Showing posts with label JUMUIYA AFRIKA MASHARIKI. Show all posts
Showing posts with label JUMUIYA AFRIKA MASHARIKI. Show all posts

1 Mar 2012

Wazee wa iliyokuwa Jumuia ya Afrika Mashariki wakiwa wamekaaa katikati ya jiji la Dar es Salaam wakijadili malipo yao yaliyocheleweshwa na serikali hadi leo.…

Nimekutana na picha hiyo hapo juu kwenye mtandao wa Global Publishers.Kwa kweli imenisikitisha sana kuona wazee wetu waliotumikia taifa letu kwa uadilifu wakihangaishwa miaka nenda miaka rudi kupewa mafao yao ya utumishi katika iliyokuwa Jumuiya ya Nchi za Afrika Mashariki.

Hazipiti wiki kadhaa kabla ya kusikia Rais wetu yuko kiguu na njie kwenda nje ya nchi huku akiambatana na msururu wa watu kwenye msafara.Watendaji wengine wa serikali wanatumia magari ya thamani kubwa huku ofisi zao zikisheheni samani kutoka ng'ambo.Matumizi ya viongozi wetu hayaendani kabisa na umasikini wetu.Mabilioni yalitapanywa mwezi Disemba mwaka jana katika maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru.Hivi fedha hizi zisingeweza kumaliza adha inayowakabili wazee wetu hawa?

Jamii inayopuuza wanyonge (kwa mfano wazee hawa) ni kama inasaka ugomvi usio wa lazima na Muumba.Kosa la wazee hawa ni lipi hadi wahangaishwe kiasi hiki?Chonde chonde viongozi wetu-hususan Rais Kikwete-waoneeni huruma wazee wetu hawa.Wanachodai sio posho za vikao kama za wabunge bali ni jasho lao halali.Wenzao wa Uganda na Kenya walishalipwa stahili zao zote.Kama wao waliweza kwanini sie tushindwe?

14 Oct 2010

Wastaafu wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiwa wamejilaza tayari 'kusulubiwa na gari la upupu' la FFU.Kosa lao ni kufuatilia haki na stahili zao.

Wazee wetu wakipiga swala.Hivi Kikwete angewakalia kooni mafisadi wa Kagoda na wana-EPA wengine kisingepatikana japo kiasi cha mboga kuwatuliza wazee wetu hawa?

Katika moja ya hotuba zake Bungeni,Kikwete alikumbushia umuhimu wa haki za kinadamu za mafisadi.Vipi kuhusu haki za msingi za wazee hawa wasio na hatia?

Picha ya juu na chini: Wazee wetu wakijipoza kwa mlo baada ya awamu nyingine ya danadana za kupata haki zao.Natumaini wazee hawa wanafahamu nani ni kikwazo cha ufumbuzi wa tatizo lao.Haya ndio Maisha Bora aliyowaahidi Kikwete mwaka 2005.Na hiyo ndio Ari Mpya, Kasi Mpya na Nguvu Mpya ya kutatua kero zenu.Bado mnatafuta sababu za ziada za kumnyima kura?

Picha kwa Hisani ya MICHUZI JUNIOR (Jiachie).Maelezo ya picha ni yangu binafsi.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.