Showing posts with label ENERGY SECTOR IN TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label ENERGY SECTOR IN TANZANIA. Show all posts

3 Nov 2008

Mitambo ya Richmond ikiwasili kwa mbwembwe.Kampuni hiyo ya kitapeli imerithiwa na Dowans.Picha kwa hisani ya MICHUZI

Kampuni ya Dowans Tanzania Ltd imetangaza rasmi zabuni ya kuuza mitambo yake ya kuzalisha umeme ikiwa ni miezi mitatu baada ya serikali kusitisha mkataba wake na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco). 

Dowans Tanzania Limited ilirithi mkataba wa kuiuzia umeme wa megawati 120 Tanesco kutoka kwa Kampuni ya Richmond Development LLC ambayo baadaye iligundulika kuwa ni kampuni hewa. Serikali ilifikia uamuzi wa kusitisha mkataba huo Agosti mosi mwaka huu baada ya kuridhika kuwa mkataba huo haukuwa halali wala haukuwa na nguvu kisheria. 

Serikali pia ilisema ilibaini iwapo mkataba husika ungekuwa halali, uhamishaji wa mkataba kutoka RDVCO badala ya Richmond Development LLC kwenda Dowans Tanzania Ltd, haukufuata msingi wa mkataba.“Hivyo uhamishaji haukuwa halali na ifahamike kwamba mkataba ulikuwa baina ya Richmond Development Company LLC na Tanesco na siyo na REDVCO na Tanesco,” alisema. 

Tangazo ambalo limetolewa na kampuni hiyo leo kwa vyombo vya habari, limesema watu au kampuni makini ambazo zitakuwa na nia ya kununua mitambo hiyo wanakaribishwa kuinunua. Kutolewa kwa tangazo hilo la kuuza mitambo yake, huenda ikawa ni ishara ya kampuni hiyo kufungasha virago baada ya kimya kingi tangu mkataba huo usitishwe. 

Baada ya kusitishwa kwa mkataba huo, Tanesco imekuwa ikitumia pamoja na vyanzo vingine vya umeme, mitambo yake ya megawati 100 iliyojengwa na Kampuni ya Watsilla ya Finland ili kufidia upungufu uliotokana na kuondoka Dowans. Tanesco pia imekuwa ikinunua umeme kutoka kwa kampuni za Songas na IPTL. 

Siku chache baada ya kusitishwa kwa mkataba huo, mmoja wa maofisa wa Dowans aliiambia HabariLeo kuwa walikuwa na njia nyingi za kufanya na mitambo hiyo ikiwa kuikodisha au kuiuza kwa watu wengine. “Kukatishwa kwa mkataba haina maana hatuwezi endelea na kazi, tutatafuta wateja wengine kama kampuni za migodi na kuwauzia umeme au tunaweza kukodisha mitambo yenyewe,” alisema ofisa huyo. 

Kwa mujibu wa tangazo hilo, mitambo hiyo ina mashine tano za uzalishaji wa umeme ambazo mnunuzi atazinunua kwa bei ya hali yake ilivyo kwa wakati wa kununua. “Vifaa vyote ikiwa pamoja na vipuri na vifaa vingine vya pembeni vipo na vitauzwa kwa pamoja kama bidhaa moja,” lilisema tangazo hilo. 

Mkataba kati ya Tanesco na kampuni ya Richmond Development LLC umekuwa ni mmoja wa mikataba ambayo ilivuta hisia za watu wengi kitu ambacho kilisababisha kuundwa kwa Kamati iliyokuwa chini ya uenyekiti wa Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe (CCM), ambako kutokana na ripoti hiyo, aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa alijiuzulu. 

Wengine waliojiuzulu ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha ambaye alikuwa Waziri wa Wizara hiyo na kabla ya kuhamishiwa Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kutokana na mapendekezo ya ripoti hiyo, serikali iliahidi kuyafanyia kazi mapendekezo ya ripoti hiyo, ambapo moja ya hatua iliyochukuliwa ni kusitisha mkataba na Dowans.

 CHANZO : HabariLeo

I SMELL SOMETHING FISHY HERE.HII TENDA YA KUTANGAZWA KWA PRESS RELEASE INAZIDISHA SUSPICION YANGU.KWANINI ISIWE TANGAZO LA ZABUNI GAZETINI BADALA YA KU-SEEK ATTENTION KWENYE MAGAZETI,AMBAYO MENGI YAO HUWA HAYANA MUDA WA KU-READ BETWEEN LINES YANAPOPATA STORIES?I SUSPECT KUNA DILI INATAKA KUCHEZWA HAPA.POTENTIAL BUYER WA MITAMBO HIYO ATAKUWA TANESCO (CLICK HAPA NA HAPA KUPATA HINT). ITANUNULIWA KWA UTARATIBU UNAOONEKANA TRANSPARENT (HIVI TRANSPARENCY INA UMUHIMUWOWOTE  KATIKA KUNUNUA BIDHAA BOMU?) KISHA MITAMBO HIYO (AMBAYO "WAMBEA" WANADAI NI INJINI MBOVU ZA NDEGE) ITAISHIA "KUBUMA".DOWANS WAKATI HUO ISHAKUWA KAMPUNI MFU,KAMA MZAZI WAKE RICHMOND.LET'S WAIT AND SEE!

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.