Showing posts with label BUNGE. Show all posts
Showing posts with label BUNGE. Show all posts

18 Apr 2015


Kwa mujibu wa tovuti ya Bunge letu la Muungano, kama nilivyoi-access saa 11.02 alfajiri kwa saa za hapa Uingereza, marehemu wabunge hawa hapa chini wameendelea kuorodheshwa kwenye tovuti hiyo sio tu kama bado wapo hai bali pia ni wabunge katika majimbo husika.

Ninaamini kabisa kuwa taasisi muhimu kama Bunge ina fungu la kutosha kwa ajili ya huduma zake mbalimbali, ikiwa ni pamoja na tovuti yake. Na hata ingekuwa haina fungu, kufanya marekebisho kwenye tovuti hiyo ni jambo la dakika chache tu, na lisilo na gharama yoyote.

Hakuna ubaya kwa wabunge marehemu kuendelea kuwepo katika tovuti ya Bunge iwapo ukweli kwamba waheshimiwa hao sasa ni marehemu utabainishwa, hususan katika kipengele kinachoonyesha muda wa utumishi wao katika mhimili huo muhimu wa dola.

Pengine hili ni suala dogo lakini kwa hakika Bunge ni moja ya vitambulisho vya taifa letu, na tovuti yake ni njia rahisi kwa Watanzania na wasio-Watanzania kupata habari na taarifa zinazoihusu taasisi hiyo. 

Licha ya kasoro hiyo, nilipofanya search ya majina ya baadhi ya wabunge, hakukuwa na matokeo yoyote.Ukitaka kuhakikisha, tafuta jina la Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete, kwa mfano.








Ni matumaini yangu kuwa Ofisi ya Bunge letu itarekebisha kasoro hii haraka iwezekanavyo

CHANZO: Screenshot za picha kutoka tovuti ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano

5 Feb 2012


WAJIPANGA KUKWAMISHA MUSWADA  MABADILIKO YA KATIBA
Midraji Ibrahim, Dodoma
SASA ni dhahiri kuwa wigo wa mpasuko kati ya wabunge wa CCM na Serikali unazidi kupanuka, baada ya wabunge hao kugoma kukutana na Rais Jakaya Kikwete mjini Dodoma.Katika kikao chao kilichofanyika Ijumaa usiku ukumbi wa Pius Msekwa mjini hapa, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, aliwaomba wabunge hao kukutana na Rais Kikwete ili kuwasilisha malalamiko yao dhidi ya Serikali badala ya kuendelea kuikwamisha bungeni.Wabunge hao wanadaiwa kukataa rai hiyo huku wakimweleza waziwazi Pinda kwamba, itakuwa ni kumkosea heshima na adabu Rais, iwapo watakutana naye halafu wakwamishe marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba inayotarajiwa kufikishwa bungeni wiki ijayo.

“Itakuwa siyo heshima kukutana na Rais halafu tukwamishe muswada wa marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, kwa sababu tumejipanga kuhakikisha kwamba haupiti,” vilieleza vyanzo vyetu vya uhakika kutoka ndani ya kikao hicho.

Badala yake, wabunge hao walikubali kuteua miongoni mwao watu watano ambao wataonana na Rais Kikwete leo atakapowasili mjini hapa akitokea Mwanza kwenye Sherehe za Maadhimisho ya Miaka 34 ya CCM.

Wazungumzaji wakuu kwenye kikao hicho wanadaiwa walikuwa pamoja na,  Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na Mbunge wa Shinyanga, Steven Masele.
 
Marekebisho hayo yalitarajiwa kuwasilishwa kesho, lakini walikataa hadi Ijumaa kwa kile walichodai kuwa, wengi wao watakuwa hawajarejea kutoka Mwanza  kwenye sherehe za maadhimisho ya CCM.

Inadaiwa na wabunge hao wa CCM kuwa, marekebisho hayo yanalenga kukimaliza chama hicho na kukiweka madarakani Chadema baada ya kuondolewa kwa wakuu wa wilaya, kushiriki mchakato wa katiba na kazi hiyo kukabidhiwa wakurugenzi wa halmashauri.

“Hii ni dhahiri kuwa marekebisho haya yanaiumiza CCM na kuisimika Chadema madarakani. Kuwaondoa Ma-DC kwenye mchakato wa katiba na kuweka wakurugenzi wa wilaya ambao wote ni Chadema, hatuwezi kukubali kamwe,” kilieleza chanzo chetu.
Pia, inadaiwa na wabunge hao kuwa marekebisho waliyopewa Dar es Salaam kwenye kamati, ni tofauti na yale yaliyowasilishwa bungeni, huku kukiwa na ongezeko la kurasa nne.

Hata hivyo, inadaiwa baada ya wabunge hao kugoma kukutana na Rais Kikwete, alisimama Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uratibu na Uhusiano), Stephen Wasira, akiwataka kupitisha marekebisho hayo kwa sababu ni agizo la Rais, hali iliyosababisha azomewe huku akitupiwa maneno ya kashfa.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge hao ambao hawakupenda kutajwa majina yao, walisema athari wanayoiona mbele kwa kutopitishwa kwa marekebisho hayo, Chadema watapeleka mashtaka kwa umma kwamba sheria ile ilipitishwa kulinda CCM, hivyo haina manufaa kwa umma.

“Lakini CCM hatujajipanga, kila siku anayesimama jukwaani anazungumzia kujivua gamba, kwa hali hii tusubiri mashambulizi mazito siyo tu kutoka kwa Chadema hata nchi za nje,” kilieleza chanzo chetu.

Pia, wabunge hao wa CCM wanadai kuwa miongoni mwa sababu za kukwamisha marekebisho hayo, ni kile walichodai Rais Kikwete kuwadharau kutokana na wao kupitisha muswada wa sheria hiyo, halafu yeye (Kikwete) anakutana na Chadema dakika chache na kukubaliana na hoja zao.

“Sisi tumekaa hapa (bungeni) kwa zaidi siku mbili na akili zetu timamu, tukapitisha muswada ule, anakutana (Kikwete) na Chadema dakika chache anatuletea marekebisho! Hiyo ni dharau na hatuwezi kukubali,” alilalamika mbunge mmoja.

Kura ya kukosa imani na Rais
Katika kikao cha wabunge hao kilichofanyika Alhamisi wiki hii, baadhi yao walihoji sababu zinazokwamisha masuala mbalimbali serikalini kutopatiwa ufumbuzi, huku Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo, akipendekeza kwamba kama tatizo ni Rais Kikwete, watumie utaratibu wa kumpigia kura ya kutokuwa na imani.

Shelukindo anadaiwa alitaka kujua sababu za masuala mbalimbali kukwama na kutopatiwa ufumbuzi wa haraka na kwamba, iwapo tatizo ni Rais Kikwete, wapo tayari kufuata utaratibu wa kumpigia kura ya kutokuwa na imani.

Hata hivyo, Mbunge wa Simanjiro, Christopher Olle Sendeka, alisimama na kumtaka mbunge huyo kufuta kauli yake, suala ambalo Shelukindo alikubali.

Pia, katika kikao hicho kiliwataka Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Haji Mponda, Naibu wake, Dk Lucy Nkya na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Blandina Nyoni, kujiuzulu kutokana na kuwa chanzo cha mgomo wa madaktari.

Katika kile kinachoonyesha mpasuko huo kuchukua sura mpya, wabunge hao wamekuwa wakikwamisha miswada ya Serikali, suala ambalo siku zilizopita walikuwa wakiipitisha hata pale yanapokuwepo malalamiko kutokana kwa wananchi, kwa kile kilichokuwa kikielezwa kuwa ni ‘msimamo wa chama.’

CHANZO: Mwananchi

16 Feb 2011



Pichani ni Mbunge John Komba wa CCM 'akiwa makini' kwa kuuchapa usingizi Bungeni Dodoma.Hata huyu naye anastahili 'zawadi' ya milioni 90?

Hivi kweli inaingia akilini kusikia kwamba Serikali ya Kikwete ina mpango wa kuwapatia wabunge shilingi milioni 90 kila mmoja "kwa sababu inazojua yenyewe?Majuzi tu tumesikia habari kwamba Serikali hiyo hiyo inatembeza bakuli kwa wahisani ili wasaidie 'kuokoa jahazi' la hali mbaya ya Bajeti ya 2010/11.

Lakini pia tunakumbuka Kikwete alivyokuwa mkali kwa watumishi wa umma walipotishia kugoma kushinikiza kulipwa mishahara inayoendana na hali halisi ya maisha.Sasa kama ilishindikana kuwalipa wafanyakazi wa umma mishahara bora haya mabilioni ya kuwazawadia wabunge yanatoka wapi?

Naona kuna kila jitiahada za watawala wetu kukaribisha yanayojiri huko Arabia na Mashariki ya Kati.Japo inauma kuona mabilioni ya shilingi yakizawadiwa kwa waheshimiwa kama huyo anayechapa usingizi,lakini hatua hiyo inaweza kuwa blessing in disguise kwa maana kwamba huenda ikawahamasisha Watanzania kuiga mifano ya 'walalawima' wenzao wa Tunisia na Misri,na hatimaye kufanikiwa kuleta 'Uhuru wa Pili' (wa kwanza ulikuwa wa kumwondoa mkoloni.Wa pili ni wa kuwaondoa mafisadi)

23 Feb 2010

Angalia "mchemsho" huu  wa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano Samuel SITTA.Anarusha tuhuma nzito dhidi ya wanaharakati wanaokusudia kuandamana kupinga "mahitimisho ya mjadala wa Richmond bungeni" ilhali katika habari husika ameshindwa kuthibitisha tuhuma hizo.Kibaya zaidi,yeye mwenyewe aliporushiwa tuhuma kama hizo aligeuka mbongo.Hebu soma kwanza habari husika (hasa maneno ya rangi nyekundu)

Salim Said
SPIKA wa Bunge Samuel Sitta amewashukia wana-mtandao wa asasi za kiraia zinazotetea usawa wa jinsia, haki za binadamu na maendeleo ya ukombozi wa Wanawake, akisema wanatia mashaka na kwamba wanaendeshwa na utashi binafsi wa wajanja wachache, huku wenyewe wakisema maandamano yapo palepale.
Wanaharakati hao, walitangaza maandamano makubwa ya amani yatakayoendeshwa nchi nzima kupinga kuvungwavungwa kwa hoja za mikataba ya Richmond, TICTS, TRL, taarifa ya uchafuzi wa mazingira kwa kemikali za sumu katika mgodi wa North Mara na ukiukwaji wa haki za binadamu, Loliondo.
Akizungumza na Mwananchi jana Spika Samuel Sitta alipingana vikali na madai ya wanaharakati hao, kuhusu Bunge na kueleza kwamba mtu yeyote akitaka kupima uwezo na uzuri wa bunge katika maamuzi na kusimamia serikali aangalie rekodi ya kazi za bunge kuanzi mwaka 2005 hadi sasa.
'Mimi sikubaliani na wanaharakati hawa hata kidogo. Maandamano ni haki yao na waandamane, lakini hawawezi kupima kazi za bunge kwa kuangalia kipindi cha mitafaruku ," alisema Spika Sitta.
Spika Sitta alisema kuimarisha Bunge si kazi ya lele mama, bali ni mapambano yanayohitaji ujasiri wa hali ya juu.
"Mimi naamini kwamba bunge letu limeimarika katika kuisimamia serikali ukilinganisha na lilikotoka, wanaharakati wanapaswa kujua pia kuimarisha bunge ni mapambano," alisema Spika.
Kuhusu suala la bunge la mfumo shirikishi wa demokrasia, Spika Sitta alisema hilo ni kinyume na katiba, lakini aliwataka wanaharakati hao wajaribu kujenga hoja.
"Mimi naona mfumo wa demokrasia ya uwakilishi bungeni ni mzuri tu, kwa sababu unapatikana kupitia uchaguzi ambayo ni ridhaa ya wananchi, lakini mfumo shirikishi utapatikana wapi.
"Huwezi kushirikisha mashirika au taasisi hizo katika bunge, kwanza zinamwakilisha nani, kwanza haziwawakilishi wanawake ni utashi tu wa baadhi ya wajanja," alihoji Spika Sitta.
Alisema mitandao hiyo inatia mashaka kwa wahisani kwani baadhi ya taasisi zinakula fedha bila ya kupeleka mrejesho kwa wahusika.
"Mambo yote ya bunge yanajadiliwa hadharani na kila mtanzania anayetaka anasikia, lakini je mambo ya hawa wanaharakati na mitandao yao yanajadiliwa na nani," alihoji Spika Sitta.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Concern for Development Initiatives in Africa (ForDIA), Bubelwa Kaiza alisema ujumbe wao mkubwa katika maandamano hayo, ni kwamba hoja hizo zimevungwavungwa na bunge halitambui nguvu na mamlaka liliyopewa kikatiba, badala yake linafanya kazi kwa maslahi ya vyama vya siaasa na sio wananchi.
"Wapo wanaotaka tusiandamane, lakini huo ni woga wao tu, maandamano yapo palepale nchi nzima, tuna sababu za msingi za kuandamana kwani bunge halikuwajibika katika kushughulikia hoja mbalimbali katika kikao cha 18, badala yake limezivungavunga hoja hizo kwa maslahi ya vyama vyao vya siasa.
"Sisi pamoja na wananchi hatukuridhika kuhusu hoja zile zilivyohitimishwa, hakuna pia aliyewajibishwa, kwa hiyo tunaitaka serikali iachane na mfumo wa demokrasia wakilishi na ianzishe mfumo wa demokrasia shirikishi wa bunge ili wabunge waweze kuwajibika moja kwa moja kwa wananchi," alisema Kaiza.
CHANZO: Mwananchi

Tatizo kubwa linalomkabili Spika wetu Samuel Sitta ni uropokaji,yaani kuongea bila ktafakari athari zinazoweza kusababishwa na matamshi yake.Kama kiongozi mkuu wa chombo chenye dhima ya kutunga sheria za nchi,Sitta alipaswa kutambua kuwa baadhi ya kauli na tuhuma alizotoa dhidi ya wanaharakati ni za kihuni.Na bahati yake ni kwamba wanaharakati hao hawana muda wa kumburuza mahakamani kuthibitisha kashfa alizotoa dhidi yao.

Hivi Spika Sitta anaweza kuuthibitishia umma kuwa mitandao inatia mashaka kwa vile baadhi ya taasisi zinakula pesa bila kurejesha fedha kwa wahusika?Ameyajuaje hayo?Hivi hao wanaotoa fedha zao (wanaofadhili mashirika hayo) wamekuwa wajinga kiasi gani cha kutohitaji taarifa za matumizi ya fedha wanazotoa?

Sitta ni mropokaji kwa vile yeye alipotuhumiwa kukumbatia ufisadi katika ofisi ya Bunge aliwaka kama nini akidai ni njama za mafisadi dhidi yake.Iweje leo akurupuke kuwatuhumu wanamtandao kwa vile tu wameonyesha nia ya kuandamana kupingana na ubabaishaji wa Bunge linaloongozwa na Sitta?

Sitta asijione Mungu-mtu.Kila Mtanzania ana haki kama yeye Sitta kutoa mawazo yake hadharani alimradi havunji sheria za nchi.Kama Sitta anaona Bunge analoongoza limefanya vizuri katika utendaji kazi wake,si lazima kwa kila Mtanzania kuona hivyo au kukubaliana na mtizamo wa aina hiyo.Na ni vigezo vipi anavyoweza kutuonyesha Mheshimiwa Sitta kuwa Bunge lake limewajibika ipasavyo?Huko kutuzuga kwa zaidi ya miaka miwili kuwa yeye na wenzake ni wapambanaji dhidi ya mafisadi kisha kusalimu amri kama kondoo walionyeshewa mvua?

Na hata kama Bunge analoongoza Sitta linawajibika akama anavyotaka tuamini,si ndio kazi yake?Na si kazi ya kawaida kwani kwa mshahara wa mamilioni na kiinua mgongo cha mamilioni mengine kwanini waheshimiwa hawa wasiwajibikie kwa kiwango cha juu?

Sitta anakasirika kwa vile alitangaza kuwa "mjadala umefungwa",na kwa jinsi anavyojihisi ni Mungu-mtu anaona kitendo cha wanaharakati "kuendeleza mjadala" ni kama "wanavunja amri ya Mungu".Katika habari husika hapo juu,Sitta anathibitisha ubinafsi wake kwa kurudiarudia kutumia neno "MIMI".Anaweza kuwa sahihi katika mtazamo wake binafsi,lakini jamii hailazimiki kuafikiana nae wala kushurutishwa kutenda atakayo yeye.





26 Jun 2009


Hili ndio "BUNGE LENYE MENO"!Juzijuzi mbunge mmoja wa CCM kaomba Mungu alilaani Baraza la Mawaziri kwa kushindwa kutimiza majukumu yake.Mwingine kadai serikali ina ugonjwa na inahitaji maombezi (na kwa kawaida magonjwa yanayohitaji maombezi ni yale yasiyotibika kama vile ukimwi,nk).Jana mbunge mwingine wa chama hicho tawala amewafananisha mawaziri na mbwa.Na pengine moja ya mambo yatakayokumbukwa zaidi katika historia ya bunge letu tukufu ni jinsi kikao hiki cha bajeti kinavyoonekana "mwiba mkali" kwa mawaziri,at least according to walio mahiri katika kuripoti pasipo kusoma kati ya mistari (reading between the lines).

Sina maneno ya huruma kwa baadhi ya wabunge hawa wa CCM.Ni wanafiki wanaohangaika kutumia vizuri nafasi hizi za mwisho mwisho kujitengenezea mazingira ya kurejea bungeni hapo mwakani.Lakini ili haki itendeke,ni vema kuwatofautisha wanafiki hawa kwa makundi.Kuna kundi la wabunge waliojitokeza mapema (kabla hata ya joto la uchaguzi wa mwakani halijaanza kupanda) kukemea ufisadi na vitendo vingine vinavyokwaza maendeleo ya taifa letu.Sio siri kwamba wabunge kama Selelii,Kimaro,Killango,Mwambalaswa,Mwakyembe na wengineo wamejitokeza kuwa sauti adimu ndani ya CCM dhidi ya ufisadi.Na tunafahamu vituko wanavyofanyiwa na watu walewale wanaopaswa kuwaunga mkono.

Kundi la pili ni la wababaishaji walio njia panda; upande mmoja hawana nia ya dhati ya kupambana na ufisadi au pengine ni sehemu ya mfumo unaodumisha ufisadi,upande mwingine wanafahamu fika kwamba miongoni mwa ajenda za uchaguzi mkuu ujao ni ufisadi na namna wawakilishi wetu walivyoshiriki katika mapambano dhidi ya ufisadi.

Pia kuna makundi mengine mawili: la kwanza linajumuisha wababaishaji wanaokwenda bungeni kwa vile tu ndio mahala pao pa kuchuma shs 7,000,000/= za mshahara kiulaini.Hawachangii hoja,hawaongei lolote japo si mabubu,wapo wapo tu.Kuwepo au kutokuwepo kwao bungeni hakutambuliki kwa vile wanaongeza tu idadi ya wabunge.Kundi la pili ni la watetezi wa ufisadi.Hawa ni wepesi wa kuomba mwongozo wa Spika kila maslahi yao au ya wadau wenzao wa ufisadi yanapoguswa.Nadhani mmesikia "Dokta" Mzindakaya alivyotumia Maandiko Matakatifu kutetea ufisadi .Ila hawa wanaocheza na vitabu vya Mungu,nadhani ndio wanaostahili kulaaniwa zaidi kwani wamevigeuza kama manifesto za usanii wao wa kisiasa!

Uzuru wa makundi haya mawili ya mwisho-la tatu na la nne-ni kwamba angalau yanajumuisha wabunge tunaofahamu wanaposimamia.Aidha ni wazembe na mabubu wasioongea (aidha kwa aibu ya kuongea,au "heri mie sijasema",au uzembe tu) au ni watetezi wa mafisadi.Hawa si wanafiki as such kwa vile wameji-identify kwetu kuwa ni viumbe wa namna gani.

Tofauti kati ya makundi hayo ni ndogo mno contrary to inavyosomeka na kusikika kwenye vyombo vya habari.Hapa nataka kuzungumzia makundi mawili ya mwanzo-la kwanza na la pili.Hawa wote ni wana CCM,na kwa namna yoyote ile hawawezi kujitenganisha na matatizo yanayosababishwa na chama hicho tawala.Na hili si la kufikirika kwa sababu tayari wengi wa wabunge wa kundi la kwanza wamekuwa wakikumbana na kadhia mbalimbali kutokana na msimamo wao dhidi ya ufisadi,na guess what,kadhi hizo ni kutoka kwa wenzao ndani ya CCM.

Mawaziri wanaolaaniwa na kufikia hatua ya kuitwa mbwa wanatoka CCM pia.Hii sio vita ya wenyewe kwa wenyewe kama inavyoweza kutafsiriwa kiuzembe.Huu ni unafiki,period.CCM isingefika hapo ilipo laiti "wapambanaji hawa" wangekuwa na mkakati wa dhati wa kuleta mabadiliko ya kweli.Wanachofanya muda huu ni cha kibinafsi zaidi kuliko kitaifa.Wanaweza kurudi bungeni hapo mwakani baada ya wapiga kura wao "kuzugika" na CVs za wawakilishi wao tangu 2005 hadi 2010.Kurudi kwao bungeni kutapelekea CCM kuendelea kuwa yenye wabunge wengi bungeni,na hivyo kupelekea kuendelea kwa haya tunayopigia kelele kila siku.

Siamini kama kuna mkakati kwa Selelii na wenzake kuleta mageuzi ndani ya CCM.So far,kelele zao hazijasaidia kukitenganisha chama hicho na ufisadi,implying that kelele zao zimebaki kuwa kelele tu.Wana options mbili: waendelee kupiga kelele lakini wabaki kuwa sehemu ya chama kinachohusishwa na ufisadi au wajondoe ndani ya chama hicho na hivyo kubainisha kuwa kuwa kwao ndani ya CCM ilikuwa ni sehemu tu ya maisha yao ya kisiasa lakini cha muhimu zaidi kwao ni Tanzania na ustawi wa Tanzania.Yes,si lazima kuwa mbunge wa CCM ili kupata fursa ya kupigania maslahi ya taifa.Mifano hai ipo;Dkt Slaa,Zitto Kabwe,nk sio wabunge wa CCM,lakini sote tunafahamu michango yao katika kupambana na ufisadi.

Unafiki wa wabunge hao wa CCM unasababishwa na kitu kimoja kisicho na msingi: UBINAFSI WA KISIASA.Ni hivi,kwa CCM,umoja na mshikamano ndani ya chama hicho ni muhimu zaidi kuliko umoja na mshikamano wa taifa.Na hilo ni matokeo ya chama hicho kuamini kwamba ni chenyewe tu kinachoweza kudumisha mshikamano na umoja wetu.Kwa lugha nyingine,kimebinafsisha uwezo,dhamira,jitihada na nguvu za Watanzania zaidi ya milioni 35 ambao si wanachama wa chama hicho (takwimu za karibuni zinaonyesha idadi ya wanachama wa CCM ni takriban milioni 4 tu).Japo ni kweli kwamba chama hicho kimetoa uongozi uliosaidia kudumu kwa amani na mshikamano huo,Watanzania wenyewe ndio waliofanya kazi ya msingi zaidi kufanikisha hilo.Upendo na upole wetu (ambao mara nyingi umeishia kutumiwa vibaya na wanasiasa walafi) ndio sababu kuu ya kwanini tumeendelea kubaki kisiwa cha amani (kwa maana ya kutokuwa vitani).

Ni ubinafsi wa kisiasa unaopelekea CCM kuweka mbele maslahi ya kisiasa badala ya maslahi ya taifa.Sote tumeshuhudia mara kadhaa wabunge wa chama hicho tawala wakiitisha vikao "vya kuwekana sawa" kila zinapojiri hoja nzito bungeni.Kuwekana sawa kwa maslahi ya nani?Hivi cha muhimu ni hoja ipite tu au ipite ili ilete mabadiliko chanya kwa wananchi?

Lakini ili upate mfano sahihi zaidi kuhusu ubinafsi wa wabunge hawa ni pale Dkt Slaa alipotamka bayana kwamba mishahara ya wabunge ni mikubwa mno kulinganisha na hali halisi ya uchumi wetu.Kwa umoja wao (huku wakipata sapoti kutoka kwa wabinafsi wengine waliojificha kwenye vyama vya upinzani) walimzomea Dkt Slaa na kumzongazonga kana kwamba kawatukana.Hivi ina maana wabunge hawa wanaotuzuga kuwa wanatetea maslahi yetu hawaelewi kuwa wakati wao wanazawadiwa takriban shilingi 7,000,000/= mwezi (wastani wa shilingi laki 230,000/= kwa siku sawa na takriban shs 10,000/= kwa saa) takriban Watanzania 36,000,000 wanaoishi kwa chini ya shilingi 3000/= kwa siku?

Hadi kufikia tamati yake na mabiloni kadhaa kutumika,kikao hiki cha bajeti kitashuhudia kila aina ya vituko kutoka kwa wanafiki hawa.Ukidhani hizo dua dhidi ya mawaziri na "matusi" ya kuwaita mbwa ndio hatua kali kabisa,subiri usikie "makombora" zaidi.Na kama kawaida ya vyombo vyetu vya habari,kurasa zitapambwa na maneno mazito kama "Bunge moto juu","Wabunge wachachamaa",na ubabaishaji mwingine kama huo.Lakini pamoja na yote hayo,makadirio ya wizara za mawaziri wanaoombewa dua mbaya na kuitwa mbwa yatapitishwa na wabunge haohao wanaotuzuga kuwa "wana hasira na mawaziri".

20 Jun 2009


Orodha ya wabunge bubu bungeni yawekwa hadharani

Na Leon Bahati

WAKATI tukielekea mwaka wa lala salama wa Bunge la mwaka 2005-2010, huku baadhi ya wabunge wakiibuka mashujaa kwa kutoa michango mizito inayoitingisha serikali, imebainika kuwa baadhi yao hadi sasa hawajawahi kuuliza hata swali moja wala kuchangia.

Uchunguzi huo umefanywa na Mwananchi Jumapili kwa msaada wa tovuti ya bunge ambako kila mchango wa mbunge hurekodiwa kwa kuonyesha swali la msingi au la nyongeza alilouliza, majibu yake na mchango aliotoa.

Kati ya wabunge 319 walioko katika Bunge la sasa ambao hawajawahi kuuliza maswali ya msingi wanakadiriwa kufikia 50 na wasiouliza maswali ya msingi wala nyongeza ni zaidi ya 30.

Mawaziri na wabunge ambao pia ni wakuu wa mikoa, hawajahusishwa kwenye hesabu hizo kwa sababu wapo upande wa serikali na wote wamekuwa hawaulizi maswali. Wengine ambao hawakuhusishwa kwenye vipengele hivyo ni Spika na Naibu Spika, lakini wote wameonyeshwa kuwahi kuchangia hoja mbalimbali.

Kwa mujibu wa mtandao huo, Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz ndiye pekee ameonyeshwa kuwa hajawahi kuuliza swali lolote wala kuchangia jambo lolote tangu Bunge limeanza.

Wabunge wengine ambao wameonyeshwa hawajawahi kuuliza maswali, lakini wamekuwa wakichangia hoja mbalimbali nao ni Yusuf Makamba (Katibu Mkuu wa CCM); John Shibuda, Harith Mwapachu, Ali Haji Ali, Omar Sheha Musa, Abdallah Sumry, Gideon Cheyo, Juma N’hunga, Nazir Karamagi, Anna Abdalah, Ali Haji Ali, Thomas Mwang’onda, Salum Khamis Salum, Hassan Rajabu Khatibu na Felix Mrema.

Wengine ni Philemon Sarungi, Edward Lowassa, Andrew Chenge, Abdisaalam Issa Khatib, Dk Ibrahim Msabaha, Zakia Meghji, Kingunge Ngombale Mwiru, Salimu Yusufu Mohamed, Salum Ahamed Sadiq, Omar Sheha Mussa, Manju Msambya na Benedict Ole-Nangoro.

Wabunge ambao pia ni wakuu wa mikoa ufanisi wao wa kuchangia bungeni ni mdogo ni Abdul Aziz – Iringa (7); Dk James Msekela – Dodoma (6); Monica Mbega – Kilimanjaro (3); Dk Christine Ishengoma-Ruvuma (4) na William Lukuvi – Dar es Salaam (3). Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba aliwahi kutoa michango bungeni mara mbili tu.

Katika Kundi la wabunge 13 wanaoongoza kwa kuuliza maswali ya msingi linaongozwa na Mgana Msindai (CCM) mwenye maswali 34 na kufuatiwa na William Shellukindo (29); Diana Chilolo (28), Paschal Degera (28), George Lubelege (25), Raphael Mwalyosi (24) na Mhoga Ruhwanya (23).

Wabunge wengine kwenye kundi hilo wana maswali 22 kila mmoja nao ni, James Msalika, Job Ndugai, Zitto Kabwe, Herbert Mtangi, Victor Mwambalaswa na Lucy Owenya.

Wabunge 11 vinara wa kuuliza maswali ya nyongeza ni Dk Wilbrod Slaa (71), Hamad Rashid Mohamed (71), Mgana Msindai (67), Esther Nyawazwa (58), George Lubelege (56), Diana Chilolo (54), Hafidh Ali Tahir (52), Geofrey Zambi (50) na wawili waliofungana kwa kuuliza 49, Jenista Mhagama na John Kilimba (49).

Katika kundi la kutoa michango mbalimbali kwenye vikao vya bunge linaongozwa na Naibu Spika Anne Makinda (495); akifuatiwa na Spika, Samweli Sita (494). Wengine ni Jenister Mhagama (193); Job Ndugai (147); Zitto Kabwe (125); Dk Slaa (106); Andrew Chenge (89); Suzan Lyimo (87); William Shelukindo (77); Geofrey Zambi (73); John Kilimba (69) na mawaziri wawili waliofungana kwa kufikisha michango 67 ambao ni Shamsa Mwangunga, Waziri wa Maliasili na Utalii na Waziri wa Miundombinu, Dk Shukuru Kawambwa.

Mawaziri wengine wanaofuatia ni Dk Mary Nagu (64); Profesa David Mwakyusa (59); William Ngeleja (50); Mwanasheria Mkuu wa Serikali; Johnson Mwanyika (47); Dk Makongoro Mahanga (45); Profesa Jumanne Maghembe (45); Stephen Wasira (41) na John Chiligati (40).

Akizungumzia kuhusu kumbukumbu hizo wiki iliyopita, Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alisema kuwekwa kwa taarifa hizo hakuna maana zaidi ya kuweka kumbukumbu za michango ya wabunge, lakini akasema kulikuwa na marekebisho kwa wakati huo.

Alipotafutwa tena jana, alisema tovuti hiyo ya Bunge imefanyiwa marekebisho makubwa ili wananchi waweze kupata kwa undani kumbukumbu mbalimbali za vikao vya Bunge.

Pamoja na maboresho hayo, Dk Kashililah alisema: "Tuna mpango wa kuongeza maboresho zaidi yakiwepo ya kuwezesha watu kufuatilia vikao vya Bunge kupitia tovuti hiyo."

Licha ya baadhi ya wabunge kuwa na mchango hafifu, Bunge la sasa limeonekana kuwa mwiba mkali kwa viongozi serikalini hususan mawaziri, kutokana na baadhi ya wabunge kuwabana katika mambo mbalimbali ya utendaji mbovu na ufisadi, huku kufupishwa kwake kukipunguza nafasi ya kuuliza maswali na kuchangia kwa baadhi yao ambao walikuwa hawajafanya hivyo.

Katika kipindi hicho miongoni mwa hoja nyingine zilizosisimua ni mjadala wa Kamati Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk Harrison Mwakyembe kuhusu utoaji wa zabuni ya umeme wa dharura iliyotolewa kwa kampuni ya Richmond Development Limited (LLC); na kusababisha Rais Jakaya Kikwete kuvunja baraza la mawaziri baada ya aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa kujiuzulu pamoja na mawaziri wengine wawili.


CHANZO: Mwananchi

18 Jun 2009


Hivi karibuni watunga sheria (wabunge) wetu watatu "waliungana" kuandika kitabu walichokipa jina "BUNGE LENYE MENO".Ukiangalia sehemu ndogo tu ya wasifu wa wabunge hao utamaizi kuwa "muungano huo wa uandishi" ulikuwa ni mithili ya "ndoa za makaratasi" (marriages of inconvenience).

Dkt Wilbroad Slaa,Spika Samuel Sitta na John Momose Cheyo!Nadhani kitu pekee kinachoweza kuwafanya wafanane ni "wote ni wabunge",and the similarity stops there.Wakati Dkt Slaa amejijengea jina kubwa kama kinara wa mapambano ya ufisadi,ni vigumu kum-define Spika Sitta linapokuja suala la mapambano dhidi ya ufisadi.Lakini si vigumu kukumbuka kuwa ni Sitta huyuhuyu aliyempa kadi nyekundu Zitto Kabwe alipombana ex-waziri Nazir Karamagi kuhusu sakata la Buzwagi.Na ni Sitta huyuhuyu aliyetishia kumshtaki Dkt Slaa alipoibua tuhuma ufisadi ndani ya Benki Kuu akidai kuwa ni ushahidi wa kufoji!Eti leo tunaambiwa Spika huyuhuyu nae ni kinara wa mapambano ya ufisadi!


Tukija kwa John Cheyo,nadhani amebaki kuwa UDP,kwa maana ya one-man party.Sera yake ya mapesa ilijaa utani ambao ungekuwa na maana zaidi kwenye sanaa za maigizo kuliko katika siasa makini.Amebaki kuwa jina tu.Sidhani kama kunamfano wowote hai unaoweza kutumika kumtambulisha Cheyo kama mwanaharakati wa mapambano dhidi ya ufisadi.


Sasa hao ndio waandishi wa kitabu BUNGE LENYE MENO.Lakini kwa vile nafahamu kwamba uchambuzi makini unahitaji kwenda mbali zaidi ya kuangalia personalities,naomba kugeukia hoja yangu ya kupingana na ya akina Sitta kuwa bunge la sasa lina meno.Binafsi nasema kama ni meno basi ni ya plastiki.Nadhani unafahamu mtoto mchanga anapoanza kuota meno huwa yanaota meno ambayo yanaitwa meno kwa vile tu yamekaa sehemu yalipo meno.Ukimnywesha uji wa moto basi kilio chake hapo ni balaa!Ni meno machanga yasiyomudu kutafuna vitu vigumu.


Na ndio bunge letu lilivyo.Utasikia kelele,vitisho,na vitu kama hivyo kila waheshimiwa wanapokutana hapo Dodoma ambapo mwisho wa siku akaunti zao zinaingiza kipato cha zaidi ya mwezi mzima kwa Mtanzania wa kawaida,huku kila mwisho wa mwezi wakiondoka na mamilioni lukuki.Basi angalau kipato chao kingeendana na hali halisi ya uchumi wa nchi yetu.


Wabunge wa CCM,ambao wanatengeneza zaidi ya robo tatu ya bunge letu,ndio vichekesho zaidi.Utamsikia huyu akisema hili kabla ya mwenzie kumkalia kooni akitaka mwongozo wa Spika kwa madai ya "kukiuka kanuni za bunge".Lakini ukifuatilia kwa makini,mara nyingi mwongozo huo huombwa pale anapojitokeza mbunge mmoja kuelezea yale yanayozungumzwa na Watanzania wengi mitaani,kwa mfano ishu ya ufisadi.Sasa kwa vile kuna wabunge wenye deni kubwa zaidi kwa CCM na vigogo wake,njia pekee ya kulipa deni hilo ni kuomba mwongozo wa Spika ili kuwaziba midomo wale wanaoongea yasiyopendeza masikioni mwa watawala.


Majuzi,Mbunge wa Nzega Lukas Selelii amemwomba Mungu awalaani mawaziri kwa madai kwamba wamekuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya ufisadi nchini.Mbunge wa Pangani Mohammed Rished akaomba mwongozo....sijui kuonyesha anafahamu zaidi sheria za Bunge au kwa vile yaliyoongelewa na Selelii hayakumpendeza mbunge Rished.Kwani si kweli kwamba maamuzi mengi yaliyopelekea skandali za ufisadi yalipitishwa na Baraza la Mawaziri?Kabineti ingetimiza wajibu wake tungekuwa na Richmond?au Kiwira?Au TICTS?au Buzwagi?Au IPTL?Orodha ni ndefu.Sasa Rished alihitaji mwongozo kwa vile Selelii kumuomba Mungu awalaani watu waliofanya maamuzi yaliyopelekea ufisadi ni kosa la jinai au?Halafu tunaambiwa tuna "bunge lenye meno"!In this case,haya wala si meno ya plastiki bali ni mapengo kabisa.


Fuatilia kwa karibu mjadala wa Bajeti unavyoendelea huko Dodoma.Kuna kauli za uchungu kutoka kwa baadhi ya wabunge kama Selelii,Mwambalaswa,Mpendazoe na,kama kawaida,wabunge wa upinzani kama vile Dkt Slaa.Lakini kauli pekee hazimsaidii Mtanzania masikini asiyejua hatma ya maisha yake.Kelele hizi zimekuwepo tangu bunge hili linaanza.Ndio,zimesaidia kuundwa kwa kamati mbalimbali kama ile ya Mwakyembe.Lakini kuunda kamati kisha kutofanyia kazi mapendekezo yake ni sawa na ufisadi tu.Ikumbukwe kuwa kamati hizo hutumia mamilioni ya fedha za walipa kodi.Ukubwa wa gaharama za kuendesha kamati za aina hiyo ungeweza kupunguziwa maumivu laiti mapendekezo yanayotolewa yangekuwa yanafanyiwa kazi.Hadi leo wahusika wa Richmond (achana na yule decoy mwenye kesi mahakamani) wanaendelea "kupeta".


Laiti Bunge lingekuwa na meno,isingetosha kwa Lowassa,Msabaha na Karamagi kujiuzulu tu.Walipaswa wakabidhiwe kwa vyombo vya dola.Kadhalika,watendaji wa serikali waliotajwa kuhusika walipaswa kuwajibishwa mara moja.Badala yake,hadithi zimeendelea kila kinapojiri kikao kingine cha bunge,huko waandishi wetu mahiri wa kunukuu wakija na vichwa vya habari kama "Moto kuwaka Bungeni","Ishu ya EPA kuibuliwa tena Bungeni"...Huwezi kuwalaumu sana kwa vile vyombo vya habari vinaendeshwa kibiashara na kichwa cha habari chenye mvuto kinauza gazeti!


Bunge lenye meno lisingekuwa linapigwa danadana na Waziri Ngeleja kuhusu ishu ya Kiwira.Bunge lenye meno lisingekubali mkataba wa TICTS uendelee kuwa hoja ya moto kila kikao lakini inayoishia kuwa ya moto pasipo mabadiliko,only for it kuwa ya moto tena kwenye kikao kingine.Yayumkinika kusema kuwa kama ni moto wa hoja,basi ni wa njiti ya kiberiti kwenye upepo mkali;hudumu kwa sekunde tu.


Sintajadili zaidi kwa vile itakuwa sawa na kupre-empty muswada wa chapisho naloandaa kama mapitio (majibu?) ya kitabu hicho cha wabunge hao.Ila kwa kifupi,si rahisi kuwa na bunge lenye meno wakati wabunge wenyewe wanaishi maisha tofauti na hao wanaopaswa kuwawakilisha bungeni (nikimaanisha maslahi yao).Tusidanganyane,mtu anayelipwa milioni 6 na ushee kwa mwezi hawezi hata chembe kuwa mwakilishi mzuri wa mtu asiye na uhakika wa kukamata angalau shs 10,000 kwa mwezi.Haya ni matabaka mawili tofauti,na japo kinadharia wabunge wanapaswa kuwa sehemu ya tabaka tawaliwa kwa maana ya uwakilishi wa wananchi,maslahi yao makubwa yanawaingiza kwenye tabaka tawala na hivyo kuwaweka kwenye mgongano wa moja kwa moja direct confrontation) na tabaka tawaliwa la wananchi wa kawaida.Katika hali hiyo,serikali kwa maana ya the executive branch of the government,inapata free pass kwani wanaopaswa kuihoji nao wanajikuta wakihojiwa na wanaowawakilisha.Kiuhalisia,mpiga kura is hardly represented bungeni.


Lakini tukiweka kando suala la kipato na matabaka,tatizo la msingi zaidi kwenye bunge hili ni kutanguliza mbele maslahi ya chama badala ya maslahi ya nchi.Umoja na mshikamano ndani ya CCM unatafsiriwa kuwa ni muhimu zaidi kuliko umoja na mshikamano wa kitaifa.Wengi wa wabunge wa CCM wanahofia kuzungumzia baadhi ya masuala yanayolihusu taifa ambayo kwa namna moja au nyingine yanaifanya CCM inyooshewe kidole.Hakuna mbunge wa CCM anayeweza kuzuia bajeti ya wizara flani,hata kama ni mbovu namna gani,kwa vile akifanya hivyo atatafsiriwa kuwa anavunja mshikamano wa chama.Mbunge katika bunge lenye meno hawezi kuogopa tafsiri ya chama chake,bali wapigakura wake.

Kwa anayehitaji nakala ya bure ya kitabu hicho cha BUNGE LENYE MENO (as an ebook),tuwasiliane.

5 May 2009


(Photo courtesy of ZENJIDAR)
By Rodgers Luhwago, Dodoma

Speaker of the National Assembly Samuel Sitta has sturdily defended the proposal by legislators to increase their monthly package to 12m/- ($9,078), adding that the move has been wrongly judged by critics.

Tanzanian MPs, who currently make 7m/- ($5,292) per month - only 1.8m/- of which is their taxable basic salary - want to increase their base salary to 3m/- and additional allowances to 9m/-.

The proposed 12m/- ($9,078) package would put parliamentarians in the range of Kenya`s MPs, who earn a minimum of Ksh851,000 ($11,335) every month, of which only the basic salary of Ksh200,000 ($2,664) is taxed. Some of the allowances making up additional Ksh651,000 ($8,560) include funds for gym memberships and unspecified ‘entertainment` costs.

Ugandan lawmakers pocket the least of MPs in the region, bringing home Ush2.6m ($1,214) in basic monthly salary and Ush7m ($3,271) including night, subsistence and fuel allowances, according to The Monitor newspaper.

This income is still far above average salaries in most other sectors, the newspaper says.

To put things in perspective, with the proposed salary Tanzanian MPs would make $108,936 per year, while Kenyan MPs currently make $136,020 per year.

Members of Congress in the United States make $174,000 a year, which is all taxable income unlike the Tanzanian and Kenyan salaries.

Tanzania`s GDP is $16.18bn and Kenya’s is $29.3bn, while the United States GDP is around $14 trillion, close to 1,000 times the size of Tanzania`s economy.

Should the proposed increase in pay go through for Parliamentarians, Tanzanian MPs will be earning close to $30,000 more than their South African equivalents, who now earn R714,618 ($79,822) a year after giving themselves an 11 percent annual salary increase effective last April.
But reacting to the ongoing debate about the newly proposed package, the Speaker furiously described the reports as total exaggeration aimed at pursuing a malicious agenda against the legislature.

In an exclusive interview with The Guardian on Sunday over the weekend in his Dodoma office, Speaker Sitta said he was surprised at how closely some individuals and members of the press were following legislators` salaries while turning a blind eye to the wages of the other working cadres in the government.

``Is it fair to include a sitting allowance, per diem and other charges into an MP`s monthly pay? Is it also justifiable to include the salary of an assistant to an MP`s monthly pay? By the way, why are MPs the only ones targeted when it comes to emoluments?`` Sitta queried.

He said permanent secretaries, regional and district commissioners, ministers and judges are among the senior working cadres in society but you rarely hear people talking about their earnings.

``Let`s just take a simple example: the fuel charge for the district commission is separately paid, and this applies to the charges for water, electricity and the salary of his aides.

Why don’t you include all this in the DC’s salary? Instead we find it simple to do this to an MP?`` he said.

According to the Speaker, the implementation of the Five-Year Corporate Plan 2009-13 that the Parliament launched mid this week, includes employing research assistants for MPs whose salaries would be paid by the government. ``Is it logical and fair to take the salaries of these research assistants from the legislators’ monthly salaries?`` he asked.

``In the public service sector there is what is described as personal emoluments, which is a salary of the public servant and other charges.

However, due to the absence of MPs` offices in their constituencies, the salaries for their assistants are being included in the legislators` salaries but this does not mean that the whole money belongs to the MP,`` he said.

The Speaker said the allowances paid to the MPs are just the same as the allowances paid to all other public servants of such a rank, adding that all senior officers are paid per diems and sitting allowances.

He said, according to the public service system, per diems and sitting allowances are never taken as an official income of the person.

``In fact the per diem paid to the MPs is sometimes not sufficient when he travels to places like Arusha. We are sometimes forced to pay for hotel accommodation in Arusha.

Now, why make other charges as part of an individual`s income? Very unfortunately this is done to MPs only. No one is saying that permanent secretaries are highly paid,`` Sitta said.

If the same calculations were made for the permanent secretaries, he said, they would be found to be earning between 14m/- and 15m/- per month.

He said people have diverted public attention from deliberating on embezzlement of public funds and corruption to questioning legal expenditures by combining personal income and other charges paid to MPs, describing them as the legislators` monthly salaries.

``Things paid for in the office of the legislator are stationeries, water, power and telecommunication and all this costs 735,000/- per month.

The same items may cost higher in the office of the DC but we don’t include such costs in the DC`s salary,` he said. He said the salary of an MP is 1.8m/-.

The Speaker was reacting to reports that Parliament last year passed the National Assembly Act, 2008 which, among other things, improves legislators` salaries and other charges.

The new Act is expected to be operational after the 2010 general election.

Speaking last Wednesday during the launching of the Five-Year Corperate Plan 2009-2013 Sitta said the Plan aimed at making Parliament an effective institution that is more people-centred.

According to the Speaker, the strategic objectives of the plan include enhancing MPs` overall effectiveness for better service to the general public and enhancing individual effectiveness of MPs by providing them with properly equipped offices at constituencies and Parliament premises.

The plan, which is expected to cost 373.9bn/- during implementation, will involve giving Members of Parliament staff assistants and upgraded data services and constantly reviewing their emoluments and welfare packages to keep MPs and staff appropriately motivated.

Commenting on the for MPs’ per diem and allowances to be taxed, Speaker Sitta said that is subject to the change of the Income Tax Act, 2004.

However, he said if allowances are to be taxed then that has to be applied to all workers in the country and not MPs alone.

``To be frank I don`t agree with people who want allowances to be taxed. You can’t give a person a subsistence allowance and again tax it. It is absolutely meaningless,`` he said.

AT LEAST SOME OF US NOW CAN FINALLY MAKE SENSE WHY HIS HONOURABLE SAMUEL SITTA BRANDED HIMSELF "THE SPEAKER OF STANDARDS AND SPEED."

30 Apr 2009


Spika wa Bunge, Samuel Sitta amesema kuna maazimio mengi ya Bunge ambayo serikali imekuwa inasuasua kuyatekeleza. Kutokana na hali hiyo, amesema katika mkutano ujao wa Bunge wa bajeti, atatekeleza wajibu wake na serikali isije kumlaumu atakapoanza kutekeleza wajibu huo.

Kauli hiyo ya Spika aliitoa kutokana na majibu yaliyotolewa na serikali kupitia Naibu Waziri wa Miundombinu, Hezekiah Chibulunje, alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Vunjo, Aloyce Kimaro (CCM). Mbunge huyo alitaka serikali kuunda kamati huru ambayo itachunguza na kushughulikia waliohusika kuuza nyumba za serikali na kusababisha hasara. Naibu Waziri huyo alisema serikali inatekeleza maazimio ya Bunge ambayo yalitokana na Mbunge huyo kuwasilisha hoja binafsi bungeni....ENDELEA


HII HAIJATULIA.INA MAANA AWALI SPIKA ALIKUWA HATEKELEZI WAJIBU WAKE IPASAVYO NA NDIO MAANA HALAUMIWI AU...?HALAFU HAYA MAMBO YA LAWAMA YANATOKA WAPI WAKATI SPIKA (NA BUNGE) NA SERIKALI HAWAFANYI MAMBO KWA AJILI YAO BINAFSI BALI UMMA WA WATANZANIA?


HIVI BUNGE LETU LIMEGEUKA KUWA MALI YA SPIKA AU SPIKA NI KIONGOZI TU WA BUNGE?MAANA KAMA KUTAKUWA NA LAWAMA (KAMA ANAVYOTAHADHARISHA SPIKA) BASI ZITAELEKEZWA KWA BUNGE NA SIO SPIKA (AMBAYE PIA NI MBUNGE).


OK,TUWEKE HILO KANDO.JE KUNA HAJA YA KUTAHADHARISHANA KWAMBA MSIPOFANYA HIVI MIE NTAFANYA VILE?KWANI HAKUNA UTARATIBU MAALUM WA KUFUATWA PINDI HALI KAMA HIYO ANAYOZUNGUMZIA SPIKA IKITOKEA?


KUBINAFSISHA-IN THE SENSE KWAMBA NIKISEMA INYESHE ITANYESHA OR VICE VERSA- TAASISI KAMA BUNGE NI HATARI.


na Ratifa Baranyikwa, Dodoma

WAKATI Bunge zima likimwandama Mbunge wa Karatu, Dk. Wilibrod Slaa (CHADEMA), kutokana na msimamo wake kuwa posho za wabunge ni kubwa na kutaka zipunguzwe, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ameungana na wabunge wengine kwa kusema kuwa posho hizo ni ndogo na kutaka ziongezwe.

Ingawa hakutaja jina, lakini kauli hiyo ya Waziri Mkuu imeonekana dhahiri kumjibu Dk. Slaa anayetaka mishahara na posho za wabunge zipunguzwe, kwamba ni kubwa mno ukilinganisha na watumishi wengine wa umma.

Pinda aliyasema hayo jana mjini hapa wakati akizindua mpango mkakati wa Bunge wa miaka mitano, wenye nia ya kulifikisha Bunge katika kiwango cha juu cha ufanisi.

Katika uzinduzi huo uliofanyika katika Ukumbi wa Pius Msekwa mjini hapa, Pinda alitumia mwanya huo kuchomeka suala la posho za wabunge, ambalo limekuwa agenda kubwa katika mkutano wa 15 wa Bunge unaomalizika leo.

Akielezea hatua ambazo serikali imekuwa ikizifanya kwa upande wa Bunge, Pinda ambaye aliorodhesha hatua kadhaa za kuboresha maslahi ya Bunge, alisema lengo la serikali ni kuboresha maslahi na posho za wabunge ambazo kwa sasa bado ni ndogo.

“Lengo la serikali kwa Bunge ni kuboresha maslahi na posho za wabunge ambazo kwa kweli kwa sasa hazifikii stahiki, lengo ni kuhakikisha Bunge linaboreshewa maslahi ili liweze kufanya kazi yake stahiki na kwa kiwango cha kuridhisha,” alisema Pinda.

Awali, akizungumzia malengo makubwa saba ya mpango mkakati huo, alisema moja ya malengo hayo ni kuboresha maslahi na stahiki za wabunge ili kuliwezesha Bunge kutekeleza majukumu yake ya kikatiba ipasavyo.

Mbali na malengo hayo, mengine ya mkakati huo ni kuboresha muundo na utendaji wa ofisi za Bunge ili kuongeza ufanisi na uwajibikaji, pia kuboresha mazingira ya utendaji kazi ya sekretarieti ya Bunge.

Limo pia suala la kukuza na kuimarisha ushiriki wa Bunge kuwafikia wadau mbalimbali kupitia mikutano, machapisho, vyombo vya habari na njia nyingine ya mawasiliano, pamoja na kukuza na kuinua vipaji vya wabunge.

Kwa upande wa serikali, mbali na malengo ya kuboresha maslahi na posho za wabunge kwa kuzingatia mazingira ya utendaji wao wa kazi, na hali ya uchumi, Pinda pia aliyataja malengo mengine kuwa ni kuwezesha Bunge kuwa na ukumbi mzuri wa kisasa unaotosheleza mahitaji, lengo ambalo kwa sasa tayari limekwishatekelezwa.

Kwa mujibu wa Pinda, lengo lingine ni kuanzishwa kwa mfuko maalumu wa Bunge ambao ulianza kutumika mwaka 2007/08, kuwashirikisha katika ziara za nje za viongozi wa kitaifa, lakini pia kuharakisha ujenzi wa ofisi za wabunge katika majimbo yao.

Tangu alipotoa kauli hiyo akiwa kwenye moja ya mikutano ya chama chake cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, amekuwa akiandamwa na wabunge wenzake katika mkutano huu wa 15, wakipinga hoja hiyo kwa madai kuwa inawachonganisha wabunge na jamii.

Hali hiyo ilisababisha Dk. Slaa afikie hatua ya kuzomewa mara kadhaa kila jina lake linapotajwa kwenye vikao vya ndani na nje.

Mbunge huyo, hata hivyo, alisisitiza kwamba anasimama katika hoja zake, ikiwamo ya posho za wabunge kutaka kutazamwa upya.

Alisema ataendelea kuisimamia hoja hiyo kwa sababu anataka kuwapo kwa uwazi katika mishahara wanayolipwa viongozi mbalimbali wakiwamo wabunge.



26 Mar 2009


YAANI HADI INATIA KIZUNGUZUNGU.HEBU SOMA HABARI IFUATAYO KISHA TUSHIRIKIANE KUJIBU MASWALI NILIYOWEKA BAADA YA HABARI HII

Bunge mradi wa ulaji

na Mwandishi Wetu

WAKATI baadhi ya wabunge wakiendelea kulumbana kupitia katika vyombo vya habari kuhusu masuala mbalimbali yanayogusa maslahi ya taifa,imebainikawamekuwa wakichuma mamilioni ya fedha kupitia katika malipo yao halali ya mishahara, posho na fedha nyingine zisizotokana na malipo yao rasmi wanayostahili.

Uchunguzi uliofanywa na Tanzania Daima Jumatano umethibitisha pasipo shaka kwamba, fedha ambazo wabunge wamekuwa wakichuma kwa njia mbalimbali kwa kutumia nafasi zao za uwakilishi, zinaweza zikawa sababu mojawapo muhimu ya kuibuka kwa makundi yanayosigana ndani ya Bunge na hususan miongoni mwa wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Kwa mujibu wa uchunguzi huo, gazeti hili limefikia hatua ya kutilia shaka kwamba, mzozo wa hivi karibuni, kati ya Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe na mwenzake wa Igunga, Rostam Aziz, kwa kiwango kikubwa unakuzwa kutokana na sababu za maslahi binafsi zaidi kuliko madai ya uzalendo na maslahi ya taifa.

Shaka hiyo ya Tanzania Daima Jumatano inatokana na ukweli kwamba, wabunge hao wawili ambao wote wawili ni wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kwa namna moja au nyingine wamepata kuwa au wanayo maslahi ya wazi na ya moja kwa moja katika sekta ya nishati.

Kauli ya hivi karibuni ya mmiliki wa Kampuni ya Dowans Tanzania Ltd, Mohammed Al Adawi, kukiri kwamba aliwekeza katika sekta ya nishati kwa ushawishi wa Rostam sambamba na ile ya kubainisha kuwa kampuni ya mbunge huyo ilipata kuingia katika zabuni ya kutaka kufanya kazi za ujenzi katika mradi wa kuzalisha umeme wa dharura, ni ushahidi wa wazi wa namna mwanasiasa huyo alivyo na maslahi ya moja kwa moja katika sekta ya nishati.

Kama ilivyo kwa Rostam, taarifa za hivi karibuni, zilizothibitishwa na Mwakyembe mwenyewe
kuwa ni mmoja wa wakurugenzi waanzilishi wa Kampuni ya Power Pool East Africa Ltd yenye malengo ya kuzalisha umeme wa upepo kutoka mkoani Singida, ni ushahidi kwamba naye anayo maslahi ya moja kwa moja katika sekta ya nishati.

Kuingia kwa Rostam na Mwakyembe katika sekta ya nishati, kwa kiwango kikubwa kunaonyesha namna wabunge, hususan wale wa CCM walivyojizatiti kutumia fursa zao za kisiasa kujinufaisha kiuchumi, nyuma ya kivuli cha uwekezaji
kupitia sheria ya soko huria.

Kama hiyo haitoshi, mzizi wa fitina kuhusu ukweli kwamba Bunge limekuwa likitumiwa kama kiota cha wanasiasa kuvuna mamilioni, zilithibitishwa mkoani Kilimanjaro juzi na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilibrod Slaa ambaye alisema mshahara anaolipwa mbunge kwa mwezi unafikia sh. milioni saba, hiyo ikiwa mbali na posho nyingine.

Dk. Slaa alitaja kiwango hicho cha mshahara wake wakati akihutubia wakazi wa mji mdogo wa Hedaru, wilayani Same katika mfululizo wa mikutano ya Operesheni Sangara inayoendeshwa na CHADEMA.

Wakati Dk. Slaa akibainisha ukweli huo, uchunguzi wa Tanzania Daima Jumatano umebaini pia kuwa wabunge wanaweza kujikusanyia mamilioni ya shilingi kwa kuhudhuria vikao mbalimbali vya kamati za kudumu za Bunge, semina na safari za ndani na nje ya nchi.

“Ndugu zangu, afadhali msijue mshahara anaolipwa Dk. Slaa kama mbunge, mkijua nalipwa shilingi ngapi mnaweza hata kunipiga mawe,” alisema Dk. Slaa wakati akihutubia mkutano huo na kuitikiwa na sauti za wananchi wakimtaka ataje mshahara wake.

“Mnataka kuujua mshahara wangu, ninalipwa sh milioni saba kwa mwezi. Haki iko wapi? Mimi nalipwa milioni saba, na posho yangu kwa siku ni sh 135,000. Haya ni malipo makubwa mno, fedha ninayopata kwa siku inaweza kuzidi hata mshahara wa mwezi mzima wa polisi. Muulizeni yule polisi pale analipwa shilingi ngapi msikie.

“Juzi nimetaja posho za wabunge na kusema zipunguzwe, lakini Spika wa Bunge analalamika eti naingilia haki na madaraka ya Bunge, sasa leo nasema ninalipwa jumla ya shilingi milioni saba kwa mwezi, acha posho za bungeni. Kweli hii ni haki?” alisema Dk. Slaa.

Alisema kuwa akiwa raia huru, ana haki ya kutaja kwa hiari yake kiwango cha mshahara wake, hasa pale anapoona kuwa kulipwa kiwango hicho ni kutowatendea haki mamilioni ya Watanzania maskini wanaolipa kodi zao wakitegemea serikali iwakomboe kutoka kwenye lindi la umaskini.

Dk. Slaa alisema wabunge wengi wa CCM akiwamo Spika wa Bunge, Samuel Sitta, hawawezi kuunga mkono hoja hiyo kwa vile wapo bungeni kwa ajili ya kutafuta maslahi yao binafsi.

“Wafanyakazi wengi na Watanzania wanateseka kwa mishahara midogo na maisha duni, mamilioni haya ya fedha kwenda mifukoni mwa watu ni aibu kwa nchi na CHADEMA tunasema hapana, fedha hizi ziende katika masuala ya kusaidia jamii na kuongeza mishahara ya walimu, polisi, mahakimu na watendaji wengine,” alisema Dk. Slaa huku akishangiliwa na mamia ya wakazi wa Hedaru waliohudhuria mkutano huo.

Alirejea kauli yake ambayo amekwishakaririwa akiitoa mara kadhaa kuwa Spika Sitta, anapaswa kujiuzulu nyadhifa alizonazo katika CCM, ili awe huru kuliongoza Bunge kwa maslahi ya Watanzania badala ya kushinikizwa na maslahi ya chama chake.

Dk. Slaa alitoa kauli hiyo ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba, kushangazwa na hatua ya Rais Jakaya Kikwete kuendelea kuwateua wabunge wa CCM kuwa wajumbe katika bodi za mashirika ya umma.

Akizungumza wiki iliyopita katika mkutano uliondaliwa na Jukwaa la Wahariri, Prof. Lipumba alisema, hatua hiyo ya Rais Kikwete mbali na kuwahalalishia wabunge ulaji, inazoretesha utendaji wao katika kuyasimamia ipasavyo mashirika hayo ambayo utendaji wake wa kazi unapaswa kusimamiwa na taasisi hiyo muhimu ya dola.

Wakati hali ikiwa hivyo katika mishahara ya wabunge, Tanzania Daima Jumatano limebaini kuwa wabunge wamekuwa wakilipwa mamilioni ya fedha wakati wanapokutana na baadhi ya taasisi za umma ambazo kamati za Bunge zinazisimamia shughuli zake.

Taarifa za hivi karibuni ambazo gazeti hili limezipata zinaonyesha kuwa, Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (Tanesco) lilitumia jumla ya sh milioni 16 kwa ajili ya kulipa posho na usafiri wabunge kutoka majimboni mwao, pamoja na makatibu wawili waliohudhuria kikao cha dharura kilichowakutanisha Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, Kamati ya Bunge ya Kamati ya Nishati na Tanesco.

Taarifa kutoka ndani ya ofisi ya Bunge, zinaeleza kuwa licha shirika hilo kuwa na hali mbaya kifedha, lililazimika kuingia gharama hizo baada ya ofisi ya Bunge kuitaka Wizara ya Nishati na Madini kuwagharamia wabunge hao kwa sababu Bunge halikuwa na fedha katika kikao chake cha Desemba mwaka jana.

Katika hali ya kushangaza, habari za wanakamati hao wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini kulipwa posho na gharama zao nyingine na Tanesco wakati wakihudhuria kikao hicho zimewafanya wabunge, Katibu wa Bunge na Spika kutofautiana.

Spika Sitta, jana alilithibitishia Tanzania Daima Jumatano kuwa, wajumbe wa Kamati ya Nishati na Madini walilipwa posho na gharama za usafiri kwa sababu Bunge halikuwa na fedha wakati Waziri wa Nishati na Madini, Ngeleja alipotaka kukutana na kamati hiyo ili kupata ushauri.

Lolote linaweza kutokea kutegemea na nani amewaita, kama wameitwa kusaidia jambo ambalo halimo kwenye utaratibu wa Bunge wanalipwa na aliyewaita. Na katika hili ilikuwa hivyo, ninalifahamu vizuri sana, waziri aliomba kukutana na kamati wakati muda wa Bunge ukiwa umepita, Katibu wa Bunge alimuandikia akimueleza kuwa Bunge halina fedha ila kama wizara yake inaweza, basi ilipe posho na gharama za wabunge hao kusafiri hadi Dar ili aweze kukutana
nao.

“Hivyo ndivyo ilivyokuwa, sasa mimi sijui kama ililipa wizara, Tanesco au nani, la msingi hawakulipwa na Bunge, na kama wabunge ambao ni wanakamati wanakanusha hili, ni watu wa ajabu kwa sababu sijui wanaogopa nini kueleza ukweli,” alisema Spika.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli, William Shellukindo (CCM), alipozungumza na gazeti hili kupitia simu yake ya kiganjani, alikana kupokea senti tano kutoka Tanesco wakati wakihudhuria kikao hicho na kueleza kuwa, kamati yake iliitwa na Spika na malipo yalifanywa na Bunge.

Hatukumuomba mtu hela, sielewi lolote, sisi tuliitwa na Spika na malipo yetu yalishughulikiwa na Bunge,” alisema Shellukindo na kusisitiza kuwa, kanuni za Bunge zinaeleza wazi kuwa wabunge wanapokuwa katika vikao vilivyo na baraka za Spika, iwe bungeni au nje ya Bunge, posho na gharama zao nyingine zinalipwa na Bunge na si taasisi nyingine yoyote.

Alipoulizwa kuhusu hilo, Waziri wa Nishati na Madini, Ngeleja alieleza kuwa Tanesco ililazimika kulipa gharama hizo kwa wabunge licha ya kikao hicho kufanyika kwa ridhaa ya Spika, baada ya Bunge kueleza kuwa halikuwa na fedha kwa ajili ya kulipa posho na gharama za usafiri kwa wabunge.

Wakati wanasiasa hao wakivutana kuhusu mfumo huo wa ulipaji posho, Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashillilah, alipotafutwa na Tanzania Daima Jumatano
ili kutoa ufafanuzi wa jambo hilo, alieleza kuwa wabunge wote wanapokuwa katika shughuli za Bunge, ikiwamo vikao vya kamati za kudumu za Bunge, posho na gharama
zao nyingine zinalipwa na ofisi ya Bunge, na si vinginevyo.

Alisisitiza kuwa, Tanesco haiwezi kuliwalipa posho wabunge wakiwa katika kikao cha kamati ya kudumu ya bunge na kuongeza kuwa katika utumishi wake ndani ya taasisi hiyo, hajawahi kuona fedha za Tanesco zikitolewa kwa ajili ya kulipa posho wa wabunge.

CHANZO: Tanzania Daima

MHESHIMIWA SPIKA ANASEMA WABUNGE WA KAMATI HUSIKA WALILIPWA NA TANESCO.WAZIRI NGELEJA NAE ANATHIBITISHA HILO.MBUNGE SHULIKINDO ANAKATAA TAARIFA KUWA WALILIPWA JAPO SENTI TANO,NA KATIBU WA BUNGE ANAWEKA BAYANA TARATIBU ZA MALIPO KWA WANAKAMATI ZA BUNGE.
JE NANI MKWELI NA NANI ANAONGOPA?
JE ANAYEONGOPA ANAFANYA HIVYO KWA SABABU GANI?
SHERIA NA TARATIBU ZINASEMAJE KUHUSU KUONGOPA KWA AINA HIYO?
NA ADHABU GANI INATOLEWA KWA KOSA LA AINA HIYO?

10 Sept 2008

Pamoja na kuchukua sabbatical leave ya lazima katika uandishi wa makala katika gazeti la Raia Mwema,blogu hii itaendelea kuwaletea kinachojiri kila wiki katika jarida hilo mahiri huko nyumbani.Miongoni mwa habari zilizochukua uzito wa juu katika toleo la wiki hii ni pamoja na kauli ya Spika wa Bunge la Muungano,Samuel Sitta,kwamba amejiandaa vya kutosha kufuatia taarifa kwamba watuhumiwa wa ufisadi wameingiza sumu huko Bongo kwa lengo la kuwadhuru Sitta na Mbunge wa Kyela,Dr Harrison Mwakyembe.Sidhani kama inahitaji kujumlisha mbili na mbili kupata jawaba as to akina nani watakuwa the usual suspects wa unyama wa aina hii.Zaidi BONYEZA HAPA kusoma habari hiyo na nyingine motomoto.

5 Mar 2008

Makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inatoa lawama kwa wale ambao baada ya kutajwa kwenye Ripoti ya "Tume ya Mwakyembe" wamekuja na ngonjera za ukabila,eti kuna mpango wa ethnic cleaning dhidi ya kabila flani.Pia makala hiyo inatoa changamoto kwa Bunge kutumia kasi ile ile ya "mwewe" (kama iliyomshukia Zitto Kabwe) kuwashukia wale wote wanaoikejeli Ripoti hiyo ilhali hilo ni kosa kisheria.Kadhalika,wito unatolewa katika makala hiyo kuharakisha uchukuzi wa hatua pindi yanapoibuka mambo yanayohitaji actions dhidi ya wahusika.Sambamba na hilo ni changamoto kwa wansheria "kununua kesi" dhidi ya mafisadi na vikundi vya kijamii kutoishia kulalamika tu bali kuchukua hatua dhidi ya mafisadi.Makala inamalizika kwa wito kwa CCM kutodhani taarifa kwamba kuna kundi la "Agenda 21" ni hadithi za kuvuta muda tu.Onyo la makala kwa chama hicho ni kwamba wakizembea,basi itakuwa kilio pindi maji yatakapozidi unga usiku wa manane wakati maduka yote yashafungwa.Pamoja na habari za makala nyingine zilizofanyiwa utafiti wa kina,soma makala yangu hiyo kwa KUBONYEZA HAPA

6 Feb 2008

Makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema iliandaliwa kabla ya "kimuhemuhe" kilichoanza leo huko Bungeni.Kwa kifupi,makala hiyo inaelezea namna siasa inavyoboa (au ni wanasiasa ndio wanaoboa?) na kutoa mfano wa namna baadhi ya wahafidhina katika chama cha Republicans "wanavyotiana vidole kwenye macho" kufuatia mwenendo mzuri wa harakati za Seneta John McCain kuingia White House kwa tiketi ya chama hicho.

Pia makala hiyo inagusia vimbwanga vya siasa za huko nyumbani kwa kuonyesha mshangao wa namna Spika Samuel Sitta "alivyoruka kimanga" kwamba aliwahi kuweka vikwazo dhidi ya harakati za Dr Slaa kufichua ufisadi wa BoT.Pia makala inazungumzia "utoto" wa CCM (licha ya kuwa majuzi ilitimiza miaka 31) pale inapodai kuwa yenyewe ndiyo iliyoibua hoja ya ufisadi.Hivi Chama hicho kimeishiwa busara namna hiyo hadi kusahau kwamba sababu ya mawaziri wake kuzomewa mikoani ilikuwa ni reactions za wananchi dhidi ya jitihada za vigogo hao kuua hoja za wapinzani kuhusu ufisadi!!!?
Lakini kali zaidi ni pale Spika wa Bunge alipotoa maelekezo kwa Naibu wake kwamba "asikurupuke" kuendesha mijadala ya Richmond na BoT/EPA hadi yeye (Spika) ataporejea kutoka ziarani Marekani.Angalau sasa tunaelewa kwanini Spika alitaka kutumia mbinu za kupoteza muda katika mjadala wa Richmond,kwani RIPOTI YA KAMATI TEULE YA BUNGE KUHUSU MKATABA KATI YA SERIKALI NA KAMPUNI HIYO (BONYEZA HAPA KUISOMA)imemu-implicate Spika kwa namna flani (kwa vile Kituo cha Uwekezaji-IPC-kikiwa chini ya uongozi wa Sitta,kiliiruhusu Richmond iwekeze pasipo kuchunguza uwezo halisi au uwepo wa kampuni hiyo).

Pamoja na makala nyingine zilizokwenda shule ndani ya gazeti hilo,bingirika na makala yangu hiyo kwa KUBONYEZA HAPA.


13 Jul 2007

Asalam aleykum,

Baada ya matukio ya hivi karibuni yaliyotuweka matumbo moto kufuatiwa mahayawani flani kuamua kuendesha kampeni yao ya kishetani ya kutaka kulipua mabomu huko London na hapo Glasgow (Waskotishi bado hawaamini kuwa ugaidi umeingia kwenye ardhi yao) sio wazo baya kuanza makala hii kwa habari “nyepesi nyepesi.” Gazeti la Daily Mail la hapa liliripoti hivi karibuni kuhusu matokeo ya utafiti yaliyoonyesha kuwa wanaume wenye aibu wana nafasi kubwa ya kupata magonjwa ya moyo kuliko wale wasio na aibu!Hizi tafiti nyingine…we acha tu.Kwa mujibu wa gazeti hilo,utafiti huo ulifanyika kwa kipindi cha miaka 30 uliwahusisha maelfu ya wanaume ambapo watafiti kutoka chuo kikuu cha Northwestern cha Chicago,Marekani walipokuwa wanafanya ufuatiliaji wa wawaliowahoji kwenye utafiti huo walibaini kuwa asilimia 60 kati yao (waliohojiwa) walikuwa wameshafariki,huku chanzo kikuu cha vifo kikiwa “heart attack” (nadhani kwa Kiswahili sahihi ni msongo wa moyo).Mambo hayo!

Na ukisikia duniani kuna mambo usidhani ni utani.Mzembe mmoja amekamatwa huko New Hampshire (Manchester) baada ya kushindikana kwa jaribio lake la kutaka kufanya uporaji benki huku akiwa amejivika matawi ya miti kama “camouflage” (kificho) yake.Jamaa huyo,James Coldwell,aliingia kwenye tawi la benki ya ushirika ya Citizens,huku akiwa amejivika majani na kuwatisha wahudumu wa benki hiyo kabla ya kufanikiwa kuondoka na kitita cha fedha,lakini alinaswa na polisi muda mfupi baadaye kwani triki yake ya “uninja wa majani” haikumsaidia kwa vile majani hayo hayakufunika sura yake,na wanausalama waliweza kuitambua vizuri kwenye CCTV.

Jumuiya ya Ulaya (EU) nayo ilijikuta kwenye wakati mgumu hivi karibuni baada ya kutoa filamu fupi kwa ajili ya promosheni ya kuhamasisha Jumuiya hiyo ambapo wahusika kwenye filamu hiyo ya sekunde 44 yenye jina “Let’s Come Together” walikuwa wakifanya “ngono nyepesi” (soft porn).Wapinzani wa wazo la Muungano wa nchi za Ulaya waliishambulia EU kwa kupoteza fedha za walipa kodi kwa kutengeneza filamu hiyo waliyoiona kuwa ni mwendelezo wa ubabaishaji wa Jumuiya hiyo.Nilipomtumia rafiki yangu flani habari hiyo kutoka gazetini alitania kwa kusema labda na sie tunahitaji “kampeni chafu” kama hiyo ya EU “kuuza” wazo la Muungano wa Afrika Mashariki ambao unaelekea kuwakera wadau wengi.

Nae mwanamama Amy Beth Ballamura amaepigwa marufuku kutia mguu kwenye pwani yoyote ya Uingereza baada ya kufanya majaribio zaidi ya 50 ya kujiua kwa kurusha baharini.Miongoni mwa sababu zilizopelekea kuchukuliwa kwa hatua ya kumdibiti mwanamama huyo ni pamoja na kuzitia huduma ya uokoji (emergency services) gharama ya zaidi ya pauni milioni 1 (zaidi ya shilingi bilioni mbili za huko nyumbani) kila wanapoitwa kwenda kumuokoa.Lakini pamoja na “tamaa” yake ya kujitoa roho,askari mmoja aliambulia tuzo ya ushujaa mwaka 2003 baada ya kusikia kelele za kuomba msaada kutoka baharini na kuamua kujitosa majini kufuata kelele hizo,ambapo alifanikiwa kumuokoa mwanamama huyo mwenye umri wa miaka 44.Cha kushangaza ni kwamba kama kweli alikuwa na nia ya kujitoa uhai sasa hizo kelele za kuomba msaada zilikuwa za nini?

Enewei,baada ya "nyepesi nyepesi" hizo (zote ni habari za kweli na wala sio kuwa “nawapiga fiksi” wasomaji wangu wapendwa) sasa tuangalie mambo ya muhimu zaidi huko nyumbani.Kwanza niseme siafikiani na hoja za Waziri wa Sheria Mama Nagu kwamba Bunge halipaswi kufanya kazi ya kupitia mikataba kabla ya kutiwa saini ili libaki na uhalali wake wa kuiwajibisha Serikali kwa mujibu wa dhamana ya mgawanyo wa mamlaka, kuchunguzana na kuwajibishana.Siafikiani naye kwa sababu hoja za baadhi ya wabunge kuwa mikataba hiyo ifikishwe kwao kabla ya kusainiwa zilizingatia ukweli kwamba kuna mapungufu makubwa yanayoendelea katika suala zima la kusaini mikataba mbalimbali.Mantiki nyepesi (simple logic) inaweza kutueleza kwamba maslahi ya nchi ni muhimu zaidi ya huo mgawanyiko wa madaraka.Hivi kwa mfano wazo la mikataba kuletwa bungeni lingekubaliwa,halafu nchi inufaike kwa kuingia mikataba yenye maslahi kwa Taifa,tatizo linakuwa wapi?Hivi kipi bora,kulinda mgawanyiko wa madaraka huku mikataba ya ajabu ajabu ikiendelea kuwepo au “kupindisha sheria” kwa kuileta mikataba hiyo bungeni kabla haijasainiwa halafu nchi ikanufaika nayo?

Pia nimesoma kwenye gazeti moja la huko nyumbani kwamba lile tishio la wafugaji huko wilayani Kilombero limerejea tena.Nitamke bayana kuwa hili linanihusu binafsi kwa vile mie ni “mwana wa pakaya” naetokea mitaa ya huko.Hawa wafugaji ni wakorofi,watovu wa nidhamu na wavunja sheria wakubwa.Maagizo kadhaa yameshatolewa kuwataka waheshimu sheria za nchi lakini wameamua kuweka pamba masikio.Mamlaka husika zinapaswa kuliangalia suala hili kwa makini zaidi kwani wanachofanya wafugaji hao sio tu kinahatarisha amani (mifugo yao inakula mazao ya wakulima,na hilo pekee linatosha kuzusha ugomvi) lakini pia hawawatakii mema wakulima kwani kwa kuswaga mifugo yao kwenye mashamba wanamaanisha kuwa wanataka wakulima hao wakose chakula na hela wanazojipatia kwa kuuza akiba ya mavuno yao.Hili ni bomu la wakati (time bomb) kwani japo hakuna bondia wa Kindamba (kama yupo basi samahani kwani sijamsikia) lakini hiyo haimaanishi kuwa mtu atakaeswaga mifugo yake kwenye mashamba ataachwa afanye anavyotaka.Hapo itakuwa kuchukua sheria mkononi,na japo mie ni mpinzani mkubwa wa kuchukua sheria mkononi,natambua dhahiri kuwa mtu “anapoletewa za kuleta” anaweza kabisa kuiweka sheria kando,hususan pale haki yake inapopuuzwa kwa makusudi.Kwa vile mkoa wa Morogoro umebahatika kuwa na RC ambaye ni “mjeshi” mstaafu basi hapana shaka Brigedia Jenerali Kalembo huyo atatumia “mbinu za medani” kuwadhibiti wafugaji hao wenye uhaba wa nidhamu.

Kikao cha Bunge kinaelekea ukingoni na miongoni mwa hoja nilizovutiwa nazo ni ile ya Mheshimiwa Shabiby (wa Gairo) kuhusu ujanja unaofanywa na baadhi ya wamiliki wa mabasi makubwa ya abiria.Alieleza kuwa mengi ya mabasi yanayotumika sasa yamefanyiwa “usanii” kwa kuweka mabodi mapya kwenye “chasis” na injini za malori au za kale.Kuna jina moja tu linalowafaa “wasanii” hawa nalo ni “WAUAJI.” Wanathamini sana kukwepa gharama za kununua mabasi mapya lakini hawajali hata chembe madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na vitendo vyao vya “kuunda mabasi feki.” Kwa upande mwingine tuseme bila kuonekana aibu kwamba mabasi ya namna hiyo yanafahamika hata bila kuwa na ujuzi wa umakanika kwani ulifika pale stendi ya mabasi Ubungo unaweza kukutana na basi ambalo linaonekana dhahiri kuwa bodi yake “imepachikwa” sehemu isiyostahili.Trafiki yeyote aliyehitimu mafunzo yake vyema na mwenye uchungu na maisha ya Watanzania wenzie hawezi kuliruhusu basi “lililovimba mbavuni utadhani lina ujauzito” liendelee na safari,na mabasi ya namna hiyo yako mengi tu.Wanaofanya hivyo wanajua bayana kuwa wanavunja sheria na kuhatarisha maisha ya abiria wao lakini hawajali kwa vile hakuna aliyechukuliwa sheria hadi leo.Si ajabu tukisikia kuwa baadhi ya mabasi hayo yanatumia injini za matrekta au hata za mashine za kusaga….(nashindwa kumalizia,nimekabwa na kicheko japo jambo hili sio la kuchekesha hata chembe.)

Mwisho,wakati Gavana wetu keshatamka bayana kuwa hatojiuzulu (utadhani alijichagua mwenyewe kwenye posti hiyo),sie wapenzi wa Simba tunajipoza kwa kusherehekea ubingwa wetu ambao kidogo umetibuliwa na hizi habari za viongozi kugombea mapato ya mechi huko Morogoro.Wito kwa watani wetu wa jadi Yanga ni huu:Micho akirudi (kama kweli atarudi) ashauriwe kukutana na Twalib Hilal apewe darasa kuwa ukocha sio sawa na ukatibu mwenezi wa klabu: ukocha ni vitendo vingi maneno machache lakini Mserbia Micho kila siku “anachonga” kuhusu hili au lile lakini matunda ya kazi yake kwenye dimba ni haba.Enewei,asilaumiwe sana kwani alishawahi kusema kuwa wachezaji wake hawafundishiki,na katika mechi ya juzi anaweza kuongeza sababu kuwa “lile tumbo la kuendesha” limechangia kukosa ushindi.

Alamsiki






Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.