Showing posts with label DOKTA WILBROAD SLAA. Show all posts
Showing posts with label DOKTA WILBROAD SLAA. Show all posts

14 Apr 2015



Sikiliza Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt Slaa akihojiwa na kitumo kimoja cha redio cha WIBC 93. FM cha Marekani

Bonyeza HAPA kusikiliza

10 May 2011



Leo ni tarehe 10/05/2011,na deadline aliyotoa Ridhiwani Kikwete,mtoto wa Rais Jakaya Kikwete,kwa Katibu Mkuu wa Chadema,Dkt Willibroad Slaa,na Mwenyekiti wa DP,Mchungaji Christopher Mtikila,imemalizika jana.Ridhiwani alitoa dealine ya siku saba kuwataka Dkt Slaa na Mtikila wamwombe radhi kufuatia tuhuma zao dhidi yake kuwa amekuwa bilionea kwa njia za kutilia shaka.

Ni mapema mno kubashiri chochote lakini habari ifuatayo inaweza kutoa mwangaza kuhusu uwezekano wa Ridhiwani kwenda mahakamani kama livyotishia au kutokwenda (which would imply tuhuma hizo dhidi yake ni za kweli).Soma kwanza habari yenyewe


Mtoto wa Rais Kikwete ang’aka

na Janet Josiah

MTOTO wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani, amesema hataki kufuatiliwa maisha yake na wanasiasa hasa wanaomtuhumu kuwa ni bilionea huku akisisitiza kuwashughulikia waolimchafua.

Ridhiwani, alisema hayo jana alipozungumza na Tanzania Daima akitakiwa kueleza hatua atakazochukua baada ya muda wa siku saba aliowapa Mwenyekiti wa Demokratic Party (DP) Mchungaji Christopher Mtikila na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Dk. Willbrod Slaa kupita.

Awali, mtoto huyo wa Rais aliwataka wanasiasa hao wamwombe radhi katika kipindi cha siku saba vinginevyo angewapeleka mahakamani kwa kuwa wamemchafua pamoja na familia yake.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwa njia ya simu, ili kujua lini angekwenda mahakamani kuwafungulia mashtaka viongozi hao, alijibu kwa jazba kwamba jambo hilo linahusu maisha yake hivyo haoni sababu ya kufuatiliwa na vyombo vya habari.

“Jambo la kuwafikisha wanasiasa hao mahakamani si jambo lenu, hilo ni jambo linalonihusu mimi na maisha yangu hivyo nitachokifanya nakijua mwenyewe,” alisema Ridhiwani huku akisisitiza kwamba hata alipozungumza na waandishi wa habari juma lililopita alisema lengo lake ni kuueleza umma na sio kufuatiliwa maisha yake.

Kwa nyakati tofauti Mchungaji Mtikila na Dk. Slaa, walimtuhumu Ridhiwani kwa ukwasi huku wakiitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kumchunguza.



Pasipo nia ya kufanya hitimisho lolote,nashindwa kumwelewa Ridhiwani anaposema "jambo la kuwafikisha mahakamani wanasiasa hao si jambo lenu..."Hivi sio Ridhiwani huyuhuyu aliyeitisha mkutano na waandishi wa habari,ambapo pamoja na mambo mengine alikanusha tuhuma zilizotolewa na wanasiasa hao,na akawataka wamwombe rahdi vinginevyom angewafikisha mahakamani?Sasa kama jambo la kuwafikisha mahakamani wanasiasa hao si jambo lao (wanahabari) kwanini basi aliitisha mkutano nao na kuwaelezea same thing anachodai hakiwahusu?

Waandishi wa habari wana kila sababu ya kumhoji kama atawafikisha Slaa na Mtikila mahakamani au la.Kwanini?Kwa sababu,kwanza,alitamka hayo mbele ya waandishi hao hao wa habari,na pili,yeye ni mtoto wa Rais na ametuhumiwa kuwa bilonea kwa mgongo wa baba yake.Sasa hakuna Mtanzania asiyependa kujua kama madai ya wanasiasa hao ni zushi mtupu au yana ukweli ndani yake.

Wito wangu kwa Ridhiwani ni huu:TIMIZA AHADI YAKO YA KWENDA MAHAKAMANI.Tuhuma za wanasiasa hao dhidi yako si ndogo,kwani licha ya kukugusa wewe binafsi zinamgusa pia baba yako ambaye ni Rais wetu (na ambaye siku za karibuni ametangaza kuwa anadhamiri kuukalia kooni ufisadi).Usipokwenda mahakamani itaonyesha kuwa tuhuma hizo zina ukweli.

And to make matter even worse,Dkt Slaa na Mtikila wanaweza kukufungulia kesi ya kuwakashifu,kwani ulidai ni wazushi tu.Sasa kama sio wazushi then go to the court as you promised,bearing in mind kwamba wewe ni mwanasheria.

Enewei,tunasikiliza WHAT'S NEXT!

Ngoma inogire!

3 May 2011


Sakata linalomhusu Ridhiwani Kikwete,mtoto wa Rais Jakaya Kikwete-kwa upande mmoja,na Katibu Mkuu wa Chadema Dkt Willibroad Slaa na Mwenyekiti wa chama cha DP,Mchungaji Christopher Mtikila-kwa upande mwingine,linaanza kupamba moto baada ya wanasiasa hao kumjibu Ridhiwani.Kimbembe hicho kilianza kwa kauli zilizotolewa na Dkt Slaa na Mtikila ambao katika nyakati tofauti walimtuhumu Ridhiwani kuwa bilionea aliyepata fedha isivyo kihalali akitumia mgongo wa baba yake,Rais Kikwete.

Tuhuma hizo zilipelekea Ridhiwani kuitisha mkutano na waandishi wa habari ambapo licha ya kukanusha kuwa sio bilionea-na kudai kuwa magari ya kifahari anayoonekana akiendesha mara kwa mara ni ya kuazima kutoka kwa marafiki zake-alitoa siku saba kwa Dkt Slaa na Mtikila kuthibitisha madai yake vinginevyo atawafikisha mahakamani.

Sasa,kama habari ifuatayo inavyoonyesha,wanasiasa hao wamemtaka Ridhiwani awahi kwenda huko mahakamani,na wao watatumia fursa hiyo kuthibtisha madai yao.Nisikumalizie uhondo,soma mwenyewe hapa chini

Slaa, Mtikila wamtega mtoto JK

Tuesday, 03 May 2011 21:50
Leon Bahati na Raymond Kaminyoge

KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa, amemtega mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani, akisema akifanikiwa kukifikisha chama hicho mahakamani atakuwa amefanikiwa kula mfupa ambao uliwashinda vigogo waliowatangazwa hadharani kuwa ni mafisadi nchini.

Dk Slaa alitoa kauli hiyo jana alipotakiwa kutoa msimamo wake kuhusu kauli ya Ridhiwani aliyoitaoa Dar es Salaam juzi, kuwa atamfikisha mahakamani ili kuthibitisha kauli yake kwamba mtoto huyo wa rais ni bilionea aliyepata utajiri wa kutisha kipindi kifupi.

Ridhiwani alimpa siku saba Dk Slaa, kuanzia jana awe amekanusha kauli hiyo ya kumtuhumu kuwa fisadi, vinginevyo atamfikisha mahakamani.
"Sisi tunasema atangulie huko mahakamani sisi tutakuja nyuma," alisema Dk Slaa.

Dk Slaa ambaye katika uchaguzi uliopita aligombea urais na kutoa upinzani mkubwa kwa Rais Kikwete aliyetangazwa kuwa mshindi, alisema kauli za kushtakiwa wanapotangaza taarifa za ufisadi hadharani zimekuwa za kawaida.

Alisema wengi waliwahi kutoa kauli kama hiyo kupitia vyombo vya habari baada ya kuwatuhumu hadharani kuwa ni mafisadi, lakini wakashindwa kwenda mahakamani.

"Chadema tuna uzoefu tulipotaja orodha ya mafisadi walitutishia kuwa watatushtaki mahakamani tukawaambia watangulie sisi tutakuja nyuma, lakini walishindwa kutekeleza ahadi yao," alisema Dk Slaa na kuongeza kuwa, iwapo Ridhiwani atafanya hivyo atakuwa amevunja rekodi ambayo imewashinda watu wazito.

Katibu huyo ambaye umaarufu wake ulikuja kwa kasi kipindi cha miaka 15 aliyokuwa Mbunge wa Karatu, Arusha, alijigamba kuwa hawazungumzi jambo bila vielelezo ndio maana wanajiamini kwa kila wanachokisema hadharani.

Dk Slaa alitupia lawama Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), kwamba amekuwa akisisitiza ifutwe kwa sababu inashindwa kufanya kazi yake, ikiwamo kufanya uchunguzi kwa watu wanaotuhumiwa kupata utajiri katika mazingira yenye utata.

Katika mkutano na waandishi wa habari, Ridhiwani alikanusha kuwa kijana bilionea kama Dk Slaa anavyomtuhumu.Alisema anamiliki shamba mkoani Pwani, lenye ukubwa wa ekari 1.5, gari ndogo na akaunti kwenye benki ya CRDB, NBC na Stanbic, ambazo hakutaja kiasi cha fedha.

Dk Slaa alipinga vikali kauli hiyo na kwamba, alimaliza shule miaka michache iliyopita, lakini sasa ni bilionea na utajiri huo aliupata kwenye mazingira ya utata.

Wakati huohuo, Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila, alisema atatoa uthibitisho mahakamani kuhusu mali alizozitaja kuwa zinamilikiwa na Ridhiwani.“Siwezi kumuomba radhi mtu, nina uhakika wa kuwa kijana yule anamiliki mali ambazo hajazipata kwa njia halali, itakuwa vizuri ikiwa atanipeleka mahakamani, kwani huko ndiko nitakakoonyesha uthibitisho wangu,” alisema Mchungaji Mtikila.

Jumamosi iliyopita, Mtikila alikaririwa na vyombo vya habari akisema, Ridhiwani ni bilionea anayemiliki nyumba za ghorofa, malori, kampuni za ujenzi wa barabara na ardhi.
CHANZO: Mwananchi

Uzuri wa sakata hili upo katika pembe nyingi.Kwanza,Ridhiwani ni mwanasheria kitaaluma,kwahiyo yayumkinika kuamini kuwa tishio lake (la kuwapeleka Dkt Slaa na Mtikila mahakamani iwapo watashindwa kuthibitisha tuhuma dhidi yake) lilikuwa sio danganya toto.Pili,Ridhiwani ni mtoto wa Rais Kikwete,na kwa vile tuhuma hizo zinamhusisha pia baba yake (kwa maana ya kutumia fursa ya urais kumnufaisha mwanaye) inatarajiwa kuwa suala hapa sio kujisafisha yeye tu bali pia baba yake.

Lakini kwa upande wa pili ni wasifu wa Dkt Slaa,na pengine Mtikila.Wengi tunafahamu kuwa Mtikila na mahakama ni kama mtu na nyumbani kwake.Japokuwa siku za karibuni amekuwa na msimamo unaoyumba lakini bado anatambulika kuwa anapoamua kupigania haki basi atakwenda umbali wowote ule pasipo kuchelea madhara ya kufanya hivyo.

Kwa Dokta Slaa,wengi tunamfahamu kama mmoja wa wanasiasa adimu kabisa ambao ni nadra kutoma matamshi pasipo kuyafanyia utafiti wa kutosha na kuwa na uthibitisho.Yayumkinika kuamini kuwa Dkt Slaa alikuwa akifahamu vema kuwa kwa vile Ridhiwani ni mwanasheria,na pia asingependa kuona jina lake na la baba yake yanahusishwa na ufisadi hadharani,ni lazima angetishia kwenda mahakamani kama sio kwenda kabisa huko mahakamani kufungua kesi ya madai.Kwa mantiki hiyo,na kwa kurejea historia ya Dkt Slaa,inawezekana kuamini kuwa alikuwa na uhakika na alichosema,sambamba na kuwa na ushahidi mzito kuhusu madai hayo.

Enewei,siku saba si nyingi.Leo ni siku ya pili,tumebakiwa na siku tano.Tusubiri kusikia kauli kutoka kwa Ridhiwani Jumatatu ijayo ambapo siku saba alizotoa zitakuwa zimekwisha muda wake.

Ngoma inogire!

23 Apr 2011


TUHUMA za ufisadi ambazo Dk. Willibrod Slaa amemshushia Rais Jakaya Kikwete, zimezima mbwembwe na majigambo ya “mapambano dhidi ya ufisadi” ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), MwanaHALISI limeelezwa.

Mwishoni mwa wiki, ikiwa ni wiki moja tangu CCM itangaze “kujivua gamba” la ufisadi, Dk. Slaa amemtuhumu Rais Kikwete kushindwa kusimamia rasilimali za taifa kwa kuruhusu au kunyamazia wizi wa Sh. 249 bilioni.

Fedha hizi ni zile za mfuko wa madeni ya taifa.

Aidha, Dk. Slaa amesema Rais Kikwete ameshindwa pia kusimamia matumizi ya Sh. 70 bilioni zinazodaiwa kurejeshwa na wezi waliokiri kuiba kutoka akaunti ya EPA “ambazo hadi sasa hazijulikani matumizi yake.”

“Udhaifu huu wa Kikwete na serikali yake umechangia ufisadi wa kiwango cha juu katika matumizi ya fedha za umma,” ameeleza Dk. Slaa.

Kwa mujibu wa nyaraka za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ambazo Dk. Slaa amenukuu, Sh. 70 bilioni zilidaiwa kuingizwa katika Benki ya Rasilimali (TIB) na baadaye zikadaiwa kuwa zilitolewa ili kuanzisha benki ya wakulima ambayo haijaanzishwa.

Dk. Slaa alidondosha makombora hayo kwenye mkutano mkubwa wa hadhara katika uwanja wa Chipukizi mkoani Tabora, Jumamosi alasiri.

Kwenye mkutano huo, Dk. Slaa aliwataja pia rais mstaafu Benjamin Mkapa, makamu mwenyekiti mstaafu wa CCM John Malecela, katibu mkuu mstaafu wa CCM, Philip Mangula, waziri wa ujenzi, John Magufuli na ofisa wa ngazi ya juu wa mamlaka ya mapato ya taifa (TRA), Placidius Luoga kuwa wameshiriki ufisadi.

“Hawa, kwa njia mbalimbali, ama wameruhusu au wameidhinisha au wamenyamazia ufujaji wa raslimali za taifa,” Dk. Slaa aliuambia mkutano wa hadhara uliohudhuria na umati wa wananchi.

Hii ni mara ya pili kwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuanika majina ya wale kinaowaita “vigogo wala nchi” kwa kuwahusisha na ufujaji wa fedha na raslimali za taifa.

Akiwa na wanasheria wa chama hicho, Mabere Marando na Profesa Abdallah Safari, Dk. Slaa alisoma jina moja baada ya jingine na kutoa maelezo juu ya ushiriki wa kila mmoja katika alichoita kufisidi taifa.

Tayari kishindo cha CHADEMA mjini Tabora kimeleta kizaazaa ndani ya CCM na kufanya nderemo za juu ya kujivua gamba kuonekana kama tamthiliya.

Haya yanatokea wakati katibu mkuu mpya Wilson Mukama anasema atapambana na “mafisadi” na kwamba atawaandikia barua kuwataka wajiondoe kwenye chama.

Naye katibu mwenezi mpya, Nape Nnauye, akinusa kishindo cha Tabora, amejiingiza katika malumbano na CHADEMA. Jumapili mjini Zanzibar, alidai kuwa CHADEMA kinatumiwa na “mafisadi” ili kumchafua Rais Kikwete na mtoto wake Ridhiwani.

Lakini kwenye mkutano wa Tabora, hakuna kiongozi yeyote wa CHADEMA aliyetaja jina la Ridhiwan, jambo ambalo limetafsiriwa kuwa Nnauye alitarajia kuona jina la mtoto huyo wa rais katika orodha ya watuhumiwa.

Wakionekana wamejipanga na kufanya kile walichokiamini, Dk. Slaa na timu yake walianza kueleza kile walichoita, “wizi mkubwa usioweza kuvumilika” uliofanywa na viongozi wa CCM na watendaji serikalini.

Alikuwa Profesa Safari aliyeanza kumtuhumu Mkapa kuwa ameingiza nchi katika matatizo makubwa kwa kuruhusu uuzaji holela wa nyumba za serikali. Alisema nyumba hizo ni sharti zirejeshwe serikalini na bila masharti.

“Tunataka nyumba hizo zirejeshwe mara moja. Iwapo hilo halikufanyika, tutatumia nguvu ya umma kuzirejesha,” alieleza Prof. Safari huku akishangiliwa.

Naye Marando alisema hakuna kiongozi yeyote ndani ya CCM, akiwamo Rais Kikwete, anayeweza kujinasua katika tuhuma za wizi wa mabilioni ya shilingi za EPA zilizokwapuliwa ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Akiongea huku akiwa na nyaraka kadhaa mkononi alizodai zilitumika kukwapulia mamilioni hayo, Marando alisema katika wizi huo, Mkapa ndiye kinara mkuu.

Aliwataja wengine waliohusika na wizi huo kuwa ni Rais Kikwete, Rostam Aziz na Edward Lowassa. Marando aliituhumu serikali kwa kushindwa kuwafikisha mahakamani watuhumiwa wakuu wa wizi wa EPA, badala yake imeshitaki “vidagaa.”

“Mimi nimepata nyaraka zinazoonyesha kuwa John Kato, ndiye William Kemhondo na Francis William ni Barack Goda. Wote hawa wawili ni wafanyakazi wa kampuni ya Caspian Limited, inayomilikiwa na Rostam Aziz.

Akasema yuko tayari kuendesha kesi dhidi ya Kagoda bure na kuahidi kuwa haitafika mwaka 2015 kabla hajawatia gerezani watuhumiwa wote.

Ndipo ikafuata zamu ya Dk. Slaa. Akaanza kueleza wizi ulivyotokea na akasoma tuhuma ya kila mmoja. Akasema orodha yake ya sasa, itaongezeka kwa kadri nyaraka na ushahidi unavyokusanywa na kupitiwa na timu ya wanasheria wa chama chake.

Akiongea kwa staili ileile ya Mwembeyanga, ambako alitangaza orodha ya kwanza ya watuhumiwa 11 wa ufisadi, miaka mitatu iliyopita, Dk. Slaa alisema, “Kuna watu wananituhumu kwamba mimi namsakama Kikwete kwa kuwa ni muislamu. Mimi siangalii dini ya mtu, kabila lake wala sura yake.”

Akivuta pumzi, Dk. Slaa alisema, “Ninachoangalia ni nchi yangu. Ndiyo maana huko nyuma niliwahi kumkemea Sumaye (Fredrick Sumaye) ambaye ni ndugu yangu, kabila langu na dini moja. Lakini pale serikali ilipolegalega katika kusimamia rasilimali za taifa, nilimkemea bila woga.” Ndipo alianza:

Jakaya Kikwete: Huyu ameshindwa kusimamia rasilimali za taifa kwa kuruhusu au kunyamazia wizi wa Sh. 249 bilioni pamoja na Sh. 70 bilioni zilizorejeshwa na wanaodaiwa kuwa wezi wa EPA. Fedha hizo, kwa mujibu wa nyaraka za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), zilidaiwa kuingizwa katika Benki ya Rasilimali (TIB) na baadaye zikadaiwa kuwa zilitolewa ili kuanzisha benki ya wakulima.

Nyaraka zinaonyesha kuwa pamoja na fedha hizo kutolewa TIB, hadi sasa kinachoitwa benki ya wakulima hakijaanzishwa. Alitoa siku 90 kwa Kikwete kueleza mahali ziliko fedha hizo, vingevyo yeye na chama chake wataamini kuwa fedha hizo zilitumiwa na CCM katika uchaguzi mkuu uliopita.

“Huyu Kikwete amefadhiliwa na wezi, ndiyo maana ameshindwa kuchukua hatua kwa wezi hao,” alieleza.

Dk. Slaa amesema anatoa siku 90 kwa serikali kueleza zilipo fedha za DECI, Sh. 70 bilioni za EPA, Sh. 249 bilioni kutoka deni la taifa na mabilioni mengine ambayo yamegunduliwa na mkaguzi wa hesabu za serikali.

Katika tuhuma za Mwembeyanga, CHADEMA walimtuhumu Kikwete, kwa wadhifa wake wakati huo, kusaini “mikataba mibovu” ya madini na makampuni ya kimataifa, iliyosababisha upotevu wa utajiri mkubwa na kuifanya serikali ishindwe kuhudumia vizuri wananchi wake.

Inadaiwa Kikwete alisaini mkataba na kampuni ya SAMAX Limited iliyopewa leseni ya kuchimba dhahabu katika eneo la Lusu, wilayani Nzega, Mkoa wa Tabora, mradi ulioleta mateso kwa maelfu ya wachimbaji wadogo baada ya kuondolewa kwenye makazi yao kwa nguvu.

SAMAX iliuza mradi wake kwa Ashanti Goldfields ya Ghana kwa kiasi cha dola za Marekani 253 milioni. Nao Ashanti waliuza mgodi huo kwa kampuni ya Resolute Limited ambao ndio wanamiliki mgodi wa Golden Pride ulioko Lusu, Nzega uliofunguliwa Novemba 1998.

Kikwete anadaiwa pia kusaini mkataba na kampuni ya Kahama Mining Corporation Ltd (KMCL) ambayo ni kampuni tanzu ya Sutton Resources ya Canada.

Mara zote wananchi waliswagwa nje ya makazi yao ya miaka mingi ili kupisha wawekezaji na hawakulipwa fidia kwa mali zao. Takriban wananchi 400,000 waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo la Bulyanhulu, Kahama waliachwa bila makazi.

Baadaye Sutton iliuza KMCL na Bulyanhulu kwa kampuni ya dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto, Canada kwa dola 280 milioni. Leo hii Bulyanhulu ni moja ya migodi tajiri kwa dhahabu katika Bara la Afrika.

Benjamin Mkapa: Anatuhumiwa kushiriki au kubariki, au kunyamazia ukwapuaji wa fedha za EPA na kubariki uuzaji wa nyumba za serikali.

Kwa mujibu wa upinzani, ufisadi mkubwa ulitendeka chini ya utawala wa Mkapa.

Aidha, Mkapa anatuhumiwa kushiriki, moja kwa moja au kwa kutumia ndugu na/au washirika wa karibu wa familia yake, kumilikisha asilimia 85 ya hisa za kampuni ya Kiwira Coal Mines Ltd., inayochimba mkaa wa mawe huko Kiwira, Mkoani Mbeya kwa kampuni ya Tanpower Resources Limited inayomilikiwa na baadhi ya watu wa familia yake.

John Malecela: Ametuhumiwa kusaidia baadhi ya watuhumiwa waliokwapua mabilioni ya shilingi katika akaunti ya EPA. Upinzani ulionyesha hata baadhi ya vimemo vya Malecela vinavyodaiwa kutumika katika kufanikisha wizi.

Dk. Slaa amesema nyaraka ambazo Marando amemkabidhi zinaonyesha kuwa Malecela alisaidia wizi kufanyika.

Philiph Mangula: Ametuhumiwa kusaidia wizi wa EPA kwa maslahi ya chama chake na wao binafsi. Dk. Slaa alisema vimemo alivyoandika Mangula vilikuwa vya kumwelekeza gavana wa benki kuu wakati huo, Daudi Balali.

John Magufuli: Ametuhumiwa kutumia madaraka ya umma kwa maslahi binafsi. Magufuli ametajwa kuwa ndiye aliyepeleka katika baraza la mawaziri waraka uliotaka serikali iuze nyumba za umma na kutumia ruhusa hiyo kujimilikisha moja ya nyumba hizo.

Mbali na yeye kujiuzia nyumba hizo, Magufuli akagawa baadhi ya nyumba za serikali kwa ndugu na jamaa zake; hata mtu mmoja “chini ya mwaka miaka 18.”

Placidius Luoga: Anatajwa kwa kuingizia serikali hasara ya Sh. 800 bilioni kwa hatua yake ya kuzuia magari ya kampuni ya Tango Transport ya mjini Dar es Salaam, kwa miaka 10 kwa kisingizio cha kutolipa kodi.

Dk. Slaa amesema hatua hiyo ilisababisha mhusika kwenda mahakamani na sasa serikali imeamriwa kumlipa mlalamikaji kiasi hicho cha fedha. Dk. Slaa ameeleza kuwa serikali imeanza kulipa na tayari imetoa Sh. 500 milioni.

Pamoja na kuingiza hasara kiasi hicho kwa serikali, Luoga bado ni mwajiriwa TRA.

Katika orodha ya Mwembeyanga iliyotaja watuhumiwa 11, Edward Lowassa alituhumiwa kuhusika na kashfa ya kampuni ya City Water iliyopewa uendeshaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) mwaka 2002.

Mwanasheria Tundu Lissu aliyefafanua dai hilo alisema, anajua kilichomo katika mkataba huo ndiyo maana anamtuhumu Lowassa kuwa mhusika katika kadhia hiyo.

Lissu ni mmoja wa mawakili wa serikali katika shauri la City Water kwenye Mahakama ya Kimataifa nchini Uholanzi ambayo inashughulikia usuluhishi wa mgogoro unaotokana na kukatishwa kwa mkataba wa City Water.

Kabla ya kukatishwa mkataba, Citywater walikwishasababisha hasara ya dola 12.5 milioni, hivyo kuthibitisha onyo lililotolewa na Benki ya Dunia mapema juu ya uwezo duni wa kampuni hizo.

Lowassa anatajwa pia kwa kuhusika kwake na kashfa ya kampuni ya Richmond Development Corporation (RDC) iliyopewa zabuni ya kuzalisha megawati 100 za umeme wa dharura mwaka 2006.

Miongoni mwa watuhumiwa ufisadi katika orodha ya mwaka 2007, ni pamoja na Nazir Karamagi, Daudi Balali, Nimrod Mkono, Rostam Aziz, Patrick Rutabanzibwa, Gray Mgonja, Basil Mramba na Andrew Chenge.

Karamagi anatuhumiwa kukaidi maoni ya Kamati ya Ushauri ya Madini ambayo ilimtaka asisaini mkataba wa Buzwagi hadi hapo serikali itakaporekebisha sheria na sera ili ipate mapato zaidi.

Gavana Balali alituhumiwa mambo mengi ikiwa ni pamoja na kufumbia macho ufujaji wa mali za umma unaofikia Sh. 522, 459,255,000 kupitia mradi wa ujenzi wa majengo pacha ya BoT jijini Dar es Salaam na Gulioni huko Zanzibar; na hongo ya dola 5 milioni kutoka kampuni ya Skanska Jensen ya Sweden ambayo ilipigwa marufuku kushiriki zabuni ya ujenzi wa majengo ya BoT.

Balali alituhumiwa pia kuidhinisha malipo ya dola za Marekani 118,396,460.36 kwa kampuni muflisi ya Meremeta Ltd., kupitia benki ya nchini Afrika Kusini. Meremeta ilikuwa ikichimba dhahabu Buhemba, wilayani Musoma.

Gavana alituhumiwa pia kudhinisha malipo ya dola za Marekani 13,736,628.73 kwa kampuni ya Tangold Ltd., kwa madai kuwa ni ugharimiaji wa “mali na madeni ya Meremeta Ltd yaliyohamishiwa kwenye kampuni mpya ya Tangold ambayo inamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100.”

Hata hivyo, iligundulika kuwa Tangold Limited ni kampuni ya kigeni iliyosajiliwa kwa mara ya kwanza nchini Jamhuri ya Mauritius na baadaye kuandikishwa nchini Tanzania kama tawi la kampuni ya kigeni.”

Wakurugenzi wa Tangold Limited, kwa mujibu wa taarifa zilizoko BRELA, ni pamoja na Daudi Balali. Gray S. Mgonja, Andrew J. Chenge, Patrick W.R. Rutabanzibwa na Vicent F. Mrisho.

Andrew Chenge alituhumiwa, miongoni mwa mengine mengi, kuishauri vibaya serikali na kuwa mkurugenzi katika kampuni ya kigeni ya Tangold Limited iliyoshiriki na/au kufaidika na malipo haramu ya dola 13,736,628.73.

Basil Mramba alituhumiwa, pamoja na mambo mengine, kushinikiza kampuni ya Alex Stewart (Assayers) Government Business Corporation ya Washington DC, Marekani, kupewa kazi ya kukagua hesabu za makampuni ya uchimbaji dhahabu nchini.

Rostam Aziz alituhumiwa kushiriki katika ukwapuzi wa mamilioni ya shilingi kutoka BoT uliofanywa na kampuni ya Kagoda Agriuculture Limited.

Nimrod Mkono alitajwa kutokana na barua ya CAG iliyobainisha kuwa Benki Kuu ilikuwa ikilipa kampuni yake ya Mkono & Co. Advocates, malipo makubwa zaidi, kuhusiana na kesi ya Valambhia, ambamo BoT inadaiwa jumla ya Sh. 60 bilioni

CHANZO: Mwanahalisi

5 Jan 2011

Picha Hii Inatoa Maelezo Alfu Kidogo.Ukiangalia kwa Makini Utamwona Rostam Kama Kalizimishwa Kuinua Mkono,huku Kikwete Akiwa as if Anampigia Debe Bosi Wake...na Tabasamu Juu!Lol,Ama Kweli Rais Tunaye,Si Mchezo

Dk. Slaa: Kikwete ajiuzulu
• Asisitiza anahusika na Dowans, aahidi kutoboa siri
na Janet Josiah

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilibrod Slaa, sasa amekuja na hoja mpya ya kumtaka Rais Jakaya Kikwete ajiuzulu kutokana na kuhusika moja kwa moja na sakata la Dowans iliyorithi mikoba ya Richmond.

Dk. Slaa ametoa kauli hiyo nzito jana katika mahojiano maalumu na Tanzania Daima Jumatano, ikiwa ni siku moja baada ya Ikulu kutoa taarifa ya kejeli na vijembe vya mitaani dhidi yake kuhusu sakata hilo.

Akizungumza kwa utulivu na umakini mkubwa, Dk. Slaa alisema Rais Kikwete alipaswa kujiuzulu kabla ya aliyekuwa Waziri Mkuu na swahiba wake mkubwa, Edward Lowasa, kuchukua hatua hiyo Februari 7, mwaka 2008, mjini Dodoma.

Yaani Kikwete Mpaka Kaikamata Mic Kuhakikisha Kuwa Debe Analompigia Swahiba Wake ni La Nguvu Kweli Kweli!Kama Alivyowahi Kusema Lowassa,Wawili Hawa Hawakufahamiana Mtaani.Wametoka Mbali.BIRDS OF A FEATHER..
Mawaziri wengine waliojiuzulu kutokana na sakata la Richmond lililozua mjadala mkali nchini ni pamoja na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini wakati huo, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha ambaye alikuwa waziri wa wizara hiyo kabla ya kuhamishiwa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki (EAC).

Akitoa ufafanuzi wa taarifa ya Ikulu iliyotolewa juzi na Kurugenzi ya Mawasiliano, Dk. Slaa alisema mkuu huyo wa nchi hawezi kukwepa kuhusishwa na sakata la Dowans, kwani alilijua hata kabla mitambo yake haijaingizwa nchini.

"Nataka niwatoe Watanzania wasiwasi kwamba ingawa kurugenzi ya mawasiliano imetoa taarifa ya kumsafisha Rais Kikwete na kunikashifu mimi kwa lugha ya mtaani, nawaambia alipaswa kujiuzulu kabla na anatakiwa ajiuzulu sasa, kwani anahusika moja kwa moja na uingiaji wa mkataba wa Kampuni ya Richmond na baadaye na Dowans" alisema Dk. Slaa.

Alimtaka Rais Kikwete kutambua kuwa hawezi kukaa kimya kwa kisingizio cha kuhatarisha amani na utulivu wakati wananchi wanaibiwa mabilioni ya fedha na mafisadi wachache kupitia kampuni feki ya Dowans.

Akirejea historia ya vita dhidi ya ufisadi aliyoiasisi bungeni, Dk. Slaa aliwataka wananchi wakumbuke kuwa taifa lilipokumbwa na tatizo la umeme kabla ya mitambo ya Richmond kuingia nchini, Rais Kikwete alikwenda Marekani kwa ziara ya kikazi.

Alisema aliporejea nchini, alizungumza na waandishi wa habari kuhusu tatizo hilo na kuahidi kuwa serikali yake inalifanyia kazi na siku chache baadaye, rafiki yake wa karibu, Rostam Azizi, Mbunge wa Igunga (CCM), naye alikwenda Marekani.

"Rostam aliporejea kutoka Marekani baada ya siku chache tukaanza kusikia mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura kutoka Kampuni ya Richmond inatarajiwa kuwasili. Kweli ilitua nchini katika Uwanja wa Mwalimu Nyerere na shughuli nyingine zilifungwa uwanjani hapo kupisha ushushaji wa mitambo ya Richmond" alisema Dk. Slaa.

Kwanini Rostam Asiwe na Furaha?Kuendesha Nchi ya Watu Takriban Milioni 50 kwa Kutumia Remote Control si Jambo Dogo Ati!

Huku akisisitiza kuwa ana ushahidi wa anachokisema, Dk. Slaa alisema hata baada ya Richmond kushindwa kuzalisha umeme na kusababisha mawaziri kujiuzulu, serikali ya Kikwete iliamua kuingia mkataba na Dowans iliyorithi shughuli za Richmond na hatua hiyo Rais Kikwete pia aliijua.

"Dowans nayo ikashindwa kuzalisha umeme, mwisho Bunge katika moja ya maazimio yake liliridhia uamuzi wa kuvunja mkataba huo, lakini leo Serikali inadaiwa fidia ya sh bilioni 185, je, Rais Kikwete anaweza kukwepa kwamba hana mkono wake hapo?" alihoji.

Kutokana na hayo, Dk. Slaa alimtaka Rais Kikwete amtaje mmiliki halali wa Dowans ili kuwatoa kiu Watanzania wanaohitaji kumjua.

"Sitaacha kuzungumzia masuala yanayowagusa Watanzania na mali, hasa katika kipindi hiki ambacho Watanzania wanataka kuibiwa fedha zao, wakati wa kukaa kimya umekwisha" alisema Dk. Slaa.

Alisema hashangazwi na kejeli za Ikulu na kuwataka Watanzania kukumbuka alipoanza kuwalipua mafisadi, Rais Kikwete aliwahi kutamka kwamba kelele za mlango haziwezi kumnyima mwenye nyumba usingizi na kamwe kelele za chura hazimzuii ng ombe kunywa maji.

Kaaazi Kweli Kweli
"Lakini baada ya sisi kuamua kupambana na Richmond, Rais Kikwete alikiri linamnyima usingizi na hili la Dowans litamnyima usingizi zaidi katika kipindi hiki cha mwisho cha uongozi wake" alisema Dk. Slaa.

Ili kumaliza kelele za Dowans, Dk. Slaa alimtaka Rais Kikwete kumtaja mmiliki wake ambaye anataka kuwaibia Watanzania mabilioni ya fedha.


 
Wakati Dk. Slaa akimkaba koo Rais Kikwete, mjadala wa Dowans hivi sasa umewavuruga hata viongozi wa serikali tangu ilipoamriwa ilipwe sh bilioni 185.

Aliyekuwa Spika wa Bunge lililopita, Samuel Sitta, hivi karibuni alikaririwa akiitaka serikali iache kuilipa Dowans kwa madai kuwa ni mradi wa mafisadi watatu.

Kauli hiyo ilipingwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ambaye alisema kuwa suala la malipo ya Dowans lipo kisheria na ikithibitika serikali haiwezi kukata rufaa, italazimika kulipa mabilioni hayo.

Juzi Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu imeelezea kukerwa kwake na hatua ya Dk. Slaa kumtaja Rais Kikwete kuwa alihusika katika uzembe uliosababisha taifa kutakiwa kuilipa Kampuni ya Dowans sh bilioni 185 kama fidia.

Taarifa hiyo kali ya Ikulu iliyobeba ujumbe wenye maneno ya kebehi na ya mitaani ya kumwita Dk. Slaa mtu aliyechanganyikiwa na mzabinazabina ilisainiwa na Salvatory Rweyemamu, ambaye kabla ya kwenda Ikulu alikuwa mmoja wa wahariri watendaji, aliyekuwa akiheshimika kwa kutumia lugha fasaha na ya staha.

Rweyemamu katika taarifa yake hiyo iliyoonyesha waziwazi kuandikwa na mtu mwenye hasira, chuki na dharau ama kwa Dk. Slaa, CHADEMA na Tanzania Daima, alikwenda mbali na kumwita kiongozi huyo wa kisiasa kuwa ni mtu hatari.

Katika mahojiano maalumu na gazeti la Tanzania Daima Jumapili, mwishoni mwa wiki, Dk. Slaa alikaririwa akisema chanzo cha suala la Dowans kutakiwa kulipwa fidia limetokana na uzembe wa serikali na Rais Kikwete mwenyewe anahusika kuileta Kampuni ya Richmond ambayo baada ya kuonekana ya kitapeli iliamua kurithisha kazi zake kwa Dowans.

VYANZO: Habari kwa Mujibu wa Tanzania Daima.Picha Kutoka Vyanzo Mbalimbali Mtandaoni.

19 Nov 2010


Pichani kwa hisani HAKI NGOWI

Suala ambalo limetawala maongezi ya Watanzania wengi kwenye social media kwa leo ni kitendo cha wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kususia hotuba ya Rais Jakaya Kikwete wakati anazindua Bunge jipya mjini Dodoma.Kwanza niweke wazi msimamo wangu kuwa naunga mkono uamuzi huo wa Chadema.Sifanyi hivyo kwa minajiki ya kukipenda chama hicho bali ni katika kuzingatia ukweli kuwa Chadema wametumia HAKI yao ya Kikatiba na kidemokrasia kuonyesha upinzani wak kwa vitendo.Nimeandika HAKI kwa herufi kubwa kwa vile neno hilo ni muhimu katika "kuwahukumu" Chadema.

Baadhi ya wenzetu wamekishutumu vikali kitendo hicho huku wengine wakikiita "utovu wa nidhamu wa hali ya juu".Lakini wakati wenzetu hao wanatumia HAKI zao za Kikatiba na kidemokrasia kuwalaumu Chadema,hawataki kutafakari japo kidogo kuhusu HAKI kama hizo kwa chama hicho,yaani HAKI yao ku-protest kwa amani dhidi ya mwenendo mzima wa uchaguzi uliopelekea Jakaya Kikwete kuwa Rais tena.

Inawezekana tukio hilo linaonekana sio la kawaida kwa vile ni mara ya kwanza kutokea nchini.Lakini kwa wanaojishughulisha kufahamu kinachoendelea sehemu nyingine duniani watafahaku kuwa hali hiyo imeshatokea kwenye mabunge mbalimbali,kwa mfano nchini Afrika Kusini,Gambia,Sudan, India,Pakistan na Iraki,to mention only a few.

Kwa namna moja au nyingine,vipengere dhalimu vya Katiba yetu vimewaacha Chadema na alternatives chache zaidi ya hatua kama hiyo ya leo kwa vile Katiba yetu inanyima uhuru wa kupinga matokeo ya ushindi wa Rais mahakamani hata kama ushindi huo umepatikana kwa njia zisizo halali.Leo mapungufu hayo makubwa kwenye Katiba yetu yanaweza kuonekana kama jambo dogo.Lakini yayumkinika kuamini kuwa inaweza tokea tukapata Rais dikteta ambaye ameshindwa kwa mabavu lakini tukajikuta hatuna njia ya kupinga "ushindi" wake kwa vile Katiba inamlinda.

Tatizo la Katiba nyingi katika "Nchi za Dunia ya Tatu" na hususan barani Afrika ni ile tabia hatari ya katiba hizo kutumika kwa mahitaji na maslahi ya watawala walio madarakani.Na kwa vile wengi wa watawala hao ni walafi na waroho wa madaraka,na kwa vile madaraka makubwa waliyonayo yanawapa uhuru wa kufanya lolote wapendalo,katiba hizo huwekwa viraka hapa na pale sio kwa minajili ya ustawi wa taifa husika bali kikundi kidogo cha watawala.

Laiti Katiba ingekuwa inaruhusu ushindi wa Rais kupingwa mahakamani basi ni dhahiri Chadema wangeshafungua kesi.Kuna wanaosema "sasa wakitoka nje ya Bunge ndio inasaidia nini?"Majibu ni mengi ila hapa nitatoa machache tu.Kwanza,ikumbukwe kuwa Chadema ndio chama kikuu cha upinzani bungeni.Pamoja na uchache wa idadi ya wabunge wao ukilinganisha na wale wa CCM,hadhi ya chama kikuu cha upinzani ni kubwa na muhimu ndani na nje ya nchi.Pamoja na mazingira na sheria kandamizi dhidi ya vyama vya upinzani,kwa nchi masikini kama Tanzania kuna kila sababu ya sote kuonekana tumeshikamana hata kama mshikamano huo ni wa kinafiki na unawanufaisha zaidi mafisadi.Ndio maana basi nchi wafadhili zilikuwa zikiwakalia kooni watawala wetu kuhusu upatikanaji wa suluhisho la kudumu huko Zanzibar,ambapo hatimaye CCM kwa shingo upande (na licha ya ngebe za akina Makamba) leo hii tunashuhudia serikali ya umoja wa kitaifa huko Zanzibar.

Of course,hali ya kutoelewana huko Zanzibar ilikuwa serious sana hasa kutokana na vurugu za uchaguzi zilizopelekea mauaji ya watu kadhaa,ukweli unabaki kuwa msimamo thabiti wa chama kikuu cha upinzani visiwani humo,yaani CUF,kutotambua matokeo ya chaguzi mbalimbali,sambamba na kelele walizopiga kwa jumuiya ya kimataifa ndivyo vilivyopeleka leo hii kuwepo serikali ya umoja wa kitaifa.

Kwahiyo wanaohoji umuhimu wa wabunge wa Chadema kususia hotuba ya Kikwete wanapaswa kuelewa kuea msimamo imara sambamba na matendo yanayothibitisha msimamo huo yanasaidia kuleta mabadiliko yanayokusudiwa.Leo pale Dodoma kulikuwa na wawakilishi wa nchi na jumuiya mbalinbali za kimataifa.Vyovyote itavyokuwa,wameguswa na tukio hilo ambalo kwa hakika limetia dola utawala wa Kikwete.Baadhi ya nchi hizo ni wafadhili ambao bila wao basi mambo yanakuwa si mambo.

Lakini jingine la muhimu ni kufikisha ujumbe kwa Kikwete na serikali yake (including vyombo vya dola na Tume ya Uchaguzi) kuwa zama za "ndiyo mzee" zimefika kikomo.Hata kama Katiba inaendelea kuhalalisha sheria dhalimu (kama hiyo inayonyima fursa ya kupinga ushindi wa rais mahakamani) mwanya mdogo wa uhuru wa kidemokrasia kupingana pasipo kupigana unawezesha Chadema kuzalisha harakati mpya za mapambano dhidi ya udhalimu lakini pasipo vurugu au umwagaji damu.Kwa tunaotaka kuona Tanzania yenye kuheshimu na kuzingatia haki na stahili za Watanzania,kitendo cha leo cha Chadema kinafungua ukurasa mpya wa matumaini.Kadhalika,kitendo hicho ni hatua kubwa na muhimu ya kukua kwa demokrasia yetu kutoka vyama vinavyokubali yaishe hata pale penye uthibitisho kuwa vimejumiwa kwenye chaguzi,kwenda kwenye zama ambapo uchakachuaji wa chaguzi unaharamishwa hadharani tena kwenye live tv.Message delivered!

Ni wazi kuwa tukio la leo limemgusa Kikwete na serikali yake kama ambavyo limewagusa Watanzania wengi na jumuiya ya kimataifa.Yayumkinika kuwa inawezekana nguvu kubwa iliyotumika kuchakachua matokeo ya uchaguzi uliopita sasa itaelekezwa katika kuihujumu Chadema ili idhoofike na hatimaye kuachana na msimamo wake wa kukataa kumtambua Kikwete.Zitafanyika jitihada za kuwqgombanisha viongozi wa chama hicho kama ilivyokuww kww NCCR-Mageuzi ya Mrema.Kuna uwezekano pia wa Dokta Wilbroad Slaa kuzushiwa zengwe zaidi ya lile ya maisha yake binafsi.Lakini hayo yanaweza kupita pasipo madhara makubwa kwani hata Baba wa Taifa na wenzake walipokuwa wanahangaikia ukombozi wa Tanzania kutoka himaya ya mkoloni walikumbana na vizingiti hivyo.Haya ni mapambano kati ya wenye uchungu na nchi yao dhidi ya wale wanaotaka kuigeuza nchi yetu kuwa "shamba la bibi" na makao makuu ya ufisadi.

Sie Wakristo tunaamini kuwa mwenye haki ataanguka saba mara sabini ( hapa simaanishi kuanguka kama kule kwa Kikwete pale Jangwani) lakini mwishowe atasimama.Kukubali uchakachuaji wa kura kutapelekea matokeo ya ain moja tu: uchakachuaji zaidi.Historia inatufundisha bayana kuwa kukubali kitu kibaya hakusaidii hata chembe kitu hicho kibaya kugeuka kizuri au athari zake kupungua.Wanaoshauri Dkt Slaa na Chadema "wakubali matokeo" hawana tofauti na wanaoweza kusema tuache mapambano dhidi ya malaria au ukimwi kwa vile magonjwa hayo yamekuwepo miaka nenda miaka rudi.

Laiti Nyerere na mashujaa wengine wa mapambano dhidi ya mkoloni wangepatwa na mawazo hayo ya "kukubali yaishe" leo hii tungeendelea kuwa chini ya mkoloni ( I know kuna watakaosema bora mkoloni kuliko fisadi.Mie nasema ukoloni na ufisadi ni mbaya kama ilivyo kwa kansa na ukimwi.Hakuna cha nafuu,wote ni maadui wanaostahili kuangamizwa).Na laiti Nyerere "angekubali yaishe pale Nduli Idi Amini alipotuvamia,basi huends leo tungekuwa sehemu ya Uganda chini ya dikteta Idi Amini au mrithi wake.

Giving up is not an alternative.Mapambano ya kudai haki (kwa amani) lazima yaendelee.Waingereza wana msemo kwamba kukubali kitu pungufu kwa minajili ya bora liende hatimaye hupelekea kupata kilicho pungufu zaidi ya kilichostahili kupatikana.Kadhalika,hatua zote za mabadiliko huanza kwa hatua chache na pengine ndogo lakini zenye impact na hatimaye kutengenrza mazingita mazuri kwa hatua kubwa zenye impact kubwa zaidi na pengine zenye kuweza kuandika historia mpya.Vilevile,actions speak louder than words.Na hiyo imethibitka leo kwani japo Chadema walishatangaza kuwa hawatomtambua Kikwete uzito wa tamko hilo haukuwagusa wengi kulinganisha na tukio la leo la kususia hotuba ya Kikwete.

And by the way,hotuba hiyo ilikuwa na tofauti gani na hotuba lukuki alizotoa wakati wa utawala wake 2005-2010?Hivyo vipaumbele sijui 13 (or were they 19) tulishavisikia kwenye kampeni za 2005 na zikarudufiwa kwenye kampeni za mwaka huu.Kama kuna yeyote aliyechukulia vimpaumbele hivyo seriously all I can say asubiri muda si mtefu atabaini "imekula kwake" as they say in the streets.




Video kwa hisani ya Mwanakijiji

10 Nov 2010


Muungwana mmoja amenitumia comment ambayo kwa hakika imenigusa sana.Naomba niinukuu
Mbona umekatisha mijadala ya kuendeleza nchi ghafla mno. nilitegemea utakuwa na tasmini ya matokeo ya uchaguzi lakini umezimika ghafla. Vipi au jamani inakuwaje uchungu na nchi unakuwa kwa muda tu? Au wameshakutishia na wewe?
Naelewa kwanini mzalendo huyu anataka tufanye tathmini ya uchaguzi mkuu ambao wengi wetu tuliupa umuhimu wa kipekee kutokana na mwenendo wa mambo ulivyo huko nyumbani.Baada ya kushuhudia taifa likienda mrama kwa kugubikwa na ufisadi ilionekana ni lazima Watanzania wenye uchungu wa dhati kwa nchi yao wachukue hatua zinazostahili.Na hatua mwafaka ilionekana kuwa ni kuing'oa CCM madarakani.

Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dkt Wilbroad Slaa,ameweka bayana msimamo wake kuwa uchaguzi huo ulichakachuliwa.Baadhi ya taasisi zilizotuhumiwa kufanya uchakachuaji huo zimejitokeza hadharani na kukanusha tuhuma hizo.Haihitaji hata cheti cha kozi ya siku 1 ya uchambuzi wa siasa kumaizi kuwa hakuna hata mmoja kati ya wanaotuhumiwa atakiri mchango wake katika kuirejesha CCM madarakani.Wakubali ili waadhibiwe?

Kadhalika,kuna dhana iliyojengeka kuwa katika uhalisia barani Afrika na katika baadhi ya nchi "za dunia ya tatu" sio rahisi kwa chama tawala kushindwa uchaguzi,na ikitokea kimeshindwa basi yayumkinika kuhitimisha kuwa hayo ni matokeo ya uzembe wa chama husika au migogoro ndani ya chama hicho.Hebu chukulia mfano mazingira ya uchaguzi wetu.Vyombo vya dola vilionyesha waziwazi kuipendelea CCM huku watendaji wa taasisi zinazopaswa kuwa huru wakijibidiisha kumlinda mgombea wa chama tawala.Ndio maana haikumtia hofu Mhariri wa Daily News,gazeti linaloendeshwa kwa kodi za walalahoi,kutamka bayana kuwa Dkt Slaa asingeweza kuwa rais hata baada ya miaka mitano.Kujiamini huko hakukutokana na uimara wa CCM bali ndoa ya kifisadi kati ya taasisi za umma na chama hicho tawala.

Tulisikia taarifa kadhaa kuhusu watendaji wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kutowatendea haki wagombea wa vyama vya upinzani.Kadhalika,ilifika mahala Msajili wa Vyama vya Siasa akaamua kuweka wazi mahaba yake kwa CCM na kujipachika jukumubla kuitetea hata pale ilipokosea waziwazi.

Sasa unaweza kujiuliza,"kama tulishaona mwenendo wa aina hiyo ie wa kuitengenezea CCM mazingira ya ushindi,kwanini tulijipa matumaini kuwa Dkt Slaa angeibuka mshindi?".Jibu rahisi kwa mtizamo wangu ni kwamba kulikuwa na matumaini kuwa sauti kubwa ya umma ingeweza kukwaza jitihada zozote za uchakachuaji.Au hata kama jitihada hizo zingefanyika basi zingezidiwa nguvu na sauti hiyo ya umma.

Naomba kukiri hadharani kuwa hofu yangu kubwa haikuwa kwenye mikakati ya kundi dogo lakini lenye nguvu kubwa la mafisadi bali MTAJI MKUU WA CCM yaani umasikini wa Watanzania walio wengi.CCM inategemea sana masikini na hata matokeo "halali" yanathibitisha hilo ambapo maeneo yaliyogubikwa na umasikini ndio yaliyoipa CCM kura nyingi.Huu ni uhusiano ambao kitaaluma unaweza kuelezwa kama wa mnyanyasaji na mnyanywasaji (abuser-abused relationship).Mnyanyasaji anawekeza nguvu nyingi kumwaminisha mnyanyaswaji kuwa pasipo uwepo wake (mnyanyasaji) basi mnyanyaswaji hatakuwa na maisha.Ndio hadithi za amani na utulivu,umoja wa kitaifa,mshikamano,na madude mengine kama hayo.

Kitaaluma,mnyanyaswaji anaweza kufikia mahala akawa anaskia raha kunyanyaswa (punch drunk).Ni kama hali ya kuzowea makonde kwa bondia.Hakuna maelezo mengine mwafaka ya kuelezea namna watu wanaoamka wakiwa hawajui siku iyaisha vipi,wanaotembea maili kadhaa kusaka maji safi japo wafadhili wanamwaga fedha za miradi ya maji,wanaoshinda juani kutwa nzima na kulala vibambazani wakiuza peremende lakini bado wanaandamwa na jeshi la mgambo huku polisi wakiwawinda wawabambikizie kesi,wanaokwenda mahospitalini na kuambulia matibabu hewa kwa vile hakuna madawa,watu wenye watoto ambao makalio yanaota sugu kwa kukaa sakafuni mashuleni,watu ambao haki zao hazipatikani bila kutoa "kitu kidogo" kisha watu haohao wakipigie kura chama kinachostawisha mateso yao.

Na kwa waliodhani akina sie tuliokuwa tukipiga kelele za nguvu kutaka CCM iondoke tulikuwa na chuki binafsi basi matukio mawili yaliyojiri hata masaa 72 hayajapita baada ya CCM kurejea madarakani yanapaswa kuwafumbua macho.Tukio la kwanza ni la mtuhumiwa wa ufisadi wa rada,Mzee wa Vijisenti Andrew Chenge kuchukua fomu ya kugombea Uspika kisha kufanya press conference iliyojaa ngebe,nyodo na dharau kwa wote wanaokerwa na ufisadi.Binafsi,naamini kuwa Chenge katumwa na kundi flani linalotaka kuifakamia keki ya taifa kwa kasi ya marathon hasa kwa vile wanaelewa kuwa Awamu hii ya Tano inaweza kuwa ni lala salama.Chenge ameonyesha bayana kuwa anataka kuwa Spika ili kusafisha majina ya "waliosingiziwa kuwa mafisadi".

Lakini kubwa zaidi ni hisia zangu kuwa Chenge ana baraka kamili za uongozi wa juu wa CCM ikiwa ni pamoja na Mwenyekiti Jakaya Kikwete.Si bado tunakumbuka jinsi Kikwete alivyokwenda jimboni kwa Chenge kumpigia debe na kisha akatetea uamuzi wake wa kuwapigia debe watuhumiwa wa ufisadi kwa kudai kuwa kinachowakabili ni tuhuma tu.Kama tuhuma si tatizo mbona Bashe aliondolewa kwenye mchakato wa mchujo wa kupata wagombea ubunge kwa tiketi ya CCM kwa tuhuma kuwa sio raia wa Tanzania?Kwahiyo tuhuma kwa Chenge,Mramba,nk zinapaswa kubaki tuhuma tu lakini kwa wengine tuhuma ni sawa na hukumu!

Na kwa wanaidhani Chenge anafanya utani mbaya ( a bad joke) basi labda hawaielewi CCM vizuri.Chenge anaweza kabisa kupitishwa katika mfumo wa "kidemokrasia" wa CCM.Yea,kama ameendelea kuongoza kamati ya maadili ya chama hicho na kupitishwa kugombea ubunge (na kushinda) iweje basi kuukwaa uspika liwe suala gumu?Nguvu anayo,sababu anazo,sapoti anayo na VIJISENTI anavyo.Kipi cha kumzuwia kumrithi Samuel Sitta?

Tukio la pili linahisiana na hilo la kwanza ambapo Taasisi ya Kuzuwia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imekurupuka na kudai kuwa Chenge alishasafishwa katika tuhuma za ufisadi wa rada.Yaleyale ya kuisafisha Richmond japo angalau katika ishu ya Richmond serikali ya Kikwete ilikuwa na umri wa zaidi ya mwaka madarakani.Safari hii vimbwanga vimeanza hata kabla ya wiki kumalizika tangu iingie madarakani!Maumivu ya kichwa huanza polepole...

Na kwa kuthibitisha kuwa kura za kuirejesha CCM madarakani zilikuwa kura za kuubariki ufisadi,Ubalozi wa Uingereza umeishushua TAKUKURU kwa kutoa ufafanuzi kuhusu suala la ufisadi wa rada.Sijui nani ameipa TAKUKURU madaraka ya kusafisha watuhumiwa lakini hata sie tusio na uelewa mkubwa wa masuala ya sheria tunafahamu kuwa jukumu la kuhukumu ni la mahakama.Badala ya taasisi hiyo kumpeleka Chenge mahakamani ili kama kusafishwa asafishwe huku,yenyewe imekurupuka na utetezi wake wa kifisadi pasipo hoja za msingi.Hii yote ni katika kuandaa mazingira mazuri kwa Chenge kuwa Spika wa Bunge jipya.

Nitaendelea na tathmini yangu kadri siku zinavyosonga mbele.Najua kuna mengi tu ya kuyazungumzia hasa tukizingatia mazingaombwe yaliyotawala Awamu iliyopita hivyo ni suala la muda tu kabla hayajajiri mengine mengi ya kuwasuta wale wote waliotarajia miujiza kutoka kwa CCM.

3 Nov 2010

MGOMBEA urais kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (Chadema), Dk Willibrod Slaa amesema, atayakataa matokeo ya urais yatakayotangazwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) kwa kuwa kumefanyika wizi mkubwa wa kura.Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Dk Slaa alisema, kama NEC inaitakia mema nchi hii, ifute matokeo yote ya urais na uchaguzi urudiwe upya.

Dk Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, alisema wamekuwa wakifuatilia matokeo ya nchi nzima kwa umakini mkubwa na wamegundua kuna wizi mkubwa wa kura kwenye nafasi za urais na ubunge.

"Kuna uchakachuaji mkubwa wa kura na kazi hiyo inafanywa na usalama wa taifa,"alisema Dk Slaa

Chanzo: Mwananchi
ENDELEA KUFUAtILIA BLOGUNI HAPA

30 Oct 2010



Ndugu Watanzania wenzangu wote kwa ujumla mtakaosoma ujumbe huu, Salaam toka Mbeya Vijijini, ndio tumeanza mikutano midogo ya kufunga kazi asubuhi hii na tutahitimisha baadaye.

Ninashukuru sana kwa maneno ya heri kwa siku yangu ya kuzaliwa hapo jana na ningekuwa sina shukrani kama ningeacha ipite bila kusema asante kwa maneno mema mliyonipatia humu na kwenye facebook na hata waliopata nafasi kwa njia ya simu. Ninawashukuru vile vile kwa mashauri mbalimbali, na pia kwa sala na dua zenu.

Ninashukuru sana na ninaona fahari kuwa ni mwanachama mwenzenu.

Kampeni zote zinaisha leo na kesho ni siku ya Uchaguzi Mkuu kama mnavyofahamu. Kwa upande wangu nimetembelea karibu maeneo yote ya nchi yetu kubwa, nimekutana na watu mbalimbali na nimeona mengi. Nimeona mengi yenye kutia matumaini na faraja na nimena mengine ya kuhuzunisha na kukatisha tamaa. Yote kwa ujumla yake yamenipa picha ya kuelewa zaidi Taifa letu hasa kuhusu mafanikio tuliyoyapata mpaka hivi sasa na changamoto tulizonazo.

Ninaelewa vizuri zaidi sasa kupitia mang’amuzi binafsi hali ya Taifa letu ilivyo na ya kwamba ni lazima tubadili mwendo na huko tunakokwenda maana tutafika mahali ambapo tutashindwa hata kujiuliza tulifikaje. Watu makini hawawezi kuendelea na njia ambayo wanajua wamepotea. Kuendelea kung’ang’ania kwenda wakati mnajua mmeshapotea ni kutukuza kiburi cha kujiona. Taifa letu limepotea njia na hata kama tukijitahidi kwa nyimbo na masimulizi mbalimbali kuhalalisha huko tunakokwenda bado tutakuwa tumepotea.

Ni kwa sababu hiyo nilipoombwa kugombea Urais nilitambua uzito wa mzigo huu mkubwa kwani utahusiana moja kwa moja na kubadilisha mwelekeo wa taifa letu na kuanza kutengeneza pale palihorabiwa, kuinua kilichoanguka na kumwagilia kilichoanza kunyauka. Hili linahitaji mawazo mapya, uthubutu wa kiuongozi na mtazamo mpya wa nini Taifa letu linahitaji. Ndugu zangu, Taifa letu linahitaji mabadiliko makubwa ili tuweze kujipa sisi wenyewe na watoto wetu nafasi ya kuweza kufanikiwa huko mbeleni.

Mabadiliko haya siyo mabadiliko ya mapambo yaani kuhamimisha maua na vitambaa sebuleni wakati nyumba inanuka na nichafu. Wote mliosikiliza au kumwangalia mgombea mwenzangu jana ni wazi hana ahadi ya mabadiliko yoyote makubwa isipokuwa mwendelezo wa yale yale yaliyotufikisha hapa. Ni kutokana na hilo natambua kuwa kura ya kesho siyo kura ya kawaida; siyo kura kama ya 2005 au ya miaka kabla yake.

Kura ya kesho ni kura ya kuchagua kuendelea na vile tulivyo kwa miaka mitano ijayo au kubadilika ili tuanze upya kwa njia sahihi na kwenda ambako sote tunakujua tunataka kwenda. Ninaamini tunachohitaji ni mabadiliko yatakayoanzisha mwamko wa kuanza kulijenga upya taifa letu. Hili ndilo lililonifanya nikubali pale Chama changu kiliponiomba ninyanyue bendera ya Chadema kwenye uchaguzi huu katika nafasi ya Urais.

Naweza kuwaahidi mengi na kwa maneno matamu ya kila aina. Hata hivyo ninawaahidi kitu kimoja kwa uhakika wa asilimia 100. Mkinichagua kuwa Rais wenu na mkiwashawishi ndugu, jamaa na marafiki zenu kufanya hivyo nami nikachaguliwa, nitawapatia uongozi ambao utaifanya miaka 49 iliyopita kuwa ni ya masimulizi ya njozi za jinamizi kwani nitaongoza timu ya watu ambao watakuwa wamejitokea muda, elimu, ujuzi na vipya vyao katika kujenga taifa letu upya. Katika miaka mitano ijayo tutafanya mambo ambayo CCM na utawala wake imeshindwa kufanya kwa karibu miaka hamsini.

Tutawapa nafasi Watanzania hatimaye nao wafurahia matunda ya uhuru wao na vile vile kuweza kuanza kujenga Taifa la kisasa ambalo litakuwa ni tamanio nakinara cha mabadiliko ya kiutawala, kiuchumi na kiutendaji katika Bara letu. Tuna uwezo, tuna sababu na tuko tayari kuwatumikia.

Naomba sana kura zenu hapo kesho ili niwe Rais wenu katika awamu ya tano. Kura yako ina nguvu ya kubadilisha mwelekeo wa taifa letu. Usiuze, usiache kuitumia na pale utakapoitumia itumie kwangu, kwa wagombea Ubunge Chadema na wagombea wetu wa Udiwani ili tuweze kuhakikisha yote tuliyowaahidi tutayatimiza na zaidi.

Msiwe na shaka, hata toka Ikulu nitaendelea kuwa mwanachama mwaminifu wa mitandao hii na kuwapa taarifa mbalimbali moja kwa moja na kujibu maswali mtakayokuwa nayo kuhusu serikali yenu pale inaponipasa mimi kutolea kauli. Asanteni!!


Mungu Ibariki Tanzania Mungu Ibariki Afrika.


DR W P SLAA - MGOMBEA WA URAISI CHADEMA

26 Oct 2010

Add caption


WAINGEREZA WANA MSEMO "IF SOMEONE HAS SOMETHING BAD TO SAY ABOUT YOU,IT'S PROBABLY BECAUSE THEY HAVE DON'T HAVE NOTHING GOOD TO SAY ABOUT THEMSELVES",YAANI KWA KISWAHILI,UKIONA MTU ANA BAYA LA KUSEMA KUHUSU WEWE BASI PENGINE NI KWA VILE HANA JEMA LA KUSEMA KUHUSU YEYE MWENYEWE.

RAIS ALIYE MADARAKANI NI JAKAYA MRISHO KIKWETE.CHAMA KILICHO MADARAKANI NI CHAMA CHA MAPINDUZI.SASA CHA KUSHANGAZA,AJENDA KUBWA YA KIKWETE NA CCM IMEKUWA KUHUSU "KWANINI DAKTA SLAA HAFAI,KWANINI CHADEMA WAONGO,KWANINI AHADI ZA DKT SLAA/CHADEMA HAZITEKELEZEKI" NA UPUUZI MWINGINE KAMA HUO.HIVI RAIS ALIYEKUWA MADARAKANI MIAKA MITANO NA ANAYETOKA CHAMA AMBALO LIMETUTAWALA MIAKA NENDA MIAKA RUDI HAWANA LA KUTUELEZA KUHUSU WAO WENYEWE BALI KUMVALIA NJUGA DOKTA SLAA NA CHADEMA KANA KWAMBA AKINA LIPUMBA NA WAGOMBEA URAIS WENGINE WANAGOMBEA UBUNGE AU UDIWANI?

JIBU LIPO KWENYE HUO MSEMO WA WAINGEREZA.KIKWETE NA CCM HAWANA JIPYA AU ZURI LA KUWAELEZA WATANZANIA ZAIDI YA KUDURUFU AHADI ZA MWAKA 1995,2000 NA ZAIDI 2005.HAWANA JIPYA ZAIDI YA KUBAHATISHA MBINU YAO MAARUFU YA "TUPENI KURA TUMALIZIE TULIYOANZA AWAMU HII".YAANI TUWAPE TENA KURA WAMALIZIE KUMALIZA RASLIMALI ZA TAIFA? HELL NO!TUWAPE TENA MIAKA MITANO WAMALIZIE UBIA WAO NA MAFISADI KUSAFISHA KILA KILICHOPO.HAPANA,NO,NEVER!

WAMETUNYANYASA KIASI CHA KUTOSHA.
WAMETUDHARAU KIASI CHA KUTOSHA (NDIO MANA AHADI LEO HAWATAKI KUOMBA MSAMAHA KWA MAKOSA YA UFISADI)
WAMETUTESA KIASI CHA KUTOSHA.
UMEFIKA WAKATI WA KUWAAMBIA NOT ANY MORE. IMETOSHA.WAMETUIBIA VYA KUTOSHA LAKINI SASA TUKIWAREJESHA TENA MADARAKANI SIO TU WATATUFILISI BALI PIA TUTAONEKANA WAJINGA KWA KUWARUHUSU WATUFANYE WAJINGA.

CHAGUA DOKTA WILBROAD SLAA KWA TANZANIA MPYA YENYE NEEMA NA MAENDELEO
MSTAAFISHE KIKWETE KWA MANUFAA YA UMMA
WATIMUE MAFISADI TUREJESHE NCHI MIKONONI MWETU

INAWEZEKANA.TIMIZA WAJIBU WAKO KWA KUMPIGIA KURA DOKTA SLAA HAPO JUMAPILI



25 Oct 2010



Siku moja nilikuwa na mazungumzo na babu mmoja wa Kiskotish.Kwa vile ilikuwa ni safari ya masaa kadhaa kwenye treni kutoka mji mkuu wa Uingereza,London kuelekea mji wa kaskazini mashariki mwa Scotland,Aberdeen,tulipata wasaa wa kuongea mengi.Babu huyo ameshawahi kukaa Tanzania,na anajua maneno mawili matatu ya Kiswahili.Swali moja aliloniuliza,na ambalo limeendelea kuumiza kichwa changu hadi leo ni kwanini Tanzania ni masikini licha ya utajiri mwingi ilionao na watu wakarimu,wapenda amani na wenye kiu ya maendeleo.Sio siri,nilijiumauma kutoa jibu la kueleweka.

Uzuri kuhusu hawa wenzetu ni kwamba hawajui kumwonea mtu aibu.Babu huyo alinieleza waziwazi kuwa nimeshindwa kumpa jibu la kuridhisha sio kwa vile sifahamu kwanini Tanzania ni masikini bali nimeona aibu tu ya kutoa jibu sahihi.Na huo ni ukweli.Nilijua nikimwambia kwamba tatizo kubwa kwa maendeleo ya Tanzania ni uongozi,angeweza kuniuliza "kwani viongozi hao ni wakoloni au Watanzania wenzenu?"

Katika maongezi yetu babu huyo alinipa fundisho moja muhimu ambalo nadhani sote tunapaswa kulitilia maanani.Alinieleza kuwa zamani hizo wakati Uingereza inajengwa,Waingereza hawakuwa wanafikiria kuhusu mahitaji yao tu bali pia mahitaji ya vizazi vijavyo.Alifafanua kuwa kadri anavyoelewa,Waingereza wengi wanajibidiisha sio tu kwa ajili ya leo bali hata miaka 200 ijayo.Akanipa mfano wa namna walivyojenga treni za chini ya ardhi,hospitali zao kuubwa kama kijiji kizima,vyuo vilivyotapakaa sehemu kubwa za miji na maendeleo mengineyo.

Akatanabaisha kuwa wengi wa walioshiriki katika ujenzi huo wa Uingereza ya leo kwa sasa ni marehemu.Na akanikumbusha kuwa japo wakati wanajituma kujenga nchi yao walikuwa wanafahamun kuwa watafaidi matunda ya jitihada zao kwa muda mfupi tu kabla Mungu hajawachukua lakini hiyo haikuwakatisha tamaa kwa vile walifahamu kuwa vizazi vijavyo vingetaraji waliowatangulia wangetumia nafasi zilizokuwepo muda huo kuwaandalia mazingira mazuri ya kuishi.

Nifupishe stori.Jumapili ijayo tuna Uchaguzi Mkuu ambao binafsi nauona kama tukio muhimu kabisa kwa historia ya nchi yetu.Takriban miaka 50 baada ya uhuru kuna wenzetu wengi tu ambao wanaishi katika mazingira mabovu kuliko kabla ya ujio wa mkoloni.Lakini pia,kuna wachache ambao angalau wanamudu mahitaji ya msingi ya kila siku.Ni kundi hili ambalo ningependa kuelekeza rai yangu kwao.

Hebu tutafakari stori za huyo babu niliyekutana nae kwenye treni.Laiti kizazi chao kingeridhika na hali waliyokuwa nayo wakati huo basi huenda Uingereza ya leo isingekuwa imepiga hatua kama ilivyo sasa.Laiti wangekuwa wabinafsi wa kufikiria maslahi yao tu wasingejihangaisha na mipango ya maendeleo ambayo matunda yake yangeonekana baada ya vifo vyao.Lakini kwa vile waliweka mbele maslahi ya jamii badala ya maslahi binafsi,hawakusita kujenga msingi wa jamii ya Uingereza kwa wakati huo na karne kadhaa baadaye.

Tunaweza kuendelea kuwalaumu wakoloni kwa kukwaza maendeleo yetu.Lakini wakoloni walishaondoka takriban miaka 50 iliyopita.Sasa badala ya kupiga hatua,kuna nyakati tunajikuta tunarudi nyuma zaidi ya wakati wakoloni wanaondoka.

Na japo siwatetei wakoloni,lakini angalau wao walikuwa na excuse.Hawakuwa Watanzania wenzetu.Hawakuwa na uchungu na nchi yetu wala vizazi vijavyo.Vipi kuhusu viongozi wetu wa sasa?Hivi sio hawa waliosomeshwa bure buleshi lakini leo wanakataa katakata kuwa elimu ya bure haiwezekani?Kama iliwezekana wakati huo ambapo hatukuwa na maendeleo ya kutosha,kwanini ishindikane wakati huu ambapo tumeweza kugundua vyanzo mbalimbali vya mapato?

Tukiridhika na mishahara inayotuwezesha kwenda Twanga Pepeta kial wikiendi,au vikao vya bia kila jioni kisha tukasahau kuwa kuna wenzetu (na wengi wao ni ndugu zetu kabisa) huko vijijini hawana uhakika wa kifungua kinywa,wamesahau ladha ya chumvi kwenye mlo kwa vile chumvi imegeuka anasa japo iko kibwena huko Uvinza,sukari imegeuka muujiza hata huko Kilombero ambako wana kiwanda cha sukari na miwa inayozalisha sukari inaozeana mashambani.Kuna wenzetu ambao wali nyama au ugali nyama ni milo inayowezekana kwenye sherehe,misiba au wanapobahatika mara moja kwa mwaka kupelekwa hotelini licha ya maelfu kwa maelfu ya ng'ombe,mbuzi,kondoo na wanyama pori lukuki,sambamba na mchele,mahindi,mihogo,mtama,nk.

Sasa hali hii itaendelea hadi lini?Tunaweza kupuuza shida za wenzetu hawa ambao ni wengi kuliko sie lakini ni dhahiri kuwa ndani kabisa ya nafsi zetu tunateseka tunapokumbuka kuwa punje za wali tunazosafisha kwa minajili ya kuzitupa zinahitajika kwa udi na uvumba katika nyumba moja au nyingine.Hivi kama hawa "wazungu" na ubinafsi wao (hawa familia ni baba,mama na watoto.Habari za shangazi,binamu,mjomba,babu,bibi ni kama kachumbari kwenye mlo: inapendeza lakini sio muhimu). waliweza kuvikumbuka vizazi vijavyo na hivyo kujenga nchi zao hadi kufikia zilipo leo,wakni sie ambao familia ni zaidi ya mume,mke na watoto?

Kuna wenzetu wanaokumbatia mafisadi kwa vile tu wanahofia kuwa mafisadi hao wakiondoka basi nao hawatakuwa na namna ya kumudu maisha yao.Hiyo si kweli kwani hata nyakati za mkoloni kuna waliokuwa wanatumikia wakoloni na kuwakandamiza waafrika wenzao,lakini watu hao waliendelea kuwa hai,huru na kumudu maisha yao...tena kwa njia halali pasipo hofu ya kuonekana wasaliti.

Kura utakayopiga Jumapili ijayo ni zaidi ya kura yako binafsi.Ni kura kwa ajili ya memba wote wa ukoo wako (ambao katika mazingira ya kawaida kuna wengi tu wenye kuhangaika na maisha ya kila siku),rafiki zako wa zamani ambao baada ya kukosa nafasi ya kuendelea na masomo wakajaribu bahati zao kwenye kilimo lakini jitihada zao zinakwazwa na vyama vya ushirika vinavyojua kukopa zaidi kuliko kuuza mazao.Ni pamoja na wale ambao waliamua kufany kazi za wito kama ualimu au uuguzi lakini sasa wanajiuliza kama "wanafanya kazi ya Kanisa" kwani licha ya mshahara kuwa kijungujiko lakini pia hauna uhakika wa kufika katika muda stahili.Kuna wale jamaa zako walioamua kujiari lakini wanaandamwa na polisi na kubambikiwa kesi za bangi,uzururaji,nk kila wanaposhindwa kutoa rushwa kwa askari au mgambo.

Wafikirie hawa wakati unapiga kura.Weka kando mafanikio yako binafsi.

Na kwa wale wanaoteseka kwa vile watawala wamekuwa bize zaidi na kuongeza idadi ya magari yao ya kifahari,kuongeza idadi ya mahekalu yao,kuongeza idadi ya nyumba ndogo zao,na matumizi mengine ya anasa kama hayo,huu ndio wakati wenu wa kulipa kisasi.Kama mlibebwa kwa malori kwenda kwenye mkutano wa Kikwete au mgombea mwingine wa CCM,well,hakuwaomba bali walijipendekeza wenyewe.Hivi hamsangai ukarimu huu wa ghafla umetoka wapi?Hamjiulizi kuwa wakati mnahangaika kupeleka wagonjwa na akina mama wajawazito hospitalini kwa vile hakuna magari ya vimulimuli wao walikuwa wantembelea magari ya thamani huku wakiwatimulia vumbi,lakini ghafla leo wanawabeba kwenye malori mkawasikilize.MSIDANGANYIKE.Mkishawapa kura,hamtawaona tena mpaka mwaka 2015.

Japo nimesema kuwa uchaguzi huu una umuhimu wa kipekee,lakini ni muhimu kukumbuka kuwa tulikuwa na chaguzi kama hizi huko nyuma,na wa karibu zaidi ni wa mwaka 2005.Hivi hamkupata matumaini Kikwete alipoahidi maisha bora kwa kila mmoja wenu.Je mmeshayaona maisha hayo bora?Kama bado,kwanini mnataka kumwamwini tena safari hii japo amekaa madarakani miaka mitano na ameshindwa kutimiza ahadi aliyoweka mwenyewe bila kushikiwa mtutu wa bunduki (hakulazimishwa)?

Na yule mbunge aliyeahidi miujiza lakini akaishia kuongeza kitambi chake na idadi ya watoto kupitia hawara zake,kwanini umpe tena kura?Unataka aendelee kukusanifu?Maana ulifanya makosa mwaka 2005 ukiamini kuwa ahadi zake zilionyesha anakujali.Lakini miaka hii mitano iliyopita inatosha kukuthibitishia kuwa huyo ni tapeli wa kisiasa,na hakuna tapeli anayeaminika.Lakini sio yeye tu bali hata chama chake.

Hesabu umri wako.Halafu jiulize lini ulianza kuisikia CCM.Kumbuka magapi wameahidi katika miaka yote hiyo uliyokuwa unawafahamu.Linganisha maendeleo yako na hao wenye CCM halisi.Kwanini bado unaendelea kukiamini chama hiki?Kama waliahidi 1995 hawakufanya,lakini wakarejea tena kuahidi mwaka 2000,na hawakufanya.Na bila aibu wakarejea tena mwaka 2005,na safari hii wakiahidi kuwa wanajua matatizo yako na ya familia yako.Wakaahidi pia kuwa maisha yako yatakuwa bora kwa vile hilo linawezekana.Na wakaonyesha namna watakavyowezesha maisha bora kwa kila Mtanzania.Je wametimiza?

Lakini pengine wameshindwa kutimiza kwa sababu za kibinadamu.Sasa kwanini badala ya kukuomba msamaha na kueleza kwanini wameshindwa kukuletea maisha bora,wanakufanya mjinga kwa kukuahidi yaleyale waliyoahidi mwaka 2005 na kutoyatekeleza?Kumbuka: ukiwachagua tena hutokuwa na sababu ya kuwalaumu kwani wameshakuthibitishia kwa miaka kadhaa kuwa hawawezi kukusaidia lakini ukaendelea kuwaamini.Sasa,japo inakera kuona unaendela kuwaamini matapeli hawa,ni muhimu kukumbushana pale tunapokosea.Kufanya kosa si kosa bali kurejea kosa.Na umesharejea makosa hayo mara kadhaa.Sasa umefika wakati wa kusema IMETOSHA.

Nimalizie kwa kukumbusha kuwa katika uchaguzi huu tumebahatika kumpata Nyerere wa pili.Huyu ni Dokta Wilbroad Slaa.Kama ambavyo Nyerere alijitoa mhanga kuhakikisha mkoloni anaondoka,Dokta Slaa amethibitisha kuwa ni mzalendo mwadilifu ambaye ameamua kupambana na mafisadi hadi watokomee.Kama aliweza kuwakalia kooni mafisadi alipokuwa mbunge tu,jiulize atakayofanya atapokabidhiwa urais.Wakati akiwa mbunge silaha yake pekee ilikuwa ni maneno,lakini tukimkabidhi dola atakuwa na nyenzo mbalimbali za kuipeleka nchi yetu inapostahili kwenda.

Usihadaishwe na wasiwasi kuhusu wizi wa kura.Kuiba wataiba lakini ili waweze kuiba za kutosha kuwabakiza mafisadi madarakani itategemea zaidi idadi ya kura tutakazompa Dokta Slaa.Ni rahisi kuiba kura chache lakini ni vigumu kuiba maelfu au mamilioni ya kura.Wingi wa kura kwa Dokta Slaa utakuwa silaha muhimu ya kuwatia aibu mafisadi katika kujaribu kuchakachua kura au matokeo ya uchaguzi huo.

INAWEZEKANA.TIMIZA WAJIBU WAKO

1 Oct 2010

"Ufisadi Oyeee.Tupeni tena miaka mitano tuwakwangue kabisa".Of course ni unatarajia nini hapo?

Mgombea wa CCM,Jakaya Kikwete akiendelea na ngwe ya kuwatetea rafiki zake.Alianza na Lowassa,akaenda kwa Mramba,kisha kwa Mzee wa Vijisenti Chenge,na sasa kwa "baba lao" Rostam Aziz.Ama kweli Tanzania bila ufisadi inawezekana!

Wakati "ndege wenye manyoya yanayofanana wakiruka pamoja",Dokta Slaa anaendelea na darasa la kuwahamasisha wenye uchungu na nchi yao kufanya kila liwezekanalo kuwang'oa "ndege hao"


Wananchi mjini Songea wakimsikiliza Rais Mtarajiwa kwa makini
Picha zote kwa hisani ya Jamii Forums

29 Sept 2010


CHADEMA: Synovate wahini mahakamani
*Slaa asema wanazo nyaraka za utafiti wao.
*Adai kuna mbinu za 'kuchakachua' matokeo.

Na Tumaini Makene

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeivaa kampuni utafiti ya Synovate kikisisitiza kuwa kina matokeo ya utafiti uliofanywa na kampuni hiyo ya kupata matokeo yaliyotoa ushindi wa asilimia 45 kwa chama hicho na mgombea wake wa urais, Dkt. Willibrod Slaa.

Synovate hivi karibuni ilikanusha habari kuwa haijawahi kufanya utafiti wala kuficha matokeo hayo yaliyodaiwa kuipa CCM na mgombea wake Rais Jakaya Kikwete asilimia 41, huku ikitishia kulishtaki gazeti moja liliwakariri viongozi wa CHADEMA wakieleza utafiti huo.

Akizungumzia matokeo hayo jana, Dkt. Slaa alisema "Synovate wakimbie haraka mahakamani, tunazo document (nyaraka), hata gazeti lililotishiwa kushtakiwa lisiwe na wasiwasi, huu ni wakati wa kuvunja heshima ya Synovate kitaifa na kimataifa.

"Walifanya utafiti na katika swali namba GP 06 waliuliza, 'uchaguzi ukifanyika sasa hivi nani utampigia kura kuwa rais wa Tanzania?' na majina yote yaliweka pale ya wagombea, sasa wanakanusha nini, waende haraka sana mahakamani, vinginevyo credibility (heshima) yao tutaivuruga nchi nzima na kimataifa, alisema huku akionesha nyaraka hizo kwa mbali.

Dkt. Slaa alisema katika nchi nyingine taasisi za maoni zinakuwa huru, hazipendelei chama chochote kile.

Katika hatua nyingine, CHADEMA kimemshutumu serikali ya CCM inanyoongozwa na Rais Jakaya Kikwete kikidai kuwa imepanga kutumia mbinu chafu ili kuhujumu Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.

Kimesema kuwa kinazo taarifa za uhakika kuwa kati ya mbinu hizo chafu ambazo zinatumiwa au zinataka kutumiwa na serikali kukibeba Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi wa mwaka huu ni kutoa maelekezo kwa Usalama wa Taifa na kujipanga kuchapisha karatasi bandia za kupigia kura nje ya nchi.

CHADEMA kimesema kuwa njama hizo ni aina ya ufisadi kwa kuwa zinahusisha matumizi mabaya ya madaraka na raslimali za nchi kukisaidia chama kimoja cha siasa-CCM, hivyo hazipaswi kuvumiliwa kwani zina lengo la kuingilia maamuzi ya wapiga kura na kuvuruga amani ya nchi.

Kimesema kuwa iwapo mbinu hizo chafu zitafanikiwa kwa kuharibu uchaguzi na kupanga matokeo ya kuipendelea CCM na mgombea wake wa urais, "Rais Kikwete ndiye atabeba lawama na laana zote juu ya yale yatakayotokea. Usalama wa Taifa wakanushe kama hawajapewa maelekezo na kama sasa hawazunguki mikoani."

Hayo yalisemwa jana Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibroad Slaa alipokuwa akizungumza na waandishi ambapo alisisitiza kuwa siku zote chama hicho kimekuwa kikisema kuwa amani ya nchi wakati wa uchaguzi imekuwa ikivurugwa na chama tawala kwa nia ya kutaka kung'ang'ania madaraka, kinyume na maamuzi ya Watanzania.

"Leo tumewaita kuzungumzia juu ya mambo matatu, maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA hasa juu ya ubunge wa viti maalumu, uchaguzi mkuu wa mwaka huu na suala la Synovate (kampuni inayojihusisha na kura za maoni ya watu)...juu ya uchaguzi mkuu tunazo taarifa za uhakika kuwa Serikali imetoa instructions (maelekezo) kwa Usalama wa Taifa na sasa wako mikoani wakizunguka nchi nzima, kuhakikisha Kikwete anashinda kwa hali yoyote ile.

"Tunajua mikoa ambayo wamekwisha kwenda mpaka sasa hivi na wanachofanya huko tunakijua...hii ni sawa na ile barua tuliyoikamata hivi karibuni ikiwaelekeza watendaji wa Serikali kuhakikisha CCM inashinda uchaguzi wa mwaka huu kwa hali na mali. Tunatoa angalizo mapema lolote litakalotokea mwaka huu Rais Kikwete atabeba lawama na laana zote za Watanzania.

"Kwa hali wanayoionesha ya kuhangaika mpaka sasa Kikwete ameshashindwa. Ni kigezo tosha kuwa mpaka sasa wameshashindwa uchaguzi. Tunapenda kumwambia kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni uchaguzi wa wananchi, hakuna cha Usalama wa Taifa, hakuna cha JWTZ wala FFU, waache wananchi wafanye maamuzi juu ya nchi yao," alisema Dkt. Slaa.

Dkt. Slaa ambaye pia ni Mgombea urais wa CHADEMA katika uchaguzi wa mwaka huu, lakini jana akitumia kofia yake ya ukatibu mkuu wa chama alisema kuwa wanazo pia taarifa za kina na za uhakika kuwa kuna karatasi za bandia zinachapishwa katika moja ya nchi za nje, ili zije zitumike wakati wa uchaguzi, akidai ni mwendelezo wa mbinu chafu za kuiba kura.

Alisema chama chake na Watanzania wengi wapenda haki hawatakubali mbinu hizo chafu, akisema matumizi mabaya ya madaraka na raslimali za nchi ni aina ya ufisadi ambao CHADEMA kimekuwa kikiupiga vita tangu kilipotangaza orodha ya aibu ya watu mafisadi wapato 11 nchini.

"Wanaonesha dhahiri kuelemewa...sasa wanafanya vitendo vya kuhatarisha amani ya nchi, hawaitakii mema nchi. Tunasema amani ikivunjika Kikwete atabeba lawama, hatuwezi kukubali udikteta na ubabe huu. Kutumia raslimali za serikali na matumizi mabaya ya madaraka ni aina ya ufisadi, ndiyo maana Kikwete tulimweka katika orodha ya mafisadi."

Akiongezea katika suala hilo, Mwenyekiti wa CHADEMA taifa, Bw. Freeman Mbowe alisema kuwa uchaguzi mkuu wa mwaka huu ukivurugika, Rais Kikwete, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini watapaswa kuwajibika mbele ya Watanzania.

Bw. Mbowe alisema kuwa kuna vitendo vinavyofanywa na baadhi ya viongozi hao kwa nia ya kubeba ushindi wa CCM vinaiweka matatani dhana nzima ya demokrasia na kuonekana kiini macho, hali ambayo haiwezi kukubalika.

"Tunapenda kutoa tahadhari kwa Rais Kikwete, kwa NEC na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, yaani kwa Makame (Jaji Lewis, Mwenyekiti wa NEC) na Tendwa (John, Msajili), watu hawa watatu ndiyo wenye mamlaka ya umma na wajibu wa kutoa haki, utulivu na amani katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.

"Bahati mbaya sana watu hawa watatu wana mikakati ya kuchakachua kura badala ya kutenda haki, wanaliandaa taifa kuchakachua kura...tunatoa angalizo kwa jamii nzima na jumuiya ya kimataifa demokrasia nchi hii ni kiinimacho. Msajili kwa makusudi anabadilisha na kuvunja sheria iliyotungwa na bunge ili kumsaidia Kikwete, halafu hakuna mtu yeyote anayejali wala kuchukuliwa hatua...huu ni uwendawazimu.

"Jana Shinyanga Kikwete kahutubia mpaka saa 1, karibu kila mahali anazidisha muda...tunataka jamii nzima na jumuiya ya kimataifa ituelewe, hawa watu wameshindwa siasa za hoja, wameshindwa siasa za aina zote za maana sasa wanajiandaa kwa siasa za uchakachuaji...mwaka huu kitaeleweka, hapatatosha pale wananchi watakapoamua kulinda maamuzi na kura zao," alisema Bw. Mbowe.

Aliongeza kuwa chama hicho kitaandaa malalamiko ya kuwayawasilisha kwa NEC na Tendwa juu ya vitendo vya kuzidisha muda.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Bw. Salvatory Rweyemamu alipoulizwa kuhusiana na tuhuma hizo jana, alisema hizi ni tuhuma za kisiasa na zinamhusu mgombea wa CCM, kwa hiyo aulizwe Meneja wa Kampeni wa chama hicho, Bw. Abdulrahaman Kinana.

Bw. Kinana hakupatikana kwenye simu yake ya mkononi ambayo mara kadhaa ilikuwa ikiita bila kupokewa.

Kuhusu suala la uteuzi wa majina ya wabunge wa viti maalumu wanawake ndani ya CHADEMA, Dkt. Slaa alijigamba kuwa chama chake kimeweka historia nchini kwa kuwa chama cha kwanza kutumia njia ya kisiasa na kisayansi kupata wabunge hao, huku akisema sheria ya uchaguzi inayolazimisha vyama vya siasa kuwasilisha majina hayo siku 30 kabla ya uchaguzi ni chanzo cha zoezi hilo kutofanyika kwa ufanisi mapema, hivyo watairekebisha wakipewa ridhaa ya kuongoza nchi.

"Njia ambayo consultant (mshauri) wetu atawaeleza vizuri imeondoa kabisa yale mawazo ya wabunge kutoka upande mmoja wa nchi, dhana ya mchezo mchafu mtu kumweka girlfriend wake, uswahiba na unafiki mwingine, hii ni kwa sababu CHADEMA tumedhamiria kuchukua dola na tunaenda kuchukua dola. Hivyo ilikuwa lazima tujipange vizuri kupata wabunge kutoka nchi nzima, maana hata katika majimbo tumesimamisha wabunge 185," alisema Dkt. Slaa.

Kwa upande wake mtaalamu mshauri aliyepewa kazi ya kuratibu utaratibu wa kuwapata wabunge wa viti maalumu, Dkt. Kitila Mkumbo alisema kuwa kwa uchanganuzi aliofanya kwa kutumia vigezo vya jumla kama vile umahiri, bidii, dhana ya uwakilishi wa wananchi kupitia wabunge wa viti maalumu na kila kanda kupata nafasi, itasaidia CHADEMA kupata wabunge makini kama ilivyokuwa katika bunge lililopita.

"Mbali ya vigezo hivyo vya jumla nilitumia vigezo vingine kwa sayansi ya takwimu ambavyo vilikuwa ni elimu, uzoefu wa uongozi kisiasa, uzoefu wa uongozi nje ya siasa, ugombea ubunge jimboni, mchango wa hali na mali katika shughuli za chama na kampeni zinazoendelea, umri katika chama, ambapo kila kigezo kilikuwa na sehemu ndogondogo tofauti ambavyo ndivyo tulitolea maksi.

"Kwa kweli kwa ukokotoaji wa vigezo hivyo CHADEMA imepata wabunge mchanganyiko wenye sifa mbalimbali kutoka karibu kila eneo la nchi katika kanda mbalimbali, kwa kweli ilikuwa lazima kuzingatia vigezo vingi kwani CHADEMA kinajiandaa kuunda serikali.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.