Showing posts with label HASHEEM THABEET. Show all posts
Showing posts with label HASHEEM THABEET. Show all posts

18 May 2011


Hasheem Thabeet afanya.....

Na Brighton Masalu

STAA wa mpira wa kikapu, duniani akicheza katika Ligi ya NBA nchini Marekani, Hasheem Thabeet Manka ‘Super Tall’ (pichani) amefanya kufuru ya fedha baada ya kumwaga fedha ukumbini na kuwaacha watu wagombanie, twende mstari kwa mstari.

Paparazi wa gazeti hili lenye heshima ya nyota tano kwa habari za mastaa Bongo, alishuhudia tukio hilo live wikiendi iliyopita katika Ukumbi wa Bilicanas uliopo Posta, jijini Dar es Salaam ambapo handsome boy anayecharaza fimbo katika muziki wa kizazi kipya, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’ alikuwa akipiga shoo babkubwa.

Awali kasuku wa gazeti hili alimshuhudia Hasheem akikatiza kwa madaha ukumbini humo, akiwa ameongozana na wapambe wake waliokuwa wakimuandalia njia, kisha kukaa sehemu moja na kuanza kula bata kwa mtindo wa ‘tingisha kama imeisha, leta nyingine’.

Wakati shoo ikiendelea Hasheem aliinuka na wapambe wake kuongoza mbele kama kawa, kisha wakaelekea jukwaani alipochomoa burungutu moja la ‘nyekundu nyekundu’ tupu na kumkabidhi Dully Sykes ambaye aliongeza manjonjo baada ya kutuzwa na supastaa huyo.

Hakuishia hapo, aliposhuka jukwaani, alizama mfukoni na kutoa burungutu lingine kisha akalirusha juu na mashabiki kuanza kugombania.

Wakati watu wakiendelea kukanyagana wakigombea mkwanja huo wa ‘sadakalawe’ Hasheem na wapambe wake walitoka nje na kuingia kwenye gari aina ya Hummer na kuondoka kiwanjani hapo.

“Duh! Ebwana ee, jamaa huyu ni noma yaani minoti yote hiyo kaiachia watu wanyang’anyane? Hii ni kufuru, kweli mshkaji fedha imemkubali,” alisika jamaa mmoja akisema ukumbini hapo.

Hasheem Thabeet amerejea nchini hivi karibuni akitokea Marekani anapoishi, yupo kwa mapumziko mafupi. Ni Mtanzania pekee anayeipeperusha bendera ya Tanzania kwenye ligi ya NBA ya mpira wa kikapu nchini humo.

Na yafuatayo ni maoni ya wasomaji wa gazeti hilo

Comment by Eddie Mourice Junior 1 hour ago
Kwa hili umechemka hasheem even if ur money!
Comment by KUU LA MAADUI 7 hours ago
Dogo pesa ni zako lakini kwa hii ya leo umetimba ,sikujua kama na wewe bado mgeni na pesa aise kwa nini unafanya hivyo hujui kama anaweza kufa mtu katika kugombania minoti halafu wewe ukastakiwa kwa kusababisha vifo ,aise umeniuthi unakuwa mrefuuu 22222222 nje ndani mfupi acha ulimbukeni najua hata ndugu zako hawata fuhia upuuzi huo,kama unapesa unakuwasha utumie katika mambo mazuri mungu atakubariki sio kurushia walevi.
Comment by Minja Frank 7 hours ago
Ona mwenzio mwenye kipaji cha mpira wa kikapu kama wewe Dikembe Mutombo wa DRC kajenga Hospital kubwa tu Kinshasa. Wewe wamwaga pesa yako kwenye masanga. Saidia nchi yako!!!
Comment by Alphoncene Gerald 8 hours ago
Sina hata cha kuchangia
Nachoka kabisa
Comment by Miriam John Mndolanga 8 hours ago
Ulivyofanya ndivyo nafsi yako ilivyokutuma, kwa upande wako ni sawa tu ila ni vema hela unayoitolea jasho na kusumbuka sana hadi kuipata ungeiwekeza kwa makundi yenye mahitaji maalum na Mungu atakubarikia zaidi ya ulichotoa. Jifunze kupitie kwa waliofanya kama hivyo wameishia wapi?
Badilika Hasheem, usijijengee sifa mbaya kwa jamii yako.
Comment by julius manning 8 hours ago
huo ni ulimbukeni mkubwa akumbuke akina Tyson walikuwa na hela kuliko yeye lakini leo je
Comment by swalih/waziri 8 hours ago
huo niulimbukieni wakati familia nyengine pesa yakula mtihani wewe pesa unazigawa kwa walevi inshlwa mungu akulaani uje kuzikumbuka sikatowe misaada makanisani msikitini na mashuleni wewe unagawa kwa walevi ili upate jina kuwa umegawa pesa<.
Comment by Matu 8 hours ago
Pesa ni sabuni ya roho lakini pesa nazo zina upepo wake...wakati ukuta...pesa ni kama maua..huchanua na kusinyaaa kwa mtoto wa manka sasa zimechanua...!
Comment by anna [email protected] 8 hours ago
Ama kweli masikini akipata matako huria mbwata, hivi wewe umesahau tabu zote ulizopita, haya baba wakati wako hivi humuoni mwenzio yule modo anaitwa matata kila mwaka anatoa msaada kwa yatima wewe unagawa pesa kwa walevi, una akili nyingi sana mtoto wewe, ina maana hata kule kijijini kwenu huna wanaohitaji msaada, utakuja juta baadae na hao wapambe huta waona sana watakucheka, wapi nice??? unalewa sina
Comment by ikk 8 hours ago
Kweli minoti unaigawa kwa watu wenye ziada tele, tena Klabu? Wakati kuna watoto yatima huko makete wanalea wadogo zao, tena kwa kupika pombe za kienyeji?
Laana huanza polepole!
Comment by Sebastian Salatiel Shemhilu 9 hours ago
DUUH!! HII NI DHARAU YA FEDHA AU JEURI YA FEDHA? HASHEEM TOA PESA ZAKO KWA YATIMA KULIKO KUWAPA PESA WALEVI NAMNA HIYO.MUNGU ATAKUPA ZAIDI.

Comment by Mapresha Getebariadi 9 hours ago
Hela iko wapi wenye fedha hawafanyi hivyo hapo alikuwa anawachanganya warembo waanze kujimwaga kwake. Kama anahela si asomeshe hata yatima 2 tu.
Comment by edmas 9 hours ago

Haya bana, wakati wako huu. Alikuwepo Mr. Nice naye alifanya kufuru ya pesa, sasa yupo apeche alolo, kushnei.
Comment by furaha Tausi 9 hours ago
WEE HASHEEM WEWE KWANINI HIYO HELA USIWASAIDIE HATA WATOTO WA MITAANI JAMANI HATA WALE WATOTO WALIOKO OCEAN ROAD HOSPITAL WANAUMWA KANSA?? MUNGU ATAKULAANI SHAURI YAKO

14 May 2010

Picha kwa Hisani ya SARAH wa Angalia Bongo.

Bila shaka ushaskia msemo wa Kiswahili 'Kufa Kufaana'.Nadhani kwa kimombo ndio tunachoita 'blessing in disguise'.Na ndivyo inavyoelekea kutokea katika sakata la 'ugomvi' kati ya msanii T.I.D na supastaa wa mpira wa kikapu,Mtanzania Hasheem Thabit,anayechezea timu ya Memphis Grizzliers kwenye ligi maarufu ya NBA huko Marekani.Katika pitapita yangu mtandaoni nimekuta habari hiyo imeshadakwa na vyombo vya habari vya kimataifa.Why not wakati Hasheem ni jina kubwa huko Marekani?

Sasa yayumkinika kusema kuwa sakata hilo limemnufaisha T.I.D 'kiaina' kwa vile katika kuripoti habari hiyo jina lake pia limekuwa likitajwa kama inavyoonekana katika habari ifuatayo kwenye mtandao wa kituo cha runinga cha FOX MEMPHIS cha huko Marekani:

MEMPHIS, Tenn. - The agent for Memphis Grizzlies center Hasheem Thabeet has told the team that an alleged incident involving Thabeet and R&B singer T.I.D never took place.


FOX13 Sports Director Matt Stark spoke with Ugo Udezue, Thabeet's agent, by phone Tuesday night, and Mr. Udezue said the allegations that Hasheem had knocked out the singer were completely false.


Udezue acknowledged that Thabeet was in a nightclub last weekend when an altercation broke out, but that the Grizzlies center was in a private section of the club and being protected by three bodyguards at the time, which is the norm for Thabeet when staying in Tanzania. Udezue says his client was immediately removed from the club, and was stunned later to hear the allegations that he had been involved.


Udezue said he believes the singer made the story up as a publicity stunt, and to get his music played on the radio.


Habari hiyo imekamata kasi kwenye mtandao kama inavyoonyesha HAPA.Japo natambua kuwa msanii T.I.D  'ana jina' kiasi chake katika anga za kimataifa,lakini ni dhahiri tukio hili linaweza kuwa limemtangaza zaidi kuliko ilivyokuwa hapo awali.

I just hope ugomvi huo haukuwa publicity stunt na publicity iliyojitokeza kwa T.I.D ni coincidental tu.Otherwise,mastaa wa kimataifa wataendelea kukutana na zahma kama hizo kwani zinaelekea kuwa na manufaa kwa upande mmoja wa wahusika wa tukio.

Ama kweli kufa kufaana!

26 Jun 2009


Kwa mujibu wa MZEE WA CHANGAMOTO,Hasheem Thabeet amenyakuliwa na klabu ya mpira wa kikapu ya Memphis Grizzlies katika draft ya NBA.

Hii ni miongoni mwa njia mwafaka-na nafuu-za kuitangaza Tanzania.Kila la kheri Hasheem.Mafanikio yako ni zaidi ya kufanikiwa kimichezo,umeingia kwenye orodha ya vitambulisho vya Tanzania kama vile Mlima Kilimanjaro,madini ya Tanzanite (japo mafisadi wamepania kuyamaliza kama walivyomaliza dhahabu ilivyo huko Tulawaka),Hifadhi ya Selous na vivutio vinginevyo.Kuna cha zaidi kuhusu mafanikio yako.Umevunja "utamaduni" wa Kitanzania wa ku-settle for less.Angalia timu yetu ya taifa,kwa mfano.Tumekuwa na Maximo kwa muda sasa,na wajuzi wa michezo wanatuambia tumepiga hatua.Kupiga hatua kwa kutoka sare na Senegal?Angalia Simba na Yanga,kila msimu wanahangaika na "wachezaji wa kimataifa",lakini huhitaji kuwa mtaalam wa soka kumaizi kuwa ma-pro" hao ni wababaishaji tu na hawajasaidia kuzifanya klabu hizo zitambe katika anga za soka la kimataifa (na tunaambiwa kocha wa Yanga ni profesa wa soka!Lakini msimu wa pili huu hakuna kombe la kimataifa na wana-Yanga wameridhika,sio na mafanikio ya klabu yao bali kuwa na kocha mgeni "profesa wa soka").Angalia baadhi ya mitazamo yetu.Shangwe na vigelegele tukisikia Zeutamu kakamatwa ilhali majambazi wa Kagoda bado wanapeta,na huku tukizugwa kuwa eti ufisadi wa Meremeta na Tangold ni siri za taifa! (Na kweli ni siri maana ni nadra kwa wizi kufanyika hadharani).

Mafanikio yako yanaweza kuwa chachu kwa Watanzania wengine kuondokana na unyonge wa kifikra kwamba kila baya linalotusibu ndio destiny yetu.Na ni kwa namna hiyo ndio mafisadi wanazidi kutufisadi kwa vile wanatambua unyonge na udhaifu wetu wa kukubali matokeo kirahisi.

Hongera sana,Hasheem.Sote tunajivunia jina lako.

15 Apr 2009


STORRS, Conn. - University of Connecticut junior men’s basketball player Hasheem Thabeet (Dar Es Salaam, Tanzania) has chosen to give up his final season of eligibility and enter his name into the 2009 NBA Draft, it was announced Tuesday.

“After spending time with my family and friends and speaking with Coach Calhoun, I have decided to give up my final year at UConn and enter my name in the 2009 NBA Draft,” said Thabeet. “I have had a great experience at Connecticut and cannot thank my coaches and teammates enough. I look forward to the challenge of playing professionally and know that my time here at UConn has prepared me to be successful in the future. I also want to thank all of the fans in Husky Nation that have followed my career, especially those from my homeland of Tanzania, and hope they will all be as supportive of me at the professional level as they have been to this point.”“Hasheem is more than ready to make the move to the next level,” said head coach Jim Calhoun. “He has been one of the most dominant defensive players in the history of college basketball and I am certain that where ever he ends up in the NBA, he is ready to be equally successful. He is a special player and even more special as a person. He will truly be remembered as one of the great players in UConn history, not only for his accomplishments, but also because of the type of person he is.”

Thabeet was named First Team All-American in 2008-09 by the NABC and the John R. Wooden Award. He was the NABC National Defensive Player of the Year and BIG EAST Defensive Player of the Year in each of the past two seasons and was the 2008-09 BIG EAST Co-Player of the Year. He averaged 13.6 points, 10.8 rebounds and 4.2 blocked shots per game (No. 2 nationally) in 2008-09 and helped lead the Huskies the 2009 NCAA Final Four and a 31-5 final record.Thabeet is the 11th player at UConn to declare early for the NBA Draft and nine of the previous ten were drafted in the first round. Eight of the ten were taken in the lottery portion of the first round

I’m not surprised at this. Thabeet is definitely a lottery pick and could be one of the top three picks. I’d expect Blake Griffin from Oklahoma to go No. 1 overall.
It could now be a long season for the Huskies as they will now need to replace Thabeet as well as A.J. Price, Craig Austrie and Jeff Adrien. Kemba Walker should fill-in nicely at the point and will need Stanley Robinson to play consistently like he did throughout the NCAA Tournament - soxanddawgs.com/2009-04-14 Thabeet is heading to the NBA .

SOURCE: Da Subi

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.