Showing posts with label CAN 2008. Show all posts
Showing posts with label CAN 2008. Show all posts

23 Jan 2008

Rafiki yangu mmoja amenitumia barua-pepe muda mfupi uliopita baada ya kusoma makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema.Hakuwa na pongezi wala malalamiko bali alidai kwamba wakati anasoma makala hiyo alijiskia kama anaongea nami uso kwa uso japo tuko umbali wa maili elfu kadhaa.Ni kweli,napoandika makala huwa najitahidi kadri ya uwezo wangu kuiwasilishalisha kwa kutumia staili ya mazungumzo (conversational style).Lakini sio mazungumzo kama ndani ya semina-elekezi,warsha,kongamano au semina bali yale yanayoweza kuwa yanafanyika mahala ambapo "tunaongea kwa kijinafasi" (comfortably).

Tukiachana na hilo,makala yangu ndani ya toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inagusia michuano ya soka ya Mataifa ya Afrika huko Ghana,na kuielezea kwamba ni moja ya habari njema chache kutoka bara hilo,hasa kwa vile kwa takriban mwezi sasa habari zinazotawala kutoka huko ni kuhusu vurugu zinazoendelea Kenya zilizotokana na matokeo ya uchaguzi mkuu nchini humo.Kwa kutumia mfano hai,makala hii pia inaelezea ugumu anaoweza kukabiliwa nao Mtanzania pindi akidadisiwa chanzo cha umasikini wa nchi yetu,kabla ya kuwachambua mafisadi wa fedha na wale wa mawazo.Pamoja na habari na makala nyingine zilizokwenda shule katika jarida hilo la Raia Mwema,bingirika na makala hiyo kwa KUBONYEZA HAPA.

Ukimaliza kusoma makala hiyo,unaweza kuangalia clips hizi za versions mbili za Jesus Walks ya Kanye West.Naamini nasi tunahitaji nguvu za kiroho kukomesha ufisadi huko nyumbani.



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.