Showing posts with label HAPPY NEW YEAR. Show all posts
Showing posts with label HAPPY NEW YEAR. Show all posts

1 Jan 2020




Kwa zaidi ya miaka 10 sasa nimekuwa na utaratibu wa kufanya ubashiri kuhusu yanayotarajiwa kutokea katika mwaka mpya, zoezi ninalolifanya siku ya kwanza ya mwaka mpya husika.

Mwaka huu 2020 unatarajiwa kuwa mgumu sana kwa Tanzania. Na bila kuumauma maneno, ugumu wa mwaka huo utachangiwa na "utawala wa mkono wa chuma" - unaozidi kuota mizizi -wa Rais John Magufuli. 

Moja ya matukio yatakayotawala vichwa vya habari mwaka huu ni pamoja na watu kadhaa maarufu kutoka kada mbalimbali "kupotea." Wahanga wakubwa wanatarajiwa kuwa wanaharakati wanaodiriki kukemea maovu mbalimbaliyanayofanywa na utawala wa Rais Magufuli.

"Kupotea" huko kutaendelea kufanya tishio la "Watu Wasiojulikana" liendelee kuwasumbua Watanzania kama ilivyokuwa mwaka jana 2019.

Kinachotarajiwa kufanya hali kutokuwa nzuri ni pamoja na hofu isiyo na msingi aliyonayo Rais Magufuli kuhusu uwezekano wa yeye kuchaguliwa kuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM na uwezekano wa yeye kushinda nafasi hiyo. 

Hofu hiyo inachangiwa na kile Waingereza wanasema "the guilty are always afraid." Sio siri kwamba Rais Magufuli amejitahidi sana kuwavunja moyo watu wengi tu ambao sio tu walikuwa na matarajio makubwa kwake bali baadhi yao  - ikiwa ni pamoja na mie -walishiriki kumnadi kwa nguvu zote katika kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Kubwa zaidi lililowavunja moyo watu hao ni "valid excuse" ya Rais Magufuli kuwa Watanzania waelekeze nguvu zao kwenye kuchapa kazi ilivyogeuka kuwa excuse ya kuwanyima raia haki zao za msingi. Kukandamiza haki ya kikatiba ya vyama vya upinzani kufanya shughuli zao za kisiasa, kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari, kuwabambikiziawatumbalimbali kesi zisizo na kichwa wala miguu, kuendeleza siasa za chuki, ubaguzi na ukanda wa mchana kweupe, matusi ya hadharani dhidi ya watendaji mbalimbali wa serikali, na mlolongo wa vitu visivyopendeza. 

Kwa vile Rais Magufuli anafahamu kuwa "amewageuka" wengi wa waliomnadi na kumuunga mkono, anajikuta akiwa kwenye kundi la "the guilty are always afraid." Gulity for what? Well, hadi muda huu serikali yake inabaki suspect number one katika "kupotea" kwakda maarufu wa Chadema Ben Saanane ambaye alikuwa critic mkubwa wa Rais Magufuli; suspect number one katika jaribio la kumuua Tundu Lissu; suspect number one katika "kupotea" kwa mwanahabari Azory Gwanda; suspect number one katika yanayodaiwa kuwa "mauaji ya mamia" huko Mkuranga, Kibiti na Rufiji (MKIRU), suspect number one katika kifo cha afisa wa hazina kitengo cha EU, Marehemu Leopold Lwajabe ambaye kabla ya kuuawa alitekwa, akateswa na kubakwa. Unyama usiomithilika.

Serikali ya Rais Magufuli ni suspect number one katika kinachodaiwa kuwa ufisadi wa kihistoria wa fedha za umma, jambo lililopelekea kuondolewa kwa CAG Prof Assad ili ufisadi huo uendelee kufichwa.

In short tema, Rais Magufuli anaishi na hofu ya kitakachomtokea pindi akiwa sio rais, iwe kwa kushindwa uchaguzi, kung'olewa madarakani au kumaliza muhula wake. Kilicho wazi ni kwamba kwa aliyokwishatenda katika miaka hii minne kuelekea mitano, sio rahisi kwake japo kufikiria kuhusu kuwa nje ya nafasi ya urais. 

Na kwa vile mbinu yake kuu ya utawala - UBABE - inaelekea kuwa na ufanisi, kwa maana ya kwamba hakuna jitihada zozote zilizofanyika kupambana na mengi yasiyopendeza yanayofanywa na utawala wake, mwaka huu unatarajiwa kushuhudia ubabe maradufu. Kwa upande mmoja ubabe huo utakuwa mwendelezo tu wa yanayojiri muda huu lakini kwa upande mwingine utakuwa ni mkakati wa kuhakikisha anarudi Ikulu baada ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba.

Talking of uchaguzi mkuu, inatarajiwa kuwa uchaguzi huo mkuu utatawaliwa na hila na vituko na hujuma na mbinu chafu maradufu ya ilivyokuwa kwenye mzaha wa kisiasa uliopewa jina la "uchaguzi wa serikali za mitaa," ambapo pasi haya, chama tawala CCM kilijitangaza mshindi kwa asilimia 99.

Wakati endapo kila kitu kitabaki "constant" (yaani endapo hakutokuwa na mabadiliko), Rais Magufuli na CCM yake watajitangaza washindi wa kishindo kwenye uchaguzi huo mkuu ambapo kura zake na za CCM zitakuwa zaidi ya asilimia 90.

Kadhalika, endapo kila kitu ktabaki "constant," vyama vya upinzani vitaambulia kati ya viti 10 hadi 20 tu (yawezekana vikawa hata pungufu ya 10) vya ubunge kwenye uchaguzi huo mkuu.

Kadhalika, kadri uchaguzi huo mkuu utakavyozidi kujongea ndivyo Rais Magufuli na CCM yake watakavyozidi kuongeza jitihada za kuwanunua wabunge na madiwani wa vyama vya upinzani ili wajiondoe kwenye vyama vyao na kutangaza kujiunga na CCM. Mkakati huo ni sehemu ya jithada za kukomboa majimbo yaliyo chini ya wabunge wa upinzani.

Sambamba na hilo ni kukua kwa "uhasama" kati ya Chadema na ACT-Wazalendo, kitu kitakachochochewa na jitihada endelevu za CCM kuhujumu vyama vyaupinzani sambamba na jitihada za mapandikizi waliomo kwenye vyama hivyo vya upinzani wakiwana jukumu moja tu- kuvikwamisha.

Ukandamizwaji dhidi ya wanasiasa utawakumba pia baadhi ya wana-CCM hususan wanaohisiwa kuwa karibu na Bernard Membe, mwanasiasa anayemnyima usingizi Rais Magufuli kwa kudhani kuwa anataka kuchuana nae kwenye kinyang'anyiro cha kuwania urais kwa tiketi ya CCM.

Kuna uwezekano mkubwa kwa wana-CCM kadhaa wenye majina makubwa kufukuzwa uanachama. Licha ya hatua hiyo, wana-CCM hao watafunguliwa kesi za uhujumu uchumi.

Kwa upande mwingine, mwaka huu utashuhudia angalau mabadiliko mawili ya baraza la mawaziri. Sambamba na hilo, endapo Rais Magufuli atafanikiwa kuwa mgombea pekee wa CCM, inatarajiwa atashinikiza kuteuliwa kwa mgombea mwenza mwingine badala ya Mama Samia. 

Kuna uwezekano wa kujitokeza matishio ya mashambulizi ya kigaidi yatakayohusiana na hali tete iliyopo kwenye mpaka wa Tanzania na Msumbiji. 

Kuhusu Idara ya Usalama wa Taifa, nabashiri kutokea kwa mabadiliko makubwa yanayoweza kupelekea Mkurugenzi Mkuu wa sasa, Diwani Rajabu kuondolewa kwenye wadhifa ho na nafasi yake kuchukuliwa na aliyewahi kuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Idara hiyo, Robert Makungu ambaye awali alitumbuliwa na kuwa RAS huko Tabora. 

Kiuchumi, vyuma vitaendelea kukaza. Na hali inatarajiwa kuwa ngumu zaidi mwaka huu kwa sababu CCM itaongeza jitihada za kukusanya fedha kwa ajili ya uchaguzi mkuu. Neno "jitihada" hapa linamaanisha mbinu chafu na za kifisadi kama ilivyokuwa kwenye skandali ya EPA/Kagoda.

Uchumi pia unatarajiwa kuwa mgumu kwa sababu kuna uwezekano wa baadhi ya nchi wahisani kusitisha misaada yao kufuatia ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu nchini Tanzania. 

Jambo jingine linalotarajiwa kuathiri uchumi na matumizi holela yanayofanywa na serikali ya Rais Magufuli bila kuzingatia idhini yabunge au/na kanuni za bajeti. 

Moja ya matukio ya nje ya Tanzania yanayoweza kuigusa Tanzania ni uhasama endelevu kati ya Rais Museveni na Kagame. Unfortunately, Tanzania ni eneo muhimu kimkakati kwa nchi zote mbili hasa kwa vile ndipo kunapotokea "vita ya kijasusi" kati ya Uganda na Rwanda. Kwamba nchi hizo mbili zinaweza kuingia vitani sio jambo lisilowezekana japo sio rahisi sana.

Kabla ya kuhitimisha makala hii, naomba kusisitiza kuwa ubashiri huu sio exact science bali ni matokeo ya mie mtumishi wako kumudu kusoma mwenendo wa mambo (trends) huko Tanzania. Japo ni rahisi kuhisi kwamba MATAGA na Praise Teram watatafsiri ubashiri huu kuwa ni "kazi ya kibaraka wa mabeberu kuiombea mabaya Tanzania," ukweli ni kwamba ubashiri huu umefanyika objectively.

Mwisho, haitokuwa jambo la kushangaza endapo mgombea urais wa CCM katika uchaguzi mkuu ujao hatokuwa Rais Magufuli. Si kwamba jina lake litakatwa lakini "laweza kutokea la kutokea."

Nimalizie kwa kuwatakia nyote heri ya mwaka mpya 2020.



6 Jan 2016

KWA miaka kadhaa, makala zangu za wiki ya mwanzo wa mwaka huzungumzia matukio mbalimbali yanayotarajiwa kutawala habari katika mwaka husika. Makala hii ni mwendelezo wa utamaduni huo. Inajaribu kufanya ubashiri wa baadhi ya matukio yanayotarajiwa kujiri katika mwaka huu, ndani na nje ya nchi yetu.

Nianze na ubashiri wa matukio ya kimataifa. Mwaka huu ni wa Uchaguzi Mkuu nchini Marekani. Kwa kuzingatia mwelekeo wa kampeni zinazoendelea nchini humo, ninabashiri kuwa Hillary Clinton atafanikiwa kushinda kuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Democrats, ilhali kuna uwezekano mkubwa wa Donald Trump kuibuka mgombea kwa tiketi ya Chama cha Republicans.

Hata hivyo, uwezekano huo unategemea mambo matatu muhimu. Kwanza, kwa wote wawili, nafasi zao kushinda au kushindwa zitategemea mwenendo wa uchumi wa taifa hilo kubwa duniani. Iwapo uchumi wa Marekani utaimarika zaidi, basi Hillary na chama chake watakuwa na fursa nzuri zaidi hasa kwa kutegemea uungwaji mkono wa Rais wa sasa wa nchi hiyo, Barack Obama, kujivunia rekodi ya uchumi chini ya chama chao. Uchumi ukiyumba, Trump, ambaye ni mfanyabiashara tajiri anaweza kuonekana kama chaguo sahihi kuwa rais ajaye wa nchi hiyo.

Jambo la pili, ambalo pia linawahusu wote wawili, ni hali ya usalama nchini humo. Iwapo hali itaendelea kuwa salama kama ilivyokuwa katika miaka minane ya Rais Obama, mgombea wa Democrats, ambaye ninabashiri atakuwa Hillary, atakuwa na nafasi nyingine nzuri ya kujivunia umahiri wa Rais kutoka Democrats kama Obama kulihakikishia usalama taifa hilo linalowindwa kwa udi na uvumba na vikundi mbalimbali vya ugaidi wa kimataifa. Iwapo kwa bahati mbaya kutatokea tukio lolote kubwa la ugaidi, basi hali hiyo yaweza kumnufaisha mgombea wa Republicans, ambaye ninabashiri atakuwa Trump, kwa kigezo chepesi tu kuwa Democrats wameshindwa kuiweka Marekani kuwa salama.

Jambo la tatu ni mwenendo binafsi wa wanasiasa hao wawili. Kwa upande wa Hillary, uwezekano wa yeye kuibuka mgombea wa Democrats utategemea uchunguzi unaoendelea kuhusu matumizi ya barua-pepe binafsi akiwa Waziri wa Mambo ya Nje. Japo Wamarekani wengi hawaonekani kuguswa na yaliyokwishafahamika kuwemo katika maelfu ya barua-pepe hizo, iwapo uchunguzi utabaini makosa makubwa zaidi, basi nafasi ya mwanamama huyo anayewania kuwa rais wa kwanza mwanamke wa taifa hilo itakuwa finyu, na huenda akalazimika kujiondoa katika kinyang’anyiro hicho.

Kikwazo kingine kwa Hillary ni tuhuma zilizoibuka hivi karibuni zinazoashiria uhusika wake katika tenda inayoihusisha Kampuni ya Symbion ambayo inahusu mradi wa uzalishaji umeme nchini Tanzania. Japo alichofanya mwanasiasa huyo sio kitu cha ajabu katika siasa za Marekani na hata katika nchi nyingine, ikigundulika kuwa taratibu zilikiukwa ili kupendelea marafiki zake, anaweza kuathirika vibaya na pengine kulazimika kujiondoa katika harakati zake za urais.

Wasiwasi mkubwa kuhusu Trump ni ile tabia yake ya kuwa kama bomu lililotegeshwa kwa muda (time bomb). Pamoja na kuendelea kung’ara katika kura za maoni miongoni mwa ‘wagombea’ wa Republicans, mwanasiasa huyo hana upungufu wa vioja, na fursa yake ya ushindi itategemea sana jinsi atakavyodhibiti mdomo wake kati ya sasa na wakati wa mchakato rasmi wa chama chake kuteua mgombea. Na hata akiruka kikwazo hicho, bado kuna wasiwasi iwapo Wamarekani watakuwa tayari kumchagua mwanasiasa asiyetabirika. Na endapo watamchagua, basi taifa hilo linaweza kutengwa na nchi nyingi duniani.

Iwapo Hillary hataibuka mshindi kwa tiketi ya Democrats, ninabashiri kuwa nafasi hiyo itakwenda kwa Bernie Sanders, ambaye hata hivyo ana nafasi finyu kumshinda mgombea yeyote atakayepitishwa na Republicans. Na iwapo Trump hatopitishwa, ninabashiri mbadala wake kuwa aidha Ted Cruz au Marco Rubio.

Katika anga hizo za kimataifa, ninabashiri kuwa hali nchini Burundi itakuwa mbaya zaidi ya ilivyokuwa mwaka jana. Kadhalika, ninabashiri hali ya usalama katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuzorota, hasa baada ya jitihada za Rais Joseph Kabila kutaka kuendelea kubaki madarakani.

Kadhalika, ninabashiri kuwa kundi la kigaidi la Boko Haram litaendelea kuisumbua Nigeria, huku kundi jingine la kigaidi la Al-Shabaab likiendelea kuzisumbua Somalia na Kenya. Pia kuna uwezekano wa kuwepo matatizo ya kisiasa huko Afrika Kusini na Zimbabwe yanayoweza kusababisha kung’oka madarakani kwa viongozi wa nchi hizo.

Habari za ugaidi wa kimataifa zinatarajiwa kuendelea kutawala anga za kimataifa huku makundi mawili hatari ya ISIS na Al-Qaeda yakiendelea kuwa tishio duniani, hususan nchi za Magharibi.

Kadhalika, ninabashiri kuwa eneo la Ghuba na Mashariki ya Kati kuingia katika mgogoro mkubwa utakaoligawa eneo hilo kati ya Waislam wa madhehebu ya Sunni wakiongozwa na Saudi Arabia, na wale wa Shia wakiongozwa na Iran.

Kwa huko nyumbani, ninabashiri kuwa Rais Dk John Magufuli ataendelea na utumbuaji majipu, japo habari ninayobaishiri kuwa itatawala zaidi ni kuibuka kwa skandali mbalimbali zilizojitokeza wakati wa utawala wa Rais Jakaya Kikwete na ambazo umma haukuwahi kuzifahamu. Kimsingi, harakati za Dk. Magufuli kutumbua majipu zina kila ishara ya kukutana na madudu yaliyosheheni wakati wa utawala wa mtangulizi wake.

Kadhalika, ninabashiri uwezekano wa baadhi ya mawaziri au manaibu wao kufukuzwa kwa kushindwa kuendana na falsafa ya Hapa Kazi Tu. Kwa vile si vema kumwombea mtu mabaya, ninahifadhi majina ya mawaziri ninaodhani wanaweza kuwa waathirika wa awali.

Vile vile, ninabashiri uwezekano wa kuwepo jitihada za chini chini ndani ya CCM kukwamisha dhamira ya Dk. Magufuli kukabiliana na ufisadi, rushwa, ujangili, biashara ya dawa za kulevya, na maovu mengine. Hata hivyo, jitihada hizo hazitafanikiwa.

Kwa upande mwingine, ninabashiri kuwa Dk. Magufuli ataendelea kunga’ra ndani na nje ya nchi, na dunia itaelekeza macho yake nchini Tanzania kutokana na mafanikio makubwa ya kiuongozi na jitihada za kufufua na kuboresha uchumi.

Kingine ninachoweza kubashiri ni ujio wa sura mpya nyingi katika uongozi ngazi za mikoa na wilaya, huku ikitarajiwa kuwa kama ilivyokuwa kwa Baraza la Mawaziri na Makatibu wakuu, wasomi mbalimbali wakiteuliwa kushika nyadhifa za u-RC na u-DC.

Kwa upande wa vyama vya upinzani, ninabashiri uwezekano wa jitihada za kumng’oa Mwenyekiti wa taifa wa Chadema, Freeman Mbowe, japo haitakuwa jambo la kushangaza iwapo atanusurika. Kwa kiasi kikubwa, uhai wa kisiasa wa Mbowe utategemea uhusiano wake na aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Ukawa, Edward Lowassa.

Eneo ambalo ninashindwa kubashiri kwa uhakika ni hali ya kisiasa huko Zanzibar. Hata hivyo, ninaweza kubashiri bila uhakika kuwa CCM itafanikiwa kulazimisha marudio ya uchaguzi, na kuna uwezekano CUF wakasusia. Uwezekano mwingine ni kurejewa kwa kilichofanyika baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, yaani kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa. Ubashiri sio sayansi timilifu (exact science) kwa hiyo nitahadharishe kuwa baadhi ya niliyobashiri yanaweza kuwa kinyume.

Ubashiri huu umetokana na kufuatilia kwa karibu siasa za kimataifa na za huko nyumbani.


Nimalizie makala hii kwa kuwatakia tena heri na baraka za mwaka mpya 2016. Kwa huko nyumbani (Tanzania), kuna kila sababu ya mwaka huu kuwa mzuri kutokana na dalili za awali za utawala wa Dk. Magufuli kuiondoa Tanzania yetu katika lindi la ufisadi na rushwa, vitu vilivyochangia mno kudumisha umasikini wa nchi yetu. Lakini ili afanikiwe, ni wajibu wa kila Mtanzania kutimiza ‘Hapa ni Kazi Tu’ kwa vitendo.



30 Dec 2009


THE NATION

AND BEYOND

THE Publishers of

MwanaHALISI,

your enviable Kiswahili weekly

in Tanzania,

wish to convey to you, our

warmest Season Greetings

that bring with them

a New Year – 2010.

We have always done

our piece in Investigative

and Public Journalism;

we are now engaged in

marshalling more skills,

improving methods and

producing quality copy

for IMPACT.

We continue to rely

on your readership;

appreciation of our efforts

to produce a copy worthy

your money; attempt at becoming

a real people’s voice;

and your kind and material

support already rendered

and anticipated.

We pledge to do more

to your satisfaction.

Happy New Year!

Hali Halisi Publishers Limited, Tel/Fax 022 - 2760560

Kasaba Street, Plot 57/31A Kinondoni e-mail: [email protected]

P. O. Box 67311 Dar es Salaam, TANZANIA website:www.halihalisi.com.tz

Cel: 0784 440 073/0777 773347


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.