Showing posts with label Habari. Show all posts
Showing posts with label Habari. Show all posts

19 Aug 2016

Magufuli ni dikteta. Yeye ni nani hasa wa kutupangia mikutano ya kisiasa?” Ni kauli ya mtu mmoja kwenye mtandao wa kijamii wa twitter. Kama Magufuli ni dikteta, basi hamia Sudan ya Kusini…au Somalia,” lilikuwa jibu la mtumiaji mwingine wa mtandao huo.
Mada ya ‘Magufuli ni dikteta/Magufuli si dikteta’ ndiyo inayotawala zaidi kwenye mijadala mbalimbali, hususan, ya kijamii, ambako kwa uzoefu wangu, ni kati ya maeneo muafaka kupima maoni na mitazamo ya watu wa kada mbalimbali.
Kwa kiasi kikubwa, kambi inayodai kuwa ‘Magufuli ni dikteta,’ inajumuisha wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ambao sasa wanahamasishana kuhusu mkakati wao mpya uanaofahamika kama ‘UKUTA,’ yaani ‘Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania.’ Sina hakika neno ‘umoja’ limeingiaje hapo kwa sababu tofauti na ‘Umoja wa Katiba ya Wananchi’ (UKAWA) ulioijumisha Chadema na CUF, NCCR-Mageuzi na NLD, ‘umoja’ wa UKUTA unakihusisha Chadema pekee.
Kwa upande mwingine, kambi inayomtetea Dk. Magufuli kuwa si dikteta, inaundwa na wafuasi wa chama tawala CCM, na idadi kubwa tu ya Watanzania wengine wanaoamini kuwa si tu kwamba kiongozi huyo anafanya kazi nzuri bali pia kuna masuala ya muhimu zaidi kwa nchi yao kuliko mikutano/maandamano ya kisiasa.
Hoja ya Chadema, au UKUTA yao, ni kwamba agizo la serikali kuzuia mikutano na maandamano ya kisiasa ni la kidikteta, linakandamiza haki yao ya kikatiba ya kufanya shughuli za kisiasa, na hawahitaji ruhusa ya Rais katika utekelezaji wa shughuli zao za kisiasa.
Sambamba na hilo, malalamiko dhidi ya Dk. Magufuli na serikali yake ni kamata-kamata inayoendelea dhidi ya viongozi na wanachama wa vyama vya Upinzani. Kwa wapinzani, huo si udikteta tu bali pia mkakati wa kuviua vyama hivyo.
Pengine katika hatua hii ni muhimu kuweka bayana maslahi yangu. Katika kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita, nilimuunga mkono na kumpigia kampeni Dk. Magufuli, kwa kutumia haki yangu ya kikatiba na utashi wangu.
Kwangu, uchaguzi ulishamalizika mwaka jana. Tumeshampata Rais na serikali yake. Ninaiangalia Tanzania kama nchi na si kwa ‘lensi’ ya u-CCM au u-Chadema. Uchambuzi huu mfupi unafanyika katika mantiki hiyo, kwamba Tanzania yetu ni muhimu zaidi kuliko vyama vya siasa, na maslahi ya taifa ni muhimu zaidi ya maslahi ya kiitikadi.
Baada ya angalizo hilo, nina hoja kuu mbili ambazo ndio mtazamo wangu rasmi kuhusu ‘Magufuli ni dikteta/si dikteta.’ 
Hoja ya kwanza ni kwamba sidhani kuwa uamuzi wa kuzuia shughuli za kisiasa za vyama vya upinzani ni la busara. Katiba inaviruhusu vyama vya siasa kufanya shughuli hizo alimradi zinazingatia sheria na hazisababishi uvunjifu wa amani.
Kwa kuazima busara za Kighoma Malima, “haki haitolewi kama zawadi. Haki hudaiwa, wakati mwingine kwa nguvu,”. Wapinzani wanaona ni sawia kwao kutumia nguvu kudai haki yao.
Hivi, vyama vya upinzani vikiachwa kufanya mikutano yao (kwa kuzingatia sheria za nchi) kutakuwa na madhara gani hasa? Katika hili, naona kama Rais Magufuli anashauriwa vibaya, hasa ikizingatiwa kuwa kwa kiasi kikubwa kabisa, amemudu kumiliki takriban hoja zote za muhimu za vyama vya upinzani, hususan, vita dhidi ya ufisadi. Binafsi, ninaona zuio hilo la shughuli za kisiasa za wapinzani ni sawa na “kuwapa wapinzani kitu cha kuongea.”
Hoja yangu ya pili ni kwamba ifike mahala vyama vya upinzani vitambue kuwa mikutano na maandamano si shughuli pekee za vyama vya siasa. Kuna masuala mengine mbalimbali yanayoweza kufanywa na vyama hivyo badala ya mikutano na maandamano tu.
Ndiyo, mikutano na maandamano ni haki ya vyama vya siasa, lakini si kipaumbele kikubwa cha Watanzania, hasa katika kipindi hiki ambacho Rais Magufuli anafanya kila jitihada kuiondoa Tanzania yetu kutoka katika lindi la ufisadi ambao kwa kiasi kikubwa umechangia umasikini unaoikabili nchi yetu.
Nimalizie makala hii kwa kukumbushia kuwa huko nyuma, takriban sote – ikiwa ni pamoja na vyama vya upinzani – tuliafikiana kuwa “ili Tanzania yetu iendelee, twahitaji Rais dikteta.” Na yayumkinika kuhisi kuwa kama udikteta wawezesha kuongeza pato la taifa, kuwaibua watumishi hewa, kuwadhibiti ‘wauza unga,’ na kurejesha nidhamu ya ‘asiyefanya kazi na asile,’ basi Dk. Magufuli aendelee tu kuwa ‘dikteta.’
Barua-pepe: [email protected] Blogu: www.chahali.com Twitter: @chahali  

24 Jul 2016


Jana Julai 23, 2016 Rais Dokta John Magufuli alichaguliwa kwa asilimia 100 kuwa Mwenyekiti mpya wa Taifa wa chama tawala CCM, na mtangulizi wake, Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete, kung'atuka rasmi. Ufuatao ni uchambuzi wa kina kuhusu mabadiliko hayo ya uongozi wa juu kabisa wa chama hicho kikongwe, hasa fursa na changamoto kwa Mwenyekiti mpya Magufuli. Karibuni
Check this out on Chirbit

23 Jun 2016


Leo tarehe 23.06.2016 Uingereza itapiga kura ya maoni kuamua kuhusu hatma ya uanachama wake katika Umoja wa Ulaya (EU). Jana, nilipata fursa ya kushiriki katika mjadala mkali katika kipindi cha Dira ya Dunia cha Idhaa ya Kiswahili ya BBC Radio.

Sikiliza kwenye audio hapo chini mjadala huo (unaojiri baada ya taarifa ya habari). Karibuni


 
Check this out on Chirbit

29 Jul 2015

KWANZA ninaomba radhi kwa safu hii kuadimika kwa takriban wiki mbili mfululizo. Hali hiyo ilitokana na sababu zilizo nje ya uwezo wangu.

Pili, ninaomba kutoa angalizo kuwa makala hii, niliiandaa mara baada ya vikao vikuu vya Chama Cha Mapinduzi (CCM) huko Dodoma ambapo hatimaye chama hicho kilipata mgombea wake katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba, mwaka huu. Nimeihariri ili kufidia yaliyojiri kati ya wakati huo na hivi sasa.

Baada ya kugusia hayo, ninaomba kufanya uchambuzi endelevu kuhusu mchakato wa CCM kumpata mgombea wake wa kiti cha urais, wiki mbili zilizopita.

Nitaonekana mwenye chuki binafsi kwa CCM kama sitakipongeza chama hicho tawala kwa kumudu kufikia hatua ya kupata mgombea wake ‘kwa amani.’ Pamoja na kiu kubwa ya Watanzania kufahamu kada gani wa CCM angeibuka kidedea, kwa kiasi kikubwa mchakato wa kupata mgombea wa chama hicho ulikuwa kama ‘referendum’ kwa Rais Jakaya Kikwete, ambaye pia ni mwenyekiti wa taifa wa chama hicho tawala, kuhusu kada maarufu, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa. Swali kubwa lilikuwa, “Je Rais Kikwete ataweza ‘kumtosa’ rafiki yake?” Wengine walilielekeza swali hilo kwa Lowassa na kuwa, “Atakatwa au hakatwi?” hasa kwa kuzingatia kile kilichoonekana kama kada huyo kuungwa mkono na wanaCCM wengi.

Lakini hatimaye, maswali hayo yalipata majibu baada ya Lowassa kutokuwamo katika ‘tano bora.’ Licha ya makada Emmanuel Nchimbi, Sophia Simba na Adam Kimbisa kutangaza kutoafikiana na mchakato wa kuchuja ‘wagombea,’ zilipatikana taarifa kuwa kungekuwa na jaribio la kumng’oa Rais Kikwete katika uenyekiti wake na kuivunja Kamati Kuu ya chama hicho, masuala yaliyoishia kuwa porojo tu.

Hatimaye, chama hicho kilimtangaza Dk. John Magufuli kuwa mgombea wake, ambaye naye alimteua Samia Suluhu Hassan kuwa mgombea mwenza wake, akiandika historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kuwa mgombea mwenza, na iwapo Magufuli akishinda, atakuwa Makamu wa Rais wa kwanza mwanamke nchini Tanzania.

Huko nyuma nilifanya ‘ubashiri’ kuhusu makada gani niliodhani walikuwa na nafasi kubwa ya kupita ‘mchujo wa kwanza.’ Wakati si vigumu kuelewa kwa nini Lowassa alikatwa, bado sijaelewa kwa nini kada aliyetarajiwa na wengi kuwa angepitishwa, Jaji Agustino Ramadhani, hakumudu kuingia japo kwenye ‘tano bora.’ Binafsi ninamsikitikia kada huyo kwani kwa namna fulani, ‘kufeli’ kwake kunatia doa wasifu wake ‘wa kupigiwa mstari.’

Pia ‘kufeli’ kwa kada aliyekuwa akitajwa sana, Makongoro Nyerere, kuliwashtua baadhi ya watu lakini yayumkinika kuhisi kuwa msimamo wake mkali wa kutaka kuirekebisha CCM, na kauli yake ya ‘turudishieni CCM yetu’ ilimtengenezea maadui hususan wanaonufaika na ‘sera za ulaji na kulindana’ ndani ya chama hicho.

Nilibashiri kuwa January Makamba angefanya vizuri, na kwa hakika alifanikiwa kuingia kwenye ‘tano bora,’ hatua ambayo yaweza kumtengenezea mazingira mazuri ya kisiasa iwapo ataendelea kuwa na dhamira ya kuiongoza Tanzania huko mbeleni.

Pia nilibashiri mmoja au wawili wa makada wa kike kufanya vizuri katika ‘mchujo wa kwanza,’ na ilikuwa hivyo. Sambamba na hilo, nilibashiri uwezekano wa kuwa na aidha mgombea urais mwanamke au mgombea mwenza/makamu wa rais mwanamke, na hilo limetokea japo nilitarajia angekuwa mmoja wa makada wa kike waliojitokeza kuwania nafasi ya urais.
Kwa upande mwingine, mwathirika mkubwa kabisa wa mchakato huo ni mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru, ambaye pasipo busara aliamua kujidhihirisha kuwa anamuunga mkono Lowassa. Sidhani kama mzee huyo mwenye uzoefu mkubwa wa kisiasa ana washauri wazuri kwani alipaswa kutambua kuwa laiti ‘mgombea wake’ Lowassa akishindwa basi ‘legacy’ yake nayo itayeyuka. Kwa bahati mbaya kwake, Kingunge atakumbukwa zaidi si kama ‘swahiba wa Baba wa Taifa’ bali ‘mkongwe wa kisiasa aliyeangukia pua kwa kumuunga mkono kada aliyetoswa kwenye kinyang’anyiro cha kusaka urais.’ Waelewa wa mambo wanatahadharisha kuwa kujenga hadhi (reputation) ni kitu kinachochukua muda mrefu na kazi kubwa, lakini kosa dogo tu, linaiondoa hadhi hiyo mara moja. Ni rahisi kubomoa kuliko kujenga.

Kwa upande mmoja kuna hisia kwamba Lowassa anaweza asikubali kupoteza mtaji wake wa kisiasa (political capital) katika kilichoonekana kama kuwa na uungwaji mkono mkubwa ndani na nje ya chama chake, kwa kujiunga Ukawa. Akiwa Ukawa na akagombea urais kuhusu swali kwamba atashinda au la, si rahisi kubashiri kwa sasa.

Lakini kwa upande mwingine, jaribio la kuhama CCM linaweza kumgharimu mno mwanasiasa huyo mzoefu. Moja ya athari za wazi ni uwezekano wa kupoteza stahili kadhaa anazopata kama Waziri Mkuu wa zamani. Kadhalika, akihama CCM, chama hicho tawala kinaweza kutumia kila mbinu ‘kummaliza’ kabisa kisiasa. Kama ana washauri wazuri basi pengine ni vema angekubali tu matokeo na ‘kula pensheni yake’ kama Waziri Mkuu wa zamani, bila kuondoka CCM.

Jingine lililojitokeza katika mchakato huo ni ‘kutoswa’ kwa wasaidizi wakuu wawili wa Rais Kikwete, yaani Makamu wa Rais Dk. Gharib Bilali na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Tafsiri ya haraka ni kuwa katika miaka 10 ya utawala wa Rais Kikwete, tulikuwa na viongozi wakuu wawili wa kitaifa ambao pengine hawakustahili kuwa katika nyadhifa hizo na ndio maana wameshindwa kufaulu katika japo mchujo wa awali. Badala ya kukumbukwa kama Makamu wa Rais na Waziri Mkuu wa zamani, Dk Gharib na Pinda watakumbukwa zaidi kama wasaidizi wakuu wa Rais ambao walifeli ‘mtihani wa kurithi nafasi ya bosi wao.’

Sasa twende kwa Dk. Magufuli. Kwanza, ni kweli kuwa amekuwa akisifika kama mchapakazi. Lakini pengine hili ni matokeo ya kasumba iliyojengeka miongoni mwa Watanzania kwamba kiongozi akitekeleza wajibu wake ambao analipwa mshahara kutekeleza wajibu huo, anaonekana kama ‘malaika.’

Taifa letu limekuwa na uhaba mkubwa wa wazalendo kiasi kwamba kiongozi akitekeleza wajibu au kukemea rushwa anaonekana kama ametoka sayari nyingine. Binafsi, ninamwona Magufuli kama kiongozi wa ‘kawaida’ tu ambaye mara nyingi alizingatia matakwa na matarajio ya mwajiri wake. Kama tunawaona madaktari wakijitahidi kuokoa maisha ya wagonjwa kila kukicha huko hospitalini, au walimu wanaofika mashuleni kufundisha (wengi wao katika amzingira magumu), iweje tumwone Magufuli tofauti kwa vile tu anatekeleza mengi ya majukumu anayotakiwa kuyatekeleza?

Moja ya ‘madoa’ kuhusu uongozi wa Magufuli ni suala la uuzwaji wa nyumba za serikali, suala ambalo halijapatiwa majibu ya kuridhisha. Jingine ni ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali aliyopendekeza hatua stahiki zichukuliwe dhidi yake kama Waziri wa Ujenzi na Dk. Harrison Mwakyembe (aliyekuwa Naibu Waziri) kutokana na ufisadi unaofikia shilingi bilioni 256. Kama ilivyo kwenye uuzwaji wa nyumba za serikali, suala hili nalo pia halijatolewa maelezo ya kuridhisha.

Lakini pengine ni usahaulifu wa Watanzania wengi, au ni kile Waingereza wanaita ‘settling for less’ (kuridhika na kilicho pungufu), ile picha inayomwonyesha Magufuli akipata ‘tiba ya Babu wa Loliondo’ haionyeshi kuwasumbua wananchi wengi wanaoonekana kuwa na matumaini makubwa kwa kada huyo. Binafsi, pamoja na kuheshimu uamuzi wa Magufuli kutegemea ‘tiba hiyo ya porojo,’ nilitarajia msomi kama yeye, tena mwenye taaluma ya Kemia angejihangaisha kutafiti kidogo tu kuhusu ufanisi wa ‘tiba’ hiyo ya kitapeli. Je hili ninalolitafsiri kama ufyongo wa kimaamuzi halitojitokeza katika urais wake iwapo atashinda hapo Oktoba?

Kubwa zaidi ni uwezekano wa Magufuli kuwa ‘Kikwete mpya.’ Sio siri kuwa Rais Kikwete amekuwa ‘shabiki’ mkubwa wa utendaji kazi wa Magufuli. Hilo si kosa. Lakini pengine ‘ushabiki’ huo umechangia pia katika mafanikio ya kisiasa ya kada huyo, na haihitaji uelewa mkubwa wa siasa kubashiri kuwa huenda Magufuli akawa na ‘deni’ kwa Kikwete. Licha ya hofu yangu kuu kuwa tatizo kubwa la ‘urais wa Magufuli’ ni ukweli kuwa ni kada wa CCM ile ile iliyotufikisha hapa tulipo, wasiwasi wangu mwingine ni huo uwezekano wa kuwa na ‘Rais mstaafu by proxy,’ yaani Kikwete kuwa na ‘influence’ kwa ‘rafiki yake’ aliyepo Ikulu.

Kadhalika, ninadhani wengi hatujasahau ukweli kwamba ukosoaji mkubwa dhidi ya kada January Makamba ilikuwa uamuzi wake wa kubainisha visheni ya ‘urais wake’ aliyoiita ‘Tanzania Mpya.’ Ukosoaji huo uliegemea kwenye hoja kwamba mgombea urais kwa tiketi ya CCM atajinadi kwa kutumia ilani ya uchaguzi ya chama hicho. Na japo mgombea ana fursa ya kushiriki kuingiza malengo yake, kwa kiasi kikubwa ilani hiyo huandaliwa na chama chenyewe.

Lakini pengine sasa ndio tunatambua umuhimu wa kuwa na visheni kama ‘Tanzania mpya’ ya kada January kwani hatujui lolote kuhusu visheni ya Magufuli zaidi ya kuambiwa ni kuwa ni mchapakazi. Swali la msingi, je, uchapakazi wake utaendana na matakwa ya CCM katika ilani yake ya uchaguzi? Lakini hata kama chama hicho tawala kitamruhusu Magufuli kuandika ilani yake mwenyewe kwa niaba ya chama hicho, je ukada wake (kama ilivyothibitika katika hotuba yake ya kuombea kura huko Dodoma) hautokuwa kikwazo katika kuirejesha CCM kwenye misingi yake ya awali ya kuwatumikia wanyonge badala ya matajiri ilivyo sasa?

Mara kadhaa nimekuwa nikieleza kuwa moja ya vikwazo vikubwa kwa maendeleo ya nchi yetu ni kutanguliza itikadi ya kisiasa badala ya maslahi ya chama. Kada au mwanae anayefahamika kujihusisha na biashara haramu au ufisadi hachukuliwi hatua kwa vile ‘ni mwenzetu.’ Vyombo vya dola vinashindwa kuchukua hatua kwa kuhofia ‘kuwaudhi vigogo wa kisiasa’ Na CCM imekuwa kimbilio kwa watu wa kada mbalimbali ikiwa ni pamoja na mafisadi kwa vile sio siri kuwa uongozi katika chama hicho ni mithili ya kinga ya uhakika dhidi ya hatua za kisheria

Tanzania yetu sio tu inahitaji Rais ambaye hana deni la fadhila kwa mtu yeyote yule, atakayetumia ipasavyo nguvu anayopewa na Katiba kuiongoza nchi yetu kwa maslahi ya taifa badala ya kuweka mbele maslahi ya chama, na kwa CCM, mwanasiasa anayetambua kuwa chama hicho kimeporwa na wenye fedha –safi na chafu- na kuwatelekeza wanyonge.
Nimalizie makala hii kwa ahadi ya kuendeleza uchambuzi huu katika makala ijayo nikitarajia kuwa muda huo tutakuwa tumeshamfahamu mgombea wa tiketi ya urais kupitia Ukawa. Pia ningependa kuwahimiza Watanzania wenzangu wajitokeze kwa wingi kujiandikisha katika daftari la wapigakura .

JIUNGE NAMI TWITTER https://twitter.com/Chahali AMBAPO NINAJADILI MASUALA MBALIMBALI

8 Jul 2015

Ufuatao ni waraka kutoka kwa Chama cha DP kinachoongozwa na Mchungaji Christopher Mtikila kumpiga mwania nia ya Urais Edward Lowassa

KATIKA UCHAGUZI MKUU HUU
TUSIRUHUSU MAFISADI WALICHEZEE TAIFA
Edward Lowasa ni balaa kwa Taifa!

Democratic Party (DP) inatarajia kufikisha Mahakamani chama cha
CCM pamoja na wanachama wake sita, Edward Lowasa na wengine,
kwa mujibu wa Ibara ya 26 ya Katiba ya Jamhuri ya Tanzania, kwa kosa kubwa sana la kuvunja Katiba na Sheria za Nchi kwa kuanza kampeni ya Uchaguzi kabla ya wakati unaopasa kwa mujibu wa Sheria.

1. Tunao ushahidi mzito unaothibitisha kwamba Edward Lowasa na
wenzake walianza kampeni ya urais ndani ya chama chao kabla ya
wakati, na kwamba chama chao kiliwapa adhabu ya kutofanya siasa
kwa miezi 12. Lakini safari hii Lowasa ameanza kampeni ya urais
Arusha kwa mkutano mkubwa sana wa hadhara wa kampeni haramu
na kumwaga rushwa ya kutisha!

2. Kama ni wadhamini alipaswa kuwapata katika ofisi za chama chake, katika mikoa nane (8) tu Tanganyika na mikoa miwili tu Unguja na Pemba, wadhamini 45 tu katika kila mkoa. Lakini Edward Lowasa amefanya mikutano nchi nzima, ya kuwaahidi maelfu ya wananchi katika kila mkutano wa hadhara, mambo atakayofanya kama wakimpa kura zao awe Rais! Hii ndiyo kampeni halisi, ambayo ni ukiukaji wa Katiba na Sheria za Nchi! Uchaguzi Mkuu unaendeshwa na Sheria, hivyo ni lazima Sheria ichukue mkondo wake dhidi yake kwa kuivunja.

3. Edward Lowasa amevunja Katiba ya Nchi na Sheria ya kiwango cha
fedha kinachoruhusiwa kutumika katika shughuli halali za Uchaguzi,
kiasi kwamba CCM na Taasisi zote za uchunguzi wa kifedha nchini,
upelelezi wa Jinai na Usalama wa Taifa ni mlazima wanayo kazi muhimu sana ya kupata ukweli kuhusu haya mabilioni ya fedha yanayomwagwa nchini na fisadi Edward Lowasa, ameyapata wapi na kwa namna gani, kumehusika ‘’Money laundering’ au la, kama mapato ya mapesa hayo yote ni halali, na kama mapato hayo yote yalilipiwa kodi inayopasa kwa ajili ya Taifa.

Ni marufuku kabisa tena ni makufuru Edward Lowasa kuruhusiwa
kugombea urais, kwa sababu amevunja Katiba ya Nchi na Sheria na
Kanuni za Uchaguzi. Sifa mojawapo ya kustahili kugombea uongozi wa nchi yoyote ni maadili mema na uzingatiaji wa Sheria, Kanuni na
taratibu za Utawala wa Sheria
4. Edward Lowasa, kwa kujimilikisha maeneo nchi nzima kwa kutumia kifisadi Uwaziri wake wa Ardhi, ameliweka Taifa katika hatari kubwa ya mmwagiko wa damu baina ya wakulima na wafugaji, baada ya kueneza nchi nzima makundi ya ng’ombe wake, na kusababisha mapigano makali ya mara kwa mara kila mahali nchini kati ya wafugaji wake na wakulima. Kwa sababu ya uovu huu hata katika kampeni yake haramu Lowasa ameshindwa kusema lolote juu ya kilimo, ingawa ndio uti wa mgongo wa uchumi wa nchi yetu na ndiyo shughuli inayotunza uhai wa asilimia 95 ya wananchi!

Kwa kuwaingilia wakulima katika ardhi yao, kuwaua ovyo, kuwaonea
kiasi cha kufisha matumaini yao katika kilimo, kumeifanya kauli mbiu ya “Kilimo kwanza” kuwa porojo tu ya kisanii!

5. Edward Lowasa ni mwiko kabisa kupewa kugombea urais, kwa
sababu siyo tu aliutumia kifisadi Uwaziri wa Ardhi akajitajirisha na
kujipatia maeneo makubwa ya ardhi nchini kote, bali alitumia kifisadi
zaidi uwaziri wa nchi katika ofisi ya Waziri Mkuu, katika uagizaji wa
mashangingi ya Wabunge, mawaziri, wakuu wa Mikoa na Wilaya.

6. Edward Lowasa alikemewa mnamo mwaka 1995 na Mwalimu Nyerere anayeenziwa na CCM lama “Baba” yao, alipotaka kugombea urais, kwa sababu alikuwa fisadi papa, wala hakuweza kujitetea kwavile utapeli wote aliojitajirishia ulikuwa mezani. Leo baada ya mabiashara haramu mengi na kulipora sana Taifa kukiwa ni pamoja na utapeli wa “kununua mvua Thailand” na kuliibia Taifa mabilioni ya fedha kwa kutumia kampuni hewa ya RICHMOND, huyu ni fisadi-nyangumi. Ni mlemavu wa rushwa tu wa kununuliwa na mapesa machafu anayomwaga Lowasa, anayeweza kumruhusu fisadi Edward Lowasa agombee urais.

Sifa za mtu wa kukugombea Urais zimeelezwa bayana na Mwenyezi
Mungu katika Kumbukumbu la Torati 17:15-20, ambazo Edward
Lowasa hana hata mojawapo! Lowasa awali alikemewa na Mwalimu
Nyerere ambaye CCM wanamuenzi kama “Baba” yao, kuwa hafai kabisa kuwania urais, kwa sababu alikuwa fisadi papa, kama alivyomtangaza hata Reginald Mengi pale alipolazimika kujiuzulu Uwaziri Mkuu kwa ajili ya wizi kwa kampuni hewa ya Richmond, lakini leo akiwa fisadi la kutisha zaidi kuliko papa eti anataka urais!
Si ajabu kwamba magabacholi yalioipora vibaya sana Nchi hii kama Sigh Setti na hata Nazir Karamagi wote wamo katika genge la Edward
Lowasa! Si ajabu hata fisadi Reginald Mengi leo kuungana na fisadi
Lowasa yakizingatiwa machafu yake yeye mwenyewe, na kuhusika kwa Mengi na mauaji ya Chacha Wangwe, pamoja na mpango wa Chadema
wa kumwua Mchungaji Mtikila, waraka feki wa kujaribu kuupotosha
ukweli ukatangazwa kwa ITV yake.

Katika uwaziri wake katika ofisi ya Waziri Mkuu, na katika Uwaziri wakewa Ardhi na Uwaziri Mkuu, Lowasa alifanya ufisadi ambao katika nchi kama China zenye uchungu na maslahi ya mataifa yao angekuwa wa kupigwa risasi hadharani, lakini katika nchi yetu anatafuta urais!

7. Edward Lowasa AFYA yake imempiga marufuku kugombea Urais!
Kwa ajili ya kila ajira duniasni kote, moja ya mashart makuu ni lazima mwombaji awe na afya iliyo bora, ndiyo sababu ni lazima ajira ya kila mwombaji itegemee taarifa ya kitaalamu ya madaktari, inayothibitisha kwamba hana dosari kiafya. Sharti hili ni la lazima kwa sababu:
a. Majukumu yote atakayopewa mwajiriwa atayatekeleza kikamilifu
kwa kutumia viungo vya mwili wake, kwahiyo viungo vyake vyote
ni lazima viwe katika hali iliyo imara kwa ajili ya kazi.

b. Hata kama kwa uthibitisho wa kitaalamu wa madaktari mwajiriwa
anazo akili nzuri kichwani mwake, akiwa na hitilafu katika viungo
vingine vya mwili wake huathiri afya ya akili zake na uwezo wa
utendaji wa akili zake.

c. Kazi ya Rais ni ngumu sana, kwa sababu ni pamoja na kusimamia
shughuli zote za maendeleo ya nchi nzima, na matatizo yote
yanayowatokea wananchi wote kila walipo, na kusimamia
utekelezaji wa majukumu yote ya watendaji wote katika Taifa,
hivyo kwamba maamuzi sahihi yanatokana na afya bora yenye
kuhakikisha uwezo unaopasa wa kiakili wakati wote

d. Hitilafu katika afya hudhoofisha uwezo wa kifikira na kusababisha
maamuzi mabovu, ambayo huleta athari mbaya sana kwa Taifa. Na
udhaifu huo huathiri mpaka maadili na hata uzalendo wa huyo
kiongozi mdhaifu. Kwa mfano akipatikana Rais anayeishi kwa
matumaini, kwa hofu ya kupoteza uhai kabla hajaweka sawa
mambo yake na ya familia na jamii yake atatumikia maslahi yake
zaidi kuliko Taifa, tatizo hilo la afya likawa limelikosesha Taifa
kipaumbele, na kuliangamiza kimaendeleo!
e. Wanaowania kugombea urais ni lazima wachunguzwe kwa makini
sana afya zao, kwa sababu kukifanyika makosa akatawazwa
mwenye hitilafu za kiafya, atakwenda kuwa mzigo mzito sana kwa
Taifa, hususan ugharamiaji wa utunzaji wa uhai wake ndani na nje
ya nchi, kukosekana na umakini anaopasa kuwa nao kwa ajili ya
dhamana kubwa aliyopewa n.k.

Kutokana na AFYA yake kuwa dhaifu sana hata kwa kumwona kwa
macho tu, kabla ya uchunguzi wa kitaalamu ni kwamba Edward Lowasa hawezi kabisa kugombea Urais. Kwani amekosa sifa muhimu sana ya afya bora, ambayo ni ya lazima kwa mtu yeyote anayestahili kupewa dhamana kubwa sana ya kuliongoza Taifa. Pengine hata kugombea urais kwenyewe anatafuta kutokana na hitilafu ya kiafya, iliyosababisha udhaifu katika kufanya maamuzi, hivyo amejikuta kwa bahati mbaya anagombea asichokiweza kabisa.

Ni lazima wagombea wote wa Urais, wa Ubunge na hata wa Udiwani
wachunguzwe kwa makini afya zao kabla ya kupewa kugombea, na hata kuchunguzwa tena katikati ya muhula wa utumishi wao, kama kweli tunalithamini na kuliheshimu Taifa.

Sifa za urais ni wito au uhanga kwa ajili ya Nchi ambao ni zaidi ya
maadili ya kizalendo, maono, vipawa na AFYA BORA. Ni dhana potofu
sana kwamba sifa ya urais ni kushabikiwa na umati wa watu! Kwa
sababu wengi hufuata mapesa na husombwa hata na magari ili umati
wa kishabiki tu upatikane. Lakini kumpenda mtu huwa lazima kuwe na sababu, wakati ushabiki ni pepo mchafu au ‘psychological deficiency’.





24 Jun 2015






IT'S SPORAH CUSTOM HANDMADE WIGS... Finest Quality Handmade Custom Made Wig In Any Shade Or Length To Suit Your Style. 

Add caption

Meet the host at the Sporah Treasure Launch, Award winning Voxafrica UK Sports 360 Presenter Mr. Adesope Olajide
Meet the Co-Host, The Former model Irene Major and the wife of Canadian oil tycoon Sam Mail. 

Irene Major and Vox Africa TV presenter Adesope ready for the day.

WELCOMING THE GUESTS!








INTRODUCING LIVE PERFORMANCE
Add caption
Add caption
Add caption
Chipper Inter Performing LIVE at The Sporah Treasure Launch. 

Team Sporah making sure  that everyone is taken care.of







WELCOMING SPORAH 




And Irene Major had a question for Sporah "WHY HAIR? Why she decided to branch into hair business as a talk show queen.

Sporah talking about the Drive behind SPORAH TREASURE.




Kwa picha zaidi BONYEZA HAPA

17 Jun 2015

I am not in anyway whatsoever pretending to act like mie ndo mwenye uchungu saaana na Tanzania yetu ila kuna vitu ukivisikia kutoka huko nyumbani vinaumiza sana. Nimepata taarifa za kusikitisha sana. Goes like this: kuna watumishi flani wa serikali katika taasisi moja nyeti sana waliokuwa wakitumia utumishi wao katika taasisi hiyo kufanya kila aina ya maovu: kukodisha silaha kwa majambazi, kuwatapeli watu kwa kuwapelekea katika ofisi nyeti ili kujenga imani yao kisha kuwaliza...lakini kibaya zaidi, ninataarifiwa kuwa watu hao baada ya kufukuzwa kazi wanaendelea na uhalifu wao.Kibaya zaidi, hawa sio wahalifu wa kawaida, ni watu waliofunzwa kukabiliana na uhalifu...kwahiyo wanajua mbinu za kuepuka vyombo vya dola.

Kinachoniuma ni kwamba taasisi husika ilichukua uamuzi wa kuwafukuza kazi badala ya kuwapeleka jela, kwa sababu makosa yao kisheria yana adhabu moja tu: JELA. Sasa kwa vile baadhi ya wahusika walikuwa na mhusiano na vigogo flani, wakasamehewa kwa kufukuzwa kazi tu.Lakini naambiwa balaa wanalosababisha huo mtaani ni balaa.

Hili ndilo tatizo kubwa linaloikwaza Tanzania yetu: KULINDANA. Si kwamba wahusika walipoamua 'kuwasamehe' wahusika hao walikuwa hawajui madhara watakayosababisha mtaani, lakini kutokana na ubinafsi wao na kutojali madhara yatakayowakumba Watanzania wenzao, wakaamua kuwalinda wahalifu hao.

Ninaifuatilia taarifa hii kwa karibu, na nitaendelea kuwahabarisha.Nina majina ya wahusika lakini kuna taratibu flani inabidi nizifuate ili nisiishie kuwapa watu kisingizo cha 'kuvujisha siri za nchi.'

Jamani, Tanzania ni yetu sote.Tusifikirie tu kuhusu leo.Kuna kesho, mwaka kesho na miaka kadhaa huko mbele.Tunawaandalia nini wajukuu zetu?

10 Jun 2015

WIKI iliyopita ilitawaliwa na hekaheka za Uchaguzi Mkuu ambapo makada kadhaa wa chama tawala CCM walijitokeza kutangaza nia ya kuwania urais endapo watapitishwa na chama chao.
Kama nilivyoandika katika makala yangu iliyopita, uamuzi huo wa kuwania nafasi hiyo ni haki kwa kila Mtanzania mwenye sifa stahili. Hata hivyo, wingi wa makada wa CCM waliokwishatangaza nia ya kuwania urais, sambamba na idadi ya makada wanaotarajiwa kutangaza nia zao hivi karibuni, imezua maswali makuu mawili.
Kwanza, je utitiri huu wa wagombea ni matokeo ya kukua kwa demokrasia ndani ya CCM au nchini kwa ujumla? Swali hili linaendana na dhana halisi ya demokrasia ambapo wingi wa wagombea, wanachama au vyama vya siasa hutafsiriwa kama ishara za kukua au kustawi kwa demokrasia. Hata hivyo, mara kadhaa dhana hii imethibitika kuwa fyongo, ambapo nchi kadhaa zina idadi kubwa tu ya vyama vya siasa lakini mara nyingi vyama hivyo huwa ni kwa maslahi ya viongozi na sio kwa ajili ya kuwawakilisha wananchi. Licha ya vyama vya siasa, nchi kadhaa zina idadi kubwa ya wabunge, kama ilivyo Tanzania yetu, lakini kwa kiasi kikubwa idadi hiyo haijafanikiwa kumaanisha uwakilishi bora kwa wananchi.
Pili, je kujitokeza kwa idadi hiyo kubwa ya makada wa CCM kunachangiwa na kile kinachodaiwa kuwa urais wa Jakaya Kikwete umeshusha ‘bar’ ya wadhifa huo kiasi kwamba kila mtu anapata ujasiri wa kuitaka nafasi hiyo? Japo ni vigumu kupata mwafaka wa jumla kuhusu miaka kumi ya utawala wa Rais Kikwete, kumekuwa na hisia za mara kwa mara kwamba utawala wake umekuwa wa kirafiki zaidi, au ‘kishkaji’ kama wanavyosema huko mtaani. Teuzi mbalimbali zimekuwa zikitazamwa kama za kirafiki na sio kutokana na sifa stahili za wateuliwa. Na hili linadaiwa kuchangia mabadiliko kadhaa ya kabineti ya kiongozi huyo.
Tumeshuhudia mara kadhaa jinsi Rais Kikwete alivyopatwa na kigugumizi kuchukua hatua stahili dhidi ya watendaji wake, kikwazo kikidaiwa kuwa ni urafiki uliopo kati yake na watendaji hao walioshindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo. Sasa, urais sio uongozi wa nchi tu bali ni ulezi wa viongozi wajao ikiwa ni pamoja na marais wajao. Na ndio maana tumesikia baadhi ya watangaza nia wakijisifu kuwa wamekuwa wasaidizi wa Rais Kikwete kwa muda fulani, wakimaanisha wamejifunza mambo kadhaa kutoka kwake. Kwa hiyo ni wazi ubora au upungufu wake unawagusa walio chini yake, na katika harakati hizi za kupatikana mrithi wake, yawezekana umechangia kutuletea rundo hili la wanaotaka kumrithi.
Lakini iwe ni kukua kwa demokrasia au urais wa Kikwete umeifanya nafasi hiyo kuwa ya ‘kawaida’ kiasi kwamba mwanasiasa yeyote anaweza kujiona anaweza kuimudu, ukweli unabaki kuwa waliojitokeza kuwania nafasi hiyo hawajavunja kanuni yoyote, na Katiba yetu inawaruhusu kufanya hivyo. Hata hivyo, sisi kama wananchi pia tuna haki ya msingi ya sio tu kuwaunga mkono au kuwapinga wanaojitokeza kuwania nafasi hiyo bali pia kuwachambua, kuwapongeza au kuwakosoa. Na makala hii inajikita zaidi katika kuchambua kwa ujumla zoezi hilo la kutangaza nia ya kuwania urais miongoni mwa makada kadhaa wa CCM waliokwishajitokeza hadi sasa.
Kimsingi, ukiondoa Makongoro Nyerere ambaye aliweka bayana kuwa hawezi kutangaza ajenda zake binafsi ilhali mgombea atakayepitishwa na CCM atapaswa kuuza sera zake kwa mujibu wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho, makada wengine wote waliotangaza nia wameongelea masuala yale yale ambayo takriban kila Mtanzania anayafahamu. Nisingependa kuyaorodhesha hapa kwa vile ninaamini kila mmoja wetu anatambua tunachohitaji, tunachostahili kuwa nacho lakini hatuna na kwa nini hali iko hivyo.
Labda jambo moja la wazi ni kwamba nchi yetu ina utajiri mkubwa wa wanasiasa wenye uelewa wa hali ya juu wa matatizo yanayoikabili Tanzania yetu, sambamba na mbinu za kuyatatua matatizo hayo. Takriban kila mtangaza nia ya kuwania urais amejitahidi kwa undani kuyachambua matatizo yetu, wengine wakienda mbali zaidi na kuelezea vyanzo vya matatizo hayo, na kutoa ufumbuzi wa kuyatatua.
Swali la msingi ni hili: walikuwa wapi siku zote na ‘utaalamu huo wa matatizo yetu’ hadi nchi yetu kufikia katika hali hii mbaya tuliyo nayo sasa? Je, yawezekana licha ya takriban wote kuwa walipewa nafasi na Rais Kikwete kuwa mawaziri au manaibu waziri katika kabineti zake, walimhujumu kwa kuficha uwezo wao ili baadaye waje kutumia upungufu uliopo kama mtaji wa kuomba nafasi hiyo ya urais?
Haiingii akilini kabisa kusikia mtu akielezea lundo la matatizo yetu ikiwa ni pamoja na yale ambayo hata baadhi ya wananchi hawayafahamu, na kutoa majibu mengi zaidi ya matatizo hayo, lakini mtu huyo huyo amekuwa serikalini kwa miaka kadhaa pasipo kutumia japo asilimia 0.1 ya ujuzi anaotueleza anao kuhusu matatizo yetu.
Je, wanaotaka kutueleza kuwa haikuwa rahisi kwao kuweza kututumikia kwa uwezo wao wote kwa vile tu hawakuwa marais? Nauliza hivyo kwa sababu ghafla, hata baadhi ya mawaziri ambao waliishia kutimuliwa kwa skandali za ufisadi wanamudu kutueleza kuwa wana ufumbuzi wa matatizo yetu. Ninahitimisha kuwa huu ni utapeli wa kisiasa, kwa kimombo wanasema political conmanship.
Nadhani wanaohisi kuwa Rais Kikwete ameishusha sana ‘bar’ ya urais wanapata nguvu ya hoja hiyo kutokana na wanasiasa kama hao, ambao umaarufu wao hautokani na nyadhifa walizoshika bali skandali zilizosababisha wang’olewe madarakani. Inakera na kuchukiza kuoina wanasiasa ambao pasi kuambiwa na mtu yeyote yule wanajitambua kuwa hawafai lakini leo wanapata ujasiri wa kutaka wapewe urais. Hivi URAIS umekuwa URAHISI kiasi hicho?
Lakini hata tukiweka kando maswali hayo ya msingi, hizi hadithi tamu za kuleta matumaini kwa kila anayezisikia zitawezekana vipi ilhali pindi wakipitishwa na chama chao hawatojinadi kwa ahadi hizo bali zitakazobainishwa kwenye ilani ya chama chao?
Sawa, labda watasema kuwa ukiwa mgombea una fursa ya kushiriki uandaaji wa ilani hiyo, lakini ukweli mchungu ni kwamba CCM haitoafikiana na mgombea atakayekuja na sera za kukiua chama hicho. Ninasema ‘sera za kukiua’ kwa sababu kwa kiasi kikubwa chama hicho kimeachana kabisa na misingi yake ya asili ya kuwa mtetezi wa wanyonge na badala yake kimetekwa na mafisadi. Chama kinachojigamba kuwa ni cha wakulima na wafanyakazi kimekuwa chama cha matajiri na wasomi wasiotaka kutumia usomi wao kwingineko, bali katika siasa (kwa minajili ya ulaji).
Kibaya zaidi, wengi wa makada waliotangaza nia wamekuwa wezi wa sera za vyama vya upinzani, sera ambazo makada hao wamekuwa wakizikejeli mara kadhaa lakini ghafla wameziona zinafaa kwa vile wanaotaka tuwaamini kuwa wanaweza kutuongoza. Ninarejea tena, huu ni utapeli wa kisiasa.
Nimekuwa nikifuatilia kwa karibu maendeleo ya harakati hizo za kutangaza nia ya kuwania urais, kupitia mitandao ya kijamii. Japo Watanzania waliopo kwenye mitandao hiyo ni wachache lakini kwa kuzingatia kanuni za tafiti, wanaweza kuwa sampuli nzuri kuwakilisha mitizamo mbalimbali ya Watanzania wengi kwa ujumla. Nimebaini masuala kadhaa katika ufuatiliaji wangu: kwanza, angalau Watanzania wengi wanafahamu wanasiasa wa aina gani wasiotakiwa katika urais. Lakini hapo hapo kuna tatizo: wanajua wasiyemtaka lakini hawajui wanayemtaka.
Katika hili ninawatumia lawama nyingi ndugu zetu wa vyama vya upinzani hususan UKAWA. Hivi watu hawa wana maelezo yoyote ya maana zaidi ya uzembe kwa kushindwa kutumia fursa hii ambapo ‘CCM wanakabana makoo wenyewe kwa wenyewe’ kumnadi mgombea wao laiti wangekuwa wameshampata? Watetezi wao wanadai UKAWA wapo ‘bize’ kuhangaikia suala la uandikishaji wapiga kura. Hilo ni suala muhimu lakini lisiloweza kuwazuia wao kukamilisha mchakato wa kumpata mgombea wao.
Jingine nililogundua katika ufuatiliaji wangu ni wepesi wa Watanzania kuhadaiwa na maneno matamu yasiyoambatana na uthibitisho wowote ule kuwa ni ya kweli. Mara baada ya hotuba utasikia watu wakidai “aisee huyu jamaa anatufaa haswa…” kisa katoa hotuba nzuri. Tangu lini uwezo wa kutoa hotuba nzuri unamaanisha uwezo wa kivitendo? Kimsingi, Tanzania yetu haijawahi kuwa na uhaba wa watoa porojo. Sisi ni wazuri kweli kwa maneno ila tatizo letu ni kwenye kutafsiri maneno kuwa vitendo.
Ukitaka kujua uwezo wetu katika porojo nenda kwenye vikao vya harusi, au hata kwenye vijiwe vya kahawa. Huko kuna watu wanaongea sio tu kama wamemeza santuri au CD nzima bali pia wana uelewa na utaalamu wa hali ya juu wa fani ambazo wala hawakukanyaga darasani kuzisomea. Sasa kama hayo yanawezekana vijiweni, kwa nini nikiamua kuwania urais nisitumie uwezo wangu wote wa upigaji porojo kuwahadaa watu kuwa mimi ndiye yule waliyekuwa wakimsubiri miaka nenda miaka rudi? Pengine kufikia hapa, ninakuomba msomaji mpendwa tafuta wimbo wa ‘Ndio Mzee’ wa msanii wa muziki wa Bongofleva, Joseph Haule (Profesa Jay) kisha rejea ninachokieleza hapa.
Nimalizie makala hii kwa kuwakumbusha Watanzania wenzangu, uchaguzi mkuu ujao haupo kwa manufaa ya chama au mgombea fulani. Ni kwa ajili yetu sisi wananchi. Sisi ndio wanufaika wa uamuzi bora utakaotupatia mtu wa kuikomboa Tanzania yetu kutoka hapa ilipo na kuifikisha inapostahili kuwepo, na sisi ndio waathirika iwapo tutafanya uamuzi fyongo kama tulivyofanya huko nyuma hadi kujikuta tulipo sasa. Mtaani wanasema ‘akili za kuambiwa changanya na za kwako.’ Ninawasihi Wtaanzania wenzangu kutokuwa wepesi kuhadaiwa na hizi porojo ambazo tumekuwa tukizisikia miaka nenda miaka rudi na nchi yetu inazidi kuangamia kwa umasikini, ufisadi na mabalaa mengine.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.