Showing posts with label MAISHA. Show all posts
Showing posts with label MAISHA. Show all posts

10 Apr 2015

7 Oct 2014

10_06_DrSenga-cropped
Dokta Senga Omeonga (pichani), daktari bingwa wa upasuaji nchini Liberia, anadhani anajua jinsi gani aliambukizwa ugonjwa hatari wa Ebola.

Julai 15 mwaka huu, bosi wa daktari huyo aliingia ofisini kwake katika Hospitali ya Mtakatifu Joseph, jijini Monrovia, akiwa na mashaka makubwa. Bosi huyo, Mkurugenzi wa hospitali hiyo, alimwambia Dokta Omeonga, amepeana mkono na mtu ambaye baadaye aligundulika kuwa na ugonjwa wa Ebola, na sasa hajiskii vizuri. Mkurugenzi huyo alisema alikuwa akitapika, anasikia kuumwa na kichwa, na alikuwa na homa kali. Lakini siku mbili baadaye, baada ya vipimo vya maabara kuonyesha hajaathirika, na hofu ya Ebola kuondoka, Dokta Omeonga na wenzie walianza kumhudumia bosi wao kama mgonjwa wa kawaida wa malaria au homa ya matumbo.

"Tulivaa glovu wakati tunamhudumia, lakini si katika hali ya tahadhari sana," alisema Dokta huyo.

Wiki moja baadaye, afya ya Mkurugenzi ilizidi kuwa mbaya, na akachukuliwa vipimo vingine. Safari hii majibu yakaonyesha anaugua Ebola, ikiwa ni tukio la kwanza la vipimo vya awali kuonyesha mgonjwa hana maambukizi kabla ya vipimo vya pili kuonyesha ana maambukizi. Neno la kitabibu kwa hali hiyo ni 'false negative.'

Ghafla, kila aliyemhudumia Mkurugenzi huyo akawa katika hofu kubwa. na mwenye uwezekano wa kuwa ameambukizwa Ebola. Hospitali hiyo ikawekewa karantini, na Mkurugenzi akafariki Agosti 2, siku ambayo Dokta Omeonga alianza kutojiskia vizuri kiafya. Kati ya watumishi 20 waliomhudumia Mkurugenzi huyo, 15 walikutwa na Ebola, ikiwa ni pamoja na Dokta Omeonga. Tisa kati yao wameshafariki, ila yeye na wenzie watano wamesalimika.

Daktari huyo aliongea kwa simu na jarida la Newsweek la Marekani kutoka nyumbani kwake nchini Liberia, ambapo wiki tano baada ya kubainika kuwa hana virusi vya ugonjwa huo, bado anajikongoja kurejesha nguvu mwilini.

Hivi mtu anajiskiaje anapokuwa na Ebola?

Ni vigumu kueleza. Mie ni mtu mwenye afya njema. Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kuugua kiwango hicho. Hali ilikuwa mbaya sana sana. Unajiskia dhaifu kupita kiasi na uchovu mwingi. Unatapika na unajiskia homa na kichwa kuuma. Sio kama malaria. Ukiwa na malaria waweza japo kutembea, na unaweza kumeza dawa zako. Ebola ni tofauti kabisa. Ni kama mwili wako haupo nawe tena. Unajiskia huwezi kujihudumia mwenyewe, lazima awepo mtu wa kukuhudumia muda wote.

Ilikuwaje kwako na wenzio pale hospitali yenu ilipowekewa karantini?

Sote tulikuwa na dalili zinazofanana. Kila siku, mmoja baada ya mwingine alikuwa akilalamika kuhusu hali ilivyokuwa inazidi kuwa mbaya. Wakati mwingine tulikuwa tukicheka pamoja na kila kitu kuonekana kama kipo sawia.Lakini pale hali ilipoanza kubadilika, hakuna aliyweza japo kuamka kutoka kitandani.

Walikuwa wakichukua wagonjwa wale tu ambao walikuwa na hali mbaya kupindukia na kuwapelekea kwenye eneo la matibabu ya Ebola. Mie nilikuwa miongoni mwa waliokuwa na nafuu kidogo, kwahiyo ilibidi nisubiri kitambo. Eneo hilo la matibabu lilikuwa ni moja tu kwa jiji zima la Monrovia. Vitanda 40 tu. Ilibidi nisubiri wiki nzima kabla ya kupatia kitanda. Japo walikuwa wakitoa kipaumbele kwa watumishi wa sekta ya afya, bado ilichukua wiki nzima kupata kitanda.

Ulikuwa mmoja wa watumishi watatu wa hospitali yako kupatia dawa ya majaribio ZMapp. Ulijiskiaje ulipoanza kutumia vidonge hivyo?

Nilipewa ZMapp wiki moja baada ya kulazwa katika eneo la matibau ya Ebola. Nilikuwa nikijiskia ahueni kidogo, kuhara kulikuwa kumesimama. Nilikuwa sitapiki tena, na nilikuwa nikijilazimisha kula japo kidogo. Sikuwa na hali mbaya sana wakati naanza kutumia vidonge hivyo. Ninachoweza kusema ni kwamba labda vidonge hivyo vilisaidia kasi ya uponyaji wangu lakini huenda ningeweza kupona bila hata kuvitumia.


Ulijiskiaje kutumia dawa mbayo ilikuwa katika majaribio?

Nilikuwa na hofu kiasi. Lakini pia sikujali sana kwa sababu nilikuwa sina njia nyingine.Hiyo ilikuwa nafasi yangu ya kupata uponyaji. Kama ingenisaidia, ningeiridhia.

Wewe na wenzako mliyamudu vipi matibabu ya vidonge hivyo?

Kwa bahati mbaya, daktari aliyepaswa kupewa vidonge hivyo alifariki siku vilipowasili. Kwahiyo walimpatia mwingine aliyekuwa amepoteza fahamu. Shukrani kwa Mungu kwani hali yake ilikuwa mahututi na uwezekano wa kusalimika ulikuwa mdogo.Lakini baada ya kumeza vidonge hivyo hali yake iliboreka na kila mtu alishangaa. Siku iliyofuata alirejewa na fahamu. Siku chache baadaye aliweza kutembea. Daktari mwingine aliyepatiwa vidonge hivyo alifariki. Kwahiyo kati yetu watatu, mmoja alifariki na sie wawili tulisalimika.

Je dawa hizo zilikuwa na matokeo yasiyokusudiwa (side effects)?


Nilipatwa na matatizo katika dozi ya mwisho ya ZMapp lakini nadhani ilitokana na kasoro za kitabibu, kwa sababu hawakunipatia dawa ya kuzwia aleji niliyostahili kupewa. Nilipatwa na hali mbaya, nikawa najiskia baridi kali, shida katika kupumua vizuri, na maumivu makali ya kichwa. Hali ilikuwa mbaya sana. Kwahiyo ilibidi wasitishe matibabu na kunipatia dawa aina ya cortisone. Baada ya hapo nikawa dhaifu sana. Sikumudu japo kutoka kitandani. Baadaye nikaanza kujisikia nafuu.Nilikaa katika eneo la matibabu ya Ebola kwa wiki mbili unusu.

Wajiskiaje sasa?


Nimekuwa nyumbani kwa mwezi na wiki moja sasa. Kuna maendeleo ya kuridhisha kila siku. Nguvu zangu zanirejea. Lakini hatua ya kuwa katika afya ya kawaida inakuja taratibu sana. Bado naskia maumivu ya viungo, na udhaifu mwilini bado upo. Ni vigumu kusema lini nitakuwa nimepona kabisa- labda pengine mwezi mzima kutoka sasa. Hakuna anyefahamu hali inakuwaje baada ya kupona Ebola kwa sababu virusi vya ugonjwa huo vinateketeza kila kitu mwilini.

Je una familia?

Familia yangu haipo hapa nami, vinginevyo wote wangekuwa wameambukizwa. Wapo nchini Kanada.

Utafanya nini baada ya kupona kabisa?


Nitarejea kazini. Nitawahudumia wagonjwa kama kawaida. Kwa sasa nina kinga dhidi ya aina ya maambukizi (strain) ya Ebola niliyoambukizwa. Hiyo ni moja ya aina hatari kabisa za maambukizi ya Ebola, kwahiyo kama una kinga dhidi yake basi yawezekana kuwa na kinga dhidi ya aina nyinginezo pia.

Nitatumia zana za kujikinga. Hiyo ni lazima kwani kuna hatari ya kuwaambukiza wagonjwa wengine baada ya kuwabeba wagonjwa.  Hospitali yangu imefungwa kwa takriban miezi miwili sasa. Wizara ya Afya imenyunyizia dawa hospitali hiyo, na tuna mpango wa kuifungua tena baada ya miezi miwili.

Unadhani kwanini watumishi wengi wa sekta ya afya wameambukizwa Ebola?


Hatuna zana za kutosha za kujikinga na maambukizi. Hiyo ni changamoto kubwa na tatizo kubwa. Ndio maana hospitali nyingi zimefungwa. Hakuna zana za kutosha kwa kila mtumishi wa sekta ya afya. Wanaweza kukupatia glovu lakini wasikupe magauni rasmi ya kuhudumia wagonjwa wa Ebola. Au wanaweza wasikupe kinga ya uso (mask). Lakini sasa kutokana na misaada ya kimataifa, hali inazidi kuwa bora., na kama hatuna zana za kujikinga na maambukizi hatuwahudumii walioambukizwa. Lakini kwa kutowatibu, wagonjwa wanarudi majumbani na kuambukiza jamii zao. Hilo ni tatizo kubwa.

CHANZO: Imetafsiriwa kutoka jarida la NEWSWEEK





1 Oct 2014


Big up ndugu yangu mpendwa Sintah, a true definition of beauty and brain. Wanasema eduaction is sexy but being more educated is even sexier. 

Napenda kukupongeza sana ndugu yangu kwa kuanza kozi yako ya Postgraduate Diploma in Management of Foreign Relations. Hiyo ni on top ya Shahada yako ya Kwanza (Bachelor of Arts in Public Administration and Management) na Shahada ya Uzamili (Masters of Arts in International Relations and Diplomacy) ulizonazo. 
Ninaamini vipaji kadhaa ulivyonavyo ukichanganya na elimu yako ya kiwango cha juu vinakufanya uwe role model kwa wengi.

Keep it up ndugu yangu, sky is the limit and the world is all yours for grabbing kwani ninaamini muda si mrefu tutakuskia ukituwakilisha katika medani za diplomasia kimataifa. 

Keep it up, Sintah, I am so proud of you!

Nakutakia kila la heri na baraka.

3 Sept 2014

31 Aug 2014


Siku moja nilipokea barua-pepe kutoka kwa msomaji mmoja wa makala zangu katika jarida la Raia Mwema. Licha ya kupongeza kuhusu makala hizo, alinipa ombi ambalo kwa kiasi flani liliniacha na tabasamu. Namnukuu, "... tuna matatizo mengi huku kwetu, kila anayekuja anajali maslahi yake tu. Nakushauri ufikirie kuhusu kugombea katika jimbo letu mwakani." Nilimshukuru msomaji huyo kwa pongezi zake lakini nikamweleza bayana kuwa kamwe sintojiingiza katika uongozi wa kisiasa. Nilimfahamisha kuwa mie ni muumini wa falsafa kuwa yawezekana kuutumikia umma kwa ufanisi pasi haja ya kuwa kiongozi.

Falsafa hiyo inachangiwa na ukweli kwamba nimeshawahi kuwa kiongozi mara mbili, maishani mwangu. Mwaka 1991 nikiwa mwanafunzi wa kidato cha tano katika Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Tabora (Tabora Boys') nilichaguliwa kuwa kiranja mkuu.Lakini kwa vile shule hiyo ilikuwa ya mchepuo wa kijeshi, wadhifa wa kiranja mkuu ulikuwa ukijulikana kama Kamanda Mkuu wa Wanafunzi (Students' Chief Commander), na sare ziliambatana na 'vijimkasi' viwili mabegani.

Japo wadhifa huo ulinipa fursa ya kwanza ya uongozi, tukio moja la mgomo wa wanafunzi lililojiri wakati nipo madarakani sio tu lilinipa mtihani mgumu sana bali pia lilinionyesha sura nyingine chungu ya uongozi. Kwa upande mmoja nilipaswa kuwa kiungo kati ya uongozi wa shule na wanafunzi, lakini wakati huohuo nami ni mwanafunzi na walitarajia niwe upande wao, huku walimu nao wakitaka niwe upande wao. Kwa busara na skills nilizopata kabla ya tukio hilo, mgomo huo ulimalizika salama na sikujenga maadui upande wowote kwa vile nilisimamia kwenye kanuni na taratibu na haki.

Fursa nyingine ya uongozi ilijitokeza mwaka 2000 nilipokuwa mtumishi wa taasisi flani ya serikali huko nyumbani. Niliteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya kiutendaji (operational district/zone), nafasi niliyoshika hadi ninaondoka huko nyumbani miaka miwili baadaye. Ugumu mkubwa wa wadhifa huu ulikuwa kwenye 'kuwa macho masaa 24'...na wakati mwingine kukurupushwa usingizini na kuulizwa 'nifahamishe kilichotokea sehemu flani' ilhali sina habari ya nini kimetokea. Lakini jingine gumu lilikuwa kwenye kuwaongoza watu nilioanza ajira nao pamoja na wengine walionizidi miaka kadhaa ya uzoefu. Kadhalika, wasaidizi wetu mtaani walikuwa na matarajio makubwa ya 'uzalishaji' wao pamoja na maisha yao binafsi. Hata hivyo niliondoka nikiwa na rekodi ya kujivunia.

Kwa kifupi, fursa zote hio zilinifundisha kuwa uongozi ni mzigo mzito na unahitaji kujitolea kwa kiasi kikubwa. Ndio maana kila nikisikia mawazo ya kujihusisha na uongozi, jibu langu jepesi ni HAPANA.Not again. Sio kwamba ninakwepa majukumu lakini kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikijihusisha na uraia kama uongozi, kwa maana ya kutumainia nguvu za raia katika ujenzi wa taifa. Ndio hizo kelele tunazopiga magazetini, hapa bloguni na kwenye mitandao ya kijamii.

Lengo la makala hii sio kuelezea historia yangu au uwezo wa uongozi bali suala lililojitokeza katika mtandao wa kijamii wa Twitter juzi. Nadhani wengi wenu wasomaji mnafahamu kilichomsibu Betty Ndejembi, aliyetutoka juzi. Kabla ya kufariki kwake aliandamwa na unyanyasaji wa kutosha katika mtandao huo. Baada ya kifo hicho, mie niliungana na 'wenye mapenzi mema kwa jamii' kukemea unyanyasaji mtandaoni, kwa kimombo 'cyberbullying.' Hata hivyo, katika kuhamasisha mapambano hayo sikumtaja wala kumtuhumu mtu kuwa ni mnyanyasaji wa wenzie mtandaoni. Nilichohamasisha ndicho hicho nilichoeleza hapo juu: sie watumiaji wa mtandao kama wahanga wa unyanyasaji wa mtandaoni kuunganisha nguvu zetu dhidi ya wanaofanya vitendo hivyo. Na kwa hakika mapokeo yamekuwa mazuri sana. Watu wengi wamewasiliana nami kunifahamisha jinsi walivyokuwa wahanga wa cyberbullying.

Wito wangu kwa jamii umekuwa sio kusubiri serikali au wanasiasa kuchukua hatua ya kukomesha tabia hiyo bali sie kama wananchi na wahanga wa tabia hiyo kuunganisha kuvu na kupambana nayo. Kwa lugha nyingine, sie wenyewe tuchukue uongozi wa mapambano dhidi ya wanyanyasaji wa mtandaoni.

Hata hivyo, jioni ya leo likaibuka kundi la watu waliaonza kunishambulia vikali kuhusiana na kampeni hiyo ya kupambana na unyanyasaji mtandaoni. Kikubwa ni tuhuma kwamba mie wanayeniita 'mwanaharakati wa cyberbullying' ni 'bully' (mnyanyasaji) pia. Na mmoja wao akapata ujasiri wa kupitia tweets zangu za nyuma na kuzi-screenshot ili 'kuthibitisha kuwa mie ni mnafiki nisyestahili kukemea cyberbullying.' Wakati mwingine huwa nashangazwa na 'ujasiri' wa aina hii ambao hata kwa mwenye uelewa mdogo tu wa sheria anaweza kujua athari zake.

Hadi hapo sikuona tatizo sana japo nilishangazwa na 'hasira' za watu hao ilhali sikuwahi kuwatuhumu kuwa wao ni bullies. Na hata asubuhi nilitwiti kuhoji ''kama tunapozungumzia ufisadi, hukasiriki kwa vile wewe si fisadi, kwanini tukizungumzia cyberbullying ukasirike ilhali wewe sio cyberbully?"

Lakini katika mwendelezo wa shutuma zao dhidi yangu, mmoja wao akavuka mstari wa kisheria. Siwezi kuliongelea kiundani suala hili kwa sababu za kisheria.

Awali nilipoamua kuungana na wengine kukemea unyanyasaji mtandaoni sikudhani kwamba itafika mahala pa kuchukua vitendo kulazimisha wanyanyasaji hao waache tabia hiyo. Hata hivyo, kwa kilichotokea leo, nimeamua kuhamia kwenye vitendo.

Tuna tatizo kama Watanzania, ni wepesi wa kulalamikia matatizo yanayotukabili lakini ni wagumu kuchukua hatua za vitendo kuyatatua. Mgao wa umeme, huduma mbovu za baadhi ya makampuni, tatizo la ajali zisizoisha, ufisadi, na kadhalika. Kwa kiasi kikubwa tumekuwa watu wa kulalamika tu kana kwamba malalamiko hayo yataleta mabadiliko.

Katika hili la unyanyasaji mtandaoni, asilimia kubwa ya watu wanaotaka 'kuishi kwa amani mtandaoni' wameunga mkono japo kwa maneno haja ya kukemea unyanyasaji mtandaoni. Lakini kama ilivyojitokeza leo jioni ambapo nimekuwa mhanga wa ushiriki katika harakati hizo, bado kuna wenzetu wanadhani wana hatimiliki ya kuwabughudhi watu mtandaoni watakavyo. Inabidi tuseme enough is enough. Kwa vile haijawahi kutokea huko nyumbani kwa mtu kuingia matatizoni kutokana na alichoandika mtandaoni, watu wengi tu wanaendelea kudhani kuwa akiwa mbele ya keyboard ya kompyuta yake ana uhuru wa kunyanyasa, kudhalilisha, kutukana na kufanya matendo mengine ambayo kimsingi ni makosa kisheria.

Ukweli ni kwamba tukiacha 'njia za asili' za kudhibiti 'wakorofi' kwenye mitandao ya kijamii, yaani aidha kuwa-mute, kuwa-unfollow au kuwa-block, kuna njia za ufanisi zaidi kama vile za kisheria alimradi kuna ushahidi wa kutosha.

Hatimaye nimefikia uamuzi wa kuchukua hatua za vitendo dhidi ya unyanyasaji mtandaoni (cyberbullying). Sifanyi hivi kwa minajili ya kuingia kwenye vitabu vya historia kama Mtanzania wa kwanza kupambana na cyberbullies kwa vitendo bali ninafanya huduma kwa umma. Huhitaji kuwa kiongozi ili kuitumikia jamii. Na sihitaji madaraka ili niweze kupambana na tabia hii isiyofaa. Hakuna miujiza itakayowalazimisha wanyanyasaji wa mtandaoni kuacha tabia hiyo. Kitu pekee ni pale wanapofunzwa madhara ya vitendo vya aina hiyo.

Japo ningependa kuwa sehemu ya kundi linalopambana na suala hili, hadi sasa hakuna dalili zozote za uwepo wa mkusanyiko wa kukabiliana na tatizo hili ambalo kwa hakika linawasumbua wengi. Lakini tukisema tusubiri mpaka watu wajipange na kuunda kikundi, wenzetu wengi zaidi watazidi kuwa wahanga wa unyanyasaji huo wa mtandaoni.

Natambua ugumu wa mapambano haya lakini kila mapambano ni magumu. Natambua kutakuwa na lawama na kukatishana tamaa lakini liwalo na liwe lazima mtu flani awe mfano kwa wenzie kwamba cyberbullying is not just wrong but also a criminal offence. 

Lengo la makala hii sio kumtisha wala kumzuwia mtu kunituhumu kuwa nami ni cyberbully. Ninaheshimu uhuru wa kujieleza alimradi hauvuki mpaka.Na kitu ambacho kamwe siwezi kukivumilia  ni uvunjifu wa sheria dhidi yangu.

Ni matumaini yangu kuwa kama inavyofundisha Biblia Takatifu kuwa 'ukipiga mchungaji kondoo watasambaa,' kumwajibisha mmoja wa wanaodhani mitandao ya kijamii ni fursa ya kuwanyima wenzao amani kutapeleka ujumbe kwa wengine wanaoamini hivyo pia. Mafundisho ya Kiislam yanatueleza kwamba "ukiona jambo baya basi aidha lichukie, au likemee au liondoe." Nimeshachukia unyanyasaji mtandaoni vya kutosha, nimeukemea vya kutosha, na sasa ni wakati wa kuuondosha kwa vitendo. Haitokuwa rahisi lakini nina hakika nitafanikiwa. Inshallah!

Na mwisho, lengo la harakati ninazoanza si kumkomoa mtu au watu flani. Hao waliotumia muda wao kunishambulia ni dalili tu za tatizo, ninacholenga kupambana nacho ni chanzo cha tatizo. Mtu anaposkia baridi kwa vile ana homa, huwezi kumtibu kwa kumpa maji ya moto bali tiba ya homa. Kadhalika, unyanyasaji mtandaoni hauwezi kukomeshwa kwa kubana watu flani tu bali kulikabili tatizo lenyewe. Ifike mahala mtu ajiulize mara mbili kabla ya kuposti 'maneno yasiyofaa' dhidi ya mtu mwingine mtandaoni.

Ili mabadiliko ya kweli yatokee hasa ya kuondoa jambo baya ni lazima kujitoa mhanga. Iwapo uamuzi wangu wa kupambana na tabia hii utapelekea madhara kwangu basi na iwe. Ninaamini kuwa mwenye haki ataanguka saba mara sabini lakini hatimaye atasimama. Nikisema 'mwenye haki' simaanishi kuwa harakati hizi ni za kutafuta haki yangu bali ya wanyonge mbalimbali wahanga wa unyanyasaji mtandaoni. Tukiwakalia kimya bullies sio tu watadhani tunaridhia vitendo vyao bali pia wataendelea kutengeneza victims.

INAWEZEKANA, NA NITATIMIZA WAJIBU WANGU



29 Aug 2014


Ninaandika makala hii nikitambua bayana kuwa itamuudhi kila mtu anayeingia mtandaoni kwa minajili ya kuwanyanyasa watu wengine. Lakini siku zote ninaamini katika busara hii: kuuchukia ukweli hakuufanyi kuwa uongo. Ukweli ni ukweli na uongo ni uongo. Ukweli hauwezi kuwa uongo, na kadhalika uongo hauwezi kuwa ukweli. Kamwe asilani.

Wakati tunaomboleza kifo cha ndugu yetu Betty Ndejembi hatuwezi kukwepa ukweli kwamba siku chache kabla ya kifo chake binti huyo alinynyaswa mno kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter. Japo hadi muda huu hatuwezi kuhusisha moja kwa moja uhusiano kati ya unyanyasaji huo na kifo cha binti huyo, ukweli tu kwamba mtu akinyanyaswa masaa kadhaa kabla ya kifo chake, waweza kujenga picha flani.

Naomba ieleweke kuwa simlaumu mtu kwa sababu sina mamlaka ya kufanya hivyo bali dhima ya makala hii ni rambirambi zangu na kuzungumzia tatizo la unyanyasaji mtandaoni, sambamba na suala zima la unafiki kila kinapojiri kifo hususan cha mtu maarufu.

Tuna tatizo kubwa huko mitandaoni. Tumefika hatua ya kuwapa umaarufu watu wenye matusi ya nguoni, wazushi, wambeya, wanafiki, wanaharamu na kila aina ya binaadamu wanaostahili laana lakini twaishia kuwatukuza. Kwa Twitter, matusi imekuwa ni njia ya mkato ya kupata umaarufu. Kuna wenzetu wengi tu wenye 'umaarufu' huko Twitter, na ukidadisi chanzo cha 'umaarufu' huo, utaambiwa 'ah huyu ana matusi si mchezo!'

Kuna watu wazima na akili zao wanatumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii aidha kunyanyasa wenzao kama si kusherehesha unyanyasaji huo. Marehemu aliitwa majina kadhaa ya kumdhihaki kabla ya kukutana na mauti. Japo sijui chanzo cha 'ugomvi na aliogombana nao' (na ndio maana sikujihusisha nao kwani haukunihusu), kuna wanafiki wengi tu waliokuwa katika nafasi nzuri ya kuzima moto huo hasa kwa vile baadhi yao walikuwa wakizifahamu pande zote mbili za 'ugomvi' husika.


La kukera zaidi ambalo ni wazi litajichomoza wakati wa maombolezo haya ni unafiki: baadhi ya watu walewale waliodiriki kumwandama marehemu wakati wa uhai wake watageuka kuwa wenye uchungu mkubwa baada ya kifo chake. Hii inanikumbusha suala ambalo nimeshawahi kulizungumzia mara kadhaa, katika hali ya utani japo wenye uweli, kwamba 'wakati mwafaka kabisa wa kutafuta vipaji vya uigizaji ni kwenye misiba: watu walewale waliokuwa wakikuchukia kwa nguvu zote watageuka wenye uchungu mkubwa kwa kifo chako.

Ukiangalia baadhi ya tweets za mwisho za marehemu ni wazi kuwa binti huyo alikuwa anahitaji msaada kutoka kwa wanaomjali




Hata pasi uelewa wa taaluma ya saikolojia, tweets za aina hii zinaashiria tatizo, na laiti 'wenye upendo wa dhati' wangeingilia kati muda huo, huenda muda huu Betty asingekuwa marehemu. 


Na hizo tweets mbili ambazo ni miongoni mwa za mwisho kabisa za marehemu ni ushuhuda tosha wa jinsi alivyokuwa akisumbuliwa na wanyanyasaji dhidi yake mtandaoni. Ndio pengine kilichomuua ni maradhi ya kawaida ya kibinadamu lakini kila mwenye ubinadamu hatoshindwa kuhusisha unyanyasaji huu na hali mbaya ya afya aliyokuwa nayo hadi anafariki.

Kuna watakaolaumu kuwa ninatumia kifo cha binti huyo kwa 'maslahi binafsi.' Hapana, sina maslahi yoyote binafsi hasa ikizingatiwa kuwa sikuwa nikifahamiana na marehemu. Hakuna anani-follow na mie sikuwa nam-follow. Labda maslahi pekee niliyonayo ni upinzani wangu mkali dhidi ya unyanyasaji wa mtandaoni. Vyovyote ilivyo, marehemu alikuwa bullied kabla hajafariki na atakayetaka kukataa ukweli huo na akatae lakini utabaki kuwa ukweli usioweza kugeuka uongo. Na kwa hakika, kila aliyeshiriki kumnyanyasa binti huyo atakuwa anasutwa na nafsi yake, hata kama atatafuta hifadhi kwenye 'huu sio wakati wa kulaumiana' au 'we failed you Betty.' 

Mara nyingi nimekuwa nikiwalaumu watu wanaodai 'Instagram imekuwa mbaya' au Twitter imeharibika siku hizi' ambapo mara zote nimewakumbusha wahusika kuwa katika hii mitandao ya kijamii, ni muhimu kuwa makini katika nani wa kum-follow. Maana yangu ni kwamba ukim-follow mtu mwenye matusi, utashuhudia matusi katika anachoandika. Ukim-follow mtu wa busara, utashuhudia busara.

Hata hivyo, katika siku za hivi karibuni kumeibuka kundi kubwa tu la watu wenye busara na elimu zao lakini wepesi wa kuvutiwa na vitu vya 'kipuuzi' - umbeya, matusi, majungu, na upuuzi mwingine, na hawasiti kushea na wanaowa-follow. Ni hivi, mtu akitweet tusi, kisha ukali-retweet, utambue kuwa unalikuza (amplify) tusi hilo. Na kimsingi, kwa kiasi kikubwa, tuna-RT vitu tunavyoviunga mkono. Uki-RT tusi maana yake unaliunga mkono. Na ni wazi mwenye kujiheshimu, na kuheshimu 'watu wa maana' wanaom-follow hawezi ku-RT upuuzi.

Tatizo kubwa sasa ni kwamba waweza kuamua kuwa-follow watu unaodhani wana busara au akili za kutosha lakini ukaishia kusoma vitu vya ajabu ajabu kwenye timeline yako kutokana na haya 'mahaba' ya ku-RT vitu vya kipuuzi. 

Binafsi, nadhani chanzo kikubwa cha mitandao ya kijamii kuwa 'sehemu za kukera, kuogopesha, kunyanyasana, nk' ni ile hali ya baadhi ya wenzetu kutokuwa na vitu muhimu vya kufanya katika maisha yao. Ni wazi kwamba ukiwa busy na maisha yako hutokuwa na muda wa kubughudhi wenzako. 

Kingine kinachopelekea social media kuwa 'dunia uwanja wa fujo' ni ugonjwa mkubwa unawasumbua baadhi ya wenzetu: kusaka sifa wasizostahili. Wanasema,. ashakum si matusi, 'lugha ya mpumbavu ni matusi,' na ndo maana baadhi ya wenzetu wasio na cha maana cha kuongea katika hadhara hukimbili matusi, unyanyasaji, maneno macha

Nitamke bayana kuwa siandiki makala hii nikitegemea kuungwa mkono na wahusika wa unyanyasaji mtandaoni. Na kwa hakika kuna uwezekano mkubwa wa makala hii kuzua 'kampeni ya chuki' dhidi yangu kutokana na makala hii. Tatizo kubwa la wenzetu hawa ni kutotaka kuambiwa kuwa 'Hapana, hili ni kosa. Na kosa ni kosa, haliwezi kuwa sahihi.' Lakini pamoja na uwezekano wa 'kuwashiwa moto' kutokana na makala hii, wito wangu kwa kila mwenye busara na akili ni kuliangalia tukio hili la kusikitisha kama 'wake up call.' Tujifunze, tujisahihishe. Tuache kusherehesha vitu vya kipuuzi mtandaoni.

Ifike mahala, ukishindwa kumkemea mtu mwenye tabia mbaya mtandaoni basi chukua option  rahisi ya kum-unfollow au ikibidi kum-block. Na ifike mahala kuwafahamisha watu wanaoendekeza utoto, majungu, umbeya, unyanyasaji na upuuzi mwingine kuwa kama hawana kitu cha maana cha kufanya katika maisha yao basi isiwe sababu ya kuwasumbua wenzao wenye majukumu katika maisha yao.

Tukemee maovu badala ya kutarajia yataondoka yenyewe tu. Tuomboleze kifo cha Betty kwa kusema 'NO' kwa cyberbullies (wanyanyasaji wa mtandaoni). Tufike sehemu tuache kuwasujudia wahuni wanaodhani matusi ni sehemu ya wimbo wa taifa. Tuwakwepe waendekeza majungu, wanyanyasaji, wataka sifa za kipuuzi, na watu wasiofaa katik maisha yetu.


Wakati 'tunatafuta haki kwa marehemu Betty kutokana na unyama aliofanyiwa,' suala ambalo ni la kisheria, kilicho ndani ya uwezo wetu ni kukemea unyanyasaji mtandaoni (cyber bullying). Wakati hadi muda huu hatuwajui waliomfanyia marehemu unyama huo, takriban sote twawajua vema wanyanyasaji wa mtandaoni. Tuanze na hawa, kwani leo wamefanya kwa kwa marehemu Betty kesho itakuwa kwako.

Mwisho kabisa, ni muhimu kwetu sote kutambua kuwa tulitoka kwa udongo na tutarudi kwa udongo. Kifo ni hatma ya kila mmoja wetu.Betty ametutoka lakini nasi twaelekea huko. Visa, chuki, kunyanyasana, na vitu vingine visivyopendeza japo ni kama sehemu ya maisha yetu havipaswi kupewa nafasi katika maisha yetu haya ambayo hakuna mmoja wetu mwenye japo 'lue' ya lini yatafikia kikomo. TUPENDANE na TUHESHIMIANE.

Kwako marehemu Betty, hakuna tunaloweza kusema au kufanya sasa kurejesha uhai wako. Na hakuna neno sahihi la kuonyesha jinsi gani kifo chako kimewagusa wengi. Kubwa tunaloweza kufanya ni kukuombea kwa Mwenyezi Mungu akupatie pumziko la milele na mwanga wa milele akuangazie upumzike kwa amani. Amina.




24 Aug 2014

Kaleem, a keen cricketer, said the teachers at his school have told him other children are 'scared' of his hands

Doctors in India have been left baffled by his growing hands and many are at a loss as to what the condition is

The youngster has difficulty eating, tying his shoelaces and carrying out other basic tasks due to his  hands

Kaleem's father Shamim, 45, (pictured together above) is worried his son will never become independent

Kaleem, from India, was born with hands twice the size of an average baby and they have continued to grow

Mtoto wa miaka minne nchini India, Kaleem (pichani) amewachanganya madaktari kufuatia mikono yake kuvimba kupita kiasi na sasa imefikia uzito wa kilo 12. Mtoto huyo kwa sasa anashindwa kutekeleza japo majukumu madogo tu kama kufunga 'kamba' (laces) za viatu vyake baada ya kuzaliwa akiwa na mikono mikubwa mno.

Kaleem anadai amekuwa akibughudhiwa mno na watoto wenzie wanaomcheka kutokana na maumbile hayo ya ajabu. "Napata mguu kuvaa nguo zangu, kufunga vifungo hata kuvaa nguo ya ndani, anasema mtoto huyo ambaye mama yake alibaini maradhi yake tangu akiwa mdogo lakini hakuwa na cha kufanya kutokana na kutokuwa na uwezo wa kifedha. Wazazi wa Kaleem wana kipato kisichozidi Paundi za Kiingereza 15 (takriban Tsh 42,000) kwa mwezi.

Baba yake, Shamim, anahofu mwanae hatoweza kujitegemea maishani, na anajilaumu kwa kushindwa kumhudumia kutokana na uwezo duni wa kifedha. Dr Ratani, mkurugenzi wa kituo cha afya kilichomfanyia uchunguzi mtoto huyo anakiri kuwa maradhi hayo ni ya ajabu na magumu kutibika. 

CHANZO: The Mail Online



 Only men who suffered impotence as a side effect of illness or those evaluated by a specialist could be given the pills on the NHS
Mamia kwa maelfu ya wanaume hapa Uingereza wanatarajiwa kunufaika na uamuzi wa Taasisi ya Huduma za Afya (NHS) kulegeza masharti ya upatikanaji wa vidonge vya kuboresha nguvu za kiume, Viagra.

Hadi mwezi huu, watu pekee walioruhusiwa kupewa Viagra hospitalini ni wale ambao pungufu wa nguvu zao za kiume ulitokana na athari za matibabu ya maradhi mengine (side effects).

Lakini tangu taratibu za usajili na upatikanaji (patent) ya Viagra ilipoisha muda wake mwaka jana, bei ya vidonge hivyo imeshuka kwa asilimia 93 kwa vile makampuni mengine ya madawa yameruhusiwa kutengeneza aina zisizo asili (generic) za vidonge hivyo.

Kutokana na hali hiyo, NHS imeeleza kuwa watu wote wenye matatizo ya nguvu za kiume wanaruhusiwa kupata Viagra. Madaktari wengi wamefurahishwa na uamuzi huo wakiamini kuwa utasaidia kuboresha mahusiano ya kinyumba na hata kuokoa ndoa.

Hadi 'patent' ya Viagra inakwisha muda wake, Viagra ilikuwa ikiuzwa kwa Paundi za Kiingereza 21.27 (Tsh 58,567.39) kwa pakti ya vidonge vinne lakini bei hiyo sasa imeshuka hadi Paundi .1.45 (Tsh 3,992.61)kwa pakti moja ya vidonge vinne.



22 Aug 2014

Ijumaa ya leo imekuwa siku ngumu sana kwangu. Rafiki yangu mmoja wa karibu, mhamiaji kutoka Ireland ya Kaskazini aliyehamia hapa Uskochi, anajiandaa kwa ajili ya upasuaji wa moyo hapo Jumatatu. Leo tumeonana 'kwa mara ya mwisho' kwa vile atatumia wikiendi hii kujaindaa na upasuaji huo, na wiki Ijayo ndo shughuli yenyewe.

Nimepata wakati mgumu sana kuagana nae jioni hii wakati anaelekea nyumbani kwake nami narudi kwangu. Japo aliniaga kwa kujiamini kuwa tutaonana Jummatano ijayo, lakini hali ya uoga iligubika ujasiri wake, na kwa hakika almanusra niangushe chozi. 

Huyu bwana alipatwa na mshtuko wa moyo miezi kadhaa iliyopita. Naikumbuka vema siku hiyo. Tulipokutana asubuhi baada ya kuwasili kazini alionekana anatoka jasho japo siku hiyo ilikuwa ya baridi kali. Muda mfupi baadae alionekana anapumua kama mtu aliyekimbia umbali mrefu, na muda mfupi baadaye akaanguka na kupoteza fahamu. Tuliita gari ya kuhumia wagonjwa, na akakimbizwa hospitalini haraka. Kwa mujibu wa maelezo yake mwenyewe, alikuwa kama amekufa kwa masaa kadhaa. Lakini kubwa lililosaidia kuokoa uhai wake ni huduma ya kwanza tuliyompatia wakati tunasubiri gari la wagonjwa, vinginevyo moyo wake ungezimika moja kwa moja.

Alikaa hospitalini kwa wiki kadhaa na huko walimwekea mashine inayousaidia moyo wake kufanya kazi zake kwa ufanisi. 

Sasa upasuaji atakaofanyiwa Jumatatu ijayo ni kwa ajili ya uchunguzi mkubwa wa jinsi mashine hiyo inavyofanya kazi.Ikumbukwe kuwa mashine hiyo inafanya kazi kuusaidia moyo, na kwahiyo moyo wake bado unafanya kazi japo ni kwa msaada wa mashine hiyo iliyowekwa juu kidogo ya moyo wake, kifuani.

Kitakachofanyika Jumatatu ni kilekile walichomfanyia wakati wanaweka mashine hiyo, yaani watatumia kompyuta kufanya kazi ya moyo, na kisha kuusimamisha moyo, na kwa wakati huo uhai wake utakuwa unategemea kompyuta hiyo. Wataitoa mashine waliomwekea mwilini na kuisafisha, sambamba na kuichunguza. Kadhalika, moyo wake nao utafanyiwa uchunguzi wa kina. Yote hayo yatatokea wakati uhai wake unategemea kompyuta inayofanya kazi ya moyo.

Japo upasuaji huo haumaanishi kifo lakini kuna uwezekano-japo si mkubwa- wa moyo kurejeshwa mwilini na ukagoma kufanya kazi kama awali. Kadhalika, ile mashine inayousaidia moyo nayo inaweza kugoma 'kuwajibika ipasavyo.' Lakini cha kutisha ni ukweli kwamba wakati upasuaji huo unafanyika, rafiki yangu huyo atakuwa kama amekufa- kwa maana ya kazi zinazofanywa na moyo wa asili kutegemea msaada wa kitu cha nje- in this case ni hiyo kompyuta. Yaani kwa lugha nyingine ni kama mtu anayepumulia mashine, ikizimwa, yaweza kuwa ndio mwisho wa uhai wake.

Wakati tunaondoka eneo la kazi, rafiki yangu huyo alisema waziwazi kuwa muda huo ndo unaweza kuwa wa mwisho kwa yeye kuwepo hapo. Japo aliongea kwa utani lakini uwezekano huo upo japo si mkubwa. Teknolojia ya matibabu ya moyo imepiga hatua kubwa sana lakini si ya uhakika wa asilimia 100.

Kwangu, nabaki kumfanyia sala, upasuaji huo ufanyie salama, na tukutane tena Jumatano kama alivyoahidi mwenyewe. Nina imani na teknolojia ya matibabu ya hawa wenzetu lakini ukweli kwamba kiungo muhimu kama moyo kitasimamishwa na kazi yake kufanywa na kompyuta inanipa msisimko wa uoga. Na hilo limeonekana hata kwa 'mgonjwa' mweyewe.'

I thought si vibaya ku-share stori hii ya kuogofya ambayo inanigusa kwa kiasi kikubwa. Kwa nman flani yanikumbusha jinsi nilivyompoteza mama yangu mpendwa, ambaye nae kama ilivyo huyo rafiki yangu alipatwa na mshtuko wa moyo, akapoteza fahamu, na fahamu hazikumrejea tena hadi anafariki Mei 29, 2008.

Natumaini msomaji mpendwa utaungana nami kumwombea rafiki yangu huyo upasuaji atakaofanyiwa uwe wa mafanikio na aendelee kuishi salama. Nitawafahamisha kilichojiri Jumatano ijayo.

Asanteni

15 Aug 2014

Within 30 years, a futurist believes babies will regularly born in artificial wombs, outside of human bodies. Stock image pictured
Wanasayansi wanataraji kwamba ndani ya miaka 30 ijayo, itawezekana kutengeneza na kutunza ujauzito nje ya tumbo la mama. Teknolojia hiyo inayofahamika kama ectogenesis imekuwa ikifanyiwa kazi katika maabara tangu mwaka 200, na majaribio ya awali yalikuwa ya kutengeneza na kutunza mimba ya panya nje ya tumbo la panya ' wa kike.'

Wakati wanaounga mkono teknolojia hiyo wanadai itapunguza vifo vya watoto wakiwa tumboni kwani itarahisisha kufanya uangalizi na ufuatiliaji, wapinzani wake wanadai kuwa itaingilia utaratibu wa asili wa uzazi. Wengine wanadai kuwa hatua hiyo itaondoa hatua muhimu ya mahusiano kati ya mama na mtoto tangu akiwa tumboni.

Ectogenesis ni makuzi ya kiumbe kichanga (organism) nje ya mwili, na inatokea kwa baadhi ya wanyama na bakteria. Katika kutengeneza na kutunza mtoto nje ya tumbo la mimba, mfuko 'feki' wa uzazi wahitaji 'mrija feki wa uzazi ' (fake uterus) ili kukipatia kiumbe lishe na hewa ya oksijeni. Pia mipira maalum itahitajika ili kuwezesha kiumbe kichanga 'kujisaidia' (kutoa uchafu mwilini). Chupa inayohifadhi 'mimb' itaunganishwa na mitambo itakayofuatilia makuzi ya 'kichanga' na mimba kwa ujumla.

Kwa taarifa kamili BONYEZA HAPA

CHANZO: Daily Mail



 Kunywa maji ya kutosha 

  1. Increase Your Ejaculate Step 1 Version 2.jpg


  1. Epuka joto kwa sehemu zako za siri
    Increase Your Ejaculate Step 2 Version 2.jpg

  2. ee
  3. Epuka 'nguo za ndani' za kubana
    Increase Your Ejaculate Step 3 Version 2.jpg


  4. Epuka 'kupinda nne'
    Increase Your Ejaculate Step 4 Version 2.jpg

    .


  5. Punguza tendo la ndoa kwa muda ile kurejesha mbegu za kiume 'zilizopotea'
    Increase Your Ejaculate Step 5 Version 2.jpg
    Add caption
  1. Tumia vitamini vya Zinc na Folic Acid
    Increase Your Ejaculate Step 6.jpg


  2. Punguza kunywa soda
    Increase Your Ejaculate Step 7.jpg


  3.  Meza vitamini vya Amino Acid vya aina hizi: L-Arginine, L-Lysine na L-Carnitin Increase Your Ejaculate Step 8.jpg

  4. Jaribu 'vidonge vya asili' viitavyo Horny Goat Weed
    Increase Your Ejaculate Step 9.jpg


  5. Kula matunda na mbogamboga (hasa maharage mekundu, maji ya nazi, apples, wild blueberries, blackberry, cranberry)
    Increase Your Ejaculate Step 10.jpg


    Chua misuli ya 'sehemu yako ya siri' pasipo kufikia 'kileleni'

    1. Increase Your Ejaculate Step 11.jpg

    2. Punguza na hatimaye acha kuvuta sigara (na bangi ni adui mkubwa wa mbegu za kiume)
      Increase Your Ejaculate Step 12.jpg

      • Punguza msongo wa mawazo (stress)
        Increase Your Ejaculate Step 13.jpg

        • Fanya mazoezi mara kwa mara
          Increase Your Ejaculate Step 14.jpg

        • Zingatia ngono salama (maradhi ya zinaa yanaathiri vibaya uzalishaji mbegu za kiume)
          Increase Your Ejaculate Step 15.jpg

          CHANZO: WikiHow

        Categories

        Blog Archive

        © Evarist Chahali 2006-2022

        Search Engine Optimization SEO

        Powered by Blogger.