee Bwana uijalie familia yangu yani Baba na Mama..." lakini sasa inabidi nimtaje Baba pekee.Pia wakati wa uhai wako,nilijenga utaratibu kwamba nikipiga simu naanza kuongea na Baba kisha anapitisha simu kwako tunaanza kutia stori mbalimbali.Sasa,mama,nikimaliza kuongea na Baba huwa najikuta nasahau kuwa haupo hapo nyumbani,na kumwambia Baba akupe simu...then nakumbuka haupo.Naishia kutoa machozi.

Nikiwa mbinafsi,nitaangalia tu jinsi ninavyopata shida kukabiliana na ukweli kuwa hauko nasi.Lakini kuna rafiki yako kipenzi Baba Mzee Chahali ambaye yeye amekuwa mtu tofauti kabisa tangu ulipoondoka.Kama unavyokumbuka,baba ni mtu mkimya,mwenye marafiki wachache, na rafiki yake mkuu ulikuwa wewe.Sasa tangu uondoke,baba amekuwa mnyonge kupita kiasi.Kibaya zaid, ameendelea kudai labda yeye ndio angestahili kutangulia mbele ya haki kwa vile alikuwa amekuzidi kiumri.Kwa hakika, baba ameendelea kuwa katika wakati mgumu sana licha ya sapoti kubwa tunayompatia.

Lakini pia kuna rafiki zako wapenda Kulwa na Doto (Peter na Paul). Pengine kwa vile wao ni last borns, walikuwa wakikuchukulia zaidi ya mzazi, ulikuwa kama bibi yao, shangazi yao, na kikubwa zaidi, rafiki yao.Kila ninapoongea na wadogo zangu hawa najiskia kutokwa na machozi.Kimsingi, sidhani kama waliwahi kuwaza kuwa na maisha bila ya uwepo wako mama.

Familia yote kwa ujumla inakukumbuka sana mama.Nina mkanda wa video niliowarekodi wewe na baba mlipokuwa mnaadhimisha miaka 50 ya ndoa yenu mwaka 2005,lakini kila nikijaribu kuuangalia najikuta nabubujikwa na machozi.Katika mkanda huo uliongea mambo mengi ya msingi kuhusu maisha.Kuna nyakati nataka kuuangalia ili nirejee wosia wako lakini nashindwa kwa sababu ya uchungu.

Mama nilikupenda sana,ninakupenda sana,na nitaendelea kukupenda milele.Kwangu, japo hupo nasi kimwili,lakini unaendelea kuishi nasi kiroho.Nitazidi kukukumbuka kwa sala kila siku,na ninaamini huko uliko unapata faraja kila ninapotenda mambo kwa kuzingatia mafundisho yako.

WE MISS YOU SO MUCH MAMA MPENDWA

PUMZIKO LA MILELE AKUPE EE BWANA NA MWANGA WA MILELE AKUANGAZIE UPUMZIKE KWA AMANI AMINA

29 May 2012


Mama mpendwa,ilikuwa siku kama yale leo,miaka minne iliyopita,uliondoka hapa duniani wakati tunakuhitaji sana.Japo miaka minne inaweza kuonekana ni muda mrefu kusahau machungu,kwangu mwanao imeshindikana.Kila siku ya Mungu ninaposali kukuombea pumziko na raha ya milele huko ulipo,hujikuta napatwa na uchungu usioelezeka.Kwa kifupi,mama mpendwa,kila siku baada ya kifo chako-siku kama ya leo miaka minne iliyopita,imeendelea kuwa ni hudhuni na majonzi yasiyoelezeka.

Mama mpendwa,ulikuwa ni zaidi ya mama kwangu,kwa mumeo-Baba Mzee Chahali,na kwa wanao wote na ndugu na jamaa.Nakumbuka mwaka 2005 nilipokuja likizo nyumbani,ulirukaruka kwa furaha,ukanikumbatia na kunipakata mwanao,ukaniandalia maji ya kuoga,ukanifanya nijsikie kama mtoto mchanga.Sikujua kuwa furaha ile ya mzazi kumwona mwanae waliopoteana kitambo kidogo sintoipata tena maishani.Inaniuma sana.

Nakumbuka wakati huo ambapo wewe na Baba mlikuwa mnasherehekea miaka 50 ya ndoa yenu,ulinipa mafundisho mengi kuhusu maisha,ndoa,upendo na zaidi ni kumweka mbele Mungu katika kila ninalofanya.Kabla ya kifo chako,nilikuwa nauangalia mkanda niliowarekodi wewe na Baba,na kila nilipofanya hivyo niligundua kuwa nina bahati ya pekee kuwa na wazazi wanaonipenda kiasi hicho.Sikujua kuwa mahojiano yale ndio ulikuwa wosia wako kwangu mwanao.Kwa sasa sina nguvu ya kuangalia video hiyo,kwani kila nikijaribu naishia kububujikwa na machozi.

Nakumbua nilipokwenda chumba cha maiti na kukuona umelazwa kwenye zile friji wanzohifadhia maiti.Nilikugusa mama,nilitaraji muujiza kwamba ungeamka na ndoto ile mbaya ingeisha.Hukuamka hadi leo hii.

Mama,inaniuma sana kwani nilipokuja kukuuza Februari 2008 ulikuwa umeshapoteza fahamu.Ulipokuwa Muhimbili na baadaye St Francis,Ifakara,nilikuwa najaribu kukusemesha.Kama vile ulifahamu mwanao nimekuja kukuuguza,kuna nyakati ulikuwa unatoa tabasamu lako lenye mwanya ulionirithisha.Nikategemea utaamka na kunieleza japo neno moja.Kwa bahati mbaya hadi unafariki hukuweza kuniambia chochote.Inaniuma sana mama.

Inauma zaidi ninapopiga simu nyumbani.Nilizowea kuwa nikimaliza kuongea na Baba anakupa simu wewe tupige stori.Sasa,kila ninapompigia mzee huwa najikuta nataka kumwambia Mzee akupe simu niongee nawe,kisha nakumbuka kuwa hauko nasi.Kila simu ninayopiga nyumbani inanirejeshea kumbukumbu hizo na kuniacha mpweke,mkiwa na mwenye uchungu mkubwa.

Nyakati nyingine baadhi ya watu wangu wa karibu (ninao wengi kutokana na malezi bora uliyonipatia) huwa wananiona kama dhaifu ninapowaeleza uchungu nnilio nao takriban kila siku tangu ufariki.Siwalaum,kwani wanachojitahidi kufanya ni kunishawishi nikubali ukweli kuwa haupo nasi na haiwezekani kukurejesha.Kuna wakati wananichukiza kwani najihisi kama hawaelewi jinsi kifo chako kinavyoniathiri.Lakini baadaye akili hunirejea na kutambua wanachofanya ni kujaribu kunisaidia tu.

Mama mpendwa,sijui nisemeje.Rafiki zako wakubwa,wanao vitinda-mimba,Kulwa na Doto,ndio wananitia uchungu zaidi,kama ilivyo kwa Baba.Watatu hao pamoja na wewe mlikuwa kama marafiki.Nakumbuka siku zile nawapigia simu na kuwasikia mnacheka,mnataniana na kunipa kila aina ya faraja.Kwa sasa imebaki kumbukumbu tu.

Mama mpendwa,siku ya mazishi yako Padre alituambia maneno haya: "Mama Adelina alikuwa mtu wa watu,na kila anayemjua anafahamu hilo.Japo mnaomboleza kifo chake,lakini mnapaswa kupata faraja kuwa kutokana na matendo yake mema,Baba Yake wa Mbinguni Ameamua kumchukua.Sote tulimpenda lakini Mungu alimpenda zaidi,na ndio maana amemchukua." Maneno hayo ndio nguvu pekee inayonisaidia kumudu kufanya mambo mengine maishani.

Basi naomba nikuage tena mama kwa kumwomba BWANA AKUPATIE PUMZIKO LA MILELE NA MWANGA WA MILELE AKUANGAZIE,UPUMZIKE KWA AMANI AMEEN.

29 May 2011



Ilikuwa dakika,masaa,siku,wiki,mwezi,miezi,mwaka na sasa ni mwaka wa tatu tangu mama yangu mpendwa Adelina Mapango alipotuacha na majonzi ambayo kamwe hayatafutika.

Mara ya mwisho kuonana na mama akiwa hai ni mwaka 2005 nilipokwenda nyumbani kwa ajili ya fieldwork yangu.Novemba mwaka huo,ndoa ya Baba Mzee Philemon Chahali na Mama ilitimiza miaka 50,yaani nusu karne.Niliwarekodi kwenye video na kila ninapojaribu kuangalia mkanda huo naishia kububujikwa na machozi.Bila kujua kuwa ananiachia wosia,mama alisisitiza sana kuhusu upendo.Aliniambia kuwa nikiwa mcha Mungu nitaweza kuwapenda watu wote.Alinisisitiza kumtanguliza Mungu katika kila nifanyalo.Alininiambia pia kuwa zawadi kubwa nitakayoweza kumpa yeye na mumewe ni kufanikiwa katika masomo na maisha yangu kwa ujumla,kuwatunza wazazi na ndugu zangu,kwathamini marafiki na jamaa zangu,kuheshimu kazi na pindi nikioa,nimpe upendo mke wangu na watoto kama ambavyo yeye na baba walivyonipenda.

Mama alikuwa na upendo usioelezeka.Nakumbuka nikiwa mdogo huko Kigoma timu ya Pan Africa ilifanya ziara huko.Wakati huo,binamu yangu Gordian Mapango alikuwa bado anacheza mpira (kama winga machachari wa Pan Africa).Basi Gordian alikuja kututembelea nyumbani akiwa na rafiki zake marehemu Ibrahimu Kiswabi na mchezaji mwingine jina limenitoka.Walipoingia tu ndani mama akakaa chini na kumpakata Gordian kama mwanae mchanga vile.Japo nilikuwa mdogo lakini bado nakumbuka jinsi marehemu Kiswabi na yule mchzaji mwingine walivyoguswa na upendo wa mama kwa mtoto wa kaka yake (Gordian).

Kwa vile mwaka 2005 nilikaa Tanzania kwa takriban miezi sita hivi,nilikuwa nikienda nyumbani Ifakara mara kwa mara,kila nilipopata fursa nje ya fieldwork yangu.Kila nilipokuwa hapo nyumbani mama alisisitiza kunichemshia maji ya kuoga,kunifulia na kunitunza kama mtoto mchanga.Mama,upendo ulionipa nitaendelea kuukumbuka hadi naungana nawe huko uliko.

Nilimeshahudhuria misiba mbalimbali lakini kufiwa na mzazi ni kitu kisichoelezeka.Nakumbuka nilikuwa Kinondoni Mtaa wa Isisi pamoja na binamu yangu Gordian na marafiki wengine,na majira ya saa 4.30 usiku nikapigiwa simu kutoka Ifakara (maana wakati huo nilikuwa Dar kwa muda).Ile kupokea tu nikamsikia sista (wa kanisani) aliyekuwa mmoja ya masista waliokuwa wanamsaidia sista mwenzao (mdogo wangu) Sr Maria-Solana kumuuguza mama.Huku akilia,sista huyo akaniambia "Kaka Evarist,mama hatunaye".Nikamuuliza "unamaanisha nini?"Akaendela kusema "mama hatunaye,ametutoka".Nikawa kama nimepigwa ganzi vile.Yani ilinichukua kama nusu saa hivi,baada ya kuondoka Kinondoni na kurejea Sinza (nilipokuwa nimefikia)
 kupata fahamu kuwa hatimaye mama yangu mpendwa Adelina Mapango amefariki.

Niliongea na mama mara ya mwisho mwezi Februari 2008.Nilipiga simu nilipopata taarifa kuwa mama mkubwa (dada yake mama) alikuwa amefariki.Japo hali ya mama wakati huo haikuwa nzuri sana,alisistiza kuwa lazima aende kumzika dada yake.Nikamsihi mama kuwa kwa hali aliyonayo,na kwa jinsi alivyompenda dada yake,ni vema asiende msibani.Kumbe siku hiyo ndio nilikuwa naongea nae kwa mara ya mwisho.Siku chache baadaye akapata stroke na akapoteza fahamu.Wiki chache baadaye nikaenda Tanzania kumuuguza lakini kwa bahati mbaya hadi anafariki hakuweza kufumbua mdomo kuongea nami.

Kinachonitia uchungu hadi leo ni ukweli kwamba siku nilipomtembelea hospitalini Muhimbili baada ya kufika Dar alitoa kama tabasamu hivi.Hata baadhi ya manesi na ndugu waliokuwa wanamuuguza wakasema inaelekea mama amefurahi mwanae nimekwenda kumuuguza.Niliendelea kuwa na matumaini kuwa ipo siku atapata fahamu na hatimaye kurejea kwenye hali yake ya kawaida.Kwa bahati mbaya haikutokea hivyo hadi anafariki.
Kwa kweli bado nina uchungu mkubwa sana.Kuzidisha machungu hayo ni ndoto za mara kwa mara ambapo mama namuona mama.Pengine ni kwa vile namuwaza sana,au pengine ni kwa vile alifariki bila kuniambia chochote.Majonzi niliyonayo moyoni hayaelezeki.

Kuna tatizo jingine.Wakati mama anafariki,baba alikuwa amemzidi kama miaka 10 hivi.Ikumbukwe pia kuwa walikuwa kwenye ndoa kwa miaka 53 wakati mama anafariki.Sasa baba hadi leo hii anaendelea kuona kama yeye ndiye alistahili kutangulia kabla ya mkewe kwa vile alikuwa amemzidi umri.Baba na marehemu mama walikuwa zaidi ya mke na mume.Walikuwa best friends.Baba yangu si mzungumzaji sana,na muda mwingi aliutumia nyumbani na mkewe.Kifo cha mama kinamtesa sana baba na kila ninapoongea nae anakumbushia uchungu alionao.

Kuna tatizo jingine pia.Wadogo zangu wa mwisho ni mapacha.Baba na mama walijaliwa kuwapata mapacha hawa wakati umri umeshawatupa mkono.Kwahiyo,Kulwa na Doto wamekuwa kama wajukuu kwa baba na mama.Kwa wadogo zangu hawa,mama alikuwa ni za zaidi ya mzazi wao.Alikuwa ni mwalimu wao (akiwafundisha kupika,sala,nk),alikuwa kama bibi yao (walikuwa wanapenda sana kumtania na yeye alipenda kuwatania pia),alikuwa ni rafiki yao mkubwa kwa vile madogo hao walikuwa wanamwongopa baba,kwahiyo siri zao,habari zao na kila kitu chao walikuwa wanashea na marehemu mama.Kwa ndugu zangu hawa,kifo cha mama ni pigo kubwa sana sana.

Naweza kuandika kitabu kizima kuelezea tukio hili la kusikitisha kupita kiasi.Lakini yote ni mipango ya Mungu.Nakumbuka katika misa ya kabla ya mazishi ya mama,padre alijaribu kutuliwaza kwa kutuambia kwamba "sote tulimpenda Adelina lakini Baba yake aliyepo Mbinguni amemependa zaidi na hivyo ameamua kumchukua mwanae".

Basi,mama mpendwa,leo tunaadhimisha mwaka wa tatu tangu utuache.Pengo lako haliwezi kuzibika.Tunakukumbuka kila siku.Upendo wako,tabasamu lako la muda wote na huruma uliyokuwa nayo ni vitu tunavyoendela kuvienzi.Mafundisho uliyotupa ndio mwongozo wetu wa kila siku.

PUMZIKO LA MILELE AKUPE BWANA NA MWANGA WA MILELE AKUANGAZIE,UPUMZIKE KWA AMANI.AMINA


29 May 2010

Mama Mpendwa,

Ilikuwa saa 4.30 usiku,tarehe 29 Mei 2008 ulipotutoka.Nakumbuka nilipopigiwa simu kufahamishwa kuwa Bwana Amekutwaa,nilidhani ni ndoto tu.Japo ulikuwa umepoteza fahamu kwa zaidi ya miezi mitatu kabla ya kukumbwa na mauti sote tuliamini kuwa siku moja ungeamka ukiwa mzima.Mama,japo leo ni miaka miwili tangu ututoke,bado nahisi niko ndotoni na nimeshindwa kabisa kukubaliana na ukweli kwamba haupo nasi.Mara kwa mara nakuona ndotoni,lakini napoamka nagundua ni ndoto tu,na hiyo inazidisha uchungu na majonzi.

Baba Mzee Chahali,uliyeishi nae katika ndoa kwa miaka 50,anaendelea kukukumbuka mno.Ni vigumu zaidi kwake kukabiliana na kututoka kwako kwa vile ulikuwa ni rafiki yake mkuu,mtu wake wa karibu kabisa na kila kitu kwake kama ilivyo kwetu.Mapacha, Kulwa (Peter) na Doto (Paul) nao wameendelea kuwa na wakati mgumu kwa vile wewe ulikuwa zaidi ya mama yao.Walikutania,walicheka nawe,walikusaidia kazi za nyumbani,walikwambia furaha na majonzi yao,na waliringa kuwa na mzazi mwenye upendo kama wewe.

Japosiku zote  tangu ututoke tumekuwa na wakati mgumu sana,siku hii ya leo tunapoadhimisha miaka miwili ya kifo chako ni ngumu zaidi kwetu.Inaleta kumbukumbu zisizoelezeka na zisizostahimilika.

Kazi ya Mungu haina makosa.Tukijiuliza sana kwanini alikuchukua wakati bado tunakuhitaji sana tutakuwa tunakufuru.Tunajaribu kujifariji kwa kuamini kuwa alikuchukua kwa vile alikupenda zaidi yetu.Na tunajitahidi pia kujiridhisha kuwa huko ulipo unapata pumziko la amani na unaangaziwa mwanga wa milele ukistarehe kwa amani.Japo haupo nasi kimwili lakini siku zote tupo nawe kiroho.

Pumziko la Milele Akupe Ee Bwana na Mwanga wa Milele Akuangazie Ustarehe Kwa Amani,Amen.

14 Mar 2010


It's like you were gone yesterday.I just can't believe that you're gone.On this day,I'd be calling you and daddy to say how much I love you,mamma.But you're not there.The only comfort I have is the strong belief that you're resting in peace.And though you're not with us on this Mother's Day,you remain the best thing God could give any son.Rest in peace,mamma.You'll always be missed and remembered!Oh! My mama, happy mother’s day
You are the greatest mother I have ever had
You are my mother today
You will be my mother tomorrow
You are always my mother
You will forever be my mother

Thank you my mother for bringing me into this world
Thank you my mother for taking care of me in your womb
Thank you my mother caring for me as a toddler
Thank you my mother for feeding me since I was a baby
Thank you my mother for all the clothes you bought for me
Thank you my mother for teaching me good manners at home

Thank you my mother for sending me to school
Thank you my mother for supervising my homework
Thank you my mother for ensuring I eat before going to school
Thank you my mother for all the regular pocket money
Thank you my mother for liking my friends
Thank you my mother for all the everyday advices

My mother always remind me that fingers are not equal
As I grow up, I have seen the correlation of this analogy
To many human beings, neighbors, societies and nationalities
Oh! My mama, thank you for your words of wisdom
My mother taught me many things that I have never read in books
Thank you my mother for all your guiding philosophies

Oh! My mama, I sincerely wish everyday could be Mother’s Day
One day in a year is not enough to thank my wonderful mother
Oh! My mama, I will forever be your child
Oh! My mama, you will eternally be my mother
Thank you my mother for being my best friend
Thank you my mother for being my trusted adviser
I honestly wish you HAPPY MOTHER’S DAY!
.Rest in Eternal Peace,mamma!

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.