Showing posts with label JAKAYA MRISHO KIKWETE. Show all posts
Showing posts with label JAKAYA MRISHO KIKWETE. Show all posts

22 Dec 2010



Picha kwa Hisani ya Mjengwa

Japo haipendezi kuona jeshi la polisi likitumia nguvu kubwa kuzuwia haki ya kikatiba ya wananchi kuandamana au kugoma kwa amani,lakini nashawishika kutowaonea huruma wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma kufuatia kichapo walichopewa na askari wa FFU.Hivi sio hawa wana UDOM waliochangisha fedha kwa ajili ya kampeni za Jakaya Kikwete?Na sio hawa waliotoa tamko la kukemea haki ya kikatiba ya wabunge wa Chadema kususisa hotuba ya Kikwete huko Bungeni?

Najua si vyema kutoa lawama za jumla kwani si kila mwana-UDOM aliafiki wazo la kujikomba kwa Kikwete lililopelekea wanafunzi hao kuchangia fedha zao za ngama ili kumwezesha mwanasiasa huyo aliyekuwa mgombea wa CCM arejee madarakani.

Na kama tulivyoandika baadhi yetu wakati wa kampeni za uchaguzi wakati tunaonya madhara ya kuirejesha CCM madarakani,haijachukua muda kwa  Kikwete na serikali yake kuwalipa fadhila wasomi hao wa Dodoma.

Majuzi nilimsuta mwanahabari mkongwe Dunstan Tido Mhando baada ya kupata taarifa kuwa serikali imemtosa ubosi wa TBC.Nilimsuta kwa vile naamini wakati Tido anaombwa na WALIOMUOMBA kuja kuendesha TBC alikuwa anafahamu fika kuwa aidha anapanda mchicha au bangi,na mavuno yangekuwa mchicha au bangi,respectively.Ukikubali kutumiwa lazima ukubali kitachotekea itapojiri "expiry date" yako.

Sasa tunashuhudia kundi jingine la walioingizwa mkenge.Hawa wasomi watarajiwa wa UDOM walijikomba kwa Kikwete na CCM na kuchangia kampeni zake,sijui wakitarajia kuwa pindi mwanasiasa huyo akirejea Ikulu angewapatia muujiza gani sijui!

MLIPANDA BANGI SASA MNATARAJIA KUVUNA MPUNGA?

6 Oct 2010

BABA BABA BABA HUYO BABA BABA BABA BABA BABA HUYO...TUMBA TUMBA TUMBA TUMBA HILO TUMBA TUMBA HILO TUMBA TUMBA HILO...KIKWETE HOYEEEE...NILISEMA WALA RUSHWA NAWAJUA KAMA WAPIGA TUMBA ILA NAWAPA MUDA WA KUJIREKEBISHA...AKINA CHAHALI WANAOHOJI KUHUSU DEADLINE KWANINI HAWAHOJI PIA KUHUSU DEADLINE YA KUJIFUNZA KUPIGA TUMBA? (ACTUALLY,NIKIREJEA IKULU  NTAMSHTAKI HUYU KIJANA HUKO KIBEREGE KWA MZEE MAGU%^&£$%^)


NIMEISHIWA NA AHADI SASA.NGOJA NIJARIBU HII: NAWAAHIDI WATANZANIA KUWA MKINICHAGUA TENA NITAHAKIKISHA KILA MTANZANIA ATAKUWA NA TUMBA YAKE NYUMBANI AMBAYO UKIPIGA TU UNAPATA MAISHA BORA...SI NILIWAAMBIA KUWA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA YANAWEZEKANA?

UFISADI OYEEE,TUMBA OYEEEE

MIE NI ZAIDI YA MORIS NYUNYUSA.ACTUALLY,ZILE NGOMA ZA ULE WIMBO WA TAARIFA YA HABARI YA RADIO TANZANIA NI KAZI YANGU.MCD (BADO YUPO TWANGA?)  NA ALI JAMWAKA AJIRA YENU MASHAKANI.

HUYU ZUMA ANATAKA KULETA HABARI ZA VUVUZELA,HAJUI KAMA MIE MTOTO WA MJINI.AI NEMA NEMA,AI NEMAA AAA,AI NEMA NEMA USIPONEMA LEO UTANEMA LINI

NEMA MWANANGU NEMA
SITAKI WATANZANIA WANIKUMBUKE KWA EPA,KAGODA NA RICHMOND PEKEE.NATAKA PIA WAELEWE KUWA MIE MIE KWA KUYARUDI NDIO MWENYE,IWE ENZI ZA NZAWISA,MAYENU AU HATA MSONDO....SHALO SHALO TINA TINA,YAANI SHAA MTU MZIMA (HEHEHEEE NGWEA NA JAY MO MPO?HATA MIE BONGOFLAVA NAZIJUA PIA.SI MNAWAONA WANABONGOFLEVA KWENYE KAMPENI ZANGU?)

UWEZEKANO WA JAKAYA KIKWETE KUMALIZIA MAUMIVU YAKE YA KUBWAGWA NA DOKTA SLAA (KAMA HAWATACHAKUACHUA KURA) KWENYE UALIMU KATIKA CHUO CHA SANAA BAGAMOYO NI MKUBWA (HOME BOY COMES BACK HOME....DON'T FORGET KIKWETE NI MKWERE).TUSICHOWEZA KUWA NA UHAKIKA NACHO NI WHETHER ATAKUWA MWALIMU WA KUPIGA NGOMA (TUMBA) AU DANSI STUFFS HE FANCIES KAMA PICHA ZA HAPO JUU ZINAVYOONYESHA

HAPPY RETIREMENT MR SOON-TO-BE EX-PRESIDENT

27 Sept 2010




Video zote kwa hisani ya Coby

NAOMBA MSAMAHA KWENU WAFANYAKAZI WAPENDWA KWA KUWATOA MACHOZI YA UCHUNGU BAADA YA KUANGALIA VIDEO HIZO.LENGO LANGU SIO KUWATIA UCHUNGU BALI KUWAKUMBUSHA JEURI YA JAKAYA KIKWETE KWENU.VILEVILE VIDEO HIZI ZINAWEZA KUSAIDIA KUMPA KIKWETE AIBU YA KUUDANGANYA UMMA KUWA HAJAWAHI KUKATAA KURA ZENU WAFANYAKAZI WAPENDWA.

NAWASIHI MACHOZI YENU YASIMWAGIKE BURE BALI MTAFSIRI UCHUNGU WENU KWA KUMPATIA MGOMBEA ALIYETANGAZA HADHARANI KUWA ANAZIHITAJI SANA KURA ZENU.MGOMBEA HUYO NI DOKTA WILLBROAD SLAA WA CHADEMA.KIKWETE ALIWAADHIRI HADHARANI KUPITIA KWENYE RUNINGA,NINYI MUMSHIKISHE ADABU FARAGHANI KWENYE KISANDUKU CHA KURA HAPO TAREHE 31/10/2010.

OMBI LA BLOGU HII NI KWA KILA MFANYAKAZI ALIYEUMIZWA NA JEURI HIZO ZA KIKWETE KUHAMASISHA MKE,MUME,DADA,KAKA,MWANA,SHANGAZI,BINAMU,MJOMBA,JIRANI,MPANGAJI,SHOSTI,MSHKAJI,MWENYE NYUMBA NA YEYOTE YULE UNAYEFAHAMIANA NAE,KISHA UWAHAMASISHE WAMNYIME KURA KIKWETE NA CCM YAKE NA BADALA YAKE KUMPIGIA KURA DOKTA SLAA NA CHADEMA.CHONDE CHONDE WAFANYAKAZI,MSIACHIE NAFASI HII ADIMU.
Video zote kwa hisani ya Coby

25 Sept 2010

(Katuni kwa hisani ya FEDE)
Si maneno yangu,bali nimenukuu kutoka gazeti la Mwananchi


...Kikwete aliyeonyesha uchovu katika mkutano huo alishuka ghafla jukwaani na kuondoka baada ya kuwatambulisha wagombea ubunge, akiwaacha wananchi wakimsubiri...Hata hivyo, kuteremka ghafla jukwaani kwa Kikwete kulimaliza mkutano huo bila kufungwa rasmi huku wananchi wakibaki na maswali juu ya mustakabali wa mkutano huo uliofunguliwa na mwenyekiti wa CCM wilaya.Marwa Mwita, mkazi wa Mugumu, alisema bado anajiuliza ilikuwaje mgombea huyo akaondoka bila ya kuaga.

"Hilo ni jambo la kujiuliza, lakini huenda amechoka na anasahau alitakiwa kufanya nini. Kwanza amechelewa kufika, hakuomba radhi, kahutubia mambo yale yale ya kila mwaka".

Jamani wapiga kura,huyu mtu kachoka na anastahili apumzishwe.Yawezekana kabisa kuwa udhaifu katika uongozi wake unachangiwa na uchovu huo ambao chanzo chake kimeendelea kuwa muujiza kama ulivyo muujiza wa nani anamiliki kampuni ya kifisadi ya Kagoda.

Na ukichanganya na utitiri huu wa ahadi za kuchakachua.....

(Katuni kwa hisani ya FEDE)

12 Sept 2010












Sijui ndio dalili kuwa mwenendo wa kampeni unakwenda ovyo au ni ubabaishaji tu,lakini "mkwara" uliochimbwa na mnajimu mahiri,Sheikh Yahya Hussein,kwamba anampatia Rais Jakaya Kikwete ulinzi wa majini ni suala linalopaswa kukemewa kwa nguvu zote.Na ukweli kwamba mtajwa-i.e. Kikwete- amekaa kimya ni ushahidi tosha kuwa ananufaishwa na majini hayo.

Kwa baadhi yetu tunaofahamu yanayofanyika "nyuma ya pazia" (behind the scene) hatushtushwi kihivyo na habari hizo kwa vile siasa za Tanzania na ushirikina ni kama samaki na maji.Hakuna msimu mzuri kwa waganga wa kienyeji kama huu wa uchaguzi ambapo wanasiasa wababaishaji wanajaribu kupata msaada wa nguvu za giza ili wapate ushindi.

Awali,Sheikh Yahya alitoa tishio kuwa atakayejitokeza kuwania nafasi ya urais na Kikwete atakutwa na mauti.Well,so far tukio pekee la kutishia uhai wa mwanasiasa katika harakati za uchaguzi wa mwaka huu ni kudondoka jukwaani kwa Kikwete wakati anazindua kampeni zake kwenye viwanja vya Jangwani.Whether majini yaligoma kutumikishwa au Kikwete alikiuka masharti ya mganga wake Sheikh Yahya leaves a lot to be desired.

Binafsi natafsiri tishio hili jipya la Sheikh Yahya kama mkakati mufilisi wa Kikwete na CCM yake kuwatisha wapiga kura.Yea,kwani kama si hivyo kwanini basi mhusika asikanushe hadharani na kusema "ulinzi pekee nilionao ni huu unaotolewa na Idara ya Usalama wa Taifa".Hawa ni wataalam wa ulinzi wa viongozi na wanalipwa kwa ajili ya kazi hiyo.Sasa kama kuna ulinzi mwingine wa nguvu za giza,na ambao Kikwete anauamini,basi pengine ni muhimu kuokoa fedha za walipa kodi kwa kusitisha ulinzi anapotatiwa na "walinzi binadamu" na abaki na hayo majini ya Sheikh Yahya.

Samahani kama nitakuudhi lakini nashawishika kueleza kuwa napatab tabu sana kuelewa kwani pamoja na madudu yote haya-from sera to ushirikina,from afya mgogoro to kurudia ahadi za 2005 as if hii ndio mara ya kwanza kwa JK kuwania urais-bado kuna Watanzania wenzetu wanatamani mwanasiasa huyu na chama chake warejee madarakani.Jamani,hivi Kikwete na CCM wafanye nini zaidi ili mfikie hatua ya kusema "aah sasa basi,just go away!"?

Hivi mkiweka kando ushabiki,hizi "ahadi za fotokopi" anazotoa Kikwete zilishindikana vipi kutekelezwa katika miaka yake mitano aliyokuwa madarakani?Hata kama angejitetea kuwa muda mwingi alikuwa nje ya nchi kutalii bado alikuwa na baraza kubwa la mawaziri ambalo lingeweza kabisa kutekeleza maagizo yake.

Kama mnampenda kwa dhati basi bora msimpe kura ili aweze kupumzika kwa amani kwani kumrejesha tena Ikulu hapo Oktoba ni kumbebesha mzigo ule ule uliomshinda katika miaka mitano tunayomaliza.Hii ni kwa faida yake na yenu.Na anazidi kuwaonyesha kuwa badala ya kutegemea mambo halisi kufikia malengo yaliyokusudiwa,sasa kageukia majini.Nchi haiwezi kuongozwa kwa msaada wa majini.Na kamwe Tanzania haiwezi kupiga hatua kama miongoni mwa wasaidizi wa Rais ni majini.

MPIGA KURA,SHEIKH YAHYA AMEKUPA SABABU NYINGINE KATI YA NYINGI ZILIZOPO ZA KUMNYIMA KURA YAKO KIKWETE.KURA KWA KIKWETE ITAKUGHARIMU MIAKA MITANO IJAYO AMBAPO LICHA YA UFISADI,FEDHA ZA WALIPAKODI ZITATUMIKA KULIPA FADHILA KWA MAJINI WANAOMPATIA ULINZI WAKATI HUU WA KAMPENI.

KUMBUKA JINI LIKITOKA KWENYE CHUPA HALIRUDI.IN CASE YOU FORGET,VIDEO IFUATAYO ITAKUKUMBUSHA(GENIE IN A BOTTLE)



5 Sept 2010


Courtesy of NGURUMO

4 Sept 2010

Tunafahamu kuwa mgombea wa CCM,Jakaya Kikwete,ni mahiri sana katika kutoa ahadi.Wakati wa kampeni zake za kuwania urais kwa mara ya kwanza mwaka 2005 alitoa rundo la ahadi ambazo hata angekuwa na uwezo wa kutekeleza basi ingebidi awe rais wa milele.Kwa makusudi,badala ya kufanya marejeo ya ahadi zake lukuki za 2005,Kikwete ameendelea kutoa ahadi zaidi akijaribu kuwaghilibu Watanzania kuwa safari hii akipewa madaraka atazitekeleza.Swali la msingi ni kipi kilichomzuia kuzitekeleza katika kipindi hiki (2005-2010) na kipi kitamwezesha kutekeleza ahadi hizo katika awamu ijayo (2010-2015).

Alipokuwa kwenye kampeni zake huko mikoani aliahidi (bila aibu) kuwa tatizo la umeme sasa litakuwa historia.Last time aliposema hayo,walikuja matapeli wa Richmond.Sijui safari hii watakuja wasanii gani "kuvuna wasichopanda".Angekuwa na busara,angewaeleza Watanzania kwanini umeme umeendelea kuwa tatizo sugu nchini.Ufumbuzi wa tatizo hilo hauwezi kupatikana kwa ahadi zaidi ya zilizokwishatolewa.Kikwazo kikubwa katika upatikanaji wa ufumbuzi wa tatizo la umeme ni maslahi binafsi na ufisadi.Kuna watu wanaoombea Tanzania iwe kizani kila siku ili wauze jenereta zao.Kuna wengine wanaotaka umeme uendelee kuwa tatizo ili wapate fursa ya kutengeneza dili za kifisadi kama za IPTL,Richmond na Dowans.Na Kikwete anawajua sana watu hao lakini hana nia wa kuwachukulia hatua.Ikumbukwe kabla ya kuukwaa urais,Kikwete alishawahi kuwa Waziri wa Nishati!!!

Kadhalika,katika mwendelezo wa ahadi,Kikwete ameahidi kuleta ufumbuzi wa kudumu wa tatizo la maji jijini Dar es Salaam.Utadhani kwamba tatizo hilo halikuwepo wakati wa utawala wake,au limeanza majuzi.Na kama hiyo haijatosha,akaahidi tena kuwa daraja la Kigamboni litajengwa kwa vile zabuni ya kumpata mkandarasi imeshakamilika.Kwanini iwe baada ya kumchangua tena na sio alipochaguliwa 2005?Haihitaji hata elimu ya chekechea kutambua kuwa ahadi hizi ni hewa.ZITAENDELEA KUWA AHADI TU.

Ukimsikiliza kwa makini utagundua kuwa Kikwete hayuko serious na anachoongea.Pengine ni kwa vile anafahamu kuwa hahitaji kuwa serious kupata tena nafasi ya urais.Pengine ni tatixo la upeo tu.Hata hivyo,kumlaumu JK ni kumwonea kwa vile kama ilivyokuwa Desemba 2005,come Oktoba this year HATAJICHAGUA MWENYEWE KUWA RAIS BALI ATATEGEMEA KURA ZA WATANZANIA.Mwaka 2005 waliompigia kura na kumpa ushindi wa kishindo wanaweza kuwa na excuse kwa kudai walikuwa HAWAMJUI VEMA.Five years later,naamini kila Mtanzania anafahamu udhaifu wa kiongozi huyu.Kumrejesha tena Ikulu kwa miaka mingine mitano ni kosa ambalo litawagharimu sana Watanzania.

Ikumbukwe kuwa kama atarejea tena madarakani,kuna uwezekano mkubwa wa kuendesha nchi kwa mtindo wa BORA LIENDE kwa vile hiyo itakuwa awamu yake ya mwisho kwa mujibu wa Katiba.Kama ameweza kuwapuuza Watanzania katika kipindi hiki cha miaka mitano inayoisha huku akielewa fika kuwa itambidi awabembeleze tena wampigie kura mwaka huu,kwanini basi asiwapuuze zaidi kwa vile hatagombea tena urais hapo 2015?

Ni muhimu kwa Watanzania kutambua kuwa tusipoziba ufa tutajenga ukuta.Ufa wetu kwa sasa ni Kikwete na CCM yake.Tukiwarejesha tena madarakani hapo Oktoba tutakuwa tumejichimbia kaburi refu.Tuweke kando ushabiki wa vyama vya siasa na tuangalie maisha yetu na hatma ya taifa letu.Tusifanye mzaha kwa kuendekeza kauli "JINI LIKUJUALO HALIKULI LIKAKWISHA" (i.e. Bora Kikwete na CCM kwa vile tunawajua kuliko hao akina Dkt Slaa na Chadema tusiowajua).Problem is,jini hili safari hii litatumaliza na kutukomba kila kitu.Wameiba mabilioni ya EPA,wametutapeli na Richmond,Dowans,IPTL,Kiwira,Meremeta,Tangold,nk na hawajatosheka.Tukiwarejesha tena madarakani watatukomba kila kitu.

Bahati nzuri Mungu si Athumani.Ametuonea huruma na kumwibua mkombozi Dokta Wilbroad Slaa.Hii ni nafasi adimu,na ndio maana nguvu za giza zimekuwa zikimwandama.CCM wanajua bayana kuwa Dkt Slaa ana dhamira ya dhati kuwatumikia Watanzania.Hawampingi kwa vile ni mwanasiasa wa upinzani bali wanahofia atawafungua macho waliolala,na pia atawapora mtaji wao- yaani masikini wanaonunuliwa kwa pishi za mchele na sukari huku wakiahidi maisha bora "hewa".

Kama wewe si fisadi basi unapaswa kuwa na NIA,SABABU na UWEZO wa kumtosa JK na CCM yake hapo Oktoba.Maisha Bora ya Kweli (na sio ya kuzugana) Yanawezeka,Ila tu sio kwa wazushi hawa waliopo madarakani bali kupitia kwa Dokta Slaa na CHADEMA.

1 Sept 2010

Kama waliweza kuchakachua kadi zao wenyewe kwenye kura za maoni watashindwaje kufoji za Chadema?Na wameshamgeuza sehemu ya kufanyia mazoezi kuzuga kama anavyotabasamu hapo chini kwa kupewa "two hundred thousand USD za $300,000/="!!!!


30 Aug 2010

Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) kimewasilisha rasmi pingamizi dhidi ya mgombea wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Jakaya Kikwete kwa madai ya kukiuka Sheria ya Gharama za Uchaguzi (iliyosainiwa na Kikwete kama Rais).Imedaiwa kuwa Kikwete amenongeza mishahara ya watumishi wa umma kinyume cha taratibu,na inatafsiriwa kuwa ni rushwa.

Stay tuned!

Kwa mujibu wa mwana-Jamii Forums

26 Aug 2010

Rostam Aziz
Katika kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2005,mfanyabiashara controversial Rostam Aziz alitumia raslimali zake nyingi kuhakikisha mgombea wa nafasi ya urais kwa tiketi ya CCM,Jakaya Kikwete,anashinda kwa gharama yoyote ile.Na kutokana na utajiri mkubwa alionao pamoja na mbinu zake mbalimbali,mchango wake ulimsaidia sana Kikwete kuingia Ikulu,na sasa ni Rais wetu anayeomba tena ridhaa ya kutuongoza kwa miaka mitano ijayo.

Kati ya mwaka 2005 (baada ya Kikwete kuingia Ikulu) na sasa,Rostam ameibuka kuwa kiumbe mwenye nguvu za kutisha sio tu ndani ya CCM bali kwenye siasa za Tanzania kwa ujumla.Lakini kubwa zaidi katika kipindi hicho ni kwa mfanyabiashara huyo kuhusishwa na tuhuma mbalimbali za ufisadi na Kikwete na serikali yake kushindwa kuwaridhisha Watanzania kwamba "hamkumbatii swahiba wake huyo".Haihitaji kurejea namna Rostam alivyohusishwa na ufisadi wa EPA (Kagoda) na ujambazi wa Richmond.
Jakaya Kikwete

Mwaka 2010,yaani mwaka huu,Rostam anaelekea kurejea tena ulingoni japo si kwa wazi sana.Ushahidi wa kimazingira unaonyesha kuhusika kwa mfanyabiashara huyo katika kampeni za Kikwete.Vyombo vya habari vinavyomilikiwa na Rostam vimekuwa vikiendesha kampeni ya chuki dhidi ya mgombea urais kwa tiketi ya Chadema,Dokta Wilbroad Slaa,mwanasiasa anayeonekana kuwa  tishio kwa mfanyabiashara huyo na vitendo vyake dhidi ya maslahi ya taifa.
Magazeti yanayomilikiwa na Rostam

Na kama hilo la vyombo vya habari vya Rostam kumuandama Dkt Slaa halitoi mwangaza wa kutosha basi taarifa kwamba mwandishi mwandamizi wa kampuni ya Habari Corporation (inayomilikiwa na Rostam),Muhingo Rweyemamu,anatajwa kuwa mratibu wa kampeni za Kikwete.Itakumbukwa kuwa mwaka 2005,waliokuwa waandishi waandamizi wa Habari Corporation,Salva Rweyemamu na Dokta Gideon Shoo walitumika sana kwenye kampeni hizo.Baada ya kuingia Ikulu,Kikwete "alimzawadia" Salva ukurugenzi wa habari wa Ikulu,nafasi anayoshikilia hadi sasa.
Muhingo Rweyemamu

Kama alivyo Salva,Muhingo anasifika kwa uwezo wake wa hali ya juu wa kujenga hoja.Kwa bahati mbaya au makusudi,uwezo huo pia unatumika ipasavyo kutengeneza fitna.Wengi watakumbuka namna Dokta Salim Ahmed Salim,mmoja wa wana-CCM waliokuwa wanawania kuchuana na Kikwete,alivyoundiwa zengwe kubwa na kumhusisha na kundi la Hizbu la huko Zanzibar.Inaelekea kuwa mbinu hizohizo zimeanza kutumika dhidi ya Dokta Slaa,na kuna kila sababu ya kuamini kuwa kuna mengi yatakayoibuliwa dhidi yake.
Salva Rweyemamu  (kushoto) na Gideon Shoo

Yayumkinika kuamini kuwa waandishi wa habari wanaotumiwa kumchafua Dokta Slaa na Chadema kwa ujumla wanafanya hivyo kwa minajili ya "kupeleka mkono kinywani".Kubwa zaidi ni sapoti ya Rostam kwa Kikwete.Wakati mwaka 2005 alijibidiisha ili kufanikisha maslahi yake binafsi ya kibiashara (na amenufaika kweli-kwa kuangalia ishu za Kagoda na Richmond/Dowans) safari hii Rostam anahaha kumzuia Dokta Slaa kwa vile anafahamu fika kwamba laiti mwanasiasa huyo wa Chadema anayesifika kwa msimamo wake mkali dhidi ya ufisadi akiingia Ikulu,zama za mafisadi kutumia jeuri yao ya fedha "kuendesha serikali kwa remote control" itakuwa imefikia kikomo.

Kwahiyo,Dokta Slaa na Chadema kwa ujumla wanapaswa kuelewa kuwa safari hii Rostam ana "special mission" ya kuhakikisha "survival (kusalimika) yake.Atatumia kila raslimali aliyonayo kuhakikisha Dokta Slaa haingii Ikulu.Anafanya hivyo akifahamu wazi kuwa rais yeyote mwenye kujali maslahi ya nchi yake "atamkalia kooni" mfanyabisahara huyo na washirika wake.

Hata hivyo,kwa vile si fedha za Rostam au wanahabari wake zitakazopiga kura kwenye uchaguzi mkuu,bali mimi na wewe pamoja na kila Mtanzania aliyechoshwa kuona nchi yetu ikigeuzwa "shamba la bibi",ni muhimu kwa wapiga kura kusema HAPANA.Tusitoe fursa kwa watu wenye maslahi binafsi kuipeleka nchi yetu kwenye maangamizi.Na ni muhimu zaidi kutambua kuwa baadhi ya watu hao wana utata wa kutosha tu kuhusu asili ya mahali walipozaliwa.Hiyo inamaanisha kuwa "wakishaiingiza Tanzania kwenye mtaro",watakuwa na sehemu ya kukimbilia.

KILA MTANZANIA MWENYE KUITAKIA MEMA NCHI YETU ANAPASWA KUPAMBANA NA WAHUNI WA KISIASA WANAOTAKA KUTUWEKEA MADARAKANI VIONGOZI WANAOWAMUDU NA HIVYO KUENDELEA KUTUFISADI KAMA ILIVYOKUWA KATIKA KIPINDI CHA MIAKA MITANO ILIYOPITA.


INAWEZEKANA,TIMIZA WAJIBU WAKO

6 Aug 2010

SERIKALI ya Awamu ya Nne imeendelea kukumbwa na jinamizi la matumizi mabaya ya fedha za umma (ufisadi), baada ya kubainika kuwa imetumia sh trilioni 1.7 kwa kipindi cha mwaka 2008/2009 bila maelezo ya kina.

Uchambuzi huo ni ule uliotolewa na Shirika lisilo la kiserikali la ‘Agenda Participation 2000’ juu ya ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iliyotolewa hivi karibuni, umethibitisha kuwepo kwa ufisadi mkubwa wa fedha za walipa kodi.

Uchambuzi wa ripoti hiyo ya CAG kwa mwaka 2008/2009, umeonyesha ufisadi wa kutisha serikalini kwa kiasi cha sh trilioni 1.7 uliofanyika ndani ya mwaka huo.

“Jumla ya fedha za serikali ambazo ama zilitumiwa vibaya au wahusika wameshindwa kutoa maelezo ya kuridhisha jinsi fedha hizo zilivyotumiwa inafikia shilingi trilioni 1.7. Kwa kweli fedha hizi ni nyingi sana…”, ilisema sehemu ya taarifa hiyo ya shirika hilo.

Kiasi hicho kilichofujwa ni sawa na fedha zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya bajeti ya Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi na ile ya Miundombinu katika mwaka huo wa fedha.

Kiasi hicho pia ni sawa na mara mbili ya fedha zilizokuwa zimetengwa mwaka huo kwa ajili ya Wizara ya Afya ambayo ilipata sh bilioni 589 na mara nne ya kiasi kilichokuwa kimetengwa kwa ajili ya Wizara za Kilimo na Maji, ambazo zilitengewa shilingi bilioni 379 na shilingi bilioni 309 katika mwaka wa bajeti wa 2008/2009.

Kwa ujumla, ufisadi huo unahusisha makadirio ya fedha zilizotumiwa vibaya katika eneo la manunuzi yasiyo ya kawaida ya sh bilioni 12.8, masuala ambayo hayakushughulikiwa tangu kaguzi zilizopita sh bilioni 95.7 na misamaha ya kodi ya sh bilioni 752. 3.

Maeneo mengine ni udhaifu katika ulipaji wa mishahara uliofuja sh bilioni 3. 078, masuala yahusuyo malipo ya marupurupu sh milioni 395.8, ukiukwaji katika ununuzi wa magari wa sh bilioni 4. 018, pamoja na kiasi cha sh bilioni 203.2 zilizotumiwa vibaya au kupotea katika serikali za mitaa.

Katika ufisadi huo, Wizara ya Maliasili na Utalii ndiyo imetajwa kama mfano wa kusikitisha wa wizara zilizotumia vibaya fedha za umma.

Sehemu ya ufisadi uliofanyika ndani ya wizara hiyo inahusisha ubadhirifu wa sh milioni 12 zilizolipwa kama mishahara zaidi ya viwango halali vya mishahara ya wafanyakazi na sh milioni 53 zilizolipwa bila kutolewa viambatanisho vya kuhalalisha malipo hayo.

Sh milioni 445 pia zilitumika kulipa wastaafu, marehemu na wafanyakazi walioachishwa kazi, fedha ambazo walengwa hawakujitokeza kulipwa lakini hazikurudishwa hazina.

“Jambo jingine la kusikitisha ni kwamba Wizara ya Maliasili na Utalii ilishindwa kueleza yalipo mapato ya jumla ya shilingi bilioni 19.6,” ilisema sehemu ya uchambuzi huo wa Agenda Participation ikirejea ripoti ya CAG.

Mbali na wizara hiyo ya Maliasili na Utalii, wizara, idara au taasisi nyingine za umma zilizopata taarifa mbaya za fedha kutoka kwa CAG ni Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Jeshi la Polisi na Ofisi ya Makamu wa Rais.

Nayo Serikali ya Norway imeendelea kudai kurudishiwa sh bilioni 2.6 zilizotumiwa vibaya na Wizara ya Maliasili na Utalii.

Hata hivyo, katika taarifa ya bajeti ya wizara hiyo ya mwaka huu wa fedha, wizara hiyo ilisema kuwa ingeilipa Serikali ya Norway fedha hizo.

“Taarifa ya CAG pia inaonyesha utendaji usioridhisha katika nyanja ya mikopo iliyokuwa ikisimamiwa na taasisi za serikali kwa ajili ya wajasiriamali wadogo wadogo miongoni mwa wanawake na vijana nchini.

“Kwa mfano jumla ya sh milioni 355 zinazodaiwa kutolewa kwa wajasiriamali wanawake na vijana hazikuonyeshwa jinsi zilivyotumika. Taarifa za fedha kutoka halmashauri 41 hazikupatikana,” ilieleza taarifa hiyo.

Mashirika ya umma na mamlaka kama vile Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Shirika la Bima la Taifa (NIC), Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Shirika la Taifa la Umeme (TANESCO), Mamlaka ya Bandari (TPA) na Mfuko wa Hifadhi wa Serikali za Mitaa (LAPF) ni maeneo mengine ya upotevu mkubwa wa fedha.

Kwa mfano, ilithibitishwa kuwa jumla ya sh bilioni 58 zilizokuwa zimetolewa kama mkopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu mwaka 2006, mpaka sasa hakuna uhakika wa kulipwa kwa fedha hizo ambazo zilitolewa dhamana na serikali.

“Kinachowasikitisha wengi ni kwanini serikali bado inashindwa kuziba mianya ya baadhi ya maofisa wake kuendelea kutafuna fedha za umma,” umehitimisha muhtasari wa wachambuzi wa wanaharakati hao.


5 Aug 2010

RAIS Jakaya Kikwete amewekewa pingamizi kortini kugombea urais mwaka huu kwa madai ya matumizi mabaya ya madaraka na ufujaji wa fedha za umma katika safari zake za nje.

Hayo yameelezwa na Mwalimu Mstaafu na Mkazi wa Dar es Salaam, Bw. Paul Mhozya ambaye amefungua kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam kupinga mgombea huyo katika uchaguzi wa Oktoba 31, mwaka huu.

Akizungumza na Majira jana, Bw. Mhozya alisema amefungua pingamizi hilo chini ya hati ya dharura akiitaka mahakama kulisikiliza mapema kabla kampeni kuanza, hivyo akaishauri CCM kuteua mgombea mbadala mapema, badala ya kusubiri uamuzi wa mahakama.

Katika hati ya mashtaka yenye sababu kumi za kuiomba mahakama imuengue Rais Kikwete kwenye kinyang'anyiro cha urais Bw. Mhozya anasema, rais ametumia nafasi aliyopewa kwa mambo binafsi, amekiuka katiba na kuvunja haki za binaadamu pamoja na matumizi holele ya fedha za watanzania kwa mambo yake mwenyewe.

Gazeti la The Citizen toleo la jana lilimkariri Bw. Mhozya kuwa aliwahi kufungua kesi ya kikatiba kama hiyo mwaka 1993 dhidi ya Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi kuwa alivunja katiba kwa kuruhusu Zanzibar kujiunga na Jumuiya ya Kiislamu (OIC), lakini ikatupwa na Jaji Barnabas Samatta kuwa mamlaka ya kumwondoa rais madarakani yalikuwa mikononi mwa bunge peke yake, chini ya kifungu cha 46A cha katiba.

Bw. Mhozya alisema amefikia uamuzi wa kufungua kesi hiyo kutokana na ujeuri uliooneshwa na Rais Kikwete katika miaka mitano ya uongozi wake, hivyo ni vema akazuiwa kuurudia kwa kumzuia asirudi madarakani.

Alisema anayo orodha ndefu ya mambo mabaya aliyofanya Rais Kikwete wakati wa uongozi wake, ambayo anatarajia kuyatumia kama ushahidi na uthibitisho wa malalamiko aliyopeleka mahakamani, ambayo anaamini yatakubaliwa na kumwondoa kwenye kinyang'anyiro.

"Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi (NEC), Jaji Lewis Makame alikwishasema kuwa tume iko tayari kupokea pingamizi dhidi ya mgombea yoyote kwa maslahi ya umma na kuwa itachukua hatua stahili, ninasubiri kauli ya mahakama na ninaamini itasikiliza hoja zangu na kuzifanyia kazi," alisema.

Alisema kuwa yeye kama Mtanzania anayo mamlaka chini ya ibara ya 30 (3) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kufungua kesi dhidi ya uvunjaji wa ibara yoyote ndani ya katiba hasa zinazohusu haki za binaadamu.

Ibara ya 30 (3) inasema "Mtu yeyote anayedai kuwa sharti lolote katika Sehemu hii ya Sura hii au katika sheria yoyote inayohusu haki yake au wajibu kwake limevunjwa, linavunjwa au inaelekea litavunjwa na mtu yeyote popote katika Jamhuri ya Muungano, anaweza kufungua shauri katika Mahakama Kuu"

Bw. Mhozya anasema pamoja na kuwa Rais ana kinga kisheria lakini Kikwete hana kinga ya kuwekewa pingamizi kama mgombea kwa sasa, ndio maana akaamua kufungua kesi hii wakati huu badala ya kusubiri atakaposhinda na kuwa rais, kwani atakuwa na uwezo wa kutumia kinga yake.

Alisema katika kipindi cha uongozi wake rais amefanya safari za ughaibuni zisizo za lazima nyingi kwa fedha za umma, jambo ambalo limesababisha wananch wengi kuishi maisha ya taabu na umaskini mkubwa, huku akidai kuwa urais ni suala binafsi, akisema kuwa ndio maana alimteua mwanawe kumtafutia wadhamini.

Alisema sheria inaitaka NEC kutoa muda wa ziada kwa chama ambacho mgombea wake amekufa au ameshindwa kuendelea kukiwakilisha, ili chama hicho kiweze kuteua mgombea mwingine, hivyo anaamini kuwa baada ya pingamizi hilo kukubaliwa mahakamani, NEC itawaamuru CCM kufanya hivyo kwa kuwaongezea muda.

"Sasa kwa vile sheria inasema NEC itawaongezea muda wa kuteua mgombea mwingine, mimi nashauri wakateua kabisa mgombea mwingine na kumshauri niliyemwekea pingamizi kujitoa, hii itaepusha kupoteza muda pindi pingamizi likikubaliwa, hakuna jinsi," alisema Bw. Mhozya.



Alisema yeye anahofia zaidi mustakabali wa nchi na vizazi vijavyo kuliko anavyohofia maisha yake, hivyo pamoja na vitisho anavyopata bado hataogopa kusimamia ukweli na kuwafichua waovu kama anavyofanya.

"Nimetoka mahakamani leo (jana), nilikwenda kuwaona makarani wa wanipatie 'samansi'(hati ya kuhudhuria mahakamani iliyo na tarehe ya kusikilizwa kesi) lakini walisema bado haijatoka naamini itatoka hivi karibuni ili tukasikilizwe. Matatizo yapo na nilikwisha yazoea," alisema Bw. Mhozya.

CHANZO: Majira

Wakati hayo yakimkumba JK,aliyekuwa Mbunge wa CCM (Bariadi) Andrew Chenge a.k.a Mzee wa Vijisenti nae anakabiliwa na tishio la pingamizi kutoka kwa mmoja ya wana-CCM waliokuwa wakiwania nafasi ya kupitishwa kugombea ubunge kwa tiketi ya chama hicho
. Bonyeza HAPA Kusoma Zaidi Kuhusu Chenge.

28 Nov 2009


KINGSTON, Jamaica

RAIS Jakaya Kikwete ametaka ushirikiano zaidi kati ya Jamaica na Tanzania katika nyanja za muziki na michezo.

"Jamaica ina wanariadha wenye kasi zaidi duniani kwa sasa," alisema kwa kusifia.

Alisema kuwa muziki wa rege ni maarufu zaidi nchini Tanzania, huku akimtaja nyota wa muziki huo, Bob Marley kuwa ni maarufu zaidi nchini mwake.

Kikwete aliiomba Jamaica kuisaidia nchi yake kwa kuwapatia kocha wa ajili ya kuendeleza mchezo wa riadha.

Kiongozi wa Upinzani, Portia Simpson Miller alimweleza Kikwete kuwa wanachama wa chama chake, People's National Party nao wako tayar kushirikiana na Tanzania.

CHANZO: Mwananchi

Alimshauri rais aanzishe ofisi nchini kuratibu shughuli za ushirikiano katika ukanda wa Karibiani.

16 Nov 2009


BUSARA ZINAELEKEA KUSHINDWA KUFANYA KAZI KATIKA TANZANIA YA SASA.BUSARA ZIMEKUWA ZIKITUFUNDISHA KUWA UTU UZIMA DAWA LAKINI TUKIANGALIA JINSI MAMBO YALIVYO SHAGHALA BAGHALA LICHA YA KUWEPO KWA WAZEE-KAMA KINGUNGE NGOMBALE MWIRU-WENYE NGUVU KATIKA ULINGO WA SIASA NI DHAHIRI UTU UZIMA UMESHINDWA KUJIDHIHIRISHA KUWA NI AMANA KATIKA UONGOZI.

PIA KUNA SUALA LA ELIMU.WENGI TUNAAMINI KUWA DALILI ZA KUELIMIKA NI PAMOJA NA KUFANYA YANAYOTARAJIWA NA JAMAA,NA PENGINE KWA NIABA YA JAMII HUSIKA.YAYUMKINIKA KUSEMA KWAMBA KATIKA TANGU NCHI YETU IPATE UHURU HAIJAWAHI KUSHUHUDIA WINGI WA WASOMI KATIKA NYADHIFA MBALIMBALI ZA KISIASA NA KITAALAMU.UNGETARAJI WINGI HUO WA WASOMI UNGEIWEZESHA TANZANIA KUWA KATIKA MAHALA INAPOSTAHILI (YAANI TANZANIA YENYE MAISHA BORA YANAYOENDANA NA UTAJIRI WA RASLIMALI ULIOPO).LAKINI LICHA YA UTITIRI HUO WA WASOMI TUMEZIDI KUSHUHUDIA NCHI IKIGEUZWA SHAMBA LA BIBI HUKU UTAJIRI WETU UKITAFUNWA KANA KWAMBA KUNA MASHINDANO YA KUUMALIZA.

KWA VILE HUKO NYUMA TULIELEZWA KWAMBA ILI TUENDELEE TUNAHITAJI WATU,ARDHI,SIASA SAFI NA UONGOZI BORA,NA KWA VILE ARDHI IPO BWERERE HADI TUNAALIKA WAWEKEZAJI,NA WATU TUPO ZAIDI YA MILIONI 40,BASI NI DHAHIRI KUSUASUA KWA MAENDELEO YETU NI MATOKEO YA SIASA MUFILISI NA VIONGOZI WASIOFAA.

NI KATIKA MINAJILI HIYO NAONA UMUHIMU WA KUHOJI BUSARA ZILIZOMO KATIKA HABARI IFUATAYO



Rais Kikwete Aota kujenga safu ya vijana katika uongozi wa kitaifa
Na Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Mrisho Kikwete ameahidi kuwa kama akijaliwa kupata kipindi cha pili cha kuliongoza taifa la Tanzania, atafanya jitihada kubwa kuubadilisha uongozi wa Tanzania kuwa uongozi wa vijana.

Rais Kikwete akizungumza juzi, mjini Dar es Salaam na vijana kutoka nchi mbali mbali za Afrika wanaoshiriki katika Mpango wa Kulea Uongozi wa Afrika wa African Leadership Initiative, Rais Kikwete alisema kuwa anauthamini Mpango huo.

Alisema kuwa vijana ndiyo Tanzania ya kesho, na kama Tanzania haikuwekeza vya kutosha katika vijana na maendeleo yao, basi itakuwa haiwekezi katika hali yake ya baadaye.

Aliwaambia vijana hao ambao wanashiriki katika Mpango huo unaodhaminiwa na Askofu Mkuu (mstaafu) wa Kanisa la Anglikan Desmond Tutu wa Afrika Kusini kuwa kwa kadri miaka inavyokwenda ni lazima rika la wazee lipishe lile la vijana....INAENDELEA

CHANZO: Mwananchi

JE WINGI WA VIJANA (NA NENO LENYEWE "KIJANA" NI TETE KATIKA ANGA ZA SIASA ZETU) UTAWEZA KUIFIKISHA TANZANIA INAPOSTAHILI KUWA?JE KIKWAZO CHA MAENDELEO YETU NI WINGI WA WAZEE,UPUNGUFU WA VIJANA AU UKOSEFU WA UZALENDO MIONGONI MWA TULIWAOWAPA DHAMANA YA KUTUONGOZA?

TWENDE MBALI ZAIDI.JE KIJANA KWA MUJIBU WA SIASA ZETU NI MTU WA AINA GANI?MWENYE CHINI YA MIAKA 30,40 AU 50?JE KUNA UHUSIANO WOWOTE KATI YA UJANA NA UONGOZI BORA?JE VIJANA TUOTAKA WASHIKE MADARAKA WATAWEZA KWELI KUTONGOZA WAKATI VIBABU VINATAKA KUFIA MADARAKANI NA HIVYO KUWANYIMA FURSA VIJANA YA KUPATA UZOEFU WA UONGOZI?

NA KWA VILE SIASA ZETU ZIMETAWALIWA NA FEDHA,JE VIJANA TUONATAKA WASHIKE MADARAKA HAWATAKUWA WAMEFADHILIWA NA MAFISADI ILI KUWATUMIKIA?NA VIJANA TUNAOWAZUNGUMZIA NI VIJANA WOTE AU WATOTO WA VIGOGO?

LILILO WAZI,KWA KUZINGATIA UZOEFU WA SIASA ZETU,SI KIGEZO CHA UJANA AU HAIBA KINACHOWEZA KUTUKWAMUA HAPA TULIPO BALI NI DOZI NZITO YA UZALENDO.NA JAPO SIWEZI KUJIPAMBANUA KAMA MCHAMBUZI NILIYOBOBEA KWENYE SIASA,SIJAWAHI KUONA MAHALA PANAPOTHIBITISHA KUWA UJANA NI SAWA NA UZALENDO.

LABDA NI MUHIMU PIA KUFAHAMU KUWA HATUWEZI KUENDELEA KWA KUTOA MAJIBU MEPESI TUNAPOKABILIWA NA MASWALI MAGUMU.NI MUHIMU PIA KUKUMBUKA KWAMBA WENZETU WALIOENDELEA WANAFANYA KILA JITIHADA ZA KUPAMBANA NA UBAGUZI KWA VIGEZO VYA UMRI,JINSIA,RANGI,ASILI AU NAFASI YA MTU KATIKA JAMII.KWA MANTIKI HIYO,TUNAPOTAMANI VIJANA WARITHI WAZEE,HUKU TUKIWA HATUNA UTHIBITISHO KUWA UJANA NI TIBA YA MATATIZO YETU,TUNAWEZA KUKARIBISHA MANUNG'UNIKO KUTOKA KWA MAKUNDI MENGINE KATIKA JAMII HUKU TUKIENDELEA KUPIGA MARK TIME WAKATI TAIFA LETU LINAZIDI KUTAFUNWA KAMA MCHWA NA MAFISADI.

9 Oct 2009



Na Ramadhan Semtawa

RAIS Jakaya Kikwete aliweka hadharani matokeo ya uchunguzi wa vipimo vya afya yake, yanayoonyesha kuwa kiongozi huyo wa nchi ana afya njema baada ya tatizo la kuishiwa nguvu akiwa jukwaani mjini Mwanza Oktoba 4, kuibua mjadala.

Lakini vipimo hivyo vinaonyesha kuwa tatizo pekee linalomsumbua Rais Kikwete ni maumivu ya shingo ambayo yanatokana na kuumia nyakati za ujana au utoto.

Afya ya Rais Kikwete ilizuia mjadala baada ya kuishiwa nguvu akihutubia kwenye Uwanja wa Kirumba mjini Mwanza na kulazimika kubebwa na wasaidizi wake hadi chumba kidogo cha uwanjani hapo na ilielezwa baada ya rais kuzinduka kuwa tatizo hilo lilitokana na uchovu baada ya safari ndefu kati ya New York, Marekani na Dar es salaam na baadaye Arusha na Mwanza.

Pamoja na uchovu huo kuhusishwa na safari ndefu ya Rais Kikwete taarifa iliyopokelewa kutoka Radio Jamaica jana jioni zinasema kuwa rais atakwenda nchini Jamaica kwa ziara ya kikazi itakayoanza Novemba 24 na kumalizika Novemba 26.

Na jana daktari wa rais, Peter Mfisi alirejea tena kauli hiyo akisema uchovu, hasa wa safari, ndio uliosababisha kiongozi huyo wa nchi kuishiwa nguvu jukwaani, huku kukiwa na habari kuwa ataenda Jamaica mwezi ujao kwa safari ya kikazi.

Hii ni mara ya kwanza kwa Ikulu kuweka hadharani vipimo vya uchunguzi wa afya ya Rais Kikwete, ambaye pia aliwahi kuishiwa nguvu siku ya mwisho ya kampeni zilizomuingiza Ikulu, na kuanguka akiwa jukwaani.

Daktari wa rais, Peter Mfisi aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa vipimo hivyo ni pamoja na cha damu kwa ajili ya kuangalia virusi vya Ukimwi ambacho huchukuliwa kila baada ya miezi sita.

"Nimekuja kufafanua afya ya mheshimiwa rais kutokana na tukio la Oktoba 4, 2009 (la kuishiwa nguvu jukwaani) pale Mwanza. Tukio hilo limesababisha mshtuko kwa watu wengi na kuendelea kuwa jambo linalozua mjadala kuhusu hali ya afya ya mheshimiwa," alisema daktari huyo.

"Naelewa sababu ya wananchi kuwa na hofu na kuwepo kwa mjadala miongoni mwao. Tatizo pekee ambalo limekuwa likimsumbua rais mara kwa mara ni maumivu ya shingo yanayotokana na kuumia utotoni na wakati wa ujana.

"Baadhi ya pingili za uti wa mgongo sehemu ya shingoni ziliathirika kutokana na kuumia huko na humsababishia maumivu. Mara nyingi matatizo hayo huwapata wanamichezo na wanajeshi."

Dk Mfisi aliongeza kusema: "Tumekuwa tunamfanyia mheshimiwa rais uchunguzi wa damu yake kwa vipimo mbalimbali vinavyotumika kutambua maradhi mbalimbali yanayohusu damu yenyewe na mwili mzima wa mwanadamu. Tumekuwa tunafanya hivyo hapa nchini na hata nje kwa nia ya kulinganisha matokeo yetu na kwa vipimo ambavyo sisi tunavyo.

"Matokeo ya uchunguzi wetu yameonyesha mheshimiwa rais yuko salama, hana maradhi ya damu au kisukari, wala Ukimwi au wingi wa mafuta (Cholestrol), kiwango cha madini, tezi la kibofu wala shingo, au ya ini, au ya homoni mbalimbali zilizoko mwilini na mengine."

Dk Mfisi alifafanua kwamba, uamuzi huo wa kutoa vipimo hivyo umetokana na ridhaa ya rais mwenyewe.

"Ni ridhaa ya mheshimiwa rais mwenyewe... kutokana na kiapo changu cha udaktari na maadili yangu ya kazi, siruhusiwi kutoa hadharani undani wa habari yoyote inayohusu mgonjwa ninayemtibu bila ridhaa yake," alisema Dk Mfisi.

Kwa mujibu wa daktari huyo, baada ya Rais Kikwete kuishiwa nguvu jukwaani, alichukua vipimo muhimu wakati akiwa kwenye chumba maalumu uwanjani hapo kama ilivyo kawaida na kwamba vipimo hivyo vimeshafanyiwa uchunguzi.

Alifafanua kwamba matokeo ya vipimo vilivyochukuliwa siku ya tukio la Mwanza yalionyesha shinikizo la damu (BP) lilikuwa kati ya 130 kwa 85 (vipimo vya kitaalamu), kitu ambacho ni cha kawaida kwa mtu mwenye umri kama wa Rais Kikwete.

"Mapigo ya moyo wake yalikuwa ni 76 kwa dakika ambayo pia ni ya kawaida; sukari kwenye damu ilikuwa 5.5 ambayo nayo ilikuwa ya kiwango cha kawaida; joto la mwili lilikuwa nyuzi 37.5 ambalo ni la kawaida," alifafanua Dk Mfisi.

"Mheshimiwa Rais pia hakuwa na kiungo chochote kilichoonekana kutetereka, jambo ambalo lilithibitisha kuwa hakupata kiharusi. Mheshimiwa Rais hakuwa na matatizo yoyote ya kiafya ambayo yangeweza kuhusishwa kuwa chanzo cha tukio lile (la Mwanza)."

Hata hivyo, Dk Mfisi alisema baada ya kurejea Dar es Salaam alijaribu kuwasiliana na madaktari wenzake wa ndani na nje ya nchi ambao wamekuwa wakishirikiana nao katika kuchunguza na kufuatilia afya ya Rais Kikwete.

"Wote hao baada ya kuwasimulia kilichotokea na matokeo ya vipimo nilivyomfanyia mheshimiwa rais, kwa tafakuri zao hawakuwa na wasiwasi wowote kuwa tukio hilo lilisababishwa na jambo jingine lolote isipokuwa uchovu," alisisitiza daktari huyo wa rais.

Aliongeza kwamba mmoja wao alimuona rais siku moja kabla ya kuondoka New York ambako alipata nafasi ya kumchunguza afya ya mkuu huyo wa nchi.

Dk Mfisi, akitoa mtiririko huo wa vipimo mbalimbali na matokeo alisema: " Blood Pressure (shinikizo la damu), tunafuatilia kwa karibu sana msukumo wa damu, mwenyewe tunampa mashine ya kujipima kila siku na anafanya hivyo, kwa jumla presha yake iko kwenye viwango vya kawaida.

"Aidha, uzito wake wa mwili unaendana ipasavyo na urefu wake, mheshimiwa Rais ni mtu mwenye mazoea ya kufanya mazoezi na yuko makini katika chakula anachokula."

Daktari huyo wa rais aliweka bayana kwamba, wanahusika kwa ukamilifu na kuelekeza kuhusu chakula anachokula na kuongeza kwamba "ana nidhamu ya kujipima pamoja na mazoezi na chakula."

Kuhusu moyo, Dk Mfisi alisema tayari walishamfanyia rais vipimo vya kitaalamu vinavyofahamika kama ECHO na ECG na vingine, na kwamba matokeo yameonyesha hakuna tatizo lolote.

Akizungumzia ubongo, alisema mwaka jana Rais Kikwete alifanyiwa uchunguzi wa afya ya ubongo wake katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa kutumia kipimo cha CT-Scan na matokeo yake yalionyesha kwamba, hakuwa na tatizo pia.

Dk Mfisi alisema Rais Kikwete aliwahi kufanyiwa uchunguzi wa ini, figo, bandama na kongosho kwa kutumia kipimo cha mionzi (ultra sound), uchunguzi ambao ulibaini viungo vyote hivyo viko salama.

"Kila mwaka tunapomfanyia uchunguzi wa afya ya mheshimiwa rais, tumekuwa tunafanyia uchunguzi wa viungo vyake muhimu vya tumboni kama vile ini, figo, bandama na kongosho na kwa kupima damu yake kwa vipimo vyote muhimu," aliongeza Dk Mfisi.

Kuhusu mfumo wa njia ya chakula, ambayo huhusisha koromeo la chakula, tumbo, utumbo mdogo, Dk Mfisi aliweka bayana kwamba matokeo ya uchunguzi yameonyesha hakuna tatizo lolote.

Alisema mwaka 2007 walimfanyia kipimo cha kitaalamu cha colonoscopy mjini Paris, Ufaransa, kuchunguza hali ya afya ya utumbo mkubwa na kwamba matokeo ya uchunguzi yalionyesha kuwa hana matatizo yoyote.

Alisema daktari aliyemfanyia rais kipimo hicho aliwaambia kuwa mkuu huyo wa nchi hahitaji kufanyiwa kipimo kama hicho tena mpaka baada ya miaka saba na kwamba daktari huyo alimtania rais kwa kusema kuwa "angefurahi kuazima utumbo" wake.

Kuhusu tezi la shingo, Dk Mfisi alisema kuwa akiwa mjini New York katika safari yake ya juzi, Rais Kikwete alifanyiwa uchunguzi wa afya ya tezi la shingo pamoja na kiwango chake cha utoaji wa homoni, matokeo yaliyoonyesha hakuna tatizo, hali kadhalika uchunguzi wa tezi la kibofu ulionyesha hana tatizo.

Dk Mfisi alisema rais hana tatizo la macho, masikio na pua na kwamba uvaaji miwani wa Kikwete haumaanishi kuwa ni maradhi.

"Tunapofanya uchunguzi wa macho ukiacha ile ya kuchunguza uwezo wa kuona, tunaangalia presha ya macho na hali ya viungo vya nje na ndani, mheshimiwa Rais hana matatizo yoyote," alisema.

CHANZO: Mwananchi

WAKATI DR MFISI AKITOA MAELEZO HAYO,MHADHIRI MWANDAMIZI KATIKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM DR HAJI SEMBOJA AMENUKULIWA NA JARIDA LA RAIA MWEMA AKIELEZA KUWA URAIS NI ASASI NA SI MTU BINAFSI.

Urais si Kikwete binafsi, ni mfumo wa kitaasisi. Ni wazi kuwa Rais amesema yeye ndiye hakuzingatia ushauri wa wataalamu wake kutokana na kuwaondolea lawama. Ameamua kuwalinda kwa kubeba lawama, lakini ukitazama jambo hili kwa upana wake wasaidizi wake walipaswa kutambua tangu awali kuwa urais ni system nzima Ikulu hata mlinzi wa getini. Kwa hiyo, wasaidizi ndiyo wenye kuamua na si kila kitu kifanywe na Rais kama ambavyo wanasema sasa watajaribu kumpunguzia ratiba,” ALISEMA DR SEMBOJA NA KUSISITIZA KWAMBA“Sidhani kama ni sahihi kukubali kuwa Rais ndiye alikataa ushauri, kwa taratibu za kimfumo Rais anapangiwa kila kitu ni kama anaamriwa hivi. Kwa tukio hili ameamua tu kuwa na nidhamu ya kuwalinda wasaidizi wake, namwombea afya njema lakini ni muhimu tuzingatie kuwa wengi walioamua kufanya kila kitu wenyewe walipata matatizo, Ikulu sasa ifanye kazi kama Ikulu.”

BINAFSI NAAMINI TATIZO NI LA KIMFUMO ZAIDI.KUNA TAASISI ZENYE MAMLAKA NA WAJIBU WA KUPANGA RATIBA ZA RAIS SAMBAMBA KWA KUZINGATIA UHALISIA,USALAMA NA MAMBO MENGINE KAMA HAYO.KWA WENZETU WANAOZINGATIA KANUNI NA TARATIBU ZA KITAASISI,SI RAHISI KWA RAIS KUJIAMULIA MAMBO YAKE MWENYEWE PASIPO KUZINGATIA USHAURI WA KITAALAM.SI RAHISI,KWA MFANO,BARACK OBAMA KUJIAMULIA KWENDA MAHALA FLANI KINYUME NA USHAURI WA U.S. SECRET SERVICE.UBISHI WA RAIS KAMA BINADAMU HAUNA NAFASI KATIKA UFANISI WA TAASISI INAYOZINGATIA TAALUMA NA MAADILI.IKUMBUKWE KWAMBA LAITI RAIS AKING'ANG'ANIA KUFANYA ZIARA MAHALA FLANI KINYUME NA USHAURI WA WASAIDIZI WAKE KISHA AKAPATWA NA JANGA,WATAKAOBEBA LAWAMA NI WASAIDIZI HAO NA SI RAIS.LAKINI PIA KUNA SUALA LA FEDHA ZA WALIPA KODI ZINAZOTUMIWA NA TAASISI HUSIKA KUILINDA ASASI YA URAIS NA BINADAMU ALIYEKABIDHIWA DHAMANA YA URAIS.NI DHAHIRI KWAMBA RAIS AKIPUUZA USHAURI WA WA TAASISI HUSIKA INAMAANISHA PIA UPOTEVU WA FEDHA ZA WALIPA KODI.



UTENDAJI WA AINA YA ZIMAMOTO,AU VIBAYA ZAIDI,KULENGA SHABAHA BAADA YA RISASI KUFYATUKA,UTATUGHARIMU HUKO MBELENI.LEO HII TUSINGEHITAJI DAKTARI WA RAIA KUWEKA HADHARANI TAARIFA NYETI ZA AFYA YA JK LAITI TAASISI HUSIKA ZINGEMLAZIMISHA JK KUFUATA USHAURI WA KITAALAMU KUHUSIANA NA RATIBA AU ZIARA ZAKE.TUSISUBIRI JAMBO LITOKEE NDIPO TUANZE KUTOA MAELEZO YA KITAALAMU. BY THE WAY,TAARIFA HIYO YA DAKTARI WA RAIS INAWEZA KUZUA MJADALA USIO NA TIJA KUHUSU MANTIKI YAKE.JAPO NI VEMA KUTOA UFAFANUZI KATIKA MASUALA YANAYOZUA UTATA (I WISH NA KWELI ISHU YA KAGODA INGEKUWA HIVYO) LAKINI KUNA UWEZEKANO WA "WABISHI" KUHOJI KAMA DAKTARI WA RAIS WA AFRIKA ANAWEZA KUTOA TAARIFA "MBAYA" DHIDI YA BOSI WAKE!

KWA SASA,MAMLAKA HUSIKA ZINAWEZA KUFARIJIKA BAADA YA KUPATA UTETEZI KUTOKA KWA JK.LAKINI NI VEMA ZIKATAMBUA KUWA JUKUMU LAO SI KUMWOGOPA MHESHIMIWA BALI KUFANYA KAZI ZAO KWA KUZINGATIA MAADILI NA TAALUMA.JK KAMA MTU ANAWEZA KUTOZINGATIA USHAURI WA MAMLAKA HIZO,LAKINI JK KAMA RAIS HARUHUSIWI KUJIAMULIA MAMBO YANAYOWEZA KUATHIRI ASASI YA URAIS.UOGA NA KUJIKOMBA NI MAMBO YASIYO NA NAFASI KATIKA PROFESSIONALISM.


5 Oct 2009


KWANGU,MISINGI MIKUU YA NYERERE ILIKUWA UJENZI WA JAMII YENYE USAWA NA INAYOTHAMINI UTU WA BINADAMU.UHURU BILA USAWA NI POROJO.UMOJA KATIKA LINDI LA UMASIKINI NI SAWA NA USINGIZI WA PONO KWENYE UTANDO WA BUIBUI.NA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA HAYAWEZI KUPATIKANA KATIKA SIASA ZA KUKUMBATIA MAFISADI SAMBAMBA KUKEMEA WAPAMBANAO NA UFISADI,KUTOJUA VIPAUMBELE VYA NCHI,NA KUENDELEZA AHADI ZA MAENDELEO ILHALI ZILE ZA AWALI HAZIJATEKELEZWA.

JK AMEKUMBUKA MISINGI YA MWALIMU.MSOME KATIKA HABARI IFUATAYO:

Mwandishi Maalum, Mwanza

RAIS Jakaya Kikwete ametaja misingi mikuu mitatu iliyowekwa na Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere katika kulijenga taifa la Tanzania, misingi ambayo rais alisema ni kumbukumbu yao kuu kwa kiongozi huyo wa harakati za Uhuru wa Tanganyika.

Rais Kikwete aliwashangaa Watanzania ambao wanabeza Uhuru wa Tanzania na kufurahia wakati jina la Tanzania linaposhambuliwa na wageni.

Aliitaja misingi hiyo mikuu kuwa ni uhuru, umoja wa taifa la Tanzania, na safari ya kujenga maisha bora kwa kila Mtanzania iliyoanza hata kabla ya Tanganyika kupata uhuru wake rasmi Desemba 9, 1961.

Rais Kikwete alisema hayo mjini Mwanza juzi alipozungumza na vijana wa CCM ambao wanaanza safari ya kuelekea kijijini Butiama mkoani Mara, ikiwa ni matembezi ya kumuezi Mwalimu Nyerere ambaye alifariki miaka 10 iliyopita baada ya kuugua saratani ya damu.

Mwalimu Nyerere alifariki Oktoba 14, 1999 akiwa amelazwa hospitali ya St Thomas jijini London, Uingereza.

Vijana 166 kutoka mikoa yote ya Tanzania wanashiriki katika matembezi hayo ya siku 10 ambayo yatapitia njia ambayo Mwalimu Nyerere alitembea mwaka 1967 katika kuunga mkono na kuhamasisha Azimio la Arusha.

Kauli mbiu ya matembezi hayo ni “Uhuru na Kazi” na miongoni mwa mambo ambayo vijana hao watafanya njiani ni kukarabati Shule ya Msingi ya Mwisenge ambako Mwalimu Nyerere alipata elimu yake ya msingi.

Rais Kikwete alisema kuwa urithi mkuu ambao Mwalimu aliwaachia Watanzania ni misingi hiyo mikuu ambayo imeendelea kulifanya Taifa la Tanzania kuwapo na kuwa imara.

Rais Kikwete alisema kuwa kila taifa duniani lina waasisi wake ambao wanastahili kuendelea kukumbukwa siyo tu kwa uasisi pekee, bali pia kwa mambo ambayo waliyasimamia, waliyaamini na waliyajenga.

"Wamarekani wanaye George Washington… sisi tunaye Mwalimu Julius Kambarage Nyerere… na kila nchi ina muasisi wake ambaye anakumbukwa kwa aliyoyasimamia," alisema JK.

"La kwanza la kumkumbuka Mwalimu ni uhuru wa nchi yetu. Huyu alikuwa ni kiongozi aliyeambiwa achague kati ya siasa ama kazi ya ualimu… huyu mzee wetu akachagua siasa na utumishi wa umma bila hata kujua atakula nini.

"Akachagua kupigania uhuru wa nchi yetu. Kama mnavyojua nyote hii kazi ya siasa ni kamari... unakwenda kugombea ukijua kuna kupata ama kukosa... lakini yeye alifanya uamuzi sahihi wa kupigania uhuru,"

Rais Kikwete alisema kuwa uhuru siyo mipaka bali ni heshima ya nchi na ndiyo maana Tanzania haitasita kumkabili yoyote ambaye atajaribu kuchezea uhuru huo.

Alisisitiza: "Mwaka 1978 yule msanii na profesa wa historia na jiografia, Idi Amin alivamia nchi yetu… na sisi tukamfurumusha ili kulinda uhuru wetu na wako wenzetu ambao walipoteza maisha yao kwa ajili ya kulinda uhuru wetu. Wamelala Kaboya (mkoani Kagera) na tutaendelea kuwaenzi kwa sababu walijitolea kulinda uhuru wetu."

Rais Kikwete pia aliwashangaa watu wote ambao wanafurahia wakati heshima ya Tanzania inapobezwa na wageni.

"Uhuru siyo mipaka kama nilivyosema. Uhuru ni heshima ya taifa letu. Wako wale wenzetu wanaofurahi wakati wageni wanaposhambulia nchi yetu. Ni wajibu wetu sote kuhakikisha kuwa uhuru wetu hauchezewi na mtu yoyote,"alisema.

Kuhusu umoja wa taifa, Rais Kikwete alisema Mwalimu alihakikisha kuwa uhuru wa nchi unazaa umoja ili nchi iwe moja na isigawanyike vipande vipande kwa sababu yoyote ile.

"Aliondoa viashiria vyote vya kuvunja umoja wa taifa tokea mwanzo kabisa. Aliondoa uchifu ili kuondoa nguvu za ukabila. Alitambua hatari ya dini na akataifisha shule zote za dini ili vijana wetu waelimishwe na kulelewa kama vijana wa taifa moja na siyo vijana wa dini tofauti,"alisema Kikwete.

Rais Kikwete alisema kuwa hata kabla ya uhuru, Mwalimu alitambua kuwa ili uhuru na umoja viweze kudumishwa ni lazima wananchi wake wapate maisha bora na ndiyo maana akawatambua maadui wakuu watatu – ujinga, maradhi na umasikini- na njia za kukabiliana na maadui hao.

CHANZO:
Mwananchi

BAADHI WANAHOJI KUHUSU MANTIKI YA UHURU ALIOPIGANIA BABA WA TAIFA NA WENZAKE.TULIMKIMBIZA MKOLONI ILI TUJITAWALE NA KUFAIDI RASLIMALI ZETU KWA HAKI NA USAWA.JAPO SIO EXCUSE,LAKINI MKOLONI HAKUTUJALI KWA VILE HAKUWA MTANZANIA.LEO HII WANAOTUTENDA VIBAYA ZAIDI YA WAKOLONI NI WATANZANIA WENZETU,WENGI WAO WAKIWA WALIOSOMOSHWA KWA SHIDA NA FEDHA ZA WATANZANIA WENZAO.KUNDI JINGINE NI LA MABWANYENYE WALIOPTA URAIA KWA VIJISENTI VYAO NA WAKOLONI -MAMBOLEO WALIOREJEA KWA JINA LA WAWEKEZAJI.NYERERE HAKUPIGANIA UHURU ILI WAGENI WAJE NA DOLA MOJA NA KUONDOKA NA MAMILIONI YA DOLA,AU AKINA LOWASSA KUTUINGIZA MKENGE KWENYE RICHMOND,NA USANII MWINGINE WA KISIASA.

UHURU PASIPO UONGOZI BORA NI SAWA NA KUWA NA VOGUE LENYE DEREVA MLEVI AU KIPOFU;LITATUMBUKIA MTARONI KAMA SI KUPORWA NA MAJAMBAZI.UHURU ILHALI TUMEBANWA NA NIRA ZA MAFISADI NI UTANI MBAYA KWA WALIOPIGANIA UHURU WA NCHI YETU.WEZI WA KAGODA WAMEHIFADHIWA HADI LEO,MASHIRIKA YA UMMA YAMEGEUKA KICHAKA CHA WATU KUHUJUMU KISHA WABADILISHIWE (REJEA MATTAKA NA ATCL),WAZEMBE WANAENDELEA KULINDWA KWA VILE TU KUWABADILISHA KTATHIBITISHA MAPUNGUFU YA ALIYEWATEUA IN THE FIRST PLACE,NA HADITHI NYINGINE ZA KUSIKITISHA.

HATUKUPIGANIA UHURU KUPATA HESHIMA FEKI MACHONI MWA JUMUIYA YA KIMATAIFA BALI AMANI NAFSINI NA MIILINI MWETU KAMA WATANZANIA.

28 Apr 2009



YAH,WANASEMA NI SUALA LA MTIZAMO: KUSEMA GLASI IKO HALF EMPTY AU HALF FULL.HABARI MBILI ZIFUATAZO ZINADHIHIRISHA MANTIKI YA MSEMO HUO.

Na Boniface Meena

UMAARUFU wa Rais Jakaya Kikwete unaonyesha kuendelea kuporomoka, kwa mujibu wa ripoti ya matokeo ya utafiti uliofanywa na taasisi ya Mpango wa Utafiti wa Elimu ya Demokrasia nchini (Redet).

Ripoti hiyo pia inaonyesha kuwa utendaji kazi wa Rais Kikwete, ambaye aliingia madarakani mwaka 2005 kuongoza serikali ya awamu ya nne, umeshuka kwa asilimia 28 mwaka jana ukilinganisha na matokeo ya utafiti ya mwaka 2006.

Pamoja na kushuka kwa asilimia hiyo, utafiti huo umeonyesha kuwa wananchi waliohojiwa wanaridhika zaidi na utendaji wa Rais Kikwete, kuliko wanavyoridhishwa na utendaji kazi wa baraza lake la mawaziri ambalo utendaji wake umekubaliwa na asilimia 18 tu.

Kwa mujibu wa utafiti huo, watu wanaoridhika sana na utendaji kazi wa Kikwete ni asilimia 39.5 tu kulinganisha na asilimia 69 iliyoonyesha kuridhika naye sana mwaka 2006.

Akitoa taarifa ya utafiti huo jana kwa waandishi wa habari, mtafiti mkuu wa Redet, Dk Benadetha Killian alisema kuwa ukilinganisha takwimu za Oktoba 2006 na Oktoba 2007, asilimia ya wale wahojiwa ambao wanasema wanaridhika sana na utendaji kazi wa Rais Kikwete imepungua kutoka asilimia 69 Oktoba 2006 hadi asilimia 44 mwezi Oktoba 2007 na sasa imefikia asilimia 39.5 hadi Novemba mwaka jana.

Dk. Killian alisema kuwa ukichambua undani wa mwenendo huo utaona kwamba wakati idadi ya wanaosema wanaridhika sana iliteremka kwa tofauti ya asilimia 23, kati ya mwaka 2006 na 2007, kasi ya kutoridhika sana imepungua ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2007/08 wakati idadi ya wahojiwa ambao walisema wanaridhika sana ilipungua kwa tofauti ya asilimia 4.5 tu.

Kwa mujibu wa Dk. Killian, ukusanyaji wa maoni kwa ajili ya utafiti huo ulifanyika katika mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani na sampuli ilichaguliwa katika ngazi tatu ambazo ni wilaya na vijiji/mitaa na katika kila ngazi sampuli ilipatikana kwa kutumia mtindo wa sampuli nasibu.

"Katika kila wilaya, watafiti walitakiwa kuchagua vijiji viwili (kwa maeneo ya shamba) au mitaa miwili (kwa maeneo ya mjini) kwa kutumia njia ya sampuli nasibu. Katika kila wilaya, jumla ya watu 50 walichaguliwa kwa ajili ya kuhojiwa, 25 kutoka kila kijiji/mtaa," alisema.

"Na kati ya watu 50 waliohojiwa katika kila wilaya, 25 walitakiwa wawe wanawake na wengine 25 wawe wanaume na uchaguzi wote wa wahojiwa ulifanyika kwa kutumia njia ya sampuli nasibu."

Alisema ukiacha masuala mengine ya utendaji wa mawaziri, waliohojiwa walitakiwa kutoa tathimini yao kuhusu utendaji kazi wa Rais Kikwete katika kipindi cha takriban miaka mitatu ya utawala wake kwa kutoa maoni yao kama wanaridhika sana, wanaridhika kiasi au hawaridhiki.

Dk. Killian alisema kati ya wote waliohojiwa, asilimia 39.5 walisema wanaridhishwa sana na utendaji wa Rais Kikwete, asilimia 39.0 walisema wanaridhika kiasi na asilimia 19.3 walisema hawaridhiki na utendaji kazi wa mkuu huyo wa nchi.

Alisema hata hivyo kwa ujumla, matokeo ya utafiti wa Novemba mwaka jana yanaashiria kwamba, utendaji kazi wa Rais Kikwete bado unaonekana kuridhisha idadi kubwa ya watu pale ambapo makundi mawili ya wahojiwa yanapojumlishwa pamoja yaani wale wanaosema wanaridhika sana asilimia 39.5 na wale wanaosema wanaridhika kiasi asilimia 39 ikiwa inafanya idadi hiyo ya wahojiwa wote kufikia asilimia 78.5.

Dk Killian alisema sababu za kuridhika au kutoridhika na utendaji kazi wa serikali ya Rais Kikwete ni kutoridhishwa na ahadi yake ya kuboresha hali ya maisha. Asilimia 31.0 ya waliohojiwa walisema ameshindwa kuboresha hali ya maisha, wakati asilimia 24 walisema hajatimiza ahadi na asilimia 12.2 walisema hafuatilii utekelezaji wa ahadi zake.

"Sababu nyingine zilizotolewa na wahojiwa ni kuchagua viongozi wasiofaa asilimia 10.8, ameshindwa kupambana na rushwa asilimia 8.0, lakini pamoja na kwamba utafiti huu ulifanywa kipindi ambacho "vigogo" walikuwa wanapelekwa mahakamani kuhusiana na tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi na wengine kutuhumiwa na wizi wa fedha za akaunti ya madeni ya nje (EPA), ni asilimia 6 tu ndiyo waliotaja moja kwa moja suala hili kama sababu ya kutoridhishwa au kuridhishwa kiasi na utendaji kazi wa rais," alisema.

Alisema sababu za wananchi kutoridhika na utendaji wa serikali iliyo madarakani ni kutofuatilia utekelezaji asilimia 30.7, serikali kujihusisha na rushwa asilimia 29 na inapitisha mikataba mibovu asilimia 10.0.

Utafiti huo pia unaonyesha kuwa bunge ndio linaongoza kwa kutoridhisha wananchi baada ya asilimia kubwa ya waliohojiwa kueleza kuwa hawaridhishwi na taasisi hiyo ya kutunga sheria.

Bunge limeonekana kutoridhisha wengi tofauti na taasisi za serikali kama polisi, taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini, serikali za mitaa na kadhalika.

Dk. Killian alisema bunge linaongoza kwa kuwa na asilimia kubwa ya kiwango cha kutoridhika ambacho ni asilimia 77.4, ikifuatiwa na serikali za mitaa asilimia 75.6 wakati baraza la mawaziri linashika nafasi ya tatu kwa asilimia 63.

Kwa upande wa utendaji kazi wa Rais Amani Abeid Karume wa Zanzibar, utafiti unaonyesha kuwa asilimia 44 tu ya wote waliohojiwa wanaridhika sana, wakati asilimia 24 wanaridhika kiasi na asilimia 26 walisema hawaridhiki.

Alisema kiwango cha utendaji wa Rais Karume kimeonekana kupanda kwa asilimia 9 ukilinganisha na utafiti wa Oktoba 2007 wakati asilimia 35.5 tu ilimkubali baada ya kuporomoka kutoka asilimia 47.8 aliyopata kipindi cha hadi Oktoba 2006 na baadaye kupanda kutoka asilimia 35.5 Oktoba 2007.

CHANZO: Mwananchi



Nyota ya Kikwete Bado Yang'ara
na mwandishi Wetu


Watanzania walio wengi, zaidi ya asilimia 80, bado wana imani na Rais Jakaya Kikwete, kuliko miaka minne iliyopita alipochaguliwa kuwa Rais. Pia asilimia kubwa ya Watanzania inaridhishwa na utendaji kazi wa Rais na Serikali yake.

Kura ya maoni iliyoendeshwa na taasisi ya uchunguzi inayojitegemea ya REDET kuhusu utendaji wa Serikali ya Kikwete katika miaka mitatu iliyopita ya uongozi wake, inaonyesha kuwa asilimia 83.7 ya Watanzania wana imani naye.

Kundi hilo la Watanzania wanaothibitisha kuwa na imani na Rais Kikwete likigawanywa katika makundi ya ulinganisho wa imani, asilimia 50 inasema ina imani sana kwa kiongozi huyo, asilimia 33.7 inasema ina imani kiasi cha kutosha kwake.

Asilimia hiyo ni kubwa kuliko ile ya ushindi wa urais mwaka 2005, alipochaguliwa kwa kishindo ambapo alichaguliwa kwa asilimia 82. Hakuna mwanataaluma yeyote wa REDET ambaye alikubali kuzungumza na gazeti hili kuhusu kura hiyo ya maoni licha ya kupatikana kwa nakala ya matokeo ya utafiti huo.

Lakini habari zinasema matokeo kamili ya kura hiyo yanatarajiwa kutangazwa rasmi wiki ijayo na uongozi wa REDET. Kubwa zaidi katika ripoti hiyo, ni ukweli kuwa asilimia ya Watanzania wenye kuridhishwa na utendaji kazi wa Rais Kikwete bado iko juu.

Utafiti huo wa kisayansi na wa kina uliofanyika katika sehemu mbalimbali za nchi mijini na vijijini unaonyesha kuwa asilimia 78 ya Watanzania wanaridhishwa na utendaji kazi wake. Matokeo ya kura hizo yamethibisha kwa mara nyingine, ukweli ambao umebakia bila kubadilika kuhusu imani ya wananchi kwa Rais Kikwete na utendaji wake tangu alipoingia madarakani.

Kura zote za maoni ambazo zimefanyika tangu wakati huo, zimekuwa zikionyesha kuwa kiwango cha imani ya wananchi wake na kwa utendaji kazi wake kimebakia kwenye eneo la asilimia 80. Kura hizo pia zinaonyesha kuwa imani ya wananchi kwa wasaidizi wake wakuu ni ya juu.

Zinaonyesha pia kuwa asilimia 82.7 wana imani na Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohammed Shein akiwa nyuma ya Rais kwa asilimia moja, wakati Waziri Mkuu Mizengo Pinda anavutia asilimia 84. Utafiti huo pia unathibitisha kuwa wananchi kiasi cha asilimia 70 wana imani na Baraza la Mawaziri, wakati asilimia 66 wana imani na wakuu wa mikoa. Imani ya wananchi inashuka kidogo kwa Bunge ambalo lina asilimia 65.

Katika namna ambayo pia itakipa nguvu na kuifurahisha CCM, asilimia ya Watanzania ambao wanasema wanaridhishwa na utendaji kazi wa chama hicho ni 72.8 wakati asilimia 75.6 wanasema wana imani na chama hicho. Matokeo hayo yatakifurahisha chama hicho kwa sababu asilimia hiyo kubwa ya kukubaliwa na Watanzania imebakia ya kiwango hicho hicho kwa karibu miaka 17 tangu kuanzishwa kwa vyama vya upinzani nchini.

Mwaka 1992 wakati CCM na serikali zilipoongoza mageuzi ya kuingia katika mfumo wa vyama vingi, ilikuwa baada ya uchunguzi uliothibitisha kuwa ni asilimia 20 tu ya Watanzania waliokuwa wanataka mfumo wa vyama vingi. Kwa namna moja au nyingine, asilimia hiyo imebakia na kujithibitisha mara nyingi kupitia njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na kupitia uchaguzi mkuu ambao umefanyika tangu wakati huo na hasa uliopita uliomwingiza Rais Kikwete madarakani mwaka 2005. Kwa upande wa vyama vya upinzani, asilimia ya Watanzania ambayo inasema haina imani na vyama hivyo inabakia juu kwa asilimia zaidi ya 31.



CHANZO: HabariLeo



































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.