Showing posts with label DIASPORA FORUM. Show all posts
Showing posts with label DIASPORA FORUM. Show all posts

9 May 2011



Mkutano wa tatu wa Diaspora umemalizika majuzi jijini London huku,kama ilivyokuwa kwa Diapora I na Diaspora II,tumeishia kushuhudia zaidi picha za matukio kuliko maelezo ya mambo muhimu yaliyojiri katika mkutano huo (if there were any).Sina tatizo na watu wanaopenda kupiga picha na viongozi kwani huo ni uhuru wao wa kikatiba.Hata hivyo,nina tatizo kubwa na wale wanaodhani picha na viongozi ni muhimu kuliko kuwabana viongozi hao,hususan wanaposhindwa kutoa maelezo ya kueleweka.

Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe amekuwa sura iliyozoeleka kwenye mikutano hiyo ya Diaspora.Kwa wadhifa wake,ni mtu mwafaka kuiwakilisha serikali,sambamba na kusikia maoni,ushauri,maswali,nk kutoka kwa Watanzania wanaoshi nje ya nchi.Lakini kwa mwenendo wa ushiriki wake kwenye mikutano hiyo,yayumkinika kusema kuwa Membe amekuwa kama mtalii tu wa kutoa porojo moja baada ya nyingine badala ya kuwaeleza washiriki wa Diaspora Forums mafanikio yaliyokwishapatikana kutokana na uwepo wake au umuhimu wa mikutano hiyo (kama upo).

Usanii wa kwanza wa Membe ni katika kauli yake kuwa moja ya changamoto zinazoikabili serikali anayoitumikia ni kujua idadi ya Watanzania wanaoishi nje ya nchi.Huu ni usanii wa kitoto kwa vile Watanzania hao hajawaanza kuja nje wiki iliyopita,wala balozi za Tanzania nje-ambazo Membe ameziagiza kubuni mikakati ya kuwezesha kupata idadi ya Watanzania wanaoishi nje-hazijafunguliwa mwezi huu.

Badala ya kupachika jina la CHANGAMOTO,Membe alistahili kueleza bayana kuwa kutofahamika kwa idadi ya Watanzania wanaoishi nje ya nchi ni moja tu ya UZEMBE ULIOZOELEKA kwenye balozi zetu.Ni uzembe kwa vile umuhimu wa kufahamu idadi hiyo ya wana-diaspora umekuwepo tangu zamani hizo na sio mwaka huu tu au kwenye Diaspora Forums pekee.

Laiti washiriki wa Disapora hiyo wangekuwa serious,wangemkalia kooni Membe kumhoji kwanini zoezi hilo la kufahamu Watanzania waliopo nje ya nchi halijafanyika huko nyuma,na kwanini tuamini kuwa sasa litafanyika?Ikumbukwe Membe amekuwa Waziri wa Nje kwa miaka sita sasa,hivyo kukurupuka wiki iliyopita kukumbuka umuhimu wa kuwa na idadi ya Watanzania nje ya nchi ni sehemu tu ya ubabaishaji wake.

Membe anadai kuwa sababu ya yeye kuja London kuhudhuria mkutano huo ni kukusanya hoja kutoka kwa wadau ili ziweze kusaidia tatizo la Diaspora kupelekwa Bungeni na hatimaye kuingizwa kwenye Katiba.Come on,Membe!That's too cheap politicking even in your own standards.Yaani kukusanya hoja za Watanzania wanaoishi ughaibuni ni lazima kufanywe na waziri ilhali tuna balozi zetu na vyama mbalimbali vya Watanzania?

Na hata tukimpa Membe benefit of a doubt,kwanini asituambie namna alivyokwisha shughulikia hoja alizokusanya kwenye Diaspora I na Diaspora II kabla ya kukurupuka na usanii mwingine kwenye Diaspora III?Kama hoja za nyuma hazijafanyiwa kazi,how come hizo mpya au mwendelezo wa zile za zamani zitashughulikiwa sasa?

Japo Membe anastahili lawama,lakini washiriki wa Diapora Forums nao wanapaswa kulaumiwa kwa kuruhusu cheap lies kutoka kwa same crooked politicians year in year out.Yayumkinika kuamini kuwa udhaifu wa wahudhuriaji wa Diaspora Forums kuuliza maswali magumu yanayostahili majibu ya msingi unachangia sana kumfanya Membe awe "MGENI RASMI WA KUDUMU" kwenye mikutano hiyo kwani anajua he would easily get away with usanii wake.Unadhani angejua kuwa atakaliwa kooni kuhusu ubabaishaji wake,kwa mfano kwenye suala la dual nationality,angetia mguu kwenye Diaspora Forum iliyopita majuzi?

Lakini kilichonikera zaidi katika usanii wa Membe ni kauli yake ya kitoto kuwa eti changamoto nyingine inayoikabili Diaspora ni "WATU WENGI HAWAFAHAMU VIZURI MAANA YA DIASPORA".Utterly rubbish!Hivi Membe anaweza kutueleza amejuaje kuwa watu wengi hawafahamu maana ya Diaspora?Au,je anaweza kutuambia kwanini hawafahamu maana ya neno hilo ambalo lipo kwenye kamusi?Ungetarajia waliohudhuria mkutanio huo wamzomee Membe kwa kauli hiyo isiyo na kichwa wala miguu.Na Membe ana lipi la kutuambia katika madai yake kuwa neno Diaspora halifahamiki kwa wengi,i.e. kutofahamu maana ya neno hilo kunakwamishaje maazimio ya Diaspora Forums zilizopita?

Haya ndio matatizo ya kualika wageni rasmi wanaokuja kutalii badala ya kuzungumza mambo ya msingi.Ni dhahiri kuwa laiti waandaaji wa Diaspora Forums wangetaka mkutano huo uwe na maana wangeandaa mazingira ya kuepuka wababaishaji kama Waziri Membe ambao ni mahiri sana katika kutoa hotuba za kuleta matumaini lakini hotuba hizo zinabaki kuwa hotuba tu,na kusahaulika mara baada ya kumalizika kwa shughuli husika.

Kama kupiga konzi kwenye kidonda kibichi,Membe pasi aibu aligusia suala la uraia pacha (dual nationality).Akaanza kwa kueleza umuhimu wa uraia pacha,na kusema kuwa nchi zilizoruhusu uraia pacha zimewafanya watu wao kupata kazi nzuri zenye mishahara mikubwa na hivyo kuwawezesha kutuma fedha nyingi katika nchi wanazotoka.Huu ndio uelewa wa Waziri wa Mambo ya Nje kuhusu umuhimu wa Diaspora!!!

Labda hakupitia speech notes zake vizuri,labda hakufanya brainstorming ya kutosha kabla ya kutoa hotuba yake kwa wana-Diaspora,lakini ni wazi Membe anafahamu fika kuwa umuhimu zaidi wa uraia pacha ni suala la haki za binadamu kuliko mishahara mikubwa au kazi nzuri.Nani aliyemwambia Membe kuwa wana-Diaspora wana kazi za ovyo ovyo zisizolipa mishahara mizuri kwa vile tu hawana uraia pacha?

Kwa hoja hizi mfu,ni wazi kuwa Membe si mwakilishi mzuri wa wana-Diaspora katika kilio chao cha muda mrefu cha uraia pacha.Membe amegeuza Diaspora Forums kuwa sehemu ya kuwapa matumaini kuhusu suala hili ilhali hafanyi jitihada zozote kuhakikisha suala hilo linahama kutoka kuwa ahadi hewa na kuwa sheria kamili inayotekelezeka.

Kuhusu changamoto ya kuwawezesha Watanzania walio nje ya nchi kuchangia maendeleo ya Tanzania,Membe anapswa kufahamu kuwa kila Mtanzania aliye nje ya nchi ana connection na Tanzania.Wengine tuna wazazi,kaka,dada,wadogo,nk huko nyumbani na licha ya nchi yetu kujifanya haitambua umuhimu wa Watanzania walio nje,wameendelea kupunguza makala ya ufisadi kwa ndugu na jamaa zao huko nyumbani kwa kuwatumia fedha za matumizi na misaada mingineyo.

Katika mkutano huo,mmoja wa wajumbe alipendekeza uanzishaji wa kumbukumbu mkeka ya ujuzi na fani wazizonazo Watanzania waishio nje.Wazo zuri lakini nadhani mtoa hoja amesahau umuhimu wa data protection,na namna taarifa hizo binafsi za Watanzania walio nje zinavyoweza kuishia mtaa wa Mkwepu kwa wanaotengeneza vitambulisho feki.I would never trust fisadi awe na taarifa zangu binafsi ilhali nafahamu fika kuwa zitaozea tu kwenye mafaili kama sio kufungiuwa vitumbua na maandazi.

Kama taafira zilizokusanywa kufahamu chanzo cha milipuko ya mabomu huko Mbagala na Gongo la Mboto zimepuuzwa,mtoa hoja anataraji mijuiza gani  kwa taarifa za Watanzania walio nje kutumiwa ipasavyo?Nadhani kuna baadhi ya Watanzania wenzetu walio nje hawajishughulishi kufahamu uharamia,ufisadi,ubabaishaji,uzembe na utapeli wa kisiasa unaendelea huko nyumbani kiasi kwamba wanaweza kupoteza muda wao kuwasikiliza akina Membe "wakiuza sura" kwenye Diaspora Forums.

Unajua kwanini nasema Membe anafanya usanii kwenye suala la uraia pacha?Ameshatoa kauli kadhaa za kibabaishaji kuhusu suala hilo,moja ikiwa aliyoitoa Januari mwaka huu kwenye mkutano wa IOM ambapo alidai kuwa utafiti uliofanyika umehitimisha umuhimu wa uraia pacha,Wizara yake imeanzisha kitengo cha kushughulikia suala la Diaspora,na sheria ipo mbioni kuanzishwa.

Lakini kwenye mkutano wa Diaspora uliomalizika wiki iliyopita,Membe wala hakugusia ni lini sheria hiyo itaanza kufanya kazi.Katika mkutano huohuo wa IOM,Membe aliwazuga wajumbe kwa kuahidi kuwa sheria ya uraia pacha ingekuwa tayari kufikia mwisho wa mwaka jana.Amekuja London miezi mitano baadaye na kuendelea ngonjera hizo hizo.

Hebu sikiliza porojo za Membe kwenye Diaspora Forum II iliyofanyika mwaka jana



Na hapa pamoja na kuongelea mambo mengine,mwishoni mwa clip ifuatayo anajibu swali na Freddy  Macha kwa kuahidi tena "MWISHO WA MWAKA HUU" kama alivyoahidi mwaka jana kuwa "MWISHO WA MWAKA HUO 2010".



Enewei,kulikuwa Diaspora Forum I,ikamalizika na picha tukaona.Ikaja Diaspora Forum II,ikamalizika na picha tukaonyeshwa.Na majuzi imemekuja Diaspora Forum III,imemalizika wiki iliyopita na picha tumeziona.Tusubiri Diaspora Forum IV...bila shaka tutaendelea kushuhudia picha nyingine na usanii mwingine unaohanikizwa na maneno kama "mchakato","changamoto","vipaumbele" na usanii mwingine kama huo.Blogu hii inatoa wito kwa wana-Diaspora kujaribu kuwaonyesha Watanzania wenzatu walio nyumbani kuwa licha ya kutopendezwa na ubabaishaji wa baadhi ya viongozi wetu huko nyumbani,hatuwezi kutoa fursa kwa ubabaishaji huo kuwa exported hadi huku ughaibuni.Ili Diaspora Forums ziwe na manufaa,they need to go beyond being just another photo-ops.

9 Jul 2010

UJUMBE KUTOKA URBAN PULSE: Karibuni tena wadau wote wa kuangalia sehemu ya pili ya mada ya Uraia Pacha kutoka kwa Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe wakati akitoa hotuba kwenye Diaspora hapa Mjini Ukerewe tarehe 26.3.2010

Pia Mh Membe alisoma ujumbe kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Jakaya Kikwete akiwasifu na Kuwapongeza Watanzania katika Diaspora. Tafadhali Bonyeza chini kuangalia Video

28 Mar 2010


Kwa mara nyingine,baadhi ya Watanzania waishio Uingereza walipata nafasi ya kuhudhuria mkutano uliobeba jina la Diaspora Forum 2.Binafsi sikuhudhuria,sio kwa vile sikuona umuhimu wa kufanya hivyo bali nilitingwa na majukumu binafsi.Hata hivyo,laiti ningehudhuria ningejaribu kutoa mchango wa kwanini uhamasishaji kwa Watanzania walio nje kurejea nyumbani au kuchangia maendeleo ya taifa unaweza kuendelea milele pasipo kupatikana mafanikio yanayokusudiwa. Pamoja na nia nzuri ya kuwepo forums kama hiyo ya Diaspora,lakini ni muhimu kutambua kuwa kikwazo kikubwa cha maendeleo yetu kama taifa hakijawahi kuwa kwenye mipango mizuri.Tanzania tumebahatika kuwa na viongozi wenye uwezo wa hali ya juu katika kuongea na kubuni mipango mizuri.Lakini,kwa bahati mbaya au makusudi,wengi wa viongozi hao ni wazembe wa daraja la kwanza linapokuja suala la utekelezaji mipango including waliyoibuni wao wenyewe.Unajua kuna tofauti kati ya uzembe katika kutekeleza mawazo ya mwenzako na uzembe katika kutekeleza mawazo yako binafsi.Kwa mfano,hakuna mtu aliyeishauri CCM kuja na kauli-mbiu ya "ARI MPYA,KASI MPYA NA NGUVU MPYA" au ile ya "MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA".Uamuzi wa kuja na kauli-mbiu hiyo ulikuwa wa CCM binafsi pasipo shinikizo kutoka kwa wafadhili,viongozi wa dini,wananchi au kikundi chochote kile.Nafahamu wapo watakaobisha kuwa kauli-mbiu zote hizo zimeishia kuwa kauli-mbiu tu pasipo matokeo kuonekana,lakini ukweli ndio huo,na shurti uwekwe wazi.

Back to the Diaspora thing.Kwanza,katika mazingira ya kawaida,haihitajiki kumhamasisha mwananchi kurudi nyumbani kwake au kuchangia maendeleo ya alikotoka.Wengi wa Watanzania walioko ughaibuni hawahamasishwi kusaidia ndugu na jamaa zao walio Tanzania bali wanafanya hivyo kwa vile wanatambua kuwa ni wajibu wao.Naamini kuwa wengi wa wanaokumbuka ndugu na jamaa nyumbani wanasukumwa zaidi na namna misaada yao inavyosaidia walengwa huko nyumbani.Sidhani kama kuna mtu ambaye kila wiki au mwezi anakwenda Western Union,Moneygram au "Kwa Wapemba" kutuma pauni zake alizopata "kwa mbinde" only for watumiwa huko Tanzania kuendeleza libeneke la anasa.

Ninajaribu kutumia mfano wa ndugu na jamaa kama mahala pa kuanzia kabla ya kuangalia namna Watanzania walio nje wanavyoweza kufanya the same kwa nchi yao.Kwa bahati mbaya,forums kama Diapora 2 hazitoi sura ya pili ya hali ilivyo huko nyumbani.I wish miongoni mwa waalikwa wangekuwa taasisi zinazohamasisha Watanzania walio nje kuchangia kuleta mabadiliko ya haraka kwenye mwendendo na hatma ya taifa letu.Yah,Diaspora forums zinaweza kuhamasisha Watanzania wote walio ughaibuni kurejea nyumbani au kuchangia asilimia kadhaa ya vipato vya kujenga taifa letu "changa" (sijui lini litakua),lakini kwa hali ilivyo sasa,watakaoendelea kunufaika ni wateule wachache wafahamikao kama MAFISADI.

Na tatizo jingine linalotukabili Watanzania wengi ni usikivu uliotukuka pasipo udadisi.I hoped mshiriki mmoja angemuuliza Waziri Membe kuhusu commitment ya watwala wetu katika kupambana na ufisadi underlining mifano kama dilly-dallying za kuwachukulia hatua majambazi wa Kagoda au hili skandali jipya la trilioni za stimulus package ambapo tunaambiwa kuwa mafisadi came up with some phony companies to create another EPA-like swindle.

Binafsi napenda kuamini kuwa moja ya negative legacy za itikadi ya Ujamaa ni kwa wananchi kupenda kunyenyekea viongozi "kikasuku".Utaona wananchi wakihangaika kupata nafasi za kupiga picha na kiongozi badala ya kumkalia kooni kumuuliza kwanini mamabo yanaenda mrama.Unadhani laiti Mugabe au Waziri wake akija UK na kukutana na Wazimbabwe waishio hapa "patatosha"?And I don't mean kufanyiwa vurugu bali kubanwa na mwaswali ya msingi kwanini mambo yanakwenda mrama.Lakini kwa akina sie,mdau akishapata picha na kigogo kisha akaipenyeza bloguni basi anakuwa ame-achive lengo kubwa kabisa.

Naamini,hata kama ntapingwa,kuwa Watanzania walio nchi zinazojitahidi kuwatumikia wananchi kwa namna inavyostahili (kama hapa Uingereza,though it couldn't always be absolutely perfect) hawawezi kukwepa lawama za michango yao hafifu katika kuboresha hali ilivyo huko nyumbani.Siamini kama ni ubinafsi au imani kwamba "hata tukisema haitobadilisha kitu" bali ni kasumba ileile inayokwaza mabadiliko huko nyumbani kwamba kwa namna ya miujiza,watu walewale wanaokwaza maendeleo yetu wataamua kwa hiari yao kubadilika na kisha kuutumikia umma kwa ufanisi.Hivi,kwa Watanzania walio Uingereza,hatuoni namna Labour wanavyobanwa mbavu katika jitihada zao za kurejea madarakani?Na si kwamba wame-perform vibaya kihivyo-compared to our CCM-lakini taxpayers wa Uingereza wanaamini kuwa good is not good enough,they want better if not the best from Labour.

Juzijuzi,Makamu Mwenyekiti wa CCM,Pius Msekwa,alifanya ziara hapa UK lakini akanusurika pasipo kubanwa na wana-CCM wenzake kwamba,kwa mfano,kwanini chama hicho kinashindwa kuwachukulia hatua viongozi wanaotuhumiwa kuhusika na ufisadi.Mimi si mmoja wa wanaobeza uanachama wa CCM nje ya nchi kwa vile natambua kuwa hiyo ni haki ya kikatiba ya kila Mtanzania.By the way,kuna Democrats Abroad na Republicans Abroad which are more or less the same as na matawi ya CCM nje ya nchi.Nadhani wanaopinga uanzishwaji wa matawi ya CCM nje ya nchi au unachama wa matawi hayo wanasukumwa zaidi na ukweli kwamba kuna madudu mengi yanayolelewa na CCM huko nyumbani.Sasa inatarajiwa kuwa wana-CCM walio nje ya nchi wakisaidie chama hicho tawala kutambua kuwa mwenendo wake unawaangusha Watanzania.Na wanatarajiwa kufanya hivyo kwa vile wana advantage ya ku-compare and contrast as to kwanini,kwa mfano,Labour inaweza lakini CCM inashindwa.Yaani,kama Labour inaweza kuwakalia kooni wabunge wake kwenye expenses scandal kwanini basi CCM ishindwe kumbana mtu kama Mzee wa Vijisenti ambaye hadi muda huu ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ndani ya chama hicho?

Nimaelizie kwa kupongeza waandaaji wa Diaspora Forums kwani naamini kuwa wanachofanya kina umuhimu mkubwa.Hata hivyo,umuhimu huo unakwamishwa na ukweli kwamba mazingira ya nchi yetu kwa sasa yanakwaza wengi wa Watanzania walio nje kuchangia jitihada za ujenzi wa taifa.Hakuna anayetaka kuona fedha anazochuma kwa mbinde zinaishia kunufaisha nyumba ndogo za mafisadi huko nyumbani au kuongeza idadi ya mahekalu yao.Diaspora forums zinaweza kufanywa hata kila baada ya wiki lakini hazitazaa matunda yanayokusudiwa-au kubaki photo ops tu-laiti mwenendo wa mambo huko nyumbani hautarekebishwa.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.