Showing posts with label Karenzi Karake. Show all posts
Showing posts with label Karenzi Karake. Show all posts

23 Jun 2015

Polisi jijini London hapa Uingereza wamemkamata Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa ya Rwanda, Jenerali Karenzi Karake, kutokana na maombi ya Hispania ambako anahitajika kwa makosa ya uhalifu wa kivita.

Jenerali Karake, Mkurugenzi Mkuu wa National Intelligence and Security Services alikamatwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Heathrow, Jumamosi iliyopita, kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na polisi wa hapa jana.

"Karenzi Karake, mwenye umri wa miaka 54, raia wa Rwanda, alifikishwa mbele ya mahakama ya Westminster, (jijini London)...baada ya kukamatwa kwa kutumia hati ya Ulaya ya kusaka watuhumiwa (European Arrest Warrant) kwa niaba ya mamlaka za Hispania, ambako anatafutwa kuhusiana na uhalifu wa kivita dhidi ya raia," ilieleza taarifa iliyotolewa kwa barua-pepe.

Jenerali huyo alirudishwa rumande hadi Alhamisi.

Haikuwezekana mara moja kuwasiliana na familia ya mkuu huyu wa ushushushu au mwanasheria wake nje wa muda wa kazi jijini London. Ubalozi wa Rwanda hapa Uingereza nao haujatoa maelezo yoyote.

Mwaka 2008, jaji wa mahakama kuu ya Hisania, Fernando Andreu, aliwatuhumu viongozi 40 wa kijeshi na kisiasa wa Rwanda, ikiwa ni pamoja na Jenerali Karake, kujihusisha na mauaji ya kisasi kufuatia mauaji ya kimbari yaliyoikumba nchi hiyo mwaka 1994.

Jaji huyo aliwaona watuhumiwa hao na hatia ya mauaji ya kimbari, ualifu dhidi ya binadamu na ugaidi, makosa yaliyopelekea vifo vya mamia ya maelfu ya watu ikiwa ni pamoja na Wahispania.

CHANZO: imetafsiriwa kutoka Matthewaid.com


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.