NANI KAMTEKA MO DEWJI?
UCHAMBUZI WA KIINTELIJENSIA KWA KUTUMIA MBINU YA 'CONTRARIAN' IJULIKANAYO KAMA DEVIL'S ADVOCATE
Changamoto kuu mbili katika
kufanya uchambuzi wa kiintelijensia (intelligence analysis) ni, moja, kutambua
taarifa stahili/mwafaka za kuzifa
nyia uchambuzi husika, na mbili, ni kitu
kinachofahamika kama 'cognitive bias,' yaani kwa lugha nyepesi ni kama
upendeleo/ubaguzi wa aina flani ambao unatokea akilini bila kuamua kwa makusudi.
Kwa mfano, mchambuzi ambaye
ni kada wa CCM akipewa jukumu la kuchambua suala linalohusu Chadema, basi
anaweza kuwa anaendeshwa na ubaguzi flani kichwani pasi yeye kukusudia.
Kwahiyo, hata katika
uchambuzi huu wa kiintelijensia, huenda kukawa na cognitive bias, lakini hilo
sio lengo langu, na ninadhamiria kuongozwa na taarifa zilizopo kuliko hisia
zangu binafsi.
Kuna mbinu kadhaa za kufanya
uchambuzi wa kiintelijensia, na miongoni mwa mbinu hizo ni "Contrarian
Techniques" ambazo ni "Devil's Advocacy," "Team A/Team B,"
"High Impact/Low Probability Analysis" na "'What If' Analysis."
Katika uchambuzi huu,
nitatumia mbinu ya Devil's Advocacy ambayo hutumika zaidi katika mazingira
ambayo tayari kuna hisia flani 'kali' kuhusu suala husika.
Tukio ninalolifanyia
uchambuzi wa kiintelijensia ni kama nilivyotanabaisha kwenye kichwa cha habari,
nalo ni la kutekwa kwa Mkurugenzi wa kundi la Makampuni ya Mohamed Enterprises,
Mohammed Dewji almaarufu 'Mo.' Tukio hilo lilitokea jijini Dar es Salaam jana alfajiri,
katika eneo la ukumbi wa Colosseum.
Mbinu ya uchambuzi wa
kiintelijensia ya Devil's Advocacy ni mwafaka katika tukio hili kwa sababu kuu
moja: utafutaji wa taarifa za kiintelijensia uliofanywa tangu baada ya
kupatikana taarifa za tukio hilo, kwa kutumia njia kuu moja ya ukusanyaji
taarifa za kiintelijensia – Open Source Intelligence (OSINT) – unaonyesha kuwa
serikali inatupiwa lawama kuwa ndiyo iliyohusika kwenye tukio hilo.
Na kama ilivyoelezwa awali,
mbinu ya Devil's Advocacy ni mwafaka katika mazingira ambayo tayari kuna hisia
flani 'kali' kuhusu suala husika, na hapa hisia hiyo kali ni uhusika wa
serikali.
Katika kutumia mbinu hii,
kuna hatua kadhaa zinazopaswa kufuatwa na mchambuzi, na miongoni ni kama ifuatavyo:
· →Kuorodhesha
hisia mbalimbali
· → Kuchagua hisia
kuu moja au mbili katika hizo mbalimbali, inayoonekana kuwa na uzito zaidi
· →Rejea taarifa
zilizopatikana kuhusiana na tukio husika
· →Onyesha ushahidi
unaoweza kufanya hisia husika kuwa na uzito zaidi.
Kwahiyo tuanze uchambuzi huu
kwa kuorodhesha hisia mbalimbali kuhusiana na kutekwa kwa Mo Dewji. Hisia hizi
zimekusanywa kwa kutumia ukusanyaji taarifa kupitia vyanzo vya wazi, yaani Open
Source Intelligence (OSINT).
Hisia hizo ni kama
ifuatavyo:
·
Mo Dewji
ametekwa na serikali
·
Mo Dewji ametekwa
na watu wanaohusiana na serikali lakini hawakutumwa na serikali (rogue
elements)
·
Mo Dewji
ametekwa na watu wanaotaka kuichafua serikali
·
Mo ametekwa na
wahalifu
·
Mo ametekwa na
washirika/maadui zake kibiashara
·
Mo hajatekwa, ni
maigizo tu.
Tupitie kila hisia ili
kuweza kubakiwa na hisia kuu moja au mbili.
Mo Dewji ametekwa na
serikali:
Uzito wa hisia: Rekodi ya
serikali sio nzuri katika usalama wa raia mbalimbali, kuanzia "kupotea"
kwa kada wa Chadema Ben Saanane na kwa mwanahabari Azory Gwanda, na idadi
isiyojulikana ya watu waliopotea huko MKIRU. Kadhalika, matukio yanayohusisha
'watu wasiojulikana' na shambulizi dhidi ya Mbunge Tundu Lissu yanaongeza uzito
kwenye hisia hii. Vilevile ukweli kwamba eneo la Colosseum limezungukwa na
nyumba mbalimbali za viongozi na taasisi muhimu zenye ulinzi mkali, na hakukuwa
na jitihada za kukabiliana na watekaji, zinaweza kuashiria uhusika wa serikali.
Mapungufu ya hisia: Serikali
haina incentive katika kumteka Mo Dewji. Kwamba kama kulikuwa na tatizo lolote kama
ni kisiasa au kiuchumi basi angeweza tu kukamatwa au "kubebeshwa kesi ya
kodi" na TRA au "kesi ya ufisadi" na TAKUKURU. Ieleweke kuwa Mo Dewji
alijiweka mbali na masuala ya siasa, na yayumkinika kuamini kuwa hana maadui wa
kisiasa. Kadhalika, high profile ya Mo Dewji ilitosha kuijulisha serikali kuwa
lolote litakalomtokea mfanyabiashara huyo litakuwa na athari kubwa kwake.
Hitimisho: Mapungufu dhidi
ya hisia hii ni makubwa zaidi ya uzito wake. Kwahiyo inaondolewa.
Mo Dewji ametekwa na rogue
elements ndani ya serikali:
Uzito wa hisia hii: Kwa
kurejea matukio mbalimbali hususan yanayohusishwa na Daudi Albert Bashite,
yayumkinika kuhisi uwepo wa mkono wa rogue elements huko TISS au kwingineko.
Uzito zaidi kwenye hoja hii unachangiwa na jinsi Bashite alivyojaribu kuwa
mstari wa mbele kuelezea kuhusu suala hilo, badala ya kuwaachia polisi wafanye
kazi yao.
Mapungufu ya hisia hii: Huenda
mkakati huo ungefahamika mapema kwa taasisi kama TISS na hivyo kuweza kuzuiliwa
kabla haijatekelezwa. Hata hivyo, kuna mapungufu katika hoja hii ambayo ni
ishara zinazoashiria mapungufu makubwa ya kiutendaji ya TISS, kiasi kwamba
inawezekana taarifa hizi hawakuzipata.
Hitimisho: Hisia hii ina
mantiki, na itaendelea kuwepo katika uchambuzi huu
Mo Dewji ametekwa na watu
wanaotaka kuichafua serikali
Uzito wa hisia hii: Uzito upo
kwenye ukweli kwamba upinzani mkubwa dhidi ya serikali ya Rais John Magufuli
upo zaidi ndani ya CCM kuliko nje ya chama hicho. Ikizingatiwa kuwa kuna takriban
miezi 24 tu kabla ya uchaguzi mkuu ujao, wapinzani wa Magufuli wanaweza kufanya
tukio hilo kwa minajili ya kumchafua, na pengine kujenga hoja ya kumwekea
vikwazo kwenye kugombea urais mwaka 2020. Kwa kuzingatia incentives, wapinzani
hao wana kila cha kunufaika na kidogo cha kupoteza (a lot to gain and only a
little to lose).
Mapungufu ya hisia hii:
Mkakati mkubwa kama huu ungeweza kunaswa kirahisi tu na vyombo vya dola kama
vile TISS na hivyo kuweza kuudhibiti. Hata hivyo, kama ilivyokuwa kwenye hisia
iliyopita, kuna ishara za mapungufu ya kiutendaji kwa taasisi hiyo, hali ambayo
inaweza kuwa iliruhusu mpango huu kutekelezwa.
Hitimisho: Hisia hii ina
mantiki, na inaendelea kubaki kwenye uchambuzi huu.
Mo Dewji ametekwa na
wahalifu:
Uzito wa hisia hii: Kuna taarifa za uwepo wa magenge ya kihalifu
ya kimataifa nchini Tanzania. Taarifa ambazo hazijathibitishwa kuwa watekaji ni
'wazungu' zinaweza kusaidia kuipa uzito zaidi hisia hii.
Mapungufu ya hisia hii:
katika mazingira ya kawaida, wahalifu hao wasingependelea sehemu kama Colesseum
kuwa eneo la utekaji kwa sababu kuna idadi kubwa na nyumba za viongozi na
taasisi za serikali ambazo zina ulinzi mkali. Hata hivyo, yawezekana kuwa
wahalifu hao walishafanya reconnaissance ya kutosha na kubaini mapungufu
husika.
Hitimisho: Hisia hii japo
ina mantiki lakini kiuhalisia inaonekana kuwa sio yenye nguvu. Kwahiyo
inaondolewa.
Mo Dewji ametekwa na washirika/maadui
wake kibiashara:
Uzito wa hisia hii:
mfanyabiashara wa kimataifa kama Mo Dewji hawezi kukosa maadui. Lakini pia
masuala ya biashara za kimataifa yanaweza kuzua migongano hata miongoni mwa
washirika katika biashara husika. Kama ilivyokuwa kwenye hisia iliyotangulia,
yawezekana watekaji hao walishasoma mapungufu ya kiusalama katika eneo la
tukio.
Mapungufu ya hisia hii: Kama
ilivyokuwa kwenye hisia iliyopita, mazingira ya eneo la tukio hayakuwa mwafaka
kwa watu wenye lengo la kumdhuru mtu kuyatumia kutekeleza lengo hilo. Hata
hivyo, yawezekana wahusika walishabaini mapungufu ya kiusalama katika eneo
hilo.
Hitimisho: Hisia hii ina
mantiki lakini uwezekano wa washirika/maadui wa Mo Dewji kumteka katika
mazingira yalivyokuwa, haiingii sana akilini. Hisia hii inaondolewa kwenye
uchambuzi huu.
Mo Dewji hajatekwa ni
maigizo tu:
Uzito wa hisia hii: Kwa kuzingatia
matukio ya huko nyuma, yawezekana tukio hili ni mchezo wa kuigiza tu.
Mapungufu ya hisia hii:
Mchezo wa kuigiza ili iweje? Hakukuwa na tukio la muhimu ambalo jamii ilipaswa "kuzugwa
na kutekwa kwa Mo Dewji."
Hisia hii inaondolewa kutokana na kukosa mashiko.
Kwahiyo, hisia zinazosonga
mbele ni mbili,
• Mo Dewji ametekwa na watu wanaohusiana na serikali lakini
hawakutumwa na serikali (rogue elements)
• Mo Dewji ametekwa na watu wanaotaka kuichafua serikali
Hisia hizi mbili zinaweza
kimsingi kuwa moja, kwa sababu watu wenye nia ya kuichafua serikali wanaweza
kuzitumia rogue elements kufanya kazi hiyo. Lakini pia rogue elements hizo
zinaweza kuwatumia watu wanaotaka kuichafua serikali kutekeleza azma hiyo.
Na kwa minajili ya kuweka
rekodi sawia, kiongozi wa rogue elements hizo ni Daudi Albert Bashite, bila
shaka. Na hili linaweza kuongezewa uzito na ukweli kwamba jana Bashite
alijigeuza kama RPC au Mkuu wa Kanda Maalum ama sio msemaji wa Jeshi la Polisi.
Je ni ile "mchawi aliyemroga marehemu hujifanya mwenye uchungu kuliko wafiwa"?
Uchambuzi wa kiintelijensia
sio sayansi timilifu kwa asilimia 100 (it's not exact science), na kwa maana
hiyo inawezekana kabisa sababu ikawa nyingine nje kabisa ya hizi
nilizozichambua.
Ninachofanya hapa sio
kujifanya mjuaji bali kuchangia kwenye 'body of knowledge,' sambamba na kuhamasisha
mjadala kuhusu suala hili ambalo linaweza kuwa na athari kubwa kwa Tanzania.
Hitimisho: Ingependeza
kuhitimisha makala hii kwa kutamka bayana kuwa "hisia kuu ni hii"
lakini hisia mbili zilizoweza kuvuka mchujo zinabaki kuwa mtazamo ninaona ni
mwafaka zaidi.
Je wewe una mawazo gani?