Showing posts with label IFAKARA. Show all posts
Showing posts with label IFAKARA. Show all posts

18 Jan 2012













Picha zote kwa hisani ya Jamii Forums

26 Jun 2009

Ifakara katika picha niliyopiga mwezi Mei mwaka jana.

Mji una neema ya ardhi yenye rutuba inayokubali kilimo cha mpunga,mahindi,na mazao mengine lukuki.Ungetegemea mapinduzi ya kijani yaanzie sehemu kama hizi lakini kama kawaida ya wanasiasa wetu,maneno meeengi huku vitendo vikiishia kwenye michakato,mikakati,vipaumbele,semina elekezi na ubabaishaji mwingine kama huo.Habari hii hapo chini licha ya kunigusa kutokana na ukweli kwamba wilaya ya Kilombero ndio nyumbani,pia inawakilisha matatizo yanayowakabili mamilioni ya Watanzania wanaotegemea kilimo kama njia pekee ya kuwawezesha kuishi.Isome kwanza:

Kilombero, Ulanga wahofia njaa

na Joseph Malembeka, Kilombero

BAADHI ya
wananchi wanaoishi katika wilaya za Kilombero na Ulanga mkoani Morogoro wameiomba serikali kuingilia kati ununuzi holela wa mazao ya chakula unaofanywa na walanguzi sasa.

Ombi hilo limekuja kutokana na ongezeko kubwa la wafanyabiashara kuingia wilayani humo na kununua kwa kasi mpunga ukiwemo uliovunwa na uliopo mashambani.

Wakizungumza na Tanzania Daima juzi, John Lyapi na Selemani Kinana walisema kama serikaliikifumbia macho suala hilo kuna hatari ya wakazi wengi wa wilaya hizo kupata baa la njaa mwaka huu.

Lyapi alisema kwa sasa walanguzi hao wamevamia zaidi katika tarafa za Malinyi na Mtimbira na kuwarubuni wananchi kuwauziampunga wao kwa sh 5,000 kwa debe na huku wakiwafuatilia hadi mashambani.

Alisema kutokana na wengi wa wakulima kwa kipindi hiki wanatokea mashambani inawawia vigumu kukataa kupokea fedha hizo, kwani wengi wao huwa kama wanaanzamaisha mapya majumbani baada ya kuhamia mashambani kwa muda mrefu.

Naye Kinana mkazi wa Kilombero alisema kila kukicha bei ya mazao ya chakulaimekuwa inapanda na kushuka kutegemeana na kuongezeka kwa walanguzi hususanwakubwa.

Alisema endapo serikali itakabiliana kikamilifu na walanguzi haoitasaidia kuondoshwa chakula kingi wilayani humo na kunusuru janga la njaa.

Kwa mujibu wa wakuu wa wilaya hizo Evarist Ndikilo (Kilombero) na DkRajabu Rutengwe (Ulanga) kwa nyakati tofauti walisema tayari halmashauri zimeagizwa kuwatangazia wananchi kuacha mtindo huo.

Walisema mbali na kupiga marufuku kwa wananchi kuuza vyakula pia wanakusudia kuweka sheria itakayowasaidia, iliwaweze kujikwamua na janga la njaa kwa kutouza vyakula hivyo.

CHANZO: Tanzania Daima

Mkuu wa wilaya ya Kilombero anaweza hata kuamuru jeshi la polisi likamate wanaouza chakula,lakini haitokuwa ufumbuzi wa tatizo hilo.Bottom line is,watu wanauza akiba ya chakula chao ili kukabiliana na ugumu wa maisha.Unadhani kuna mkulima anayependa kula mbegu?

Hivi kwanini hizo trilioni moja na ushee zilizotengwa kukabailiana na msukosuko wa uchumi zisiangalie walalahoi kama hawa?Katika mpango huo ambao bado nina wasiwasi unaweza kuishia kuwa-bailout mafisadi kama si kuzua EPA nyingine,wakulima wa kawaida wamepewa kisogo licha ya hadithi za KILIMO KWANZA.

Ukitembelea Ifakara katika kipindi hiki cha mavuno utapata picha moja ya kusikitisha.Wakulima wa mji huo wanatumia takriban robo tatu ya mwaka kulima mpunga (na kilimo cha mpunga kiko very demanding huku kikitegemea kudra za Mungu kwenye hali ya hewa).Baada ya mavuno,mji huo unafurika wanunuzi wa mpunga na mchele,huku wengine wakiufuata hukohuko mashambani.Kwa vile muda huu wengi wa wakulima huwa hoi kiuchumi,bei ya mpunga na mchele huwa ni karibu na bure.Pia baadhi ya wakulima wenye mahitaji mengine muhimu kama vile nguo,sukari,nk huamua kupokea bidhaa hizo badala ya fedha (barter trade) alimradi siku ziende mbele.Na muda si muda,wakulima hao hujikuta wameuza hadi mbegu na kurejea mahala palepale walipoanzia: hawana hela,hawana chakula.

Tuna wizara ya wajibu wa kushukulikia kilimo,na tuna wizara yenye wajibu wa kuwasaidia wakulima kupata masoko ya kuaminika ya mazao yao.Pia tuna wizara inayowajibika na masuala ya ushirika.Kwa makusudi,wizara hizi zimebaki majina tu japo utasikia zinatengewa mamilioni kama sio mabilioni,sio tu kwa ajili ya "kuleta ufanisi" bali pia huduma za ukarimu-chai,chakula,nk.

Tuna takriban Watanzania wenzetu 50 wenye wadhifa wa uwaziri au unaibu waziri.Sehemu kubwa tu ya fedha za walipa kodi inatumika kuwahudumia waheshimiwa hawa.Lakini ni ukweli usiopingika kuwa utendaji kazi wao ni chini ya kiwango.Walikabidhiwa dhamana ya kutekeleza kaulimbiu ya MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA lakini yayumkinika kuhitimisha kuwa sanasana wamefanikiwa kujitengenezea maisha bora wao wenyewe na "wafadhili wao wa kisiasa".


Kwa mmiliki wa makazi hayo pichani juu,habari za Maisha Bora kwa Kila Mtanzania ni kama utani mbaya kwake.Japo amezungukwa na ardhi kijani yenye rutuba,hajui jioni itakuwaje let alone hiyo kesho au msimu ujao wa kilimo na mavuno.Ukimwambia kuwa kuna kaulimbiu mpya ya
KILIMO KWANZA anaweza kukushushia ngumi!

26 Nov 2008


Watendaji wa Ifakara wametakiwa kuangalia uwezekano wa kuzungumza na uongozi wa Kanisa Katoliki juu ya ughali wa tiba unaotolewa katika Hospitali yao ya Mtakatifu Francis. Rai hiyo imetolewa na Rais Jakaya Kikwete katika mkutano wa upokeaji taarifa ya wilaya, mkutano uliofanyika Ikulu Ndogo ya Ifakara juzi. 

Kauli hiyo ilitokana na rai ya wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini hapo ambao walitoa kilio cha tiba ghali katika hospitali hiyo na kutaka serikali iingilie kati. Hospitali hiyo inayomilikiwa na Kanisa Katoliki inadaiwa kutoa huduma kwa bei ghali baada ya wafadhili wake wakubwa wa Uswisi kujiondoa na kuingia Wataliano. 

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya, Evaristo Ndikilo akichangia hoja ya afya, alisema kwamba kwa upande wao walikuwa wakifikiri kupandisha hadhi kituo chao cha afya kukifanya kuwa hospitali. Hoja hiyo pia ilizungumzwa na Mbunge wa Ulanga Mashariki, Celina Kombani juu ya kuwapo kwa haja ya kupandisha kituo hicho, na kueleza mchakato umeshaanza. Kombani pia ni Waziri wa Tamisemi. 

Mwenyekiti wa Halmadhauri ya Ifakara, Hassan Goagoa, alisema ughali wa hospitali hiyo ambayo inatumika pia na mikoa mingine na shughuli za utafiti, kunatokana na kuongezeka kwa gharama za uendeshaji na ingawa walishauriwa kuomba udhamini zaidi wa serikali kwa kuongeza idadi ya vitanda, hali imebaki kwao kama kitendawili. Hospitali ya Ifakara tayari ina vitanda vingi kwa hadhi yake ya kuwa hospitali teule ya rufaa. Rais aliendelea na ziara yake ya Mkoa wa Morogoro ambapo jana alitarajia kuzuru Wilaya ya Kilosa.

CHANZO: Habari Leo

10 Nov 2008







14 Oct 2008

 Choo katika behewa la First Class TAZARA

Habari hii imenisikitisha sana kwa vile inanigusa binafsi.Ili nifike nyumbani Ifakara nina choices mbili ambazo zote si nyepesi.Kuna usafiri wa barabara ambao kwa hakika unahitaji moyo hasa kutokana na ubovu wa barabara kuanzia maeneo ya Ruaha/Kilombero.Kana kwamba hiyo haitoshi,wafanyabiashara wa mabasi ya abiria kwenda mikoani ni kama wameisusa barabara ya kwenda kwetu kwani takriban mabasi yote yaendayo huko ni mikweche ya daraja la kwanza.Mabasi kama Moro Best,Islam na Chimpanzee yamechoka kupita kiasi,na yanaendelea kutumika kwa vile tu  imekuwa kawaida yetu Watanzania kuvumilia mateso.Kikwazo kikubwa cha usafiri wa barabara ni msimu wa masika.Kuna eneo sugu kati ya Mang'ula na Kiberege ambapo kupita kunahitaji zaidi ya sala na trekta linalovuta mabasi yanayokwama kwenye matope.

 Kiza katika Stesheni Kuu ya TAZARA Dar es Salaam.Imagine kama stesheni kuu ni hivyo,stesheni ndogo itakuwaje!

Mkombozi wa wengi alikuwa TAZARA japo mara ya mwisho nilipotumia huduma zao (tena daraja la kwanza) nilitamani kulia:madirisha hayafungiki,taa zinawaka kwa kubembelezwa na vyoo ni kama kwenye baa za uswahilini.Ili ushuke kutoka behewani hadi kwenye platform ya stesheni ni muhimu kuwa mwanamazoezi wa short- au long-jump.Sasa ndio hata huduma hiyo ya kichovu nayo imepunguzwa ambapo kutakuwa na safari mbili tu kwa wiki,moja ya express na nyingine ya ordinary.Sishangai TAZARA kuchukua uamuzi huo kwani shirika hilo muhimu liko mahututi intensive care,hali yake ni mbaya na linasubiri kufa kifo cha kizembe siku si nyingi.

 Adha ya usafiri wa barabara kwenda kwetu Ifakara

Najua siko peke yangu ninaesononeshwa na habari hii lakini japo wanasema kilio cha wengi ni harusi ukweli unabaki kwamba Maisha Bora kwa "wana wa pakaya" yanazidi kuwa a distant pipedream.

22 Apr 2008

NINA LUNDO LA PICHA LAKINI LEO INTERNET IKO SLOW SANA.KEEP ON VISITING THE BLOG FOR MORE PICS.PICHA TATU ZA CHINI NI KUTOKA HOSPITALI YA MTAKATIFU FRANCIS IFAKARA (KUNA SANAMU YA MTAKATIFU HUYO KATIKA PICHA YA TATU).PICHA YA NNE NI MAHINDI YALIYOANIKWA KWENYE LAMI.SIJUI NDIO TEKNOLOJIA AU VIPI LAKINI THE IDEA IS SIMPLE:LAMI INAPATA JOTO UPESI NA KWA KUANIKA MAHINDI KWENYE LAMI BASI YANAKAUKA UPESI,NA MASUALA YA UGALI YANAWEZEKANA NDANI YA MUDA ULIOPANGWA.HIKI NI KIPINDI CHA MAVUNO,KWAHIYO NADHANI VIBAKA WA MAHINDI SIO WENGI.SIDHANI KAMA KATIKA KIPINDI CHA NJAA VIBAKA WATAYANUSURU MAHINDI YALIYOANIKWA BARABARANI.




21 Apr 2008

Makala yangu katika toleo la wiki hii la gazeti la Raia Mwema inaelezea kwa kirefu nightmare niliyokumbana nayo baada ya kuingia mkenge wa kusafiri "first class" ya Tazara.Hiyo ilikuwa wakati naelekea nyumbani Ifakara mkoani Morogoro.Baada ya mateso ya hiari huko Tazara,nikaamua usafiri wa kurudi Dar uwe kwa njia ya Barabara.Nadhani picha zifuatazo zinatosha kukueleza namna Maisha Bora kwa kila Mtanzania yanavyowezekana.Kuna jamaa aliyeziona picha hizi kabla sijaziposti amenitania kwamba heri wale ambao "nyumbani" ni Dar es Salaam na si Ifakara,et al kwani hawahitaji Tazara wala matrekta ya kuvuta mabasi.Nikamuuliza iwapo Dar es Salaam anayozungumzia ni ya Oysterbay na Upanga au ile ya Mwananyamala kwa Ali Maua au Mbagala Kibondemaji...kwani alijibu!?
















15 Apr 2008

MASHABIKI WA SOKA WA IFAKARA WAKIFUATILIA MECHI KATI YA TAIFA STARS NA HARAMBEE STARS YA KENYA
HUYU NYAU ANAJARIBU KU-GOOGLE NENO "UFISADI"
HIKI NI CHOO NDANI YA BEHEWA LA DARAJA LA KWANZA LA TAZARA.EVER HEARD OF A TRAIN FROM/TO HELL?
UFISADI KUTOKA CHINA: HII NI PIRACY YA DARAJA LA KWANZA (ZAIDI YA LILE LA TAZARA).MOVIES TAKRIBAN 40 ZIMELUNDIKWA KWENYE DISC MOJA.BEI MAELEWANO.HI SAMPLE NILINUNUA KWA SHS 5000.NAOMBA KUSISITIZA KUWA NILINUNUA ITEM HII KWA AJILI YA KUKUONYESHA WEWE MSOMAJI WA BLOG HII,NA SIO KUWANUFAISHA MAFISADI.TRUST ME!
UFISADI,CHINESE STYLE
HIVI UNAWEZA KU-GUESS HAPO NI WAPI?I DONT THINK SO.NI RAHISI ZAIDI KU-EXTRACT DAMU KUTOKA KWENYE JIWE KULIKO KUPATA JIBU SAHIHI KWENYE KIJISWALI HIKI.ANYWAY,HAPO NI KWENYE PLATFORM YA KUONDOKEA,STESHENI KUU YA TAZARA DAR ES SALAAM,NA HILO DUDE KULIA NDIO TRENI LA KWENDA ZAMBIA.MWANGA HAPO NI HAFIFU ZAIDI YA ZILE DISCO LIGHTS ZA KIZAMANI.NDANI YA HILO DUDE LIITWALO TRENI NI ADHABU FROM THE MOMENT UNAINGIA TILL UPOTEREMKA UENDAKO ("KUTEREMKA" IS A POLITE WORD,"KURUKA" WOULD BE MORE PRECISE)
ANGALIA KWA MAKINI "TAIFA LA KESHO" (WATOTO) WAKIFUATILIA MECHI YA TIMU YETU YA TAIFA HUKUWAKIWA WAMEKAA CHINI.HAPA NI IFAKARA.RUNINGA ZIPO MADUKANI LAKINI NI AFFORDABLE KWA WATU WACHACHE.UNYANYASAJI WA WATOTO HAPA NYUMBANI UNAPASWA KUTANGAZA JANGA LA KITAIFA.NOBODY SEEMS TO CARE JAPO KUNA WIZARA INAYOHUSIKA NA MASUALA HAYA.NA HAKUNA SEHEMU NZURI YA KUPIMA POROJO ZAMAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA KAMA HUKU UPCOUNTRY.

MORE PICS LATER,STAY TUNED!

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.