Showing posts with label DAR ES SALAAM. Show all posts
Showing posts with label DAR ES SALAAM. Show all posts

28 Mar 2009

(Photo credit:JIJI LA DAR)

Mayor threatens legal action against street name changers

SEBASTIAN MRINDOKO
Dar es Salaam

A TOP local government official in Dar es Salaam has roundly rebuked the ongoing trend of people clandestinely changing street names in the city without following proper channels, including getting the blessing of the City Fathers.

According to the Mayor of the Ilala Municipality, Abuu Jumaa, legal action will certainly be taken against such people once sufficient proof is obtained.

Referring specifically to a query by THISDAY on the name-change applied to one of the city’s most historically famous thoroughfares Kisutu Street, now apparently going by the name of ’PRAMUKH SWAMI’, Mayor Jumaa stated unequivocally:

’’My office has never received an official application to change the Kisutu Street name into an Indian name. Therefore, such an action is an insubordination to the city authority.’’

The mayor’s statement is a direct contradiction of that made last year by the former deputy mayor of the same Ilala Municipality, Mohamed Yakoub, who asserted in an interview with THISDAY that the Kisutu Street name-change had been given a formal stamp of approval.

’’All the (Ilala) municipality legal procedures were properly followed in changing the name of not only Kisutu Street, but also some other streets around the city centre,’’ Yakoub said.

But according to current mayor Jumaa, there are no records whatsoever showing the change of the traditional Kisutu name to ’PRAMUKH SWAMI.’

THISDAY last year ran a series of articles on the increasing trend of various streets within Dar es Salaam’s central business district, suddenly acquiring bizarre-sounding new names in highly mysterious circumstances.

It has been noted that skepticism is on the rise amongst members of the general public over the supposed ’secrecy’ shrouding the whole exercise, with open suggestions that corruption at certain local government levels may be involved.

The Dar es Salaam City Director, Bakari Kingobi, has conceded in the past that such street name changes could very easily cause confusion particularly for tourists who may be trying to find their way around the metropolis using officially-approved city maps.

According to Kingobi, only the city authorities have the mandate to administer such street name changes.

’’There is only one city authority - not two - responsible for administering such name-changes to the city streets. Anyone who tries to do so without informing this city authority, is violating the law and is liable for prosecution,’’ he said.

Speaking to THISDAY yesterday, Ilala Municipality mayor Jumaa said it amounted to sacrilege for anyone to change a street name on the basis of racial, tribal, or religious beliefs.

’’There are some basic criteria used to endorse suggestions for street name changes. Bias of any sort is not one of them,’’ he asserted.

He also said streets with traditionally famous names like Kisutu should be left alone, while anyone wanting to recommend a street name to suit their own needs should look for streets with no names at all � of which apparently there are still many.

According to Jumaa, the municipal authorities will seek explanations from the local government authorities regarding the Kisutu Street name-change in particular.

Any official found to have been responsible for wrongdoing in the whole episode will be taken to task through legal channels, he added.

SOURCE: ThisDay

22 Sept 2008

Kwa Dar es Salaam,na pengine kwingineko pia,sijui utaenda baa gani ambayo hawajafungulia muziki kwa sauti ya juu.Kumbe kuna maelezo ya kisayansi kwanini wenye baa wanapendelea muziki full blast.BONYEZA HAPA kupata undani zaidi.

26 Dec 2007

MAKALA HII ILIPASWA KUTOKA KATIKA TOLEO LA WIKI HII LA GAZETI LA RAIA MWEMA LAKINI HAIKUTOKA KWA SABABU ZILIZO NJE YA UWEZO WANGU.

Majuzi niliongea kwa simu na rafiki zangu wawili wa siku nyingi.Mmoja ni “mjasiriamali” anayeishi Dar es Salaam (hakasiriki ninapomtania kwamba yeye ni “misheni tauni”).Mwingine yuko Ifakara,mji niliozaliwa.Niliongea na rafiki zangu hawa kuwatakia heri na Baraka za mwaka mpya 2008.

Nikiri kwamba mara nyingi huwa namkwepa rafiki yangu wa Ifakara kutokana na mlolongo wa malalamiko anayokuwa nayo kila ninapoongea naye.Na majuzi haikuwa tofauti.Alidai mwaka mpya hauna maana yoyote kwake kwani,kwanza,kinachobadilika ni tarakimu moja tu ya mwisho katika mwaka,yaani badala ya 7 inakuwa 8.Pili,alidai kwamba jitihada zake za zamani za kujiwekea malengo ya mwaka mpya yamekuwa kazi bure kutokana na kile anachokiita “nguvu za giza”,na katika miaka ya hivi karibuni amesitisha utaratibu huo wa kujiwekea malengo ya mwaka ujao.Alinifafanulia kwamba “nguvu za giza” anazozizungumzia sio zile zinazotajwa katika Biblia bali genge la mafisadi ambao wanafanya kila linalowezekana kuhakikisha mwaka mpya unaendelea kuwa mchungu kama uliotangulia.

Huyu bwana alikuwa miongoni mwa wanafunzi waliobahatika kuendelea na masomo baada ya kuhitimu shule ya msingi.Pia licha ya kuyapenda masomo ya sayansi,alikuwa anayamudu kweli.Na uthibitisho katika hilo ni namna alivyopata pasi za juu katika Fizikia na Hisabati wakati mie niliondoka na “F” na “D” katika masomo hayo,na hatimaye nikaamua kukimbilia kwenye mchepuo wa masomo ya “Arts”.Ndoto yake ya kuwa rubani ilifikia ukingoni baada ya kumaliza kidato cha nne na kukosa nafasi ya kuendelea na masomo.Kibaya zaidi,wazazi wake hawakuwa na uwezo wa kumpeleka shule ya kulipia.Hata hivyo,alichaguliwa kujiunga na chuo cha ualimu kabla ya kuajiriwa kufundisha shule moja ya msingi katika kijiji flani tarafani Ifakara.

Nakumbuka alivyolalamika siku ya kwanza alipotia mguu kwenye kituo chake “kipya” cha kazi.Alikumbana na lundo la wanafunzi wanaobanana kwenye madarasa ambayo majengo yake yanaombea kusiwe na upepo wa nguvu kwani utaezua paa.Madawati ni machache,uhaba wa vitabu vya kufundishia ni mkubwa na nyumba ya mwalimu mkuu ni kichekesho.Alinitania kwamba ni rahisi kwake kupata mwaliko wa kuitembelea Ikulu kuliko kukaribishwa na “hediticha” wake,sababu ni kwamba makazi ya mkuu huyo wa shule ni duni kupindukia.Mbinde nyingine ni mwisho wa mwezi ambapo rafiki yangu huyu anadai inamlazimu afanye dua mfululizo ili mshahara wake upatikane katika muda mwafaka.

Kama muumini wa siasa ya Ujamaa na Kujitegemea,licha ya majukumu yake ya ualimu,ndugu yangu huyu alikuwa akijishughulisha na kilimo.Huko nako ni matatizo kama shuleni kwake.Anadai kwamba sasa amesitisha masuala ya kilimo kwani anadhani anakineemesha zaidi chama cha ushirika kuliko yeye binafsi.Alinichekesha alipodai kuwa laiti angeendelea na kilimo na kuzidi kukikopesha chama cha ushirika,basi kuna uwezekano angeishia jela baada ya kumtwanga afisa yoyote wa chama cha ushirika ambaye kila kukicha anakuja na hadithi mpya kuhusu malipo ya mazao yaliyonunuliwa kwa mkopo.

Tumrejee yule “mjasiriamali” wa jijini Dar.Huyu anatoka kwenye familia inayojiweza na ni miongoni mwa watu wasioamini kabisa kwamba elimu ni ufunguo wa maisha.Aliacha shule alipokuwa kidato cha pili,lakini ana vyeti vinavyoonyesha taaluma mbalimbali.Baba yake alimfanyia mpango wa kazi kwenye taasisi flani ambayo licha ya kuwajali watumishi wake kwa mshahara mkubwa,inasifika sana kwa rushwa.Aliwahi kuninong’oneza kwamba alipata kazi hiyo bila kufanyiwa usahili kwani baba yake na Mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa taasisi hiyo ni marafiki.

Kama rafiki yangu mwalimu alivyoamua kuacha kujishughulisha na kilimo kwa kuhofia kumng’oa mtu meno kutokana na fedha anazokidai chama cha ushirika,huyu “mjasiriamali” aliamua kuacha kazi kwa kuhofia kwenda jela pindi TAKUKURU wangejaliwa uwezo wa kunasa wala rushwa wakubwa.Baada ya kuacha kazi,sasa anaendesha kampuni binafsi “inayojihusisha na kila kitu”.Anajigamba kwamba anaweza kumpatia mteja huduma yoyote anayohitaji:iwe ni kushinda tenda bila kushiriki zabuni,kutoa mzigo bandarini kwa bei poa,kupata hati ya kiwanja isivyostahili,kuzungumza na hakimu ili kesi ifutwe,na hata kuwezesha kupatikana kwa cheti feki kinachoonyesha mteja wake hana ukimwi japo hajapima.

“Mjasiriamali” huyu anadai kwamba huduma pekee asiyoweza kutoa ni kurejesha uhai wa mtu aliyefariki,na haoni kufuru kudai kuwa hilo lingewezekana laiti Mungu angekuwa anaishi Tanzania.Wakati huwa nachoshwa na malalamiko ya rafiki yangu mwalimu,huyu mjasiriamali wangu huwa “ananiboa” na majigambo yake.Kikubwa nachonufaika kwa kuongea nae ni kupata “first-hand account” ya mtu anayeshirikiana na mafisadi kukwamisha uwezekano wowote wa ndoto ya maisha bora kwa kila Mtanzania kutimia.

“Mjasiriamali” huyu ana marafiki sehemu mbalimbali duniani,wengi wao wakiwa aidha walishawahi kuja kuchuma huko nyumbani au wanadhamiria kufanya hivyo.Wengi wa wawekezaji hao ni wale wa muda mfupi,wanaanzisha mradi na kupewa zawadi ya likizo ya kodi (tax holiday),na wakishapata faida ya kutosha wanaingia mitini.Rafiki yangu huyo ananieleza kwamba tofauti na zamani,siku hizi “wazungu” wanajua “kupenyeza rupia kwenye udhia hasa kwa vile hapo kwenye udhia kuna wanaobembeleza kupenyeshewa rupia”.Na hapo ndipo “mjasiriamali” huyu anapotengeneza ulaji wake kwa kuwaunganisha “wenye rupia” na “wanaohitaji rupia” kupindisha taratibu na sheria.

Rafiki yangu mwalimu na huyu mjasiriamali “feki” wanawakilisha picha mbili tofauti zinazoendelea kushamiri huko nyumbani.Kundi dogo la watu linaishi kwa jasho la wenzao linaendelea kuneemeka kwa kukumbatia rushwa,kuuza raslimali zetu na kupinga kwa nguvu manung’uniko yoyote kuhusu ugumu wa maisha.Kwa upande mwingine ni kundi kubwa la watu ambao liwazo lao pekee la kumaliza mwaka na kukaribisha mwaka mpya ni wao kuwa hai.Hawa ni watu ambao wanahitaji kweli baraka za mwaka mpya kwani wanaishi kwa hofu ya kupata ulemavu au kupoteza maisha kwenye hospitali ambazo badala ya kutibiwa miguu wanaweza kupasuliwa vichwa,wanapanda mabasi yenye kutumia chesis za malori na pengine injini za mashine za kusaga unga,wanaweza kubambikiziwa kesi na polisi kwa makosa wasiyofanya,wanaweza kufika kazini na kuambiwa ajira yao imefariki ghafla baada ya mwajiri wa kigeni kuamua kurejea kwao,pamoja na matatizo mengine kedekede.

Rafiki zangu hawa wawili wana mtizamo tofauti kuhusu kauli ya Waziri Ngasongwa kwamba uchumi unakua.Huyo mwalimu,ambaye mara kwa mara jina la Ngasongwa halimtoki mdomoni kwa vile ni Mpogoro mwenzake,anadai inawezekana kukua kwa uchumi kunakozungumziwa ni kwa kuongezeka idadi magari ya kisasa na ya “bei mbaya” pamoja mfumuko wa mahekalu jijini Dar es Salaam.Anatamani neema hiyo ingekuwa hivyohivyo kwenye elimu,afya,kilimo,miundombinu na huduma nyingine muhimu. “Mjasiriamali” anamuunga mkono Ngasongwa na kudai kwamba uthibitisho wa kukua kwa uchumi ni yeye “drop-out” wa kidato cha pili ambaye anamiliki gari lenye thamani ya mamilioni ya shilingi,ana hekalu huko Masaki na anamudu kuwa na nyumba ndogo takriban katika kata ya jiji.Kwa yeye kila siku ni mwaka mpya,na anadhani siku mambo yatapokwenda mrama atakimbilia nje ya nchi na kutangaza kustaafu ujasiriamali wake akiwa huko.





22 Aug 2006

KULIKONI UGHAIBUNI-21

Asalam aleykum,

Leo nina jambo muhimu sana kuhusiana na maslahi ya Taifa letu.Nawaomba wasomaji wapendwa tuwe pamoja kwa makini ili tusipoteane njiani na hatimaye kuleta tafsiri potofu ya ninachotaka kuzunguzia.Natanguliza rai-au niite tahadhari-kwa vile mada yangu ya leo ni nyeti,na ni kuhusu suala ambalo mara nyingi limekuwa likikwepwa na watu wengi.Lakini kabla sijaingia kwa undani,nielezee uzoefu wangu mimi mwenyewe katika suala hilo.

Kwa wafuatiliaji wa makala hii watatambua kwamba mara zote huwa naanza na asalam aleykum.Nimezowea sana kuwasalimia ndugu zangu kwa namna hiyo.Pengine ni kwa vile nimewahi kukaa miji ambayo salamu hiyo inatumika sana,au pengine wengi wa marafiki zangu ni Waislam.Robo ya elimu yangu ya msingi niliipata mkoani Kigoma katika kitongoji cha Ujiji.Nakumbuka kuna wakati flani katika darasa nililokuwa nasoma tulikuwa Wakristo watatu tu na waliosalia (nadhani zaidi ya silimia 90) walikuwa Waislam.Niliwahi kufundisha sekondari flani mjini Tanga na takribani robo tatu ya wanafunzi wangu walikuwa Waislam pia.Na nikipiga hesabu ya harakaharaka,katika marafiki zangu kumi bora saba ni Waislam.Hata siku moja,tangu nikiwa Kigoma,Tanga,Dar na kwengineko sikuwahi kujiona nimezungukwa na watu tofauti nami ambaye ni Mkristo Mkatoliki.Wanafunzi wenzangu,wanafunzi niliowafundisha na marafiki zangu walinichukulia kama Mtanzania mwenzao japo tulikuwa tunatoka madhehebu tofauti.Na hivi karibuni nilipokuja huko nyumbani kwa utafiti wa PhD nayosoma,wengi wa niliohojiana nao walikuwa Waislam.Sikuwahi kupata matatizo yoyote hata pale nilipokutana na wanaoitwa mujahidina.Katika levo ya familia,kaka-binamu yangu mmoja ambaye ni Mkatoliki wa kwenda kanisani kila Jumapili ana mke ambaye ni Mwislam wa swala tano.Uzoefu wangu huo mdogo unatoa picha moja muhimu:Watanzania tumekuwa tukijichanganya sana bila kujali tofauti zetu za kidini.Nikisema kujichanganya namaanisha kujumuika pamoja na sio vinginevyo.

Kuanzia kwenye miaka ya 80 kulianza kujitokeza dalili zilizoashiria kwamba mambo si shwari sana katika eneo la dini nchini.Tunakumbuka uvunjaji wa mabucha ya nguruwe,matukio kwenye msikiti wa Mwembechai,mihadhara ya kidini,suala la Ustaadh Dibagula na mengineyo.Wapo waliosema kwamba kulikuwa na kikundi cha watu wachache kilichokuwa kinachochea vurugu za kidini kuganga njaa zao.Wapo pia waliokuwa wanadai kuwa vurugu za kidini zilikuwa na sura ya kisiasa huku mara kadhaa chama cha CUF kikibebeshwa lawama.Yayumkinika kusema kuwa japo viongozi wetu walikuwa wakikemea vurugu hizo hakukuwa na jitihada za makusudi za kubaini chanzo hasa ni nini.Wanataaluma wetu nao kwa namna flani wamekuwa wakilikwepa suala hili pengine kwa vile linagusa hisia za wengi au pengine kutokana na hisia kwamba matokeo ya tafiti zinahusu migogoro ya kidini huweza kuchangia kuleta utata zaidi badala ya ufumbuzi wa matatizo.Mwalimu wangu wa zamani katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,Dr John Sivalon alichapisha kitabu ambacho kilitokana na thesis yake kuhusu mahusiano kati ya Kanisa Katoliki na Serikali ya Tanzania.Bila kuingia kwa undani kujadili kitabu hicho cha mhadhiri huyo wa Kimarekani ambaye pia ni Padre,ukweli ni kwamba kimekuwa ni nyenzo muhimu katika mihadhara na mijadala ya kidini nchini,japo sina hakika kama kimesaidia katika kuwa sehemu ya utatuzi wa matatizo yaliyopo.

Hebu sasa niingie kwenye ishu yenyewe.Katika siku za hivi karibuni kumekuwa na mijadala inayoendelea kwenye forums mbalimbali za Watanzania kwenye internet.Suala hilo ambalo limegusa hisia zangu ni madai kwamba Rais Jakaya Kikwete amekuwa akiwapendelea Waislam katika teuzi mbalimbali anazoendelea kuzifanya tangu aingie madarakani.Na pengine kinachotajwa zaidi ni ule uteuzi wake wa kwanza wa mabalozi wa mwanzo (akina Adadi na wengineo) ambao kwa mujibu wa majina yao wote ni Waislam.Pengine bila kudadisi sifa za walioteuliwa,wanaolalamika wakaangalia dini zao.Teuzi nyingine nazo zimeendelea kuzua mijadala isiyo rasmi japo sina uhakika kama na huko nyumbani nako hali ni kama hii niliyoiona kwenye mtandao.Ila niliona kwenye mtandao makala mbili tofauti ambazo nadhani zilitolewa kwenye magazeti ya huko nyumbani ambapo mwandishi mmoja mkongwe alikuwa akijibu hoja za mwanasiasa flani ambaye nadhani pia ni kiongozi wa kidini,na mada yenyewe ilikuwa ni hiyohiyo eti Kikwete anawapendelea Waislam.

Mimi siamini kabisa kwamba yeyote kati ya aliyeteuliwa-iwe kwenye uwaziri,unaibu waziri,wakuu wa mikoa,wakurugenzi na kadhalika-wamepewa dhamana zao kutokana na Uislam au Ukristo wao.Unajua kwa miaka mingi sisi tumekuwa Watanzania kwanza halafu ndio vinafuatia vitu kama Ukristo au Undamba wangu.Na ndio maana kule Ujiji,Tanga,Dar na kwingineko nilikokuwa sikuwahi kupata matatizo na waliokuwa karibu nami kwa vile cha muhimu kwetu haikuwa dini au kabila bali urafiki au mahusiano yetu kikazi.Na naamini kabisa kuwa Kikwete ni Mtanzania kwanza,na anaongoza Watanzania kwa misingi ya umoja wao na sio tofauti za kidini,na kwa mantiki hyo hata anapochagua viongozi haangalia dini bali sifa za wateuliwa.

Hata hivyo,kuna matatizo kadhaa yanayohusiana na suala la dini nchini.Tusijidanganye kwamba hatufahamu kuwa kumekuwa na manung’uniko miongoni mwa Waislam kuhusu usawa katika sekta ya elimu na ajira.Iwapo chanzo cha tatizo hilo ni sera za kibaguzi za wakoloni au kuna mbinu za makusudi za kuchochea matatizo hayo,hiyo sio muhimu sana kama ilivyo kwa umuhimu wa serikali,taasisi mbalimbali,wanataaluma na wananchi kwa ujumla kulitafutia ufumbuzi tatizo hilo.Matokeo ya awali ya utafiti wangu unaohusu harakati za Waislam nchini yanathibitisha kwamba matatizo yapo na yanajulikana ila kinachokosekana ni jitihada za makusudi za kupata ufumbuzi wa kudumu.Habari nzuri ni kwamba,hilo (la kupata ufumbuzi) linawezekana iwapo busara zitatumika na wadau kujumuishwa kwa karibu.Namalizia kwa kusisitiza kwamba wanaoleta madai ya udini wanatumia haki yao ya kikatiba kutoa mawazo yao,japo siafikiani nao.Hivi mtu anapooa au kuolewa na mtu anayetoka naye dini moja anaitwa mdini?Hapana.Kitakachojadiliwa hapo ni sifa za huyo mume au mke.Hivyohivyo,Jakaya hawezi kuitwa mdini pindi akichagua Muislam kama yeye alimradi ana sifa zinazostahili.

Alamsiki

18 Jun 2006

KULIKONI UGHAIBUNI:

Asalam aleykum,

Hivi umeshawahi kuulizwa swali moja zaidi ya mara mia na kila unapoulizwa hujiskii kulizowea swali hilo?Pengine imeshakutokea.Mimi imekuwa ikinitokea mara nyingi zaidi ya ninavyoweza kukumbuka.Ilianza nikiwa huko nyumbani.Kabila langu ni Mndamba,natokea Ifakara mkoani Morogoro.Sio siri kuwa Wandamba sio kabila maarufu ukilinganisha na makabila mengine ya mkoa naotoka,kwa mfano Waluguru au Wapogoro.Kwa hiyo kila nilipokuwa naulizwa “hivi wewe ni kabila gani” na mimi kujibu “mie Mndamba” mara nyingi swali lililofuata ni “hivi Wandamba wanatoka mkoa gani?”Au wakati mwingine nilipoulizwa mkoa naotoka na kujibu Morogoro,wengi walipenda kudhani mimi ni Mluguru.Niliposema hapana,wangeniuliza iwapo ni Mpogoro.Sikuwalaumu kwa vile mara nyingi jina la mkoa unaotoka huwa linahusishwa na kabila kubwa au maarufu katika mkoa huo.Ukisema unatoka Mwanza,watu watahisi wewe ni Msukuma,ukitoka Songea watu watahisi wewe Mngoni,au Tabora watahisi wewe Mnyamwezi,na kadhalika.

Nilipokuja huku Ughaibuni swali likageuka kuwa “wewe unatoka nchi gani?”Mara nyingi napojibu “natoka Tanzania” swali linalofuata ni “hivi Tanzania iko wapi?”Wengine wanajua iko Afrika lakini hawana uhakika ni sehemu gani katika bara hiko lenye nchi zaidi ya hamsini.Kuna wakati huwa nawalaumu wanaoniuliza swali hilo kwamba hawakuwa makini kwenye somo la Jiografia,lakini yayumkinika kusema kuwa hata kama ulipata A kwenye somo hilo sio rahisi kujua kila nchi ilipo kwenye ramani ya dunia,kama isivyo rahisi kwa kila Mtanzania kujua Wandamba wanatoka mkoa gani.Hata hivyo,kila napoulizwa ilipo Tanzania,huwa natumia fursa hiyo kufanya kazi ya wenzetu tuliowapa majukumu ya kuitangaza nchi yetu kwa kueleza kuwa nchi hiyo “iko kusini mwa Kenya na Uganda,mashariki ya DRC,Rwanda na Burundi…”,na kadhalika.Wakti mwingine natumia vivutio vyetu kujibu swali hilo,yaani nasema kuwa “Tanzania ndipo ulipo Mlima Kilimanjaro,au Ziwa Victoria,au Mbuga ya Selous…”

Wakati sote tunajua kuwa ni vigumu kwa kabila Fulani kufanya kampeni ya kujitangaza (na jitihada kama hizo zikifanyika utaambiwa unaleta ukabila) kila nchi ina jukumu la kujitangaza yenyewe.Inauma ninapoangalia kwenye runinga na kuona matangazo kama hili hapa: “mtoto huyu anahitaji sana msaada wako…anapenda kujiendeleza na elimu lakini anatoka Tanzania,moja ya nchi masikini sana duniani…kwa kutoa paundi tatu kwa mwezi unaweza kuwasaidia watoto kama huyu…”Yaani nchi yetu inapata nafasi ya kusikika lakini sio kwa sifa nzuri bali umasikini wake.Na huwezi kuwalaumu wanaotoa matangazo ya aina hiyo kwa kuwa wanafanya hivyo kwa nia nzuri,na sio jukumu lao kuitangaza nchi yetu kwa mtizamo wa kuvutia watalii au vivutio vilivyopo huko.Hiyo ni kazi ya Watanzania wenyewe.

Naamini kuna watu wana majukumu ya kuitangaza nchi yetu.Hebu nikupe mfano.Uganda inadhamini kipindi Fulani kwenye kituo cha televisheni cha CNN International cha Marekani.Zambia nao wanatoa matangazo ya kuitangaza nchi yao kwenye kituo hicho na kuwakaribisha wageni waende kushuhudia Maporomoko ya Victoria.Hata Malawi,Rwanda na Burundi nao hawako nyuma,kwani nimeshaona matangazo yao kwenye gazeti maarufu duniani la TIME.Lakini sie tuko nyuma katika eneo hili.Pengine kuna watu wanaona sio muhimu kujitangaza kwa vigezo kwamba “chema chajiuza kibaya chajitembeza.”Tunachopaswa kufahamu ni kwamba katika zama hizi za ushindani wa kuvutia watalii (na hata wawekezaji wa kweli) ni muhimu sana kuitangaza nchi yako.Ukitaka kuhakikisha nayosema sio utani ingia kwenye internet na tafuta habari kuhusu vivutio vilivyopo nchini kwetu.Ni dhahiri utagundua kuwa taarifa zilizopo ni chache,na hata hizo chache hazijitoshelezi,na mara nyingi huwa zimewekwa na wasio Watanzania.Kuna watu wengi wanaoamini kuwa Mlima Kilimanjaro uko Kenya kwa vile nchi hiyo imekuwa ikiutangaza Mlima huo kama uko kwake,na sie tumekaa kimya.Ukienda kwenye tovuti ya Bodi ya Biashara za Nje (BET) wao wanaonekana wako bize zaidi na Maonyesho ya Sabasaba.Nilipotembelea tovuti yao leo ilikuwa inasema iko kwenye matengenezo lakini inakupeleka kwenye kiungo (link) ya Maonyesho ya 30 ya Kimataifa ya Dar Es Salaam (DITF),pengine kuonyesha kuwa Maonyesho hayo (ambayo ni ya mara moja tu kwa mwaka) ni muhimu zaidi kwao kuliko kuitangaza nchi yetukila siku.Angalau Bodi ya Utalii wamejitahidi kiasi japokuwa tovuti yao haina habari za kutosha kuhusu vivutio tulivyonavyo.Tuna Kituo cha Biashara (Tanzania Trade Centre) hapa Uingereza,lakini tovuti yake ni kama imeandaliwa haraka haraka kwa vile taarifa zilizopo humo sio za kutosha sana.Wahusika wasikasirike kusoma haya nayoandika kwa sababu tumewakabidhi dhamana ya kuitangaza nchi yetu.Badala ya kuchukia kukosolewa wanapaswa waone hii kuwa ni changamoto kwao.

Kilio changu kingine ni kukosekana kwa AIR TANZANIA ya Watanzania.Kama wenzetu Kenya wameweza kwanini sisi tushindwe?Angalia Wahabeshi wa Ethiopia wanavyoweza kuchuana na mashirika makubwa ya ndege duniani na kujiingizia mapato makubwa kupitia sekta ya usafiri wa anga na Ethiopian Airlines yao.Kwa kurusha Air Tanzania “the Wings of Kilimanjaro” tulikuwa tunaitangaza nchi yetu na wakati huohuo kuujulisha ulimwengu kuwa Mlima Kilimajaro uko kwetu.Tuna vivutio vingine vingi vya kuvitangaza huku nje ikiwa ni pamoja na moja ya hifadhi kubwa kabisa duniani,Selous,na ziwa la pili kwa ukubwa duniani,Victoria.

Tukubali kwamba hatujajitahidi vya kutosha na tusisubiri kuulizwa.Hatuna sababu ya msingi ya kuwa hapa tulipo,na kwa kuwa tunatambua kuwa hatujitendei haki sie wenyewe kwa kung’ang’ania kuwa katika nafasi isiyo yetu ni lazima tuchakarike sasa.

Alamsiki

KULIKONI UGHAIBUNI:

Asalam aleykum wasomaji wapendwa wa gazeti hili.

Leo tuzungumzie muziki.Muda mfupi uliopita nilikuwa nasoma makala flani kumhusu msanii wa kizazi kipya Albert Mangwea.Yalikuwa ni mahojiano kati ya msaanii huyo na tovuti ya Darhotwire.com.Niliguswa sana na kilio cha msanii huyo ambacho kimekuwa pia kikisikika kutoka kwa takribani kila msanii wa Bongofleva.Kuna wajanja flani,(hapana,hawa si wajanja,bali ni WEZI) ambao wamekuwa wakiwanyonya vijana wetu bila hata chembe ya huruma.Wezi hawa wanafahamika zaidi kwa jina la “wadosi”.Binafsi sijui kwanini wanaitwa wadosi lakini la muhimu hawa sio jina wanaloitwa bali unyonyaji wanaowafanyia wasanii wetu.

Pengine kabla ya kujadili wizi wa mchana mweupe unaofanywa na wadosi hao,tuangalie maendeleo ya Bongofleva huko nyumbani na huku Ughaibuni.Mimi ni mfuatiliaji sana wa mambo yanayotokea huko Bongo. “Ibada” yangu ya kila asubuhi inaanza kwa kutembelea tovuti za ki-Tanzania ili kujua yanayojiri huko.Sasa,kabla ya kuja huko mwaka jana mwishoni mwa mwaka jana nilikuwa nahisi kuwa habari kwamba Bongofleva imeikamata Tanzania kwa “kasi ya tsunami” ni porojo tu.Lakini nilipokuja nilishihudia mwenyewe jinsi gani hatimaye nyimbo zinazotengenezwa na kuimbwa na Watanzania zilivyokamata soko na mioyo ya wapenzi wa muziki.Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu nilibahatika kushuhudia tamasha la “Piga Kura au Upigike” kwenye viwanja vya Biafra Kinondoni.Licha ya picha kadhaa nilizochukua kwa ajili ya kuwajulisha marafiki zangu hapa,nilijionea jinsi gani watu wa rika mbalimbali wanavyovutiwa na kazi za wasanii wa muziki wa kizazi kipya.Nadiriki kuamini kuwa mashabiki waliofika viwanja hivyo walikuwa wanawakilisha karibu kila kona ya jiji la Dar es Salaam.Kitu kingine nilichobaini ni kwamba jinsi gani wasanii wanavyotumika katika masuala ya muhiu kwa Taifa.

Nakumbuka niliwahi kusoma katika gazeti moja la huko nyumbani kwamba msanii Juma Nature “alimfunika” mwenyeji wake-mgombea aliyemwalika msanii huyo katika kampeni zake.Yaani watu walikuwa na kiu zaidi ya kusikia muziki wa Nature kuliko hotuba ya mheshimiwa huyo.Na pengine umati kubwa uliojitokeza kwenye mkutano huo ulifuata buridani hiyo ya bure.Yayumkinika kusema kuwa mchango wa wasanii katika kufanikisha uchaguzi,na hata kuwapatia ushindi baadhi ya wagombea,ulikuwa mkubwa.Kwa bahati mbaya,au pengine kwa makusudi,baada ya kukamilisha kazi ya kuhamasisha jamii kuhusu uchaguzi na wagombea,wasanii wetu wamerudi kulekule walikokuwa:wamesahauliwa na wanaendelea kunyonywa.

Napenda kuwafumbua macho wasanii wetu kwa kuwaambia kuwa muziki wao huku guhaibuni unauzika sana miongoni mwa watu waliotoka Afrika Mashariki.Wamuulize Banana Zorro aliyealikwa hapo London kwenye pati ya Muungano,wamuulize Mr Nice,Ray C na TID,na Profesa J ambaye nasikia amewachengua vilivyo huko Sweden na Holland.Wasanii wa nyumbani wakija huku wanababaikiwa kama vile akina Shaggy au Sean Paul wanavyobabaikiwa wakija huko nyumbani.Lakini,safari za nje sio jambo la kukurupuka tu,ni kitu kinachotaka maandalizi.Kwa mantiki hiyo si lazima kusafiri ili kunufaika na kazi za sanaa bali hata kutafuta namna ya kupenyeza muziki katika soko la kimataifa kunaweza sana kuwainua wasanii wetu.Hivi wasanii wetu wanajua kuwa CD zao huku zinauzwa hadi paundi 10 (zaidi ya shs 24,000/=)?Nimesoma kwenye internet kwamba tarehe 12/06/2006 kampuni moja iitwayo Townsend Records itatoa CD iitwayo Bongoflava (Swahili Rap from Tanzania) ambayo itauzwa paundi 10.99 (takriban shs 27,000/= kwa exchange rate za leo).Sijui kama na hawa ni wadosi au la,lakini huo ni uthibitisho kuwa Bongoflava ina soko zuri tu kuhu Ughaibuni.Na watu wanapenda kweli kazi za wasanii wa nyumbani.Niliporudi kutoka Tanzania jamaa zangu kibao walikuwa wananiulizia kama nimekuja na CD za Bongofleva.Kila mmoja anasema wanaposikia wasanii wetu wanakumbuka sana nyumbani.

Mheshimiwa Kikwete alinukuliwa akiwataka Watanzania walioko nje kuwasaidia wenzao walio nyumbani hasa katika nafasi za masomo.Ujumbe huo unaweza pia kupanuliwa na kuwahusisha wasanii wa nyumbani,kwa maana kuwa Watanzania walio nje hasa wale wenye upeo na mambo ya muziki wawasaidie wasanii wetu wa nyumbani kwa namna yoyote ile inayowezekana.Lakini ili hilo liwezekane wasanii wetu hawana budi “kuchangamka.”Wanaoitwa “wadosi” wanawanyonya na kuwaibia kwa vile wanajua dhahiri kuwa wasanii hao hawana njia mbadala.Jamani,dunia siku hizi imekuwa kama kijiji (japo ni kinadharia) na unachohitaji ni kwenda tu kwenye internet cafĂ© na kuperuza kurasa za mtandao kujua wapi unaweza kupata huduma au kuuza ulichonacho kwa mtu aliye bara jingine.Hapa ndipo umuhimu wa shule (elimu) unapojidhihirisha.Lakini hata kama shule haipandi,si unaweza kumwomba rafiki yako akusaidie kutafuta soko la kazi zako za sanaa nje ya nchi?

Serikali inapaswa kuwasaidia wasanii wetu kwa kuipa meno sheria ya hatimiliki.Sambamba na hilo ni wasanii wenyewe kusimama kidete kutetea maslahi yao badala ya kuendelea kulalamika au kufikiria kuingia kwenye fani nyingine kukwepa wizi wa kazi zao.Pia wasione aibu kuomba msaada kwa wenzao walio nje.Mwisho naiomba serikali ipanue vita dhidi ya wala rushwa na majambazi na kujumuisha “wadosi” pia.

Alamsiki

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.