Showing posts with label Carrie. Show all posts
Showing posts with label Carrie. Show all posts

7 Feb 2017

Related image

Mara "Makonda hili, Wema lile," mara "Mapapa, mara vidagaa." Habari kama hizo zinaumiza vichwa. Hata hivyo, kuna habari tamu, na zisizoumiza kichwa,  kwa wapenzi wa mifululizo (series) ya tamthiliya za kishushushu. Hapa twaongelea HOMELAND na 24. Zimerejea hewani kwa kasi mpya, ari mpya na nguvu mpya. Haha!

Season 6 ya Homeland imeshafika episode ya tatu sasa, na kila episode ni nzuri mno. Yaani hizo dakika 55 za kila episode ni kama zinayeyuka tu. 
Sekou
Katika episode ya kwanza, Sekou Bah, kijana Mmarekani Mweusi Muislam, ana-post video mtandaoni baada ya kurekodi katika maeneo ambayo siku za nyuma kulitokea matukio ya kigaidi. Baadaye anakamatwa na shushushu wa FBI Ray Collins na kufunguliwa mashtaka ya ugaidi.

Carrie, sasa ni mfanyakazi katika shirika lisilo la kutengeneza faida (not-for-profit organisation) linaloshughulikia kuwatetea Wamarekani Weusi walio Waislam. Anakutana na Sekou ili kuwa wakili wake.

Pia Carrie anamtembelea Quinn ambaye ni kama amewehuka kutokana na kuwekwa chumba chenye gesi ya sumu, katika hitimisho la season 5. 
Saul na Dar Adal ni mabosi wa ushushushu, na wanampa taarifa Rais mteule, mwanamama Elizabeth Kaine. Baada ya briefing hiyo, Dar anaelezwa hofu yake kuhuthu uimara wa Rais Mteule, na baadaye anakutana na jasusi wa Mossad, Tovah Rivlin.

Katika Episode ya Pili, Carrie na Reda, profesa wa sheria anayefanya kazi na Carrie, wanamuuliza Sekou kuhusu dola 5,000 zilizokutwa na FBI chini ya kitanda chake. FBI wanadai fedha hizo ni kwa ajili ya Sekou kuzipeleka Nigeria kuwasaidia Boko Haram.
Reda na Carrie
Carrie anakuja kubaini kuwa fedha hizo zilitolewa na FBI kwa rafiki wa Sekou aitwaye Saad, ambaye ni mtoa habari wa FBI, ili kumpeleleza zaidi Sekou. Carrie anamvaa Saad, ambaye baadaye anaripoti kwa FBI kuwa ametishiwa na Carrie, na hiyo inatishia uwezekano wa Sekou kupew adhabu nafuu.

Dar Adal akutana na Rais Mteule Keane kumhabarisha kuhusu programu ya nyukilia ya Iran kwa kushirikiana na Korea ya Kaskazini. Saul amtembelea Carrie na kumtuhumu kuwa ni mshauri wa siri wa Rais Mteule Keane. Dar apata picha za siri zinazomwonyesha Carrie akiingia Ikulu kwa siri.

Katika episode ya tatu, Carrie anamjulisha Sekou kuwa (yeye Carrie) 'amelikoroga' kwa kuongea na Saad, na sasa FBI wanataka kudai kifungo cha miaka 15 kwa Sekou badala ya miaka 7. Sekou anaghadhibika, anamtimua Carrie, ambaye anajisikia vibaya. Hata hivyo, anafanikiwa kupata rekodi ya siri ya maongezi kati ya Conlin wa FBI na Saad, na anaitumia kama turufu yake.
Saul
Saul anafika Abu Dhabi ili kumhoji Farhad Nafisi, 'mtu wa mafedha' wa Iran. Nafisi anajiingiza mkenge hadi kukamatwa baada ya kumtembelea kahaba ambaye kumbe ni afisa wa Mossad. Mahojiano hayazai matunda, japo Nafisi anapewa kibano kikali. Baadaye Saul anaripoti kwa Dar kuwa hakupata lolote, lakini Dar anatoa taarifa tofauti kwa Rais Mteule, kitu ambacho baadaye Carrie anamfahamisha Rais Mteule

Hiyo ndo HOMELAND SEASON 6 ilipofikia hadi sasa. Episode 4 itarushwa wiki hii. Nitakueleza hapo chini jinsi unavyoweza kuona tamthiliya hii na nyinginezo bure. 

Sintoongelea 24 kwa leo kwa sababu ndo kwanza natarajia kuangalia episode ya kwanza kati ya mbili zilizokwishaoonyeshwa. Hata hivyo, nimesoma 'reviews' zake, zote zinaisifia kwa kiwango cha juu. Ila tu ni kwamba Jack Bauer hayupo, na badala yake ni staa mweusi Corey Hawkins, aliye-act kama Dr Dre kwenye filamu ya Straight Outta Compton.



Sasa, ukitaka kuangalia Homeland, 24 na series yoyote ile, au filamu, au mechi za soka kimataifa, unahitaji kitu kinaitwa KODI. Hiki kinageuza runinga ya kawaida kuwa 'smart TV.' Kama hujawahi kufahamu kuhusu 'smart tv,' basi kwa kifupi ni zenye uwezo wa kufanya kazi kama kompyuta, ikiwa ni pamoja na kutumia internet kwenye TV hizo.

Maelezo ya jinsi ya kutumia KODI yapo HAPA. Nitaelezea kwa kirefu kuhusu kifaa hicho, kwenye mada zangu kila wikiendi kupitia #ElimikaWikiendi

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.