Showing posts with label Herd Immunity. Show all posts
Showing posts with label Herd Immunity. Show all posts

1 May 2020


Kituo cha runinga cha NTV cha nchini Kenya kiliripoti jana jioni kwamba idadi ya vifo vya korona jijini Dar es Salaam pekee kwa jana vilikuwa 50. Kutokana na unyeti wa maradhi haya, yayunkinika kuamini taarifa hiyo kwa sababu sio rahisi kwa chombo cha habari cha kitaifa kama hicho kutoa taarifa nzito kama hiyo bila kujiridhisha. 

Lakini kwa upande mwingine takriban kila anayefuatilia kinachoendelea huko Tanzania anafahamu fika kwamba serikali ya Rais Magufuli sio tu inaficha takwimu kuhusiana na maambukizi na vifo bali pia inafanya mzaha mkubwa dhidi ya jana hilo.

Taarifa nilizopatiwa alfajiri hii zinaeleza kuwa serikali imetoa mwongozo wa siri kuhusu jinsi ya kuwashughulikia wagonjwa wa korona. Kwa mujibu wa mwongozo huo, mgonjwa atakaa hospitalini wak siki tatu tu. Endapo hali ya mgonjwa haitogeuka kuwa mahututi, atarudishwa akaugulie nyumbani. Mtoa taarifa ananiambia kuwa waraka huo ni sehemu ya utekelezaji wa "herd immunity," mkakati hatari ambao kwa lugha nyepesi ni kuruhusu korona iangamize maelfu hadi mamilioni ya Watanzania kwa matarajio kuwa watajenga kinga dhidi ya ugonjwa huo. 

Licha ya uwezo wake mkubwa kiuchumi, Uingereza iliamua mapema tu kuachana na wazo hilo la herd immunity ambapo japo hadi muda huu idadi ya vifo imezidi 20,000 kwa kufuata herd immunity idadi hiyo ingeweza kuwa kubwa zaidi. Kadhalika, herd immunity ni sawa na kuangamiza watu bure kwa nchi kama Tanzania ambayo ina idadi kubwa ya watu wenye magonjwa kama ukimwi, pumu, kisukaribi, shinikizo la damu, nk ambayo yamethibitika "kuwa na ukaribu na korona" ambapo wenye maradhi hayo wamekuwa waathirika wakuu wa janga hilo. 

Endelea kutembelea blogu hii mara wa mara uweze kupata updates mbalimbali hususan kuhusu janga la korona.

Chukua tahadhari, jikinge na uwakinge na wenzio. Na heri ya Mei Mosi.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.