Showing posts with label KATIBA MPYA. Show all posts
Showing posts with label KATIBA MPYA. Show all posts

5 Apr 2014


Kimsingi, mchakato wa kupata Katiba mpya umegeuka kuwa hukumu ya Muungano wa 'Tanganyika' (Tanzania Bara) na Zanzibar. Mengi yamesahongelewas na nisingependa kuyarudia hapa, lakini suala jipya lililojitokeza ni sahihi za Marehemu Baba wa Taifa na Marehemu Karume.

Kuna taarifa kwamba baadhi ya nyaraka hazina sahihi ya Marehemu Karume, hali inayoweza kuashiria kuwa uamuzi wa Muungano ulifanywa na Nyerere pekee. Japo historia inaeleza tofauti, kwa kawaida, hati ya mkataba huwa na angalau na sahihi za wahusika wawili au zaidi kutegemea mazingira ya mkataba husika.

Lakini hata hiyo sahihi ya Nyerere yenyewe imezua utata. So far, kuna sahihi mbili (yawezekana zipo nyingine). Lakini sio tu sahihi kuwa zaidi ya moja, katika moja ya nyaraka za Muungano kuna maneno yameongezwa. Maelezo yanayotolewa ni kuwa kompyuta ilitumika...bila hata kuuliza kompyuta ilitumika kwa malengo gani, swali la msingi ni je Tanzania- au Tanganyika ilikuwa na kompyuta mwaka 1964?

Licha ya sahihi ya Nyerere, kuna taarifa pia ikwamba hata sahihi ya Katibu wa Bunge wa wakati huo, Pius Msekwa nayo ina walakini. 

Mara kadhaa katika maandiko yangu nimebainisha kuwa haileti maana kujadili muundo wa Muungano pasipo wajjumbe wa Bunge la Katiba kupatiwa nyaraka muhimu zinazohusu Muungano huo. Maelezo yaliyotolewa na wahusika ni kwamba eti kuna nakala moja tu ya moja ya nyaraka muhimu za Muungano, kwahiyo haiwezi kupelekwa Dodoma kwa kuhofia inaweza kupotea. Huu sio utoto tu bali ni ubabaishaji wa hali ya juu. Kwanini wahusika wasichapishe nakala kisha kuzi-certify as true copies of the original?

Anyway, hebu analia katika picha ya hapo juu kuhusu ipi ni sahihi halisi ya Mwalimu Nyerere.

Nihitimishe bandiko hili kwa kuyumkinisha kuwa utata unaojitokeza kuhusu nayaraka muhimu za Muungano unaashiria kwamba kuna mtu flani mahala flani anaongopa (someone somewhere is lying). Tusichojua ni kwanini?

TIME WILL TELL 

5 Oct 2013



Mnamo tarehe 9 Desemba 1961, Tanganyika ilipata Uhuru chini ya Waingereza waliokuwa waangalizi wetu tu, 

Ni nyakati hizo ambapo mataifa ya Afrika yalikuwa kwenye vuguvugu la kupata uhuru wao kamili yakiongozwa na Nchi ya Gold Coast iliyojinyakulia uhuru kutoka kwa Uingereza mnamo tarehe 6 Machi 1957, na ikawa taifa la kwanza la Afrika Kusini mwa Sahara (Sub-Saharan Africa) kufanya hivyo japokuwa Gold Coast/Ghana haikuweza kutangaza uhuru wake kamili kutoka kwa Uingereza hadi tarehe 1 Julai 1960 ambapo pia nchi ilianza kujulikana kama Jamhuri ya Ghana.

Nchi ya Gold Coast ilianzishwa na Waigereza, "Gold Coast" ni nchi ya Ghana ya leo, Neno Ghana lina maana ya Shujaa Mfalme na lilikuwa ni jina la heshima walilopewa wafalme wa Himaya ya Ghana nyakati za kale za Afrika Magharibi.

Tangu Tanganyika ipate uhuru 09/12/1961 hadi kifo chake chenye utata 1964, ilitumia KATIBA ya chama cha Ukombozi cha TANU iliyoandikwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, pamoja na mahuisho mengi yaliyopita kama yale ya 1962, 1965, 1977, 1992 bado asili ya katiba hii tuliyonayo leo ni ya MKONO wa Julius Nyerere,

Marekebisho makubwa ya Katiba yalikuwa ni mwaka 1977, lakini asili ya KATIBA ile ya Mkono wa Nyerere imeendelea kuishi na kulitendea haki Taifa na wajihi wake!

Nchi ya Gold Coast ilipopata uhuru chini ya Kwame Nkrumah licha ya kubadili jina la nchi na kuitwa Ghana, bado iliendelea kutumia asili ya katiba ya Chama cha The Convention People's Party (CPP) 

Labda kwa wale wasiojua niwafahamishe kuwa Katiba ya Tanganyika African National Union (TANU) ilinakiliwa kutoka chama rafiki cha The Convention People's Party (CPP)

Ni mashirikiano mema katika makutano ya fikra za kisiasa kati ya vijana wawili wasomi na imara ambao bara la Afrika halijapata kuwa nao kwa karne hivi sasa, si wengine ni Julius Nyerere na Kwame Nkrumah walipobadilishara fikra na kuzaa matunda ya Afrika na dunia tuyatafunayo sasa,

Nimekuwa na mtazamo hasi kabisa juu ya uhuru wa Afrika kwa mda mrefu sana hasa kwa matukio niyaonayo na niyasikiao toka Afrika,

Miaka ya 1955-1975 ni kipindi ambacho Afrika ilijitoa toka mikononi mwa mkoloni, mimi huwa naamini ni kipindi ambacho Afrika haikuwa na sifa za kuwa tayari kujitawala kwa maana ya kujipatia/kupewa UHURU,

1. Afrika haikuwa na Wasomi wakuongoza nchi

2. Waafrika walikuwa kwenye lindi la kutopea kwenye ujinga, hawakuwa tayari kwa kuupokea uhuru huo,

Mfano Tanganyika ilipata Uhuru ikiwa na wasomi wachache wenye ngazi ya shahada ya Uzamili (Masters) ambae ni Julius Nyerere, na Shahada ya Uzamivu (PHd) ni mmoja tu ambaye ni Dr Vedasto Kyaruzi, 

Na hata wale waasisi waliokuwemo kwenye harakati za kupigania Uhuru ndani ya TANU hawakuwa wasomi wa ngazi za juu zaidi ya Julius Nyerere,

Wazee hawa ni Julius Kambarage Nyerere, Ali Sykes, Lameck Makaranga, Gosbert Milinga, Gelmandus Pacha, Joseph Kimalando, Japhet Kirilo, Abubakar Ilanga, Saadan Kandoro, Suleiman Kitwara, Kisunguta Kabara, Tewa Said Tewa, Dosa Aziz, Patrick Kunambi, Joseph Kasela-Bantu, John Rupia, Abdul Wahid Sykes.

Nchi ya Gold Coast/Ghana ilipopata uhuru haikuwa na wasomi wengi wa Shahada, Stashada na Shahada ya Uzamivu na uzamili, 

Msomi wa ngazi ya juu alikuwa mmoja tu mwenye shahada ya Uzamili (Master of Science) ndugu Kwame Nkrumah 

Japokuwa usomi wa ngazi ya juu kwa watawala sio tiketi ya uwezo wa kutawala katika nchi, Hili huwa naamini ni kosa la Afrika la 1960-1975 kudai Uhuru na kupewa MAPEMA huku Waafrika hawakuwa tayari kujitawala wenyewe,

Hatua hii hunifanya niamini kuwa Afrika haikuwa imepevuka kujitawala kwa ngazi ya karne ile ya 20, huwa naamini kuwa miaka 1975-1985 ndicho kipindi ambacho Afrika ingekuwa kwenye mapito sahihi ya kujitawala, nikipindi ambacho binadamu wa Afrika angekuwa amepevuka,

Sasa ni karne ya 21, kosa lile la Karne ya 20 linajirudia katika muundo uleule kasoro nadharia tu, nalo ni upatikanaji wa Katiba mpya ya Tanzania,

Hali hii ya uhitaji wa katiba mpya kwa Watanzani ni jambo la kupongezwa na kujivunia kwa kila mtanzania, kwakuwa imedhihirika kuwa sasa Taifa limekuwa kifikra, na zaidi idadi ya wasomi katika nchi imeongezeka maradufu,


Lakini jambo la hatari na lisilokubalika nikuwa Taifa limeaminishwa kuwa Katiba Mpya itapatikana kabla ya 2015, huu ni ulaghai na wendawazimu wa wazi kabisa,

Katiba ya Watanzania haiwezi kupatikana kwa miaka mitano ama mmoja huu uliosalia, Katiba inayohitaji maridhiano, katiba inayopita kwenye misigano ya kitaifa, katiba inayohitaji elimu kwa Watanzania kwanza kamwe haiwezi kupatikana kabla ya 2015, kitakachopatikana kabla ya 2015 kitaitwa katiba ya kisiasa sio katiba ya Watanzania, 

Ninachokiamini nikuwa Watanzania tujipe muda, turuhusu fikra na mijadala huru iendelee juu ya upatikanaji wa Katiba mpya, turuhusu majibizano ya hoja ya endelee, tuyturuhusu Watanzania wote wake kwa waume, Wazee kwa vijana wote watoe ya moyoni bila kuogopa mawazo yao,

Katiba bora ya kiraia yenye matakwa halisi ya Wananchi inaweza kuchukua hata miaka 10 mchakato wake mpaka kuipata, hivyo katiba hii ambayo mchakato wake unaendelea SIO lazima isimamie Uchaguzi wa 2015 kama wanasiasa wanavyotusukuma tuamini hivyo,

Nionavyo muhimu katika kipindi hiki nikuwa, Watanzania, wanaharakati na Wanasiasa waendele kusimamia mchakato uendelee lakini upande wa pili wageuzi fikra zao, uanzishwe mchakato wa marekebisho ya Katiba hii iliyopo ili tuingie nayo kwenye uchaguzi 2015.Kinyume na hapo ni kuwalaghai Watanzania kuwa katika itapatika kabla 2015, 

Ikumbukwe kuwa Jakaya Kikwete ambae sasa ndiye rais wa Tanzania, katika historia ya siasa zake DUNIANI, hajawahi kuhitaji katiba mpya ya Tanzania wala kuizungumzia tu, hata serikali ya Chama chama Mapinduzi ambacho yeye ndiye Mwenyekiti hakijawahi kuhitaji Katiba Mpya ya Tanzania, na zaidi serikali ya Chama cha Mapinduzi iliyodumu kwa miaka 50 sasa haijawahi kuhitaji katiba Mpya ya Tanzania,

Vyama vya upinzani na Wanaharakati wa Tanzania ndio walioasisi mapambano ya kudai Katiba mpya, tena vikipita katika mapito magumu sana yenye kuhatarisha uhai wao,

Ni baada ya uchaguzi mkuu 2010 ndipo mbinyo wakudai katiba mpya ukiongozwa na chama kikuu cha upinzani nchini huku ccm na wahafidhina wake wakipinga katukatu kuwa Taifa halihitaji Katiba mpya,

Lakini KUFUMBA na KUFUMBUA Jakaya Kikwete alilitangazia Taifa kuwa linaanza mchakato wa Katiba, akitumia neno KUHUISHA katiba.

Tafakari Chukua Hatua, Busara ni mwanzo wa kukaribisha Hekima yenye nguvu za maliza tofauti katika nchi na kupata katiba ya kiraia yenye mkono wa Mtanzania

8 Apr 2012



Mwasisi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mzee Edwin Mtei, amezungumzia uteuzi wa wajumbe wa Tume ya Kuratibu Maoni ya Katiba iliyotangazwa majuzi na Rais Jakaya Kikwete.Katika bandiko lake kwenye mtandao wa jamii wa Jamii Forums,Mzee Mtei amepongeza hatua ya Rais Kikwete kuteua Tume hiyo na hatua nzima ya kuanzisha mchakato wa mabadiliko ya Katiba tuliyonayo sasa.

Hata hivyo,mwanasisasa huyo mstaafu ambaye aliwahi kuwa Gavana wa Benki Kuu katika Serikali ya Awamu ya Kwanza,ameonyesha wasiwasi wake kuhusu muundo wa Tume hiyo huku akitafsiri kuwa muundo wa Tume hiyo unadhihirisha kuwa demokrasia ya kweli ni ndoto kwa Watanzania.

Katika bandiko hilo,Mzee Mtei amehoji mantiki ya kukosekana uwiano halisi kati ya wajumbe wa Tanzania Visiwani na wale wa Bara kwa kuzingatia kigezo cha idadi ya watu,na akagusia pia kukosekana kwa uwiano wa imani ya kidini miongoni mwa wajumbe (yaani Waislam na wasio Waislam).

Tayari kauli hiyo ya Mzee Mtei inaelekea kuzua mjadala hata ndani ya Chadema,ambapo Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia chama hicho, Mheshimiwa Zitto Kabwe, amenukuliwa kwenye ukurasa wake wa Twitter akisema, "Yeyote anayeangalia #TumeyaKatiba kwa misingi ya #Dini za wajumbe amefilisika kimawazo, ni kirusi dhidi ya Utanzania wetu. Azomewe"


Bandiko halisi la Mzee Mtei ni hili hapa chini (BONYEZA PICHA KULIKUZA)




6 Apr 2011

 Tanzania Constitutional Review Bill 2011

1 Jan 2011



Heri ya Mwaka Mpya.Well,so far hakuna jipya katika mwaka huu ukiondoa mabadiliko kwenye tarakimu 2010,ambapo sasa inasomeka 2011.Kitu pekee kitakachofanya upya wa mwaka huu (na pengine hapo baadaye) ni mabadiliko.Iwe ya mtu binafsi au ya jamii.Na baraka za Mungu,ofkozi

Nimesoma hotuba ya Rais Jakaya Kikwete kuaga mwaka jana na kukaribisha mwaka huu "mpya".Naomba niwe mkweli.Hotuba hiyo imethibitisha kwa mara ya elfu kidogo kuwa Kikwete is out of touch.Najua hadi hapa msomaji mpendwa unaweza kusema "ah ee bwanaee,kweli wewe unamchukia JK.Yani hata alivyoahidi Katiba mpya bado unamlaumu?".Well,simchukii huyu Mkwere bali siridhishwi na udhaifu wake kiuongozi.

Hotuba ya Kikwete jana inatoa picha wa kiongozi wa nchi ya kufikirika.Badala ya kuwa mkweli kwa anawaowaongoza,anarejea usanii wake wa kwenye kampeni za uchaguzi ambapo yayumkinika kusema aliweka historia kwa kutoa rundo la ahadi,ilhali nyingi ya zile alizotoa mwanzo zikiwa hazijatekelezwa.

Kuna bloga mmoja ameandika makala ya kumpongeza JK kwa kuanzisha mchakato wa Katiba mpya.Tatizo la ndugu yangu huyu ni kuweka busara zake kando kila linapokuja suala linalomhusu JK.Anasahau kuwa umuhimu wa Katiba mpya sio matakwa ya Rais,na hasa ikizingatiwa bayana kuwa Katiba mpya si miongoni mwa vipaumbele vyake (if he has any at all).Lakini pia anapuuza ukweli kuwa tamko la jana ni matokeo ya moto unaowaka kwenye jamii kushinikiza jambo hilo muhimu.Sasa hata kiongozi anapofanya kile anachopaswa kufanya-yaani kusikiza matakwa ya jamii- ni sababu ya kiongozi huyo kuingizwa kwenye vitabu vya historia?This is way too low hata kwa magwiji wa kujipendekeza.

Lakini ili uelewe vema mantiki ya post hii,jaribu kusikia baadhi ya kauli za viongozi wa mataifa yenye hali njema zaidi ya Tanzania,Waziri Mkuu wa Uingereza,David Cameron,kwa mfano wa karibu na ulio mwafaka.Katika salamu zake za mwaka mpya,Cameron amekuwa mkweli kwa Waingereza na kuwaambia licha ya jitihada za serikali yake ya mseto (wa vyama vya Conservative na Liberal Democrats),mwaka 2011 utakuwa mgumu,hususan kutokana na utekelezaji wa hatua za kubana matumizi.Waziri Mkuu huyo alibainisha kuwa hakuna njia ya mkato ya kukabili mwenendo tete wa uchumi wa Uingereza ( sambamba na kuyumba kwa uchumi wa dunia) bali kufanya kinachostahili sasa ili kuepusha madhara makubwa mbeleni.Pia,Cameron,aliwafahamisha Waingereza kuwa tishio la ugaidi bado lipo juu,na akawaomba Waislam wa nchini hapa kusaidia katika mapambano dhidi ya msimamo mkali wa kidini.

Tofauti na Kikwete ambaye sehemu kubwa ya hotuba yake ilikuwa inatoa picha kuwa Tanzania iko shwari kabisa-kisiasa,kiuchumi,kijamii,nk,mwenzie Cameron hakuumauma maneno bali alifanya kile kinachopaswa kufanywa na kiongozi anayejali ncbi na watu wake.Wafadhili wetu wanakuwa wakweli kwa walipakodi wao,sie wafadhiliwa tunavishana vilemba vya ukoka kuwa mambo si mabaya.

Ukisikia namna Kikwete anavyozungumzia uchumi wa Tanzania,unaweza kudhani nchi yetu iko kwenye ngazi ya developed nations,hatutegemei fadhila za wahisani kutosheleza bajeti yetu na tunamudu kwa ufanisi huduma muhimu kwa umma.Uchumi pekee unaoleta maana kwa Mtanzania wa kawaida sio takwimu,kwa vile baba hawezi kuilisha familia yake kwa takwimu.Hakuna mwenye nyumba atakayemwelewa mpangaji wake kwa takwimu,au muuza duka atakayekuuzia bidhaa kwa takwimu badala ya fedha.Umasikini unazidi kuongezeka miongoni mwa Watanzania lakini hilo halimsumbui Kikwete kwa vile takwimu zinaridhisha.

Hebu angalia alivyozungumzia ishu ya umeme!Ahadi juu ya ahadi kama ilivyokuwa wakati wa kampeni.Lakini kingine cha msingi ni ni ahadi kuwa tatizo la umeme linatarajiwa kumalizwa within miezi 36 kutoka sasa.I wish iwe hivyo,lakini itawezekanaje kuwa hivyo katika hali tuliyonayo sasa ambapo sekta ya nishati ni kitegauchumi cha kuaminika zaidi kwa mafisadi?Je dhamira hiyo ya Kikwete ina baraka kutoka kwa akina Rostam?Je wamemwahidi kuwa hakutakuwa na Richmond na Dowans nyingine mara baada ya kulipwa shilingi bilioni 185 kama zawadi ya kutufisadi?Halafu yule bloga wa kujipendekeza anasema JK atakumbukwa kwa historia njema (kuhusu Katiba)!!!

Na wakati ameweza kutetea ongezeko la bei ya umeme,JK alijifanya hajasikia kuwa kampuni ambayo hadi leo hatujui mmiliki wake-Dowans- italipwa shs bilioni 185 licha ya utapeli na ujambazi waliotufanyia.JK alijifanya hakumbuki kauli ya Mwanasheria wake Mkuu,"Mura" Jaji Werema ( pumzika kwa aibu huko Ukuryani,bosi wako JK kakuumbua),kwamba suala la kuilipa Dowans halina mjadala.Kikwete ameshindwa kuwaambia ukweli Watanzania kuwa bei ya umeme inabidi iongezeke ili kupata fedha za kuwalipa wanaharamu wa Dowans.

Kuna wanaoweza kudai JK asingeweza kuongelea ishu ya kuilipa Dowans kwa vile ni suala la kisheria.Je alipozungumzia uwezekano wa serikali yake kukata rufaa dhidi ya hukumu ya Zombe haikuwa jambo la kisheria?

Ndio maana kichwa cha habari cha post hii kinahoji JK amejulia wapi kuwa Watanzania wanahitaji Katiba mpya ilhali yeye anaonekana kuishi nchi tofauti na wanayoishi walalahoi?Amejuaje kuhusu Katiba lakini ameshindwa kujua kuhusu Dowans?Jibu ni rahisi.He is completely out of touch with reality.Anazungumzia kubana matumizi wakati serikali yake inaendeleza matumizi ya anasa na akina Mkulo wanakodi ndege kwa shs milioni tano kuhudhuria mahafali huku shangingi lake likipelekwa "tupu".Au anajigamba kuhusu kubana matumizi kwa vile the so-called "Mtoto wa Mkulima",Waziri Mkuu,Mizengo Pinda alikataa shangingi (lakini akashindwa kuzuwia shangingi hilo kukabidhiwa mtu mwingine!)

Sijawahi kuongelea suala la Katiba mpya,na leo sintoongelea hilo.Ila kwa wanaoanza kudai kuwa yaani kwa KUAHIDI tu mchakato wa Katiba basi JK ataingia kwenye vitabu vya historia,ni vema wakatambua kuwa JK ni GWIJI LA AHADI.Pia wanapaswa watambue kuwa hii top-bottom model of constutitional reforms inaweza kutuletea kilekile tunacholalamikia kuhusu Tume ya Taifa ya Uchaguzi: vitu vinavyofanywa kiujanja ujanja kuendeleza maslahi ya makundi flani.Kinachohitajika sio tume ya mchakato wa mabadiliko ya katiba bali tume HURU ya kushughulikia mchakato huo.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.