Showing posts with label Lugumi. Show all posts
Showing posts with label Lugumi. Show all posts

24 May 2016

Sakata la kutumbuliwa kwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga, linazidi kutawala vichwa vya habari, huku maendeleo mapya yakiashiria kuwa kuna mengi yanayoweza kuwa yanaendelea 'nyuma ya pazia.'

Jana, watu waliojitambulisha kama 'wana-jimbo wa Misungwi' walitoa tamko kwa waandishi wa habari. Hebu ndugu msomaji mpendwa, fanya kulisoma tamko hilo kwanza, kisha bingirika nami kwa uchambuzi zaidi, and trust me, sintokuangusha haha!

First thing first, hawa 'wana-jimbo wa Misungwi' WAMETUMWA NA NANI? Ninauliza hivyo kwa sababu hisia yangu ya sita inanituma kuamini kuwa hawajajitolea wenyewe tu kutoa tamko hilo. Hawa wametumwa, no doubt about that. Lakini hatujui nani kawatuma.

Kwa kuitegemea tena hisia yangu ya sita, yayumkinika kuhisi kuwa hao 'wana-jimbo' ni wapambe tu wa Kitwanga. Twende mbali zaidi, ninahisi watu hao ni sawa na spika tu ya kumwezesha Kitwanga asikike.. 

Tetesi zinaeleza kuwa Kitwanga alikuwa 'mtu wa kinywaji' kitambo sasa. Na kwa wenzetu ambao hawajawahi kugusa kinywaji, ukweli upo hivi: hakuna mtu anayeitwa 'mnywaji wa muda mrefu.' Mtu wa aina hiyo ni MLEVI. Period. Na ulevi, japo si dhambi au kinyume cha sheria, una athari zake. Kuna mlolongo mrefu wa jinsi ulevi ulivyobomoa maisha ya watu mbalimbali. Kwahiyo, tukiafikiana kuwa Kitwanga ni mlevi, basi ilikuwa suala la muda tu kabla haijamlipukia. Kwa lugha nyingine, Bwana Kitwanga alikuwa kama time-bomb, muda wowote ule lingetokea la kutokea.

Mengi yameshaongewa tangu Kitwanga atumbuliwe na Rais Magufuli hapo juzi, makubwa zaidi yakiwa ni pamoja na madai kuwa ishu hiyo ni mcheoz wa kuigiza. Kwamba kutumbuliwa kwa Kitwanga ni mkakati wa makusudi wa kuiua ishu ya Lugumi. 

Siafikiani na mtazamo huo kwa sababu kama kweli Magufuli alikuwa anataka kumuokoa rafiki yake alikuwa na njia nyingi tu, moja ya wazi ikiwa ni 'kuziba masikio,' kwa maana ya kupuuza kelele za waliotaka Kitwanga atumbuliwe.

Wengine wanadai kuwa kweli Kitwanga alikuwa amelewa, lakini hakulewa kwa hiari yake bali 'kinywaji chake kilifanyiwa utaalam,' wakijaribu kutushawishi kuwa Kitwanga alihujumiwa. 

Hizi ni hisia tu zisizo na uthibithso wowote. Jamaa alikuwa 'chapombe,' na wanaomfahamu hawashangazwi na hilo tukio la majuzi au kutumbuliwa kwake. Pombe sio chai, siku ya siku lazima itamwadhiri mtu.

Madai mengine ambayo yanahusiana na hayo ya 'kinywaji cha Kitwanga kufanyiziwa' yanauhusisha utawala wa Awamu ya Nne ya Rais Jakaya Kikwete, ambako ndiko suala la Lugumi lilianzia. In fact, hizo tuhuma za 'kinywaji cha Kitwanga kufanyiziwa' zinawahusu baadhi ya watu waliokuwa karibu na utawala huo. 

Na kama msomaji ulivyoona katika 'tamko la wana-jimbo wa Misungwi' hapo juu, mmiliki wa Kampuni ya Lugumi, Said Lugumi na mtoto wa Rais Kikwete, Ridhiwani, wametajwa kuwa miongoni mwa wanaomhujumu Kitwanga.

Sawa, ishu ya ufisadi wa Lugumi ipo complex lakini kudai kuwa akina Lugumi na Ridhiwani ndo waliomfanyizia Kitwanga hadi akaishia kutimuliwa na Rais Magufuli ni hisia tu zisizo na mantiki. Haina mantiki kwa vile haiingii akilini jinsi gani hao jamaa wangemudu kumhujumu Kitwanga na wakati huohuo kumshinikiza Magufuli amchukulie hatua.

Kwa upande mwingine, Spika Job Ndugai, amejiingiza matatizoni 'kitoto' kwa kauli yake isiyo na busara ianyoashiria kuwa 'ulevi wa Kitwanga ni cha mtoto, kuna waheshimiwa wanavuta bangi na kubwia unga.' Really? Yaani Spika anawafahamu waheshimiwa wanaotenda makosa ya jinai lakini anawahifadhi!? 

Sasa, inasemekana baadhi ya wabunge wameamua kumkalia kooni awataje hao 'wabunge wavuta bangi na wala unga' na ajieleze kwanini hakuwaripoti kwa mamlaka husika.

Kadhalika, baadhi ya 'wazushi' wanamtaka Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuonyesha uthibitosho kuwa kweli Kitwanga alikuwa 'njwii' siku ile pale Bungeni hadi Rais Magufuli kuchukua hatua ya kumtumbua. Nadhani hii inalenga kumpima ubavu tu Waziri Mkuu Majaliwa kwani kila aliyeona Kitwanga akijibu swlai pale Bungeni hatoshindwa kujua kuwa alikuwa amelewa

Anyway, blogu hii inaendelea kufuatilia ishu hiyo, pamoja na ishu nyingine mbalimbali katika jamii yetu. Pia, kesho, makala yangu katika toleo la wiki hii la jarida la Raia Mwema inajadili kwa kirefu kuhusu suala hilo la Kitwanga kutumbuliwa. Usikose kupata nakala yako.

21 May 2016


Nianze makala hii kwa kumpongeza Rais John Magufuli kwa hatua aliyochukua jana ‘kumtumbua’ aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga, kwa kosa la kuingia Bungeni akiwa amelewa.

Kadhalika, ningependa kutumia fursa hii kumshukuru kwa kuwa kiongozi msikivu. Binafsi, ‘nilikomalia’ sana kuhusu uwaziri wa Kitangwa hasa kutokana na tuhuma kuwa ni mhusika katika skandali ya Lugumi (na tetesi kuwa alikuwa mlevi - japo sikuwahi kuongelea ishu hiyo ya ulevi kwa vile niliona kama suala binafsi, alimradi haliathiri utendaji wake wa kazi). 

Kwa ‘mtaani’ hatua hiyo ya Rais Magufuli inaweza kuonekana ni ya kawaida tu, yaani kiongozi aliyefanya uteuzi wa mtu flani, hatimaye kuamua kuteungua uteuzi huo. Lakini kwa hakika, hatua hiyo ya Rais Magufuli haikuwa rahisi. 

Kwa mujibu wa taarifa, Rais Magufuli na Kitwanga wamekuwa marafiki wa muda mrefu. Wajuzi wa mambo wanaeleza kuwa hata uamuzi wa kumteua Kitwanga kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ulitokana na imani ya Rais Magufuli kwa rafiki yake huyo. Ikumbukwe kuwa wizara hiyo ni moja ya wizara nyeti ambazo kwa kiasi kikubwa hukabidhiwa kwa watu wanaoaminika mno kwa rais husika. 

Kuna kipande cha video kilichosambaa mtandaoni siku za nyuma ambacho kilikuwa kinamwonyesha Rais Magufuli kabla hajawa rais wala mgombea wa CCM, akiwa na Kitwanga, na katika maongezi yao, Kitwanga anasikika akimwambia Magufuli agombee urais (japo ni katika hali ya utani). 

Lakini pia inaelezwa kuwa hata kabla Rais Magufuli hajatangaza baraza lake la mawaziri, Kitwanga alikuwa akijigamba kuwa angepewa wizara nyeti, mara baada ya Magufuli kutangaza kabineti yake, na wizara nyeti ya mambo ya ndani ya nchi akapewa baada ya kutangazwa kabineti hiyo. 

Hata hivyo, suala hili la Kitwanga linapaswa kuamsha maswali kuhuru Idara yetu ya Usalama wa Taifa na utaratibu wa ‘kuwatafiti wateule watarajiwa wa Rais,’ kitu kinachofahamika kitaalam kama ‘vetting.’ Nina uhakika wa asilimia 100 kuwa ‘dossier’ (kabrasha maalum kuhusu mtu maalum) la Kitwanga lilipaswa kueleza bayana kuhusu tabia yake ya ulevi. Je ilikuwaje sio tu akateuliwa kuwa waziri bali pia kuteuliwa kuwa waziri katika wizara nyeti kabisa kwa usalama wa raia na nchi. Je kulikuwa na mapungufu huko Idara ya Usalama wa Taifa au walieleza hilo kabla Kitwanga hajateuliwa lakini likapuuzwa? Ni vigumu kuwa na uhakika wa kipi kilitokea. 

Kwa kuwa lengo ni kwenda mbele na si kunyoosheana vidole tu bila kutoa uushauri au kuleta ufumbuzi, binafsi ninashauri wahusika waangalie wapi walijikwaa, ili wasirudie tena kosa hilo. Vetting ya wateuliwa watarajiwa ni muhimu mno kwa sababu licha ya kuiingiza gharama serikali pale inapolazimu uteuzi husika kutenguliwa, pia inahatarisha usalama wa taifa (watu wanaotimuliwa madarakani ni rahisi kuwa recruited na maadui wa taifa ili 'kulipa kisasi').

Tukiweka kando mapungufu hayo, kitendo cha Dkt Magufuli kumtumbua Kitwanga kinapeleka ujumbe mzito kwa kila mtumishi wa serikali. Kwanza, kinaashiria kuwa Rais anafanyia kazi taarifa anazoletewa (maana hakuwepo Bungeni Dodoma wakati Kitwanga akiwa 'bwii' mjengoni. 

Lakini pia kitendo hicho kinaashiria kuwa mfumo wa mawasiliano ndani ya serikali umerejea kama wa zama za Nyerere, pasipo 'taarifa kuvuja' kabla ya kufika mahali stahili. Hali hii itapelekea watendaji wa serikali ikiwa ni pamoja na mawaziri kuwa makini zaidi kwani hawajui nani anawachunguza au nini kinaripotiwa kwa Rais kuhusu wao.

Tukiweka hilo kando, binafsi nimefarijika sana baada ya kusikia taarifa za Kitwanga ‘kutumbuliwa’ kwa sababu nilipiga kelele za kutosha kuhusu uongozi usioridhisha wa mheshimiwa huyo. Nilianza kitambo kuhoji kuhusu utendaji kazi wa waziri huyo.

Suala la kwanza ‘kumshikia bango’ lilikuwa kauli zake za utata kuhusu kupambana na biashara haramu ya madawa ya kulevya. Hili nililiandikia MAKALA HII. 







Baadaye, ikaibuka skandali ya Lugumi, na kwa hakika sikuchoka kupiga kelele, hususan kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter kama inavyoonekana hapa chini 



Sambamba na kelele hizo hatimaye niliamua kuandika MAKALA HII 


Ni matarajio yangu makubwa kuwa makala hii itamhamasisha kila msomaji kuwa na msimamo, na kisha kusimama imara katika msimamo huo, sambamba na kuhakikisha kuwa anachosimamia ni sahihi, na kuendelea kuupigania hadi mafanikio yapatikane. Sio kazi rahisi lakini mara nyingi vitu vizuri, au vinavyodumu, huwa havipatikani kirahisi. 

Mwaka 2006, niliandika MAKALA HII kuhusu suala la mkataba wa kufua umeme, uliopelekea skendo ya Richmond, na nikaendelea kupiga kelele hadi mwaka Februari 2008 baada ya mhusika mkuu katika skendo hiyo, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, kujiuzulu. Hata hivyo, ishu hiyo ilinigharimu mno kimaisha. 

Na hivi majuzi, nilijaribu ‘kuwashikia bango’ wahusika wa Mamlaka ya Mawasiliano TCRA, na nikawatwanga MAKALA hii. 


Siku chache baadaye, bosi wa taasisi hiyo akatumbuliwa. 


Na majuzi tu, Ubalozi wetu hapa Uingereza ulitaka kutufanyia 'uhuni' katika ziara ya Waziri Mkuu, ambapo awali kulikuwa na mpango wa kumkutanisha Waziri Mkuu na kundi dogo tu la Watanzania wanaoishi hapa. Kelele nilizoshiriki kuibua zilisaidia, na hatimaye mkutano huo wa Waziri Mkuu ulifanywa kuwa wa wazi kwa kila Mtanzania mkazi wa hapa kuhudhuria. Nimeelezea kwa kirefu kuhusu sakata hili katika MAKALA HII.

Sitaki kujisifu kuwa kelele zangu pekee ndio zinapelekea hatua kusudiwa kuchukuliwa. Hapana. Ninachojaribu kuonyesha ni ushiriki wangu katika harakati za kudai mabadiliko kwa kupitia maandishi, “kelele zetu” iwe hapa bloguni, kwenye mitandao ya kijamii au kwa njia ya makala. Pia, kwa kuwaeleza wasomaji kuhusu mafanikio ya 'kelele zetu' inasaidia kuhamaisha watu wengi zaidi kutambua umuhimu wa harakati kama hizi katika kuleta mabadiliko kusudiwa


Mara nyingi tunapopiga kelele hizo tunaishiwa kukebehiwa, kuonekana vimbelembele, tusio na vitu muhimu vya kufanya katika maisha yetu binafsi, na shutuma kama hizo. Lakini pindi kelele zetu zinapozaa matunda, walewale waliokuwa wakitukebehi huwa mstari wa mbele “kusaka sifa.” 

Kimsingi, harakati hizi sio za kusaka ujiko au madaraka. Ni kile nilichoeleza awali: kuwa na msimamo na kusimama thabiti katika msimamo huo hadi ufumbuzi wa tatizo husika upatikane.

Nimalizie makala hii kwa kumpongeza sana Rais Magufuli kwa ‘kumtumbua’ Kitwanga. Wanaohisi kuwa kutambuliwa huko ni ‘kuficha kombe’ la ishu ya Lugumi, ombi langu kwao ni wavute subira. 

Sakata la Lugumi sasa litachukua sura mpya, na tusishangae kusikia watu wakiburuzwa mahakamani hivi karibuni. Pia suala hili la kutambuliwa Kitwanga linaweza kumpa fursa Rais Magufuli fursa ya kuwatumbua angalau mawaziri mawili hivi ambao mwenendo wao umekuwa wa kusuasua. Fursa ya kuwatumbua inatokana na kutambuliwa kwa Kitwanga ambako kutamlazimu Rais kufanya ‘reshuffle’ ndogo.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.