Showing posts with label GOOGLE. Show all posts
Showing posts with label GOOGLE. Show all posts

23 Apr 2015


Unapoingia mtandaoni kwa minajili ya ku-search kitu, uwezekano mkubwa utaenda kwenye mtambo wa kutafuta habari (search engine) wa Google. Sasa, kwenye mtandao huo, ukiingiza neno pale kwenye kiboksi cha kutafutia habari, wenyewe utaanza kubashiri maneno kulingana na herufi husika zinavyotengeneza neno. Mfano rahisi ni huo pichani juu.Ukitafuta 'What is Tanzania..." kabla hujamaliza, Google itaanza kukupa ubashiri wa unachotafuta. Kitu hicho kinajulikana kama Google autocomplete

Sasa hapa chini ni ramani ya dunia kwa mujibu wa Google autocmplete. Yaani ramani hiyo ya dunia, na kama ilivyogawanywa kwa kila bara ni kwa mujibu wa jinsi watu wanavyo-search habari kuhusu nchi husika. Kwa mfano autocomplete searches nyingi kuhusu Canada ni passport, kwa Brazil ni makahaba...na kwa Tanzania yetu ni SAFARI...Well, sio BIA YA SAFARI bali safari za utalii.


Null


Null



Null

Null

Null

CHANZO: i100


10 Sept 2014

Hacked: Hackers revealed nearly 5 million Gmail account details and passwords on the Bitcoin Security site
Takriban passwords milioni tano za akaunti za email za Gmail zimekuwa hacked na kutundikwa kwenye tovuti moja ya hackers wa Russia inayojulikana kama Bitcoin Security. Kufuatia hatua hiyo, kampuni ya Google inayomiliki Gmail imewashauri wenye akaunti za Gmail kubadili passwords zao haraka iwezekanavyo kama hatua ya tahadhari.

Hackers wamesema kwamba asilimia kubwa ya passwords walizo-leak mtandaoni ni za watumiaji wa Gmail nchini Uingereza, Urusi na Hispania, na nyingi ya akaunti hizo 'ziko hai' kwa maana kwamba zinatumika.

Kwa watumiaji wa Gmail watakuwa wanafahamu kwamba mtu akijua password yako ya email anaweza pia ku-access Google Drive na apps kadhaa zinazotumia 'credentials' za ku-log in katika akaunti ya email.

Msemaji wa Google ameeleza kwamba kampuni hiyo inafahamu kuhusu tukio hilo na inawashauri watumiaji wa huduma hiyo kubadili passwords zao.

Kadhalika, Google wanashauri kutumia mbinu inayojulikana kama 'two-steps verification' ambayo kabla ya kuweza ku-access akaunti yako inabidi uingize code uliyotumiwa kwa simu yako.

CHANZO: Habari hii imetafsiriwa kutoka kwa vyanzo mbalimbali mtandaoni




3 May 2009

24 Sept 2008





















CLICK HERE for Preview

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.