Showing posts with label Balozi Peter Kallaghe. Show all posts
Showing posts with label Balozi Peter Kallaghe. Show all posts

27 Nov 2013

Eneo la Canary wharf london ambalo Balozi Peter Kallaghe alifanya  ziara ya kutembelea kampuni ya Kitanzania, Meru Services LTD. 
Tarehe 23 Novemba 2013, Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Peter Kallaghe alifanya ziara ya kutembelea kampuni ya Meru Services inayomilikiwa na watanzania waishio jijini London, Uingereza.

Katika ziara hiyo iliyofanyika katika kitovu cha sekta ya biashara na fedha nchini Uingereza, Canary Wharf , Balozi Kallaghe alijionea huduma zinazotolewa  na kampuni hiyo katika Benki ya Kimataifa ya Credit Suisse. Pia alikutana na kuzungumza na baadhi ya watanzania wanaofanya kazi za aina mbalimbali za kuhudumia Benki hiyo .
Mkurugenzi na mmiliki wa kampuni ya Meru Services LTD, Bw. Dullah Meru akiongea machache na balozi Peter Kallaghe
Balozi Kallaghe alifurahishwa na taarifa aliyopewa kuwa kampuni hiyo imekuwa ikitoa huduma katika Benki ya Credit Suisse kwa bidii ,ujuzi na uaminifu mkubwa kwa takriban miaka 15. Aidha imekuwa ikitoa fursa za ajira kwa makundi mbalimbali ya watanzania wakiwemo wanafunzi waishio jijini London.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Axis Europe PLC Bw Dean Richards akimuelezea balozi Kallaghe Umuhimu kuwepo kwa kampuni ya Meru Servives katika eneo hilo la canary wharf.
Katika nasaha zake, Balozi Kallaghe aliitaka kampuni ya Meru Services kutambua kuwa kuaminika kufanya kazi katika kitovu cha sekta ya biashara na fedha nchini Uingereza si jambo dogo na kuisihi kampuni hiyo iendelee kuitunza heshima hiyo kwa niaba ya watanzania wote. 

Balozi pia alitoa changamoto kwa  kampuni hiyo na watanzania waishio nchini Uingereza kutumia ujuzi na uzoefu wanaopata ughaibuni kama mtaji wa kuwekeza katika sekta ya huduma inayozidi kukuwa nchini Tanzania.

Balozi alihitimisha ziara yake kwa kuahidi kuwa ataendelea kushirikiana na kampuni za kitanzania na vijana wa kitanzania wanaoishi Uingereza katika kuwaunganisha na fursa za kiuchumi zinazojitokeza nchini Tanzania wakati huu.
Balozi Kallaghe na Afisa ubalozi Allen Kuzilwa wakifuatila jambo kutoka kwa Dean
Ahmed na Dullah Meru Mkurugenzi mmiliki wa Meru Services LTD wakisikiliza kwa makini
Said Surur akimuelezea Balozi jambo wakati wa mkutano pembeni yake kulia ni Allen Kuzilwa Afisa Ubalozi
Balozi katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanayakzi wa Meru Services Ltd

PICHANI CHINI NI BAADHI YA KAZI ZINAZOFANYA NA MERU SERVICES LTD. NA  ZILIZO KAMILIKA




Mgahawa wa wafanyakazi uliofanyiwa ukarabati na kampuni ya Meru Services 

Vijana wakiwa kazini kuweka nafasi ya kwa ajili ya wafanyakazi wapya 210 wanao hamia Credit Suisse London. 
Huu ndo muonekano baada ya kazi kukamilika .
Picha za kushoto ni kabla ya ukarabati na kulia ni baada ya ukarabati
Picha za kushoto ni kabla ya ukarabati na kulia ni baada ya ukarabati
Picha za kushoto ni kabla ya ukarabati na kulia ni baada ya ukarabati



11 Feb 2013



 Mh Balozi wa Tanzania Peter Kallaghe aliandaa hafla fupi ya chakula cha jioni kwa ajili ya kumpongeza na kumkaribisha Tanzania Balozi mpya wa Uingereza nchini Tanzania Dianna Melrose tarehe 31.1.2012

27 May 2012

 Mh. Balozi Peter Kallaghe akiwasilisha barua ya utambulisho kwa Rais wa Ireland Michael Higgins


 Mh. Balozi Peter Kallaghe katika picha ya pamoja  na Rais wa Ireland Michael Higgins mara baada ya kuwasilisha barua ya utambulisho

 Mh. Balozi Peter Kallaghe na mke wake Mama Balozi Joyce Kallaghe katika picha ya pamoja  na Rais wa Ireland Michael Higgins mara baada ya kuwasilisha barua ya utambulisho


Afisa ubalozi Amos Msanjila na Mh. Balozi Peter Kallaghe katika picha ya pamoja na Rais wa Ireland Michael Higgins mara baada ya kuwasilisha barua ya utambulisho.




 Mh. Balozi Peter Kallaghe akiwa na baadhi ya watanzania waishio Dublin, 
Ireland




Baadhi ya watanzania waishio Dublin wakichagua chakula kutoka kwenye menu huku maongezi yakiendelea.




Mh. Balozi Peter Kallaghe akikabidhiwa zawadi na watanzania waishio Dublin.




 Mh. Peter Kallaghe, mama Balozi Joyce Kallaghe, Afisa ubalozi Amos Msanjila wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watanzania waishio Dublin.


Picha na maelezo kwa hisani ya Jestina George Blog

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.