Showing posts with label ELIMU. Show all posts
Showing posts with label ELIMU. Show all posts

14 Feb 2009

HEBU KWANZA MSIKILIZE KIONGOZI HUYU WA UMMA HUKO ZENJI ANAVYOJITETEA DHIDI YA WITO WA KUMTAKA AJIUZULU KISHA TUJADILI KIDOGO:



WAZIRI wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Haroun Ali
Suleiman, amesema haoni sababu ya kujiuzulu wadhifa huo kwa madai ya wanafunzi
wengi Zanzibar kufanya vibaya katika mitihani yao ya kidato cha nne.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, alisema utamaduni kama huo haupo Zanzibar na
wangejiuzulu mawaziri wengi wa elimu waliopita akiwamo Katibu Mkuu wa CUF,
Maalim Seif Sharif Hamad.

Waziri Suleiman ametoa kauli hiyo huku kukiwa
na malalamiko kutokana na matokeo mabaya ya mitihani, huku baadhi ya wanasaisa
wakimtaka awaombe radhi Wazanzibari na kutangaza kuwajibika kutokana na
kusimamia vibaya sekta hiyo.

Alisema
kimsingi Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) inapaswa kupongezwa kutokana na
mafanikio inayopata katika sekta ya elimu, ikiwamo kuongezeka kwa shule za
serikali kutoka sita kabla ya Mapinduzi hadi 134 hivi sasa
.

Inashangaza kuona watu wamekuwa wepesi wa
kulaumu pale matokeo yanapokuwa mabaya, lakini yanapokuwa mazuri hushindwa kumpa
sifa anazostahili.
Tangu kushika wadhifa huo mwaka 2001, kuna
mafanikio makubwa yaliyopatikana kwa vile kiwango cha kufaulu kimeongezeka
kutoka asimilia 77.3 mwaka 2000 hadi asilimia 84.6 mwaka 2007.

Matokeo mabaya yaliyojitokeza mwaka huu si jambo
geni
kwa vile wanafunzi wamekuwa wakifanya vizuri katika baadhi
ya wakati na mara nyingine kufanya vibaya. Akiwa ameshikilia takwimu za kufaulu
wanafunzi tangu mwaka 1971, alisema hata yeye hakufurahishwa na kiwango cha
kufaulu kuanguka mwaka huu kutoka asilimia 84. 6 hadi 77.3.

Mwaka 1982
wakati Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, akiwa Waziri wa Elimu
Zanzibar, kiwango cha kufaulu kilishuka zaidi hadi asilimia 64.4.

Haroun
alisema hivi sasa kuna sababu mbalimbali zinazochangia wanafunzi kutofanya
vizuri ikiwamo upungufu wa vitendea kazi, uhaba wa vifaa vya sayansi pamoja na
walimu wa masomo hayo.

Hata hivyo, alisema Serikali ya Zanzibar kwa
kushirikiana na Serikali ya Marekani imeanza kuchukua hatua za kuondoa uhaba wa
vifaa, ikiwamo vitabu vya sayansi na kujenga shule za sekondari 19 ambazo kila
wilaya itanufaika hapa Zanzibar.

Hadi ifikapo mwaka 2010 tatizo kwa
baadhi ya wanafunzi kukaa chini litakuwa limekwisha pamoja na kuwapo uwiano kati
ya idadi ya wanafunzi na walimu katika darasa. Hivi sasa serikali inaendelea na
programu ya kusomesha walimu katika ngazi mbalimbali ambao watatumika kufundisha
katika shule za sekondari.

Hata hivyo, ni kweli Zanzibar inakabiliwa na
wimbi la walimu wanaomaliza katika viwango vya shahada kukimbilia ajira binafsi
zenye maslahi zaidi. Ili kukabiliana na tatizo hilo, serikali imeamua kupitia
utaratibu wa malipo kwa walimu kuyaboresha zaidi.

Juzi Chama cha
Wananchi (CUF) kilisambaza taarifa kwa vyombo vya habari kikimtaka waziri huyo
kuwaomba radhi wazee na vijana wa Zanzibar kwa kushindwa kwake kuinua na kukuza
elimu Zanzibar.



JAPO SIAFIKIANI NA HOJA ZILIZOTOLEWA NA MHESHIMIWA HUYU KUTETEA UNGA WAKE,NASHAWISHIKA KUKUBALIANA NAE KWENYE KAULI YAKE KUWA UTAMADUNI WA KUJIUZULU HAUPO (SI ZANZIBAR TU BALI TANZANIA KWA UJUMLA).HEBU TUANGALIE MFANO WA CHAPCHAP HUKO ATCL,UNADHANI KWANINI HADI MUDA HUU HAKUNA ALIYEJIUZULU?MAJUZI MMOJA WA MANAIBU GAVANA BOT AMETAJWA MAHAKAMANI KUWA ANAHUSIKA KWA NAMNA FLANI KWENYE SKANDALI LA EPA,KWANINI HAJAJIUZULU KUPISHA UCHUNGUZI?BAADHI YA WATENDAJI WALIOTAJWA KWENYE TUME YA MWAKYEMBE HAWAJAJIUZULU HADI LEO,KWANINI?JIBU LISILOHITAJI TAFAKURI NI HILO ALOTOA MUUNGWANA HUYO WA ZENJE:HAKUNA UTAMADUNI WA KUJIUZULU.JE CHANZO NI NINI?KWA MTIZAMO WANGU TATIZO LIKO KWA WALIOWATEUA WA HAO WANAOPASWA KUJIUZULU.UTAMADUNI HUU UMELELEWA NA UKWELI MCHUNGU KWAMBA MTU ANAWEZA KUAMUA KUJIUZULU PINDI ANAPOBORONGA JUKUMU FLANI LAKINI ALIYEMTUA HAONI UMUHIMU WA KUFANYA HIVYO.FRANKLY SPEAKING,UKOSEFU WA UWAJIBIKAJI KATIKA MAONEO MBALIMBALI UNACHNGIWA ZAIDI NA TABIA YA KULEANA NA KUBEMBELEZANA KATI YA MABOSI NA WALIO CHINI YAO.LAITI KUNGEKUWA NA KANUNI KWAMBA "UKIBORONGA ,UNAWAJIBIKA.USIPOWAJIBIKA UNATIMULIWA" BASI SI AJABU TUNGESHUHUDIA WABABISHAJI WENGI WAKIACHIA NGAZI KUEPUKA FEDHEHA YA KUTIMULIWA AMBAYO MARA NYINGI HUAMBATANA NA KUNYIMWA MARUPURUPU YA KUMALIZA AJIRA.



INACHEKESHA (JAPO INAUDHI BAADA YA KICHEKESHO HICHO) KUMSIKIA MUUNGWANA HUYU WA KIZANZIBARI AKIDAI PONGEZI ZA "kuongezeka kwa shule za serikali kutoka sita kabla ya Mapinduzi hadi 134 hivi sasa".HUU NI UGONJWA MWINGINE UNAOSHAMIRI KILA KUKICHA;KUTUMIA TAKWIMU NZURI ZA IDADI NA KUFUMBIA MACHO TAKWIMU MBAYA ZA VIWANGO (QUANTINTY vs QUALITY).HIVI KUONGEZEKA KWA IDADI YA SHULE NI MUHIMU ZAIDI YA UBORA WA ELIMU INAYOTOLEWA KWENYE SHULE HUSIKA HATA KAMA NI CHACHE?




ANASEMA "watu wamekuwa wepesi wa kulaumu pale matokeo yanapokuwa mabaya, lakini yanapokuwa mazuri hushindwa kumpa sifa anazostahili" KANA KWAMBA PAMOJA NA MATOKEO YA MWAKA HUU KUWA MABAYA BADO WIZARA ILISTAHILI PONGEZI KWA VILE ILIFANYA VIZURI MWAKA JANA.UGONJWA ULEULE WA TAKWIMU ZA MAZURI ZINAZOTUMIKA KUFICHA TAKWIMU ZA MABAYA.




SAFARI YA MAENDELEO YA KWELI BADO NI NDEFU SANA HASA KUTOKANA NA MENTALITY YA BAADHI YA WALIOPEWA JUKUMU LA KUTONGOZA KWENYE SAFARI HIYO,KAMA HUYU MUUNGWANA WA ZENJI.

18 Jan 2008


Nimekuwa mwandishi wa makala magazetini tangu mwaka 1998,takriban miaka 10 sasa.Mtu aliyenipa changamoto la kufanya hivyo anaitwa Albert Memba,mwandishi wa zamani wa habari za michezo katika gazeti la Nipashe na Guardian.Huyu jamaa anaimudu lugha vilivyo.Nilianzaia kwenye magazeti "ya udaku" kama Sanifu (lilifariki zamani hizo) na baadaye Kasheshe na Komesha,ambako nilikuwa naandika unajimu "wa kuchekesha usio na chembe ya ukweli" (tuuite humorous horoscope) kwa kutumia jina la uandishi Ustaadh Bonge (hadi leo baadhi ya rafiki zangu wanaendelea kuniita hivyo).Baadaye nikamahimia kwenye uandishi wa makala za mambo muhimu zaidi ya vichekesho na udaku.Anyway,ni hadithi ndefu.

Nilipata wazo la ku-blog katikati ya mwaka juzi.Nitakuwa mchoyo wa fadhila kama sintampongeza Ndesanjo Macha,kwani mwongozo wake wa namna ya kuanzisha blogu ndio ulionifanya niwe hapa nilipo.Wazo la kuanzisha blog hii lilitokana na ukweli kwamba gazeti lililokuwa linatoa makala zangu halikuwa na tovuti,hivyo awali blog hii ilikuwa kwa ajili ya kuwawezesha watu wote wanaojua Kiswahili popote walipo duniani wapate fursa ya kusoma makala hizo ambazo hazikuwa mtandaoni.Baadaye nikatanua wigo wa uandishi wa makala kwa kuanza kuandika kwenye magazeti ya Mtanzania na Raia Mwema ambako makala zangu hutoka mara moja kwa wiki.

Mmmoja ya watu waliosaidia sana kuitangaza blog ni hii ni rafiki yangu Haki Ngowi.Huyu hana hiana linapokuja suala la kupromoti blog ya bloga mwenzie.Nakumbuka waungwana flani waliwahi "kunitosa" nilipowatumia ombi la kubadilishana vinganishi (exchange links) kwa vile sikuwa naendana na maudhui ya blog yao.Nawashukuru kwani walinipa changamoto kubwa sana.

Mie ni muumini wa msemo "beauty should never be imprisoned",kitu kizuri shurti kisifiwe.Lakini mpewa sifa asibweteke bali anapaswa kuendeleza jitihada (sio kwa ajili ya kupata sifa zaidi) bali kuhalalisha kwamba waliompa sifa hapo awali hawakuwa "wanampaka mafuta kwa mgongo wa chupa",au kwa lugha ya mtaani, hawakuwa "wanamzuga".Nawashukuru nyote mnaonitumia barua-pepe za pongezi kuhusu makala zinazotoka kwenye magazeti nayoandikia pamona na zile zinazotoka kwenye blog hii.Nyie ndio chachu ya ya mafanikio ya makala hizo.

Nina tabia moja ambayo imenitengenezra marafiki na maadui wengi,nayo ni kusema ukweli.Huwa sioni aibu kukiri kwamba nimejifunza kitu flani kutoka mahala flani,kama ambavyo huwa sioni dhambi kumkosoa mtu naedhani amekosea jambo flani.Huko nyuma nilishawahi kuingia kwenye mgogoro na kampuni flani ya magazeti kwa vile tu niliwakosoa pale nilipoona wamepotoka.Tofauti na matarajio yangu,waungwana hao wakaanza kuhoji kuhusu maendeleo yangu ya elimu.Binafsi,huwa sipendi kabisa majadiliano kuhusu masuala ya shule yangu kwani naamini ni suala binafsi (only exception,ni pale majadiliano hayo yanapokuwa ya kitaaluma).

Kuna bloga anaitwa Mpayukaji Msemaovyo.Laiti kungekuwa na mashindano ya kutafuta blogu zenye "kiwango cha juu cha uchungu kwa nchi" basi naamini Mpayukaji angekamata nafasi ya juu kabisa.Simsifii kwa vile tu napenda anachaondika,bali ni ukweli kwamba blog yake imekuwa ni darasa zuri kwangu kujifunza "uchungu kwa nchi yangu na mapambano dhidi ya ufisadi na mafisadi".Uzuri wa makala za Mpayukaji,ambazo hupatikana pia kwenye gazeti la Tanzania Daima,ni ile tabia yake ya kuliita jiwe ni jiwe na sio tofali (calling a spade a spade).Unajua,kuna kusifia kitu kwa matarajio ya kupewa asante flani (kitu ambacho nakipinga kwa nguvu zote) na kuna kusifia kitu kwa vile kina kila sababu ya kusifiwa,na hicho ndicho nachokifanya hapa.Kuna wakati huwa nasoma makala za Mpayukaji huko Tanzania Daima mpaka najikuta naijiwa na taswira ya nyuso za mafisadi zinavyokunjamana kwa hasira iliyochanganyika na aibu+maumivu (truth pains) kutokana na uzito wa hoja za Mpayukaji.

Nitaendelea kuwapongeza waandishi na bloggers wengine ambao wanawatumia Watanzania kwa upenyo huu "mpya" uliojitokeza (mtandao) kuwasilisha vilio,kero,manung'uniko,lawama na hata pongezi kuhusu taifa letu.Pia nitaendela kuwapongeza wenzetu wanaotuletea habari kwa njia ya picha kwani taswira (image) inaweza kuwakilisha maneno elfu kadhaa kwa wakati mmoja.

(Picha ya Mpayukaji nimeipata kutoka kwenye profile ya blogu yake pasipo idhini yake,nitaomba idhini baadaye).

Almanusura nisahau.Hivi huko nyumbani watoto wangapi wanaoamua kutoroka majumbani kwao kutokana na sababu moja au nyingine?Je kuna mahauzigeli wangapi wanaoamua kutoroka kwa waajiri wao kutokana na manyanyaso yaliyopita kiasi?Katika mfumo ambao mnyonge licha ya kutokuwa na haki ananyang'anywa hata ile haki ndogo aliyozaliwa nayo (utu),kundi hili linabaki kuwa halina mtetezi.Clip hii ya Ludacris ft Mary J. Blidge katika wimbo Runaway Love inaweza kutukumbusha wajibu wetu kama jamii


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.