Showing posts with label Let's Read. Show all posts
Showing posts with label Let's Read. Show all posts

21 May 2018



Kuna msemo usiopendeza kwamba, ukitaka kumficha kitu Mswahili, basi weka kwenye kitabu. Waswahili wengi wanaogopa maandishi kuliko virusi vya UKIMWI, except maandishi hayo yatakapohusu UBUYU, our nation's favourite.

Sasa, kwa vile lawama hazijengi, nimeamua kuendeleza utaratibu niliouanzisha huko Facebook ambapo mara kwa mara nilikuwa nawapatia watu machapisho mbalimbali BURE. Kwahiyo, angalau mara moja kwa wiki, nitakuwa naweka post yenye link ya kupakua kitabu chenye umuhimu kwako. Series hiyo ya vitabu takriban kila wiki ninaipa jina "Let's Read / Na Tusome."

Leo tunaanza na chapisho hili muhimu kuhusu "ushushushu." Ni mwongozo wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) kuhusu "kuzuga watu" (trickery) na hadaa (deception). Baadhi yenu mtakuwa mlishakipakua nilipokiweka mara mbili huko Facebook.

Pakua HAPA


Sambamba na vitabu, from time to time nitajitahidi kubandika makala mpya mara nyingi zaidi ya ilivyo sasa ambapo inaweza kupita mwezi mzima bila kubandika post yoyote ile.Tarajia mada za mbinu za kimaisha (life hacks), usalama wa mtandaoni (cybersecurity), nyeNzo za mtandaoni (internet tools), afya, na kadhalika. Hakikisha unatembelea blogu hii mara kwa mara.


Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.