Showing posts with label Homosexuality in Tanzania. Show all posts
Showing posts with label Homosexuality in Tanzania. Show all posts

11 Jun 2012


Pichani ni shoga maarufu Bilali Mashauzi ambaye ni nadra kukosekana kwenye sherehe za akinadada maarufu Tanzania


SUNDAY, JUNE 10, 2012


MSIMAMO WANGU KUHUSU USHOGA

umeibuka mjadala mkubwa leo twitter kuhusiana na group la facebook la kudai haki za mashoga tanzania. i saw this coming, Mashoga wapo, walikuwepo na wataendelea kuwepo regardless tumewakubali au tumewakataa.

kwanza niseme Imani yangu ya dini, mwenendo wangu wa maisha na jamii ninayoishi nayo hainiruhusu kukubali ushoga. Natamka kuwa siukubali ushoga kwa kuwa kiimani ya dini yangu ni dhambi, lakini pia katika mfumo wa maumbile ya mwanadamu ni kinyume.

Lakini pia Sikubali uzinzi, uasherati, ushirikina, wizi pamoja na dhambi nyengine ambazo kwa utamaduni wa mtanzania ni makosa na dini zote tunazoamini Tanzania ni makosa hali kadhalika.

jambo linalonifanya niandike makala hii ni kuweka wazi kama hata Leo mashoga wakiandamana barabarani kudai Haki zao au nikisikia serikali imeruhusu ndoa za jinsia moja, nitaumia moyoni kwa kuwa kwa imani yangu si sahihi lakini sitatoka kuungana na WANAFIKI kupinga haki za mashoga

Nimetumia neno wa WANAFIKI kwa kuwa watanzania wengi ni WANAFIKI. kati yenu, nani dini yake inaamini uasherati na uzinzi ni sahihi? kipo kitabu cha dini kinaruhusu Uzinzi? je utamaduni wa Mtanzania unaruhusu Uzinzi? na je wewe mwenyewe unaamini Uasherati na Uzinzi ni sahihi?

kama dini yako hairuhusu uzinzi, wewe mwenyewe unaamini uzinzi na uasherati si sahihi, na utamaduni wako unakataa uzinzi na uasherati, UMEFANYA NINI KUHUSU SHERIA YA TANZANIA KAMA UKIKAA NA MWANAMKE/MWANAUME ZAIDI YA MIAKA MIWILI INAITWA NDOA? nguruwe huli ila mchuzi wake unakunywa?

Sisi wenyewe, ndugu zetu, jamaa na marafiki tunasifiana uzinzi, tunafanya uzinzi, tuna facebook groups za uzinzi, kitu ambacho kitamaduni na kidini si sahihi, lakini tukisikia shoga tunapiga kelele.. huo ni unafiki

Wapo waislamu wenzangu ambao ni walevi wa pombe lakini Nguruwe hawali kwa kuwa ni Haramu, pombe ni halali? mlevi ataingia peponi kwa imani yako? Baba Yangu ana msemo "ukiamua kula nguruwe, chagua aliyenona" meaning ukiamua fanya dhambi wewe fanya tu kwa kuwa kwa mungu hakuna dhambi ndogo

Niwakumbushe kwa mungu kuna njia mbili, Ama PEPONI au MOTONI. naamini kutokana na Mafundisho yangu kwamba Shoga, Mzinzi, Mwizi, Muasherati, Muuaji pamoja na dhambi nyengine wataingia moto mmoja hivyo basi ukiamua kataza maovu, acha kwanza wewe na kemea maovu yote bila kubagua kwa kuwa hata usipofanya ushoga ukafanya wizi, utakuwa hujajinasua na moto

sikatazi watu kupinga USHOGA na hata nikikataza mimi sio Mtume wala Rais na wala neno langu sio Sheria ila nasema Siungani na nyie Kwenye kupinga haki ya Mashoga kuoana wakati mmekalia kimya uzinzi, uasherati, na ushirikina ambavyo vyote havikubaliki kwa utamaduni wa mtanzania wala kwa dini tuanzoamini watanzania

*********HAYO NI MAONI YANGU NA NDIO MSIMAMO WANGU*****



Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.