Showing posts with label ENERY CRISIS. Show all posts
Showing posts with label ENERY CRISIS. Show all posts

28 Sept 2008

Picha kwa hisani ya  Chesi Mpilipili
Shirika la Umeme Tanzania,TANESCO,limetangaza ratiba mpya ya mgao wa umeme ambao tofauti na yale masaa matano ya awali   sasa tatizo hilo litadumu kwa masaa kumi kwa siku.Ni muhimu kuwa tatizo hili linakuja wakati tatizo jingine la nishati ya mafuta likiwa halijatulia sawasawa.Angalau katika suala la kupanda kwa bei za mafuta liko nje ya uwezo wetu kwa vile linakuwa determined na soko la dunia.Lakini inakuwa vigumu kuingia akilini pale ambapo takriban kila mwaka lazima TANESCO watangaze mgao wa umeme.Na ninaposema kila mwaka najaribu ku-neglect power cuts za mara kwa mara zisizo na ratiba ambazo zimekuwa kama suala la kawaida huko nyumbani.

Kwa mtazamo wangu,tatizo kubwa zaidi linaloikabili TANESCO sio uhaba wa fedha bali namna linavyoendeshwa kisiasa.Pengine unaweza kudhani ufumbuzi wa tatizo hilo ni kulibinafsisha shirika hilo la umma.Lakini pengine kabla hujafikiri hivyo ni vema ukaangalia baadhi ya mashirika ya umma ambayo kubinafsishwa kwake hakujaweza kuyafanya yamudu uendeshwaji wa mafanikio.Mfano mzuri ni Sherika la Reli (TRC) ambapo huduma zake zimeendelea kuwa mbovu licha ya kupatiwa mwekezaji ambaye pengine mafanikio yake makubwa yamekuwa katika kuishawishi serikali impatie fedha za kumkwamua kila linapotokea tishio la mgomo wa wafanyakazi.Sikatai kwamba kuna some few success stories katika ubinafsishaji wa mashirika yetu ya umma,mfano mzuri ukiwa TBL,lakini mafanikio hayo yanaendelea kubaki kuwa mithili ya matone kwenye bahari.

Uendeshwaji wa TANESCO kisiasa ndio uliopelekea shirika hilo kusaini mkataba wa ajabu na kampuni ya IPTL.Mkataba huo umeendelea kuiumiza TANESCO kwa muda mrefu sana na hakuna dalili za kuisha kwa tatizo hilo.Ahadi za kupitia mikataba mibovu zimeendelea kubaki ahadi huko akina IPTL wakiendelea kuikalia kooni,hali inayopelekea maumivu zaidi kwa wananchi wa kawaida.

Kuna hujuma za kiwango kidogo dhidi ya TANESCo zinazofanywa na wezi wa mafuta ya transfoma,mita za luku na hata nyaya za umeme.Hujuma hizi zinazodaiwa kuwashirikisha baadhi ya watumishi wasio waaminifu wa shirika hilo haziwezi kulinganishwa hata kidogo na hujuma kubwa kama hiyo ya IPTL.Hivi inaingia akilini kweli kwa shirika kulilipa shirika jingine hata lisipotoa huduma inayokusudiwa kwenye mkataba?

Kuna Watanzania wenzetu wanaofanya kila liwezekanalo kuona TANESCO haiishi kulingana na matarajio yake na ya wateja wake.Hawa ni pamoja na wale waliotuingiza mkenge kwenye utapeli wa Richmond.Hawa wanaombea ukame ujitokeze tena ili waje na scams nyingine za kuongeza mabilioni ya shilingi kwenye akaunti zao.Ni katika mazingira ya namna hii ndipo tunapojikuta tukipatwa na hisia kwamba hata kuharibika kwa mitambo ya umeme ya Songas (ambapo imepelekea kuwepo kwa mgao huu wa sasa) kunaweza kuwa hujuma ya hao wenzetu ambao kuumia kwa wengi ndio mafanikio yao.

Kabla ya kuangalia chanzo kikubwa cha utendaji wa kiwango cha chini kabisa kwa TANESCO (mbali na uendeshwaji wa kisiasa) ni vema pia kuangalia sera nzima ya nishati nchini.Katika dunia hii ambayo nchi kama zetu za dunia ya tatu (na hivi karibuni hata kwa nchi zilizoendelea) hazina uwezo madhubuti wa kukabiliana na matukio yasiyotarajiwa (eg kupanda kwa bei ya mafuta katika soko la dunia na the current world economy crisis) ni muhimu kujitengenezea mazingira ya kuzuia madhara ya huko mbeleni.Tukiendelea kutegemea mvua zijaze mabwawa ili mitambo ya TANESCO huko Kidatu na kwingineko ifanye kazi sawasawa,tutazidi kuumia.Pasipo kuwa na chombo madhubuti zaidi ya EWURA na TPDC,ni dhahiri wafanyabiashara wa mafuta wataendelea kuuza nishati hiyo kwa bei wapendazo wao.

Lakini ili yote yawezekane ni lazima kila Mtanzania aweke mbele maslahi ya taifa badala ya maslahi binafsi.Maamuzi mengi mabovu ni matokeo ya kukithiri kwa upungufu wa uzalendo na uchungu kwa taifa letu.Wataalam tunao lakini mara nyingi ushauri wao unapuuzwa kwa vile unaonekana kuathiri maslahi binafsi ya mafisadi.Kibaya zaidi,ushauri mzuri kwa maslahi ya taifa unaweza pia kutafsiriwa kuwa ni uchochezi.Siasa inaelekea kutawala kwenye kila nyanja na professionalism inanyang'anywa nafasi yake na hamasa za kisiasa.Nothing good ever comes out of putting emotions (in this case political sentiments) in front of common sense (hapa ni maslahi ya taifa)


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.