Showing posts with label LA PRINCESSA WORLD. Show all posts
Showing posts with label LA PRINCESSA WORLD. Show all posts

16 Aug 2010

Miongoni mwa mapungufu yanayowakabili baadhi ya Watanzania wenzetu ni kushindwa kusifia pale inapostahili.Na miongoni mwa "udhaifu" wangu ni kushindwa kujizuia kumwaga sifa pale inapostahili (au kukosoa pale inapobidi).Waingereza wana msemo "beauty should never be imprisoned", yaani-kwa Kiswahili- "urembo haupaswi kuwekwa jela".Mantiki ya msemo huo ni kuhamasisha jamii kusifia vinavyostahili sifa.Na kwa kufanya hivyo tunawafanya wanaostahili sifa hizo kutambua thamani yao na pengine kuboresha zaidi wafanyayo.

Nisijizungushe sana.Leo naomba kukujulisha msomaji wangu mpendwa moja ya blogu ambazo kila napozitembelea (na ninatembelea blogu nyingi kila siku ya Mungu) hupatwa na msisimko wa aina yake.Blogu hiyo si nyingine bali ni La Princessa World.Of course,ili ufahamu ni nachoongea hapa inabidi "yai liwe linapanda" (I mean,uwe unaimudu vema lugha ya Kiingereza) kwani mdada mwenye blogu hiyo "anakichezea Kiingereza namna anavyotaka".Na hiyo ni moja ya mambo yanayovutia katika "uandishi binafsi" (kwa mfano makala magazetini au bloguni): namna mwandishi anavyoweza kucheza na lugha apendavyo kama ambavyo mwanasoka mahiri anavyoweza kuuchezea mpira atakavyo.Tuseme uandishi unaoshabihiana na vipaji vya viumbe kama Ronaldinho,Messi,Zidane,nk.

Blogu ya La Princessa World imejikita zaidi kwenye masuala ya fasheni,wenye majina (celebrities),muziki,filamu na mambo mengine ya kusisimua.Yayumkinika kusema kuwa masuala ya fasheni ni ya akinadada zaidi lakini,binafsi,kanuni yangu ya kumudu kuwa "well-rounded" ni kujifunza mambo mengi kadri inavyowezekana.Na ni katika kufanya hivyo ndipo unaweza "kukopa" ujuzi na uelewa wa wengine waliobobea katika fani zao."Ugonjwa" wangu ni siasa lakini napendelea kuitanua siasa hadi kwenye maeneo mengine ya maisha,kwa mfano siasa za urembo,muziki,filamu,nk.Hata hivyo,by "kutanua" simaanishi kuchanganya siasa na urembo,kwa mfano,bali kama ilivyo katika "siasa proper" ,ninachofanya ni kuelewa kwa undani ishu kama trends,shakers and movers,siri na mbinu,na vitu kama hivyo.

Nimalizie kwa kukusihi uwe unamtembelea La Princessa kufaidika kama navyofaidiaka mie kila napotembelea hapo.Usitafsiri kama "nampigia mtu debe" bali,kama nilivyoandika awali,napenda kuenzi vipaji vya wenzetu na   pia kila mara napenda kuwajuza (kuwajulisha) wasomaji wangu wapendwa yale yote ambayo kwa mtizamo wangu nadhani yanafanya kila ziara yako mtandaoni ikupatie kitu kipa au "kile roho yako inapenda".

Kwa La Princessa,nachoweza kuandika kwa kifupi ni kuwa umesimika kiwango (setting the bar) katika kublogu sio kwa akina dada pekee bali hata kwa bloga wa kiume.Kinachonigusa zaidi ni namna unavyocheza na lugha,kitu mabcho sio tu kinaonyesha namna unavyoimudu bali pia unavyoweza kuitumia katika namna mwafaka kumburudisha msomaji wako.

Word up!

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.