Showing posts with label BLACK AMERICANS. Show all posts
Showing posts with label BLACK AMERICANS. Show all posts

19 Mar 2008

Makala yangu katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inajaribu kudadisi chanzo cha ufisadi huko nyumbani.Je tatizo ni mfumo unaozaa na kulea ufisadi au tatizo ni watu wanaosabaisha ufisadi na kuishia kutengeneza mfumo haramu wa maovu?Lakini kabla ya kuingia kwenye mjadala huo,makala hiyo imeanza kwa discussion fupi kuhusu kipindi cha BET cha Hip-Hop vs America.Binafsi,nimetafsiri dhima ya kipindi hicho kuwa ni jamii ya Black Americans kujiuliza adui yao halisi ni nani: wao wenyewe au mfumo dhalimu uliotawaliwa na ubaguzi na nguvu za Corporate America.Basi,pamoja na habari na makala nyingine zilizokwenda shule,bingirika na makala hiyo kwa KUBONYEZA HAPA.

27 Feb 2008

Makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inazungumzia UNAFIKI: Ule wa Profesa Mwandosya kuitaka Dawasco isiwataje hadharani mawaziri wanaodaiwa maji na Mamlaka hiyo;ule wa Askofu Thomas Laizer wa KKKT Dayosisi ya Arusha kutumia neno la Bwana kuwapiga vijembe wanamwandama Lowassa,na ule wa "mabilioni ya EPA yanayorejeshwa kwa kasi."Makala hiyo imeanza kwa stori za hapa na pale,mambo ya muziki wa kufokafoka na albamu ya Jay-Z ya American Gangster ilivyosahau matatizo ya Black Americans.Stori hizo ni zinaunganishwa katika namna ile ile ya conversational style,napenda sana makala iwe mithili ya kupiga stori na msomaji,iwe kijiweni,kwenye pub,au hata barazani.Pamoja na habari na makala zilizokwenda shule,bingirika na makala hiyo kwa KUBONYEZA HAPA

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.