Showing posts with label AFYA. Show all posts
Showing posts with label AFYA. Show all posts

30 Dec 2014



Nesi mmoja aliyekwenda Sierra Leone kusaidia harakati za kukabiliana na janga la ugonjwa wa Ebola, amerudi Uingereza akiwa ameambukizwa ugonjwa huo, na hivi sasa amelazwa kwenye kituo cha maradhi ya kuambukiza cha Browlee katika Hospitali Kuu ya Gartnavel, hapa Glasgow.

Nesi huyo anatarajiwa kuhamishiwa London kwenye hospitali maalum ya Royal Free Hospital.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu wa Uskochi, Nicola Sturgeon, amewahakikishia wakazi wa Glasgow na Uskochi kwa ujumla kuwa uwezekano wa kusambaa kwa ugonjwa huo kutokana na maambukizi ya nesi huyo ni 'sawa na sifuri.'

Hata hivyo, bado kuna maswali ilikuwaje nesi huyo aliyepimwa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Heathrow, London, kabla ya kuunganisha ndege na kuja Glasgow, hakugundulika kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo hatari usio na kinga wala tiba.

Profesa Jonathan Ball, mtaalam wa 'molecular virology' katika Chuo Kikuu cha Nottingham, ameeleza kuwa kesi hiyo inaashiria ugumu wa mkakati wa kupima wasafiri kutoka nchi zilzoathirika na Ebola wanapoingia Uingereza.

Chini ni baadhi ya picha zinazohusiana na habari hii ambayo waweza kuisoma kwa kirefu HAPA

A female health worker who returned from Sierra Leone last night is being treated for Ebola at Glasgow's Gartnavel Hospital (pictured), the Scottish Government confirmed
Hospitali ya Gartnavel

Safari ya nesi aliyeambukizwa Ebola, kutoka Sieera Leone hadi Glasgow.



The health worker was admitted to hospital early yesterday morning after feeling unwell and was placed in isolation 

The ebola patient is being treated at the specialist Brownlee Unit for Infectious Diseases at Gartnavel Hospital
Kituo cha maradhi ya kuambukiza cha Brownlee

7 Oct 2014

10_06_DrSenga-cropped
Dokta Senga Omeonga (pichani), daktari bingwa wa upasuaji nchini Liberia, anadhani anajua jinsi gani aliambukizwa ugonjwa hatari wa Ebola.

Julai 15 mwaka huu, bosi wa daktari huyo aliingia ofisini kwake katika Hospitali ya Mtakatifu Joseph, jijini Monrovia, akiwa na mashaka makubwa. Bosi huyo, Mkurugenzi wa hospitali hiyo, alimwambia Dokta Omeonga, amepeana mkono na mtu ambaye baadaye aligundulika kuwa na ugonjwa wa Ebola, na sasa hajiskii vizuri. Mkurugenzi huyo alisema alikuwa akitapika, anasikia kuumwa na kichwa, na alikuwa na homa kali. Lakini siku mbili baadaye, baada ya vipimo vya maabara kuonyesha hajaathirika, na hofu ya Ebola kuondoka, Dokta Omeonga na wenzie walianza kumhudumia bosi wao kama mgonjwa wa kawaida wa malaria au homa ya matumbo.

"Tulivaa glovu wakati tunamhudumia, lakini si katika hali ya tahadhari sana," alisema Dokta huyo.

Wiki moja baadaye, afya ya Mkurugenzi ilizidi kuwa mbaya, na akachukuliwa vipimo vingine. Safari hii majibu yakaonyesha anaugua Ebola, ikiwa ni tukio la kwanza la vipimo vya awali kuonyesha mgonjwa hana maambukizi kabla ya vipimo vya pili kuonyesha ana maambukizi. Neno la kitabibu kwa hali hiyo ni 'false negative.'

Ghafla, kila aliyemhudumia Mkurugenzi huyo akawa katika hofu kubwa. na mwenye uwezekano wa kuwa ameambukizwa Ebola. Hospitali hiyo ikawekewa karantini, na Mkurugenzi akafariki Agosti 2, siku ambayo Dokta Omeonga alianza kutojiskia vizuri kiafya. Kati ya watumishi 20 waliomhudumia Mkurugenzi huyo, 15 walikutwa na Ebola, ikiwa ni pamoja na Dokta Omeonga. Tisa kati yao wameshafariki, ila yeye na wenzie watano wamesalimika.

Daktari huyo aliongea kwa simu na jarida la Newsweek la Marekani kutoka nyumbani kwake nchini Liberia, ambapo wiki tano baada ya kubainika kuwa hana virusi vya ugonjwa huo, bado anajikongoja kurejesha nguvu mwilini.

Hivi mtu anajiskiaje anapokuwa na Ebola?

Ni vigumu kueleza. Mie ni mtu mwenye afya njema. Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuugua kiwango hicho. Hali ilikuwa mbaya sana sana. Unajiskia dhaifu kupita kiasi na uchovu mwingi. Unatapika na unajiskia homa na kichwa kuuma. Sio kama malaria. Ukiwa na malaria waweza japo kutembea, na unaweza kumeza dawa zako. Ebola ni tofauti kabisa. Ni kama mwili wako haupo nawe tena. Unajiskia huwezi kujihudumia mwenyewe, lazima awepo mtu wa kukuhudumia muda wote.

Ilikuwaje kwako na wenzio pale hospitali yenu ilipowekewa karantini?

Sote tulikuwa na dalili zinazofanana. Kila siku, mmoja baada ya mwingine alikuwa akilalamika kuhusu hali ilivyokuwa inazidi kuwa mbaya. Wakati mwingine tulikuwa tukicheka pamoja na kila kitu kuonekana kama kipo sawia.Lakini pale hali ilipoanza kubadilika, hakuna aliyweza japo kuamka kutoka kitandani.

Walikuwa wakichukua wagonjwa wale tu ambao walikuwa na hali mbaya kupindukia na kuwapelekea kwenye eneo la matibabu ya Ebola. Mie nilikuwa miongoni mwa waliokuwa na nafuu kidogo, kwahiyo ilibidi nisubiri kitambo. Eneo hilo la matibabu lilikuwa ni moja tu kwa jiji zima la Monrovia. Vitanda 40 tu. Ilibidi nisubiri wiki nzima kabla ya kupatia kitanda. Japo walikuwa wakitoa kipaumbele kwa watumishi wa sekta ya afya, bado ilichukua wiki nzima kupata kitanda.

Ulikuwa mmoja wa watumishi watatu wa hospitali yako kupatia dawa ya majaribio ZMapp. Ulijiskiaje ulipoanza kutumia vidonge hivyo?

Nilipewa ZMapp wiki moja baada ya kulazwa katika eneo la matibau ya Ebola. Nilikuwa nikijiskia ahueni kidogo, kuhara kulikuwa kumesimama. Nilikuwa sitapiki tena, na nilikuwa nikijilazimisha kula japo kidogo. Sikuwa na hali mbaya sana wakati naanza kutumia vidonge hivyo. Ninachoweza kusema ni kwamba labda vidonge hivyo vilisaidia kasi ya uponyaji wangu lakini huenda ningeweza kupona bila hata kuvitumia.


Ulijiskiaje kutumia dawa mbayo ilikuwa katika majaribio?

Nilikuwa na hofu kiasi. Lakini pia sikujali sana kwa sababu nilikuwa sina njia nyingine.Hiyo ilikuwa nafasi yangu ya kupata uponyaji. Kama ingenisaidia, ningeiridhia.

Wewe na wenzako mliyamudu vipi matibabu ya vidonge hivyo?

Kwa bahati mbaya, daktari aliyepaswa kupewa vidonge hivyo alifariki siku vilipowasili. Kwahiyo walimpatia mwingine aliyekuwa amepoteza fahamu. Shukrani kwa Mungu kwani hali yake ilikuwa mahututi na uwezekano wa kusalimika ulikuwa mdogo.Lakini baada ya kumeza vidonge hivyo hali yake iliboreka na kila mtu alishangaa. Siku iliyofuata alirejewa na fahamu. Siku chache baadaye aliweza kutembea. Daktari mwingine aliyepatiwa vidonge hivyo alifariki. Kwahiyo kati yetu watatu, mmoja alifariki na sie wawili tulisalimika.

Je dawa hizo zilikuwa na matokeo yasiyokusudiwa (side effects)?


Nilipatwa na matatizo katika dozi ya mwisho ya ZMapp lakini nadhani ilitokana na kasoro za kitabibu, kwa sababu hawakunipatia dawa ya kuzwia aleji niliyostahili kupewa. Nilipatwa na hali mbaya, nikawa najiskia baridi kali, shida katika kupumua vizuri, na maumivu makali ya kichwa. Hali ilikuwa mbaya sana. Kwahiyo ilibidi wasitishe matibabu na kunipatia dawa aina ya cortisone. Baada ya hapo nikawa dhaifu sana. Sikumudu japo kutoka kitandani. Baadaye nikaanza kujisikia nafuu.Nilikaa katika eneo la matibabu ya Ebola kwa wiki mbili unusu.

Wajiskiaje sasa?


Nimekuwa nyumbani kwa mwezi na wiki moja sasa. Kuna maendeleo ya kuridhisha kila siku. Nguvu zangu zanirejea. Lakini hatua ya kuwa katika afya ya kawaida inakuja taratibu sana. Bado naskia maumivu ya viungo, na udhaifu mwilini bado upo. Ni vigumu kusema lini nitakuwa nimepona kabisa- labda pengine mwezi mzima kutoka sasa. Hakuna anyefahamu hali inakuwaje baada ya kupona Ebola kwa sababu virusi vya ugonjwa huo vinateketeza kila kitu mwilini.

Je una familia?

Familia yangu haipo hapa nami, vinginevyo wote wangekuwa wameambukizwa. Wapo nchini Kanada.

Utafanya nini baada ya kupona kabisa?


Nitarejea kazini. Nitawahudumia wagonjwa kama kawaida. Kwa sasa nina kinga dhidi ya aina ya maambukizi (strain) ya Ebola niliyoambukizwa. Hiyo ni moja ya aina hatari kabisa za maambukizi ya Ebola, kwahiyo kama una kinga dhidi yake basi yawezekana kuwa na kinga dhidi ya aina nyinginezo pia.

Nitatumia zana za kujikinga. Hiyo ni lazima kwani kuna hatari ya kuwaambukiza wagonjwa wengine baada ya kuwabeba wagonjwa.  Hospitali yangu imefungwa kwa takriban miezi miwili sasa. Wizara ya Afya imenyunyizia dawa hospitali hiyo, na tuna mpango wa kuifungua tena baada ya miezi miwili.

Unadhani kwanini watumishi wengi wa sekta ya afya wameambukizwa Ebola?


Hatuna zana za kutosha za kujikinga na maambukizi. Hiyo ni changamoto kubwa na tatizo kubwa. Ndio maana hospitali nyingi zimefungwa. Hakuna zana za kutosha kwa kila mtumishi wa sekta ya afya. Wanaweza kukupatia glovu lakini wasikupe magauni rasmi ya kuhudumia wagonjwa wa Ebola. Au wanaweza wasikupe kinga ya uso (mask). Lakini sasa kutokana na misaada ya kimataifa, hali inazidi kuwa bora., na kama hatuna zana za kujikinga na maambukizi hatuwahudumii walioambukizwa. Lakini kwa kutowatibu, wagonjwa wanarudi majumbani na kuambukiza jamii zao. Hilo ni tatizo kubwa.

CHANZO: Imetafsiriwa kutoka jarida la NEWSWEEK





25 Aug 2014

Mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola hadi hivi karibuni ulikuwa katika baadhi ya nchi za Afrika Magharibi pekee: Sierra Leone,Liberia, Nigeria, na Guinea. Sasa nchi ya tano imeingia kundini,imeripotiwa kuwa watu wawili wamefariki kwa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Kongo (DRC)- zamani Zaire- nchi iliyopo Afrika ya Kati.

Waziri wa Afya wa DRC, Dr Felix Kabange Numbi, ameeleza kuwa watu wawili wamefariki kwa Ebola, Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo.Kwa mujibu wa ripoti, tayari kuna vifo 13 vilivyosababishwa na ugonjwa huo hatari. Awali, Shirika la Afya Duniani (WHO) lilidhani vifo hivyo havihusiani na Ebola hadi ilipothibitishwa na DRC kuwa vimetokana na Ebola.

Uhusino kati ya Ebola DRC na mlipiko katika nchi za Afrika Magharibi hauko bayana, huku WHO ikieleza kuwa bado inaendelea na uchunguzi, hasa kubaini iwapo dalili za 'Ebola ya DRC' ni sawa au tofauti na ile ya Afrika Magharibi.

Hadi mwaka huu, milipuko iliyopita ya Ebola ilikuwa Afrika ya Kati, huku DRC ikiwa mhanga wa mara kwa mara. Kwa mara ya kwanza, Ebola iligundulika eneo hilo mwaka 1976

Je Ebola itaibukia wapi kwingine?

Hadi sasa kumekuwa na matukio yanayohusishwa na Ebola katika bara la Ulaya, Asia na Amerika ya Kaskazini, lakini katika matukio yote, wagonjwa walipimwa na kugundulika hawajaambukizwa ugonjwa huo. Wataalam wa afya hawana hofu ya Ebola kusambaa katika nchi zilizoendelea, kwa sababu milipuko ya ugonjwa huo hujitokeza zaidi katika nchi zenye maji yasiyo salama na zisizo na raslimali za kupambana nao, na sio mataifa tajiri kama Marekani.

Kwa sasa, uwezekano mkubwa wa kusambaa kwa Ebola katika maeneo ambayo hayajaathiriwa ni watu wanaosafiri kutoka eneo moja hadi jingine.Kwa kiwango cha nchi, uwezekano mkubwa wa kusambaa kwa ugonjwa huo ni kwa safari za ndege.

Hadi kufikia Agosti 22  mwaka huu kuna matukio 1082 ya Ebola na vifo 624 vilivyoripotiwa kutokana na ugonjwa huo hatari 

Imetafsiriwa kutoka tovuti ya kituo cha runinga cha VOX

24 Aug 2014

Kaleem, a keen cricketer, said the teachers at his school have told him other children are 'scared' of his hands

Doctors in India have been left baffled by his growing hands and many are at a loss as to what the condition is

The youngster has difficulty eating, tying his shoelaces and carrying out other basic tasks due to his  hands

Kaleem's father Shamim, 45, (pictured together above) is worried his son will never become independent

Kaleem, from India, was born with hands twice the size of an average baby and they have continued to grow

Mtoto wa miaka minne nchini India, Kaleem (pichani) amewachanganya madaktari kufuatia mikono yake kuvimba kupita kiasi na sasa imefikia uzito wa kilo 12. Mtoto huyo kwa sasa anashindwa kutekeleza japo majukumu madogo tu kama kufunga 'kamba' (laces) za viatu vyake baada ya kuzaliwa akiwa na mikono mikubwa mno.

Kaleem anadai amekuwa akibughudhiwa mno na watoto wenzie wanaomcheka kutokana na maumbile hayo ya ajabu. "Napata mguu kuvaa nguo zangu, kufunga vifungo hata kuvaa nguo ya ndani, anasema mtoto huyo ambaye mama yake alibaini maradhi yake tangu akiwa mdogo lakini hakuwa na cha kufanya kutokana na kutokuwa na uwezo wa kifedha. Wazazi wa Kaleem wana kipato kisichozidi Paundi za Kiingereza 15 (takriban Tsh 42,000) kwa mwezi.

Baba yake, Shamim, anahofu mwanae hatoweza kujitegemea maishani, na anajilaumu kwa kushindwa kumhudumia kutokana na uwezo duni wa kifedha. Dr Ratani, mkurugenzi wa kituo cha afya kilichomfanyia uchunguzi mtoto huyo anakiri kuwa maradhi hayo ni ya ajabu na magumu kutibika. 

CHANZO: The Mail Online



 Only men who suffered impotence as a side effect of illness or those evaluated by a specialist could be given the pills on the NHS
Mamia kwa maelfu ya wanaume hapa Uingereza wanatarajiwa kunufaika na uamuzi wa Taasisi ya Huduma za Afya (NHS) kulegeza masharti ya upatikanaji wa vidonge vya kuboresha nguvu za kiume, Viagra.

Hadi mwezi huu, watu pekee walioruhusiwa kupewa Viagra hospitalini ni wale ambao pungufu wa nguvu zao za kiume ulitokana na athari za matibabu ya maradhi mengine (side effects).

Lakini tangu taratibu za usajili na upatikanaji (patent) ya Viagra ilipoisha muda wake mwaka jana, bei ya vidonge hivyo imeshuka kwa asilimia 93 kwa vile makampuni mengine ya madawa yameruhusiwa kutengeneza aina zisizo asili (generic) za vidonge hivyo.

Kutokana na hali hiyo, NHS imeeleza kuwa watu wote wenye matatizo ya nguvu za kiume wanaruhusiwa kupata Viagra. Madaktari wengi wamefurahishwa na uamuzi huo wakiamini kuwa utasaidia kuboresha mahusiano ya kinyumba na hata kuokoa ndoa.

Hadi 'patent' ya Viagra inakwisha muda wake, Viagra ilikuwa ikiuzwa kwa Paundi za Kiingereza 21.27 (Tsh 58,567.39) kwa pakti ya vidonge vinne lakini bei hiyo sasa imeshuka hadi Paundi .1.45 (Tsh 3,992.61)kwa pakti moja ya vidonge vinne.



22 Aug 2014

Ijumaa ya leo imekuwa siku ngumu sana kwangu. Rafiki yangu mmoja wa karibu, mhamiaji kutoka Ireland ya Kaskazini aliyehamia hapa Uskochi, anajiandaa kwa ajili ya upasuaji wa moyo hapo Jumatatu. Leo tumeonana 'kwa mara ya mwisho' kwa vile atatumia wikiendi hii kujaindaa na upasuaji huo, na wiki Ijayo ndo shughuli yenyewe.

Nimepata wakati mgumu sana kuagana nae jioni hii wakati anaelekea nyumbani kwake nami narudi kwangu. Japo aliniaga kwa kujiamini kuwa tutaonana Jummatano ijayo, lakini hali ya uoga iligubika ujasiri wake, na kwa hakika almanusra niangushe chozi. 

Huyu bwana alipatwa na mshtuko wa moyo miezi kadhaa iliyopita. Naikumbuka vema siku hiyo. Tulipokutana asubuhi baada ya kuwasili kazini alionekana anatoka jasho japo siku hiyo ilikuwa ya baridi kali. Muda mfupi baadae alionekana anapumua kama mtu aliyekimbia umbali mrefu, na muda mfupi baadaye akaanguka na kupoteza fahamu. Tuliita gari ya kuhumia wagonjwa, na akakimbizwa hospitalini haraka. Kwa mujibu wa maelezo yake mwenyewe, alikuwa kama amekufa kwa masaa kadhaa. Lakini kubwa lililosaidia kuokoa uhai wake ni huduma ya kwanza tuliyompatia wakati tunasubiri gari la wagonjwa, vinginevyo moyo wake ungezimika moja kwa moja.

Alikaa hospitalini kwa wiki kadhaa na huko walimwekea mashine inayousaidia moyo wake kufanya kazi zake kwa ufanisi. 

Sasa upasuaji atakaofanyiwa Jumatatu ijayo ni kwa ajili ya uchunguzi mkubwa wa jinsi mashine hiyo inavyofanya kazi.Ikumbukwe kuwa mashine hiyo inafanya kazi kuusaidia moyo, na kwahiyo moyo wake bado unafanya kazi japo ni kwa msaada wa mashine hiyo iliyowekwa juu kidogo ya moyo wake, kifuani.

Kitakachofanyika Jumatatu ni kilekile walichomfanyia wakati wanaweka mashine hiyo, yaani watatumia kompyuta kufanya kazi ya moyo, na kisha kuusimamisha moyo, na kwa wakati huo uhai wake utakuwa unategemea kompyuta hiyo. Wataitoa mashine waliomwekea mwilini na kuisafisha, sambamba na kuichunguza. Kadhalika, moyo wake nao utafanyiwa uchunguzi wa kina. Yote hayo yatatokea wakati uhai wake unategemea kompyuta inayofanya kazi ya moyo.

Japo upasuaji huo haumaanishi kifo lakini kuna uwezekano-japo si mkubwa- wa moyo kurejeshwa mwilini na ukagoma kufanya kazi kama awali. Kadhalika, ile mashine inayousaidia moyo nayo inaweza kugoma 'kuwajibika ipasavyo.' Lakini cha kutisha ni ukweli kwamba wakati upasuaji huo unafanyika, rafiki yangu huyo atakuwa kama amekufa- kwa maana ya kazi zinazofanywa na moyo wa asili kutegemea msaada wa kitu cha nje- in this case ni hiyo kompyuta. Yaani kwa lugha nyingine ni kama mtu anayepumulia mashine, ikizimwa, yaweza kuwa ndio mwisho wa uhai wake.

Wakati tunaondoka eneo la kazi, rafiki yangu huyo alisema waziwazi kuwa muda huo ndo unaweza kuwa wa mwisho kwa yeye kuwepo hapo. Japo aliongea kwa utani lakini uwezekano huo upo japo si mkubwa. Teknolojia ya matibabu ya moyo imepiga hatua kubwa sana lakini si ya uhakika wa asilimia 100.

Kwangu, nabaki kumfanyia sala, upasuaji huo ufanyie salama, na tukutane tena Jumatano kama alivyoahidi mwenyewe. Nina imani na teknolojia ya matibabu ya hawa wenzetu lakini ukweli kwamba kiungo muhimu kama moyo kitasimamishwa na kazi yake kufanywa na kompyuta inanipa msisimko wa uoga. Na hilo limeonekana hata kwa 'mgonjwa' mweyewe.'

I thought si vibaya ku-share stori hii ya kuogofya ambayo inanigusa kwa kiasi kikubwa. Kwa nman flani yanikumbusha jinsi nilivyompoteza mama yangu mpendwa, ambaye nae kama ilivyo huyo rafiki yangu alipatwa na mshtuko wa moyo, akapoteza fahamu, na fahamu hazikumrejea tena hadi anafariki Mei 29, 2008.

Natumaini msomaji mpendwa utaungana nami kumwombea rafiki yangu huyo upasuaji atakaofanyiwa uwe wa mafanikio na aendelee kuishi salama. Nitawafahamisha kilichojiri Jumatano ijayo.

Asanteni

15 Aug 2014

Within 30 years, a futurist believes babies will regularly born in artificial wombs, outside of human bodies. Stock image pictured
Wanasayansi wanataraji kwamba ndani ya miaka 30 ijayo, itawezekana kutengeneza na kutunza ujauzito nje ya tumbo la mama. Teknolojia hiyo inayofahamika kama ectogenesis imekuwa ikifanyiwa kazi katika maabara tangu mwaka 200, na majaribio ya awali yalikuwa ya kutengeneza na kutunza mimba ya panya nje ya tumbo la panya ' wa kike.'

Wakati wanaounga mkono teknolojia hiyo wanadai itapunguza vifo vya watoto wakiwa tumboni kwani itarahisisha kufanya uangalizi na ufuatiliaji, wapinzani wake wanadai kuwa itaingilia utaratibu wa asili wa uzazi. Wengine wanadai kuwa hatua hiyo itaondoa hatua muhimu ya mahusiano kati ya mama na mtoto tangu akiwa tumboni.

Ectogenesis ni makuzi ya kiumbe kichanga (organism) nje ya mwili, na inatokea kwa baadhi ya wanyama na bakteria. Katika kutengeneza na kutunza mtoto nje ya tumbo la mimba, mfuko 'feki' wa uzazi wahitaji 'mrija feki wa uzazi ' (fake uterus) ili kukipatia kiumbe lishe na hewa ya oksijeni. Pia mipira maalum itahitajika ili kuwezesha kiumbe kichanga 'kujisaidia' (kutoa uchafu mwilini). Chupa inayohifadhi 'mimb' itaunganishwa na mitambo itakayofuatilia makuzi ya 'kichanga' na mimba kwa ujumla.

Kwa taarifa kamili BONYEZA HAPA

CHANZO: Daily Mail



 Kunywa maji ya kutosha 

  1. Increase Your Ejaculate Step 1 Version 2.jpg


  1. Epuka joto kwa sehemu zako za siri
    Increase Your Ejaculate Step 2 Version 2.jpg

  2. ee
  3. Epuka 'nguo za ndani' za kubana
    Increase Your Ejaculate Step 3 Version 2.jpg


  4. Epuka 'kupinda nne'
    Increase Your Ejaculate Step 4 Version 2.jpg

    .


  5. Punguza tendo la ndoa kwa muda ile kurejesha mbegu za kiume 'zilizopotea'
    Increase Your Ejaculate Step 5 Version 2.jpg
    Add caption
  1. Tumia vitamini vya Zinc na Folic Acid
    Increase Your Ejaculate Step 6.jpg


  2. Punguza kunywa soda
    Increase Your Ejaculate Step 7.jpg


  3.  Meza vitamini vya Amino Acid vya aina hizi: L-Arginine, L-Lysine na L-Carnitin Increase Your Ejaculate Step 8.jpg

  4. Jaribu 'vidonge vya asili' viitavyo Horny Goat Weed
    Increase Your Ejaculate Step 9.jpg


  5. Kula matunda na mbogamboga (hasa maharage mekundu, maji ya nazi, apples, wild blueberries, blackberry, cranberry)
    Increase Your Ejaculate Step 10.jpg


    Chua misuli ya 'sehemu yako ya siri' pasipo kufikia 'kileleni'

    1. Increase Your Ejaculate Step 11.jpg

    2. Punguza na hatimaye acha kuvuta sigara (na bangi ni adui mkubwa wa mbegu za kiume)
      Increase Your Ejaculate Step 12.jpg

      • Punguza msongo wa mawazo (stress)
        Increase Your Ejaculate Step 13.jpg

        • Fanya mazoezi mara kwa mara
          Increase Your Ejaculate Step 14.jpg

        • Zingatia ngono salama (maradhi ya zinaa yanaathiri vibaya uzalishaji mbegu za kiume)
          Increase Your Ejaculate Step 15.jpg

          CHANZO: WikiHow

        6 Oct 2013

        Kuanzia sasa , blogu hii itakuwa ikiwaletea makala muhimu za mtaalam wa afya, Dokta Joachim Mabula. Makala hizo pia hupatikana katika tovuti ya Fikra Pevu, na unaweza kufuatilia mada mbalimbali kutoka kwa Dkt Mabula kwa kum-follow huko Twitter, ambapo anatumia handle @DrMabula au Google+ +Joachim Mabula au Facebook https://www.facebook.com/DrMabula

        Makala yake ya leo inazungumzia ugonjwa wa saratani ya matiti (breast cancer): chanzo, dalili na matibabu. Ungana nae hapa chini


        Kansa ya matiti ni aina ya kansa inayojitokeza toka tishu za matiti hasa mirija myembamba inayopitisha maziwa. Ugonjwa huu (Saratani ya matiti) hutokea kwa binadamu na mamalia wengine. Idadi ya wanaume wanaopatwa na kansa ya matiti ni ndogo sana ikilinganishwa na ya wanawake. 
        Ulimwenguni pote, kansa ya matiti hubeba asilimia 29 nukta tisa ya kansa zote kwa wanawake. 
        Licha ya maendeleo ya kitiba, bado kansa ya matiti ndiyo kansa inayosababisha vifo vingi zaidi vya wanawake. 
        Nchi zilizoendelea za Amerika Kaskazini na Ulaya Magharibi ndizo zenye idadi kubwa zaidi ya watu walio na kansa, lakini idadi ya wanawake walio na kansa ya matiti inaongezeka katika bara la Asia na Afrika ambako kwa kawaida kumekuwa na idadi ndogo kiukweli. 
        Idadi ya wanaokufa kati ya wale wanaogundulika kuwa na ugonjwa huo huko Asia na Afrika ni ya juu kwasababu kansa hiyo haigunduliwi mapema. Wagonjwa wengi huja ikiwa tayari imeenea sana. 
        Kansa ya matiti huanza wakati ambapo chembe moja inajigawanya haraka sana isivyo kawaida na bila utaratibu, na hatua kwa hatua inafanyiza uvimbe. 
        Uvimbe unakuwa kansa wakati chembe zake zinapovamia tishu nyingine. Uvimbe fulani unaweza kuchukua miaka kumi hivi kabla ya kugunduliwa. 
        VIHATARISHI/VISABABISHI

        Hatari ya kupatwa na kansa hiyo huongezeka dadiri umri unavyosonga. Asilimia 80 hivi ya wanawake wenye kansa ya matiti wana umri unaozidi miaka 50. 
        Lakini jambo linalofariji ni kwamba kansa ya matiti ni mojawapo ya kansa zinazoweza kutibiwa kwa urahisi. 
        Watakao tibiwa kabla ya kansa hiyo kuenea wanaweza kuishi muda mrefu kwa ukawaida. 
        Visababishi vya kansa ya matiti bado ni fumbo. 
        Baadhi ya wanasayansi wanaamini kwamba kansa ya matiti hutokana na hatua nyingi tata ambazo huanza wakati ambapo chembe fulani ya urithi yenye kasoro inapofanya chembe zitende kwa njia isiyo ya kawaida, yaani, zigawanyike kwa kasi sana, zishambulie tishu nyingine na kuepuka kuharibiwa na mfumo wa kinga, kisha pole pole chembe hizo zinashambulia na kuharibu viungo muhimu vya mwili. 
        Jambo lingine linalohusishwa na kansa ya matiti ni homoni ya estrojeni ambayo huenda inachochea aina fulani za kansa hiyo. 
        Kwa hiyo, mwanamke anaweza kupatwa na kansa hiyo ikiwa alianza kupata hedhi mapema maishani au ikiwa aliacha kupata hedhi akiwa amechelewa isivyo kawaida, ikiwa alipata mimba ya kwanza umri wake ukiwa umesonga au ikiwa hakuwahi kupata mimba, au ikiwa alipata matibabu ya kurudisha homoni fulani mwilini. 
        Kwa kuwa chembe za mafuta hutokeza estrojeni, huenda wanawake walionenepa kupita kiasi waliofika umri wa kuacha kupata hedhi na hivyo ovari zao hazitokezi tena homoni, wakawa katika hatari ya kupatwa na kansa hiyo. 
        Pia watu walio na viwango vya juu vya insulini na watu walio na viwango vya chini vya homoni ya usingizi inayoitwa melatonia kama vile watu wanaofanya kazi usiku, wako pia katika hatari ya kupatwa na kansa hiyo. 
        Uvutaji wa tumbaku umeonekana kuongeza hatari zaidi ya kupata saratani ya matiti, kiwango kikubwa cha tumbaku iliyovutwa na kuanza kuvuta tumbaku katika umri mdogo hufanya hatari kuongezeka zaidi. 
        Mionzi na kemikali za viwandani huongeza hatari ya kansa ya matiti. Kemikali kama polychlorinated biphenyls, polycyclic aromatic hydrocarbons na dawa za kuulia wadudu huchangia kutokea saratani hiyo. 
        DALILI

        - Uvimbe wowote au kuongezeka kwa unene wa ngozi kwenye makwapa au titi. 
        - Umajimaji wowote unaotoka kwenye chuchu ambao si maziwa. 
        - Mabadiriko yoyote ya rangi au ngozi ya titi. 
        - Chuchu iliyodidimia kwa njia isiyo ya kawaida au inayowasha. 
        UCHUNGUZI KUJUA KAMA NI KANSA

        Ili kuchunguza ikiwa uvimbe una kansa sindano nyembamba hutumiwa kutoa tishu kutoka kwenye uvimbe huo na kufanyiwa uchunguzi. 
        MATIBABU

        Uvimbe ukiwa na kansa hufanyiwa upasuaji ili kuondoa uvimbe huo na tishu zinazozunguka titi. Upasuaji husaidia kuonyesha uvimbe ulipofikia (ukubwa, aina na kuenea kwake) na kuchunguza uvimbe unakua upesi kadiri gani. 
        Chembe zenye kansa zinaweza kutoka kwenye uvimbe na kusafiri kupitia mfumo wa damu au mfumo wa limfu na kuanza kukua tena mahali pengine mwilini. 
        Kuenea kwa kansa hadi kwenye viungo na tishu muhimu kama vile ubongo, ini, uboho wa mfupa au mapafu ndio hufanya ugonjwa huo uwe hatari. 
        Hivyo baada ya upasuaji, wagonjwa wengi hupata matibabu mengine ambayo yatazuia kansa isirudi na kuenea. 
        Kwasababu ya maendeleo katika matibabu ya kansa ya matiti, kumekuwa na matibabu mbalimbali ikitegemea umri, afya historia ya kansa katika familia, na aina ya kansa. 
        Wanasayansi wanajifunza mambo mengine kuhusu kansa kutia ndani kuelewa ni kwa nini kansa huenea, kudhibiti chembe za kansa ambazo haziharibiwi kupitia matibabu ya kemikali, kuzuia kugawanyika kwa chembe na kutibu kila uvimbe kwa njia hususa.


        ABOUT THE AUTHOR: 
        Clinician | Programme Officer & Social Media Manager (Cvs-Tanzania) | Bussinessman
        - See more at: http://www.fikrapevu.com/saratani-ya-matiti-breast-cancer-chanzo-dalili-na-matibabu-yake/#sthash.vAwVieVu.dpuf



        27 Jan 2009

        Kujichua,punyeto,puli,nk.Majina ni mengi kuhusu tendo hili ambalo inaaminika kuwa "faraja binafsi miongoni mwa wapweke wengi" japo huzungumziwa hadharani kwa nadra mno.Sasa wanasayansi wanadai kwamba kujichua (masturbation) kunaweza kuwa kinga dhidi ya kansa ya kibofu (prostate cancer) kwa walio na umri wa miaka 50 na zaidi.Jenga picha...unamkuta mzee wa miaka hamsini na kadhaa "anapata kinga na sabuni yake mkononi..."Au inagundulika kwamba kisa cha kila Revola inayoachwa bafuni kupotea kimiujiza ni baba mwenye nyumba "kuitumia kama kinga ya kansa"....Enewei,BONYEZA HAPA kusoma habari kamili.


        Lakini wakati nyeto inaelekea kuwa habari njema kwa wazee,wanasayansi wanadai kwamba "ngono binafsi" kwa vijana wenye kati ya miaka 20-30 inaweza kupelekea kansa hiyohiyo ya kibofu.

        Categories

        Blog Archive

        © Evarist Chahali 2006-2022

        Search Engine Optimization SEO

        Powered by Blogger.