Showing posts with label AJALI TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label AJALI TANZANIA. Show all posts

29 Apr 2015

Inasikitisha, inaumiza, inashangaza, na inaacha maswali mengi kuliko majibu kila tunaposikia “ajali yauwa...ajali yajeruhi...” Ndio, matukio ya ajali huko nyumbani yamekuwa kama jambo la kawaida kutokana na mfululizo wake, lakini hali ilivyo sasa ni ya kutisha.
Huko nyuma niliandika takriban makala mbili kuhusu suala hili la ajali, sio tu kwa vile tukio lolote linalopelekea kupotea kwa uhai wa wenzetu linaumiza nafsi bali pia kutokana na ukweli kwamba kwa hapa Uingereza ajali ndogo tu ni tukio linalokamata hisia za takriban nchi nzima, kinyume na ilivyozoeleka huko nyumbani.

Wakati ajali zinaendelea kuteketeza maisha ya Watanzania wenzetu, angalau kwa mara ya kwanza Taifa linaonekana kuguswa, na tayari zimeanza harakati za uhamasishaji dhidi ya ajali katika mitandao mbalimbali ya kijamii. Hata hivyo, ukweli mchungu unabaki kuwa ajali bado zinaonekana kama matukio ya kawaida tu.
Sijui lini taifa limeonyesha kuguswa na vifo vilivyotokana na ajali kiasi cha angalau bendera kupepea nusu mlingoti. Sijui sababu ni kwamba ajali zimezoeleka mno, au kwa vile ‘ajali haina kinga,’ au kwa sababu wahanga wengi wa ajali za barabarani ni ‘watu wa kawaida.’
Kabla sijaanza kuandika makala hii nilisoma habari kuhusu vurugu zilizotokea huko Korea ya Kusini katika maadhimisho ya mwaka mmoja tangu itokee ajali mbaya ya feri iliyosababisha vifo takriban 300. Hakuna anayefahamu kinachojiri baada ya kifo, lakini yayumkinika kuamini kuwa marehemu wasingependa kukumbukwa kwa vurugu. Lakini vurugu zilizotokea huko Korea ya Kusini ni ishara ya wananchi kukerwa na jinsi serikali yao ilivyoshughulikia janga hilo, hata kama haikuisababisha.
Hapa simaanishi kwamba Watanzania nao waingie mtaani na kufanya vurugu kuisukuma serikali ichukue hatua stahili dhidi ya ajali. Hata hivyo, ni muhimu angalau kuiamsha serikali kwa kuifahamisha kuwa hatuwezi kuangalia tu maisha ya Watanzania yakiteketea kama hayana thamani kutokana na mfululizo wa ajali. Busara kwamba ‘ajali haina kinga’ hai-apply katika nyingi ya ajali zinazotokea huko nyumbani.
Kwa mtizamo wangu, chanzo kikubwa cha ajali ni rushwa. Rushwa inayowezesha madereva wasio na sifa kuwa barabarani huku wakihatarisha uhai wa abiria wao. Rushwa inayoruhusu magari mabovu yabebe abiria na kuweka rehani uhai wa abiria. Rushwa inayofumbia macho makosa ya madereva barabarani na hivyo kuwapa imani kuwa hakuna kitu kiitwacho ‘kosa kinyume cha sheria za usalama barabarani’ alimradi dereva ana uwezo wa ‘kumpoza’ askari wa usalama barabarani.
Wanasema ‘rushwa huuwa.’ Na katika janga hili la mfululizo wa ajali, rushwa inauwa kweli kweli, na inaendelea kugharimu maisha ya Watanzania wenzetu kila kukicha.
Rushwa imekuwa sehemu ya maisha ya kawaida ya Mtanzania, na sintoshangaa iwapo baadhi ya wasomaji ‘wataniona mtu wa ajabu’ kwa kuhitimisha kuwa rushwa ni chanzo kikuu cha ajali huko nyumbani. Kwa wengi, rushwa ni tukio la muda mfupi tu linalorahisisha au kuwezesha upatikanaji wa huduma au bidhaa. Hata hivyo, ukweli mchungu ni kwamba rushwa ni kama kansa, inaitafuna jamii taratibu, na siku ya siku, madhara yake makubwa hujitokeza hadharani.
Mfano mmoja kuhusu athari za rushwa ni suala la ugaidi nchini Kenya. Wachambuzi wa masuala ya usalama wanahitimisha kuwa kwa kiasi kikubwa tu, rushwa katika vyombo vya dola nchini Kenya imewarahisishia magaidi wa Al-Shabaab kutimiza malengo yao kuishambulia nchi hiyo.
Kwa huko nyumbani tumeshuhudia matatizo mengine ya kijamii yanavyorutubishwa na rushwa. Mfano rahisi ni kushamiri kwa biashara ya madawa ya kulevya. Tanzania yetu sasa ni miongoni mwa vituo vikuu vya biashara hiyo duniani, na kilichotufikisha katika nafasi hiyo isiyopendeza hata kidogo ni urahisi wa kuingiza na kutoa madawa ya kulevya nchini mwetu. Niwe mkweli, kila ninaposikia polisi wamekamata kiasi fulani cha madawa ya kulevya, hisia yangu ya kwanza ni madawa hayo yaliyokamatwa yataishia kumnufaisha mtendaji fulani wa taasisi zenye wajibu wa kuyadhibiti.
Takriban kila dereva na abiria anafahamu jinsi askari wa usalama barabarani walivyogeuza rushwa kuwa haki yao. Kibaya zaidi, madereva wengi nao wamejenga fikra kuwa kutoa rushwa kwa askari wa usalama barabarani ni wajibu wao. Hili ni janga: rushwa kama haki wa wapokeaji na wajibu kwa watoaji.
Wakati mmoja nikiwa safarini huko nyumbani, basi nililopanda lilisimamishwa na askari wa usalama barabarani, na baada ya dakika kadhaa, baadhi ya abiria walisikika wakimhasisha dereva ‘amalizane na trafiki’ (ampe rushwa) ili safari iendelee. Hivi ndivyo rushwa ilivyoota mizizi katika Tanzania yetu.
Kwa upande mwingine, janga la ajali kuonekana kama jambo la kawaida tu ni mwendelezo wa kasumba inayolikwamisha mno taifa letu: kuzowea matatizo. Angalia tatizo la mgao wa umeme lilivyodumu miaka nenda miaka rudi pasipo Watanzania kutumia nguvu ya umma kuilazimisha serikali na Tanesco yake imalize tatizo hilo. Mgao wa umeme umekuwa stahili ya Watanzania, na kikubwa wanachoweza kufanya ni kuitukana Tanesco matusi yasiyoandikika hapa, kana kwamba matusi hayo yatamaliza tatizo hilo la miaka nenda miaka rudi.
Kwenye sekta ya huduma, hali ni hivyohivyo. Ukifuatilia kwenye mitandao ya jamii, idadi ya matusi yanayoelekezwa kwa makampuni ya huduma mbalimbali, kwa mfano makampuni ya simu, ni kubwa na inakua kila siku, lakini ‘mashujaa hao wa matusi’ hawataki kabisa kujifunza kuwa matusi yao hayabadili chochote, na ndio maana kila kukicha inawalazimu waje na matusi mapya kama si kuyarudia yale ya zamani.
Lakini kwa hali ilivyo sasa kuhusu janga la ajali, ‘usugu’ huo wa kuyazowea matatizo inabidi ifikie kikomo. Taifa lolote linalojali mustakabali wake lazima liamke inapofikia hatua ya watu 969 kupoteza maisha kutokana na ajali katika kipindi cha takriban miezi mitatu tu. Naam, tangu mwaka huu uanze, tumepoteza wenzetu takriban 300 kila mwezi kutokana na ajali, kwa mujibu wa takwimu zilizopatikana wiki iliyopita.
Katika sehemu kubwa ya makala hii nimezungumzia rushwa kama chanzo kikuu cha janga la ajali. Hata hivyo, kwa mtizamo wangu, kingine kinachochangia baadhi ya ajali ni ‘uzembe’ wa wengi wa abiria: kukaa kimya pale madereva wanapohatarisha maisha ya abiria kwa uendeshaji usiozingatia sheria za usalama barabarani. Na pengine cha kukera zaidi ni tabia iliyojengeka miongoni mwa abiria wengi kuwasifia madereva wanaodhani ni kosa la jinai kuendesha motokaa taratibu hata kwenye eneo hatari.
Inasikitisha na kuchukiza kusikia abiria wakimshangilia dereva anayeendesha basi kwa kasi au ku-overtake gari jingine pasi kuona kama kuna gari jingine linakuja kwa mbele au la. Dereva anayeshangiliwa kwa uendeshaji gari wa hatari anajenga imani kwamba huo ndio udereva stahili, vinginevyo abiria wangemkemea.
Ifike mahali Watanzania tuache kukubali kilicho pungufu (not settling for less). Ukinunua tiketi kwa ajili ya safari umenunua pia haki na stahili zako ambazo kamwe hupaswi kumruhusu dereva azichezee. Ni wazi kuwa umoja na mshikamano wa abiria kukemea madereva wanaokiuka sheria za usalama barabarani unaweza kusaidia kupunguza baadhi ya ajali zinazoepukika.
Nimalizie makala hii kwa kutoa salamu zangu za rambirambi kwa ndugu na jamaa wa Watanzania wenzetu waliopoteza maisha katika ajali mfululizo.
Pia ninaomba kufikisha ujumbe huu kwa askari wa usalama barabarani: kila shilingi mnayodai kama rushwa ili kufumbia macho ukiukwaji wa sheria za barabarani inachangia ajali na vifo vya Watanzania wenzetu. Mikono ya kila askari aliyepokea rushwa na kisha gari husika likapata ajali ina damu ya waliokufa katika ajali husika.
Kadhalika, ninatoa wito kwa madereva, hususan wa magari ya abiria, kuthamini uhai wa abiria wao, kwa kuepusha ushindani hatari barabarani, mwendo kasi na kuheshimu sheria za usalama barabarani.
Lakini kubwa zaidi kwa Watanzania wote ni kupambana na kansa hii ya rushwa ambayo sasa inalitafuna taifa kwa kuchangia ajali hizi mfululizo, kama inavyosababisha madhara mengine makubwa katika nyanja mbalimbali za maisha.

ANGALIZO: Makala hii ilichapishwa katika toleo la tarehe 22.04.15 lakini iliwekwa mtandaoni juzi. Samahani kwa kuchelewesha kui-post.


29 Apr 2010

JIJI la Tanga limfeunikwa na simamzi kuu kufatia wanafunzi 18 wa Chuo cha Kiislamu cha Shamsil-Maariff kufa papo hapo na wengine 125 kujeruhiwa vibaya, baada ya lori walilokuwa wakisafiria kutoka kwenye sherehe za maulidi kupinduka.

. Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Adolphina Kapufi aliliambia gazeti hli jana kuwa ajali hiyo ilitokea saa 5:30 usiku wa kuamkia jana katika eneo la njiapanda kuu ya Mabanda ya Papa jijini hapa.

Kapufi aliwataja baadhi ya waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni Twalib Kunemu, Juma Idd, Faraji Habib, Jahshi Rashid, Hussein Bakari, Hajji Athumani naYussuph Hussein na kwamba, kazi ya kuwatambua maiti wengine bado inaendelea.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Paschal Kanyinyi alisema kazi ya kuwatambua waliokufa na majeruhi waliolazwa katika hospitali hiyo wodi ya Galanosi inaendelea.

Kanyinyi aliwataja majeruhi waliotambuliwa kuwa ni Jumaa Salim ambaye ameumia mbavu, Makame Ahmed, Ahmed Shehe, Selemani Said na Juma Akida.

Aliwataja majeruhi ambao hali zao ni mbaya, hivyo waliokimbizwa katika Hospitali Taifa ya Muhimbili, jijini Dar essalaam kuwa ni Hemed Shaaban na Hassan Adam.

Kanyinyi alifahamisha kuwa kati majeruhi 125 walifikishwa katika hospitali hiyo usiku wa kuamkia jana baada ya kupata ajali, 70 walipata matibabu na kuruhusiwa kurejea chuoni kwao.

Kwa mujibu wa Kaimu Mganga Mkuu huyo, majeruhi 55 wanaendelea kupata matibabu katika hospitali hiyo kwa msaada wa timu maalumu ya waganga na wauguzi waliokusanywa kutoka hospitali na vituo mbalimbali vya afya mkoani Tanga kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.

Mwananchi ilifika katika Hospitali hiyo ya Bombo na kukuta idadi kubwa ya wananchi waliokusanyika katika hospitali hiyo kwa lengo la kutambua miili ya waliokufa na majeruhi.

Mwalimu wa zamu wa Chuo hicho, Ustaadh Ajali Ramadhan, alisema kuwa wanafunzi hao walikuwa wakitokea Kijiji cha Kibafuta ambako walikwenda
kuhudhuria sherehe za kuzaliwa kwa Mtume Mohamad S.A.W.

Hata hivyo, Ustaadhi Ramadhan alisema anashangaa kuona idadi kubwa ya wanafunzi waliopata ajali, kwani aliowaruhusu kutoka chuoni hapo walikuwa 60 tu.

“Nashangaa sijui ni nini kimetokea, kwani niliowaruhusu kuondoka na gari
hilo ni wanachuo 60 tu, lakini idadi ya waliopata ajali imekuwa kubwa. Sijui walipandia wapi…,” alisema mwalimu huyo wa zamu.

Kanyinyi alimshukuru Mkurugenzi wa Kampuni ya Raha Leo, Seleman Abdallah kwa kutoa dawa kwa ajili ya kuwatibu majeruhi wa ajali hiyo.

“Tunashukuru Mkurugenzi wa Raha leo, ametusaidia sana kwa kutoa dawa za
kuwatibu majeruhi na pia vifaa kwa ajili ya kusaidia kuhifadhia miili ya waliokufa,” alisema Kanyinyi.

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Meja Jenerali Mstaafu Said Kalembo alifika hospitalini hapo saa 5 .30 asubuhi na kuwapa pole ndugu wa wanafunzi waliokufa katika ajali hiyo.

Akiwa, akiwa katika wodi ya Galanosi Mkuu wa Mkoa huyo alimuagiza Kaimu Mganga Mkuu kuwaita waganga na wauguzi kutoka vituo vyote vya afya vya jijini hapa ili kuongeza nguvu, kwa vile waliopo katika Hospitali ya Bombo walikuwa wmezidiwa na kazi ya kuwahudumia majeruhi.

Katibu wa Bakwata wa Mkoa wa Tanga, Mohamed Riami alisema huo ni msiba
mkubwa uliwakumba Waislamu na Watanzania kwa ujumla, hivyo akaomba msaada wa hali na mali kuokoa maisha ya majeruhi waliopata ajali hiyo.

Ajali hii ni muendelezo wa ajali mbaya za barabarani zinazoendelea kutokea na kuua watu sehemu mbalimbali nchini hivi sasa.

Moja ya ajali hizo mbaya ni iliyotokea jijini Dar es Salaam mwezi uliopita na kuua watu zaidi ya 10 papo hapo baada ya lori la mafuta ya taa kuigonga na kulalia daladala maneo ya Kibamba katika Barabara ya Morogoro.

Katika ajali hiyo iliyotokea alfajiri, daladala ilisagawa na kuwa kama chapati; na miongoni mwa waliokufa ni mama mjazito aliyekuwa anakwenda kujifungua hospitalini akiwa pamoja na mumewe.

CHANZO: Mwananchi
.

21 Oct 2008

Albino Girl Killed For Witchcraft
Tuesday, October 21 02:52 pm
Sky News
A gang murdered and mutilated a 10-year-old albino girl in Tanzania - because they wanted to sell her body parts to witch doctors. Skip related content

Esther Charles was killed in Shilela in the western region of the African country on Sunday.

She died just hours after President Jakaya Kikwete called for a crackdown on gangs, saying the killing of albinos has "stained the country's good image".

At least 26 other albinos, mostly women and children, have been killed in different parts of the east African country over the past year.

Albinos lack melanin pigment in the skin, eyes and hair, which protects from the sun's ultraviolet rays.

But witch doctors believe they have magical powers to bring fortune, and discrimination against albinos is rife across sub-Saharan Africa.

In 2007, police in Tanzania reported several cases of people digging up the bodies of children to remove organs, in many cases the genitals and eyes, to make potions used in rituals.

Shilela councillor Joseph Manyara told a rally organised by the Tanzania Albino Society (TAS): "It is utterly stupid for some people to believe that albinos have magic powers and their parts can make them rich.

"People should be provided with education to understand that it is only through hard working that they can prosper in life and not through selling albinos' body parts."

Police said they have arrested 47 people suspected to be involved in the killings this year.

But TAS chairman Ernest Kimaya blasted authorities over the speed at which the murders were solved.

He said: "We are yet to witness any convictions and incidents of the murder of albinos are on the rise."

There are about 150,000 albinos in the country, and more than 8,000 of them are registered with the TAS.

Some families kill albino babies upon birth, Tanzanian authorities say.

And authorities in Kenya and Burundi, where albino killings have also been reported in recent months, have started to give added protection.

Some reports say albino skin is prized in the Democratic Republic of Congo, another troubled African nation where superstition is high.

SOURCE: Sky News

5 Oct 2008


JAJI Kiongozi, Salum Massati, amesema kuanzia sasa madereva watakaosababisha vifo katika ajali za barabarani watanyang’anywa leseni na hata kufungwa miaka miwili jela ili kupunguza matukio hayo.

Akizungumza mjini hapa, Jaji Massati alisema ili kufanikisha mkakati huo, Mahakama ya Tanzania imewaagiza mahakimu wake kutafsiri vizuri na kwa usahihi sheria ya makosa ya barabarani ili kuwabana madereva wazembe. 

Agizo hilo lilitolewa alipokuwa akizungumza na watumishi wa mahakama hiyo Kanda ya Iringa. 

Alisema kwa kipindi kirefu madereva wanaopatikana na hatia za kuua kutokana na makosa ya barabarani wamekuwa wakipata adhabu ndogo, jambo linalolalamikiwa kuchochea matukio ya ajali. 

“Hivi sasa mahakama zimebebeshwa mzigo huu wa lawama kana kwamba sisi ndio chanzo cha kuendelea kwa ajali nyingi barabarani kwa kuwa adhabu tunazotoa haziwiani na makosa yanayofanywa yakiwamo ya kusababisha vifo,” alisema. 

“Sheria inataka anayesababisha kifo kwa makosa ya barabarani ahukumiwe miaka miwili jela na anyang’anywe leseni yake, lakini mahakimu wetu hawatoi hukumu hiyo,” alisema. 

Alisema badala yake madereva wengi wanaokutwa na hatia za makosa hayo hupigwa faini ndogo na kuachiwa. 

Jaji Massati alisema mianya iliyopo katika sheria ya Usalama Barabarani imesababisha wakati mwingine dereva aliyesababisha ajali ambayo hata kama imeua watu 20 apigwe faini na kurudishiwa leseni yake. 

“Pale Kibaha, Pwani aliwahi kukamatwa dereva mwenye leseni feki aliyesababisha ajali na kuua, hata hivyo alipofikishwa mahakamani alihukumiwa kwa faini ya Sh 10,000 na kurudishiwa leseni yake. 

“Sidhani kama hukumu hiyo ilikuwa sahihi na inatoa fundisho kwa madereva wengine kuzingatia sheria zote za barabarani,” alitoa mfano.


Kwa mujibu wa sheria,kila mvunja sheria anapaswa kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria (kifungo ikiwa ni mojawapo ya adhabu hizo).Ajali za barabarani zinapoteza maisha ya Watanzania wenzetu kila kukicha,lakini ufisadi nao unaathiri (na pengine hata kupoteza) maisha ya mamilioni ya Watanzania kila dakika.Madereva wanaosababisha ajali na mafisadi wote ni wavunja sheria na wanapaswa kudhibitiwa kwa kuchukuliwa hatua kali ili,kwa upande mmoja,iwe fundisho kwa wengine,na kwa upande mwingine,wavunja sheria wavune wanachopanda.

Lakini pamoja na kuunga mkono mtazamo wa Jaji Kiongozi,nadhani kuna umuhimu wa kwenda mbali zaidi kuangalia vyanzo vya ajali mbali ya uzembe wa madereva.Tuchukulie madereva wa daladala kwa mfano.Mazingira yao ya kazi yanafanywa kuwa magumu na wamiliki wa daladala wenye uchu wa faida pasipo kujali sana mazingira ya kazi ya wanaowaletea faida hiyo.Na hapo tumewaweka kando askari trafiki wenye kudai rushwa waziwazi kana kwamba ni haki yao.

Hivi anayeamua kuweka chasis ya lori kwenye basi la abiria ni dereva au mmiliki wa basi hilo?Je linapopata ajali kutokana na mechanical corruption hiyo wa kulaumiwa ni dereva au mmiliki wa basi hilo?Na vipi kuhusu trafiki wanaokagua mabasi ya abiria?Au vipi kuhusu wiki ya usalama barabarani ambayo inaadhimishwa kila mwaka?Kwa mmiliki wa basi bovu kulikabidhi kwa dereva kwa ajili ya biashara inamaanisha kwamba ametoa baraka kwa lolote litakalotokea,ikiwa ni pamoja na ajali.Same could be concluded about mamlaka zinazoruhusu gari bovu kuwepo barabarani.

Hapa tunarudi kwenye tatizo lilelile la kila mara la kuangalia matokeo badala ya chanzo.Au kwa mtazamo mpana zaidi,kuhukumu vidagaa badala ya papa.Madereva wengi wa mabasi ya abiria wanalazimika kuyakubali mazingira magumu ya kazi hiyo sio kwa vile wanaipenda sana bali kutokana na tatizo zima la ajira huko nyumbani.Hakuna mtu mwenye akili timamu aliye tayari kuendesha "jeneza linalotembea" (a walking coffin),yaani magari ambayo yako barabarani kwa kudra za Mwenyezi Mungu pekee.

Sawa,madereva wanaosababisha ajali wanapaswa kuchukuliwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kifungo.Lakini pasipo kukomesha tatizo la kuwepo kwa magari mabovu barabarani,vifungo vitaendelea na ajali zitaendelea pia.By the way,kama vifungo pekee vingekuwa kizuizi cha kuvunja sheria,idadi ya wafungwa waliopo magerezani (na mazingira ya kutisha wanayoishi huko) ingetosha kukomesha uvunjifu wa sheria unaoweza kupelekea mtu kwenda gerezani.Pasipo kuangalia upande wa pili wa tatizo,yaani wamiliki wa vyombo vya usafiri wanaoweka mbele faida kuliko uhai wa abiria wao,na trafiki wanaothamini rushwa kuliko maisha ya Watanzania wenzao,basi ajali zitaendelea hata kama adhabu kwa kosa la kusababisha ajali itakuwa hukumu ya kifo.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.