Showing posts with label MKUCHIKA. Show all posts
Showing posts with label MKUCHIKA. Show all posts

11 May 2009


HIVI KARIBUNI,WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI NA UTUMISHI WA UMMA),USTAADHA HAWA GHASIA,ALITOA ONYO KALI DHIDI YA WATU WANAOJIHUSISHA NA KILE ALICHOKIITA "WIZI WA NYARAKA ZA SERIKALI".NISINGEPENDA KUREJEA REACTIONS MBALIMBALI ZILIZOTOKANA NA KAULI HIYO LAKINI MMOJA YA SAUTI ZILIZOPINGA VIKALI TAMK HILO LA GHASIA NI MBUNGE WA KARATU NA KATIBU MKUU WA CHADEMA,DR WILBROAD SLAA.MWANASIASA HUYO NGULI WA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI ALIELEZA WAZIWAZI KWAMBA NYARAKA ZINAZOFICHA UFISADI HAZIPASWI KUWEKWA KWENYE KUNDI LA NYARAKA ZA SIRI ZA SERIKALI.DR SLAA ALIELEZA BAYANA KWAMBA PINDI AKILETEWA NYARAKA ZA AINA HIYO ATAZIMIA PASI UOGA KWA VILE NI KWA NJIA HIYO NDIO TUMEFANIKIWA KUBAINI SKANDALI KAMA ZA EPA,RICHMOND NA NYINGINEZO.


NI DHAHIRI TAMKO LA WAZIRI GHASIA LILENGA KUWATISHA WATU KAMA DR SLAA.LAKINI PIA WAZIRI HUYO ALIFANYA HIVYO KWA VILE NI MIONGONI MWA VIONGOZI WA SERIKALI WENYE DHAMANA NA MASUALA YANAYOHUSU IDARA MBALIMBALI ZA SERIKALI.


BILA KUUMAUMA MANENO,HEBU TUJIULIZE: HIVI ROSTAM AZIZ ALIPOITISHA PRESS CONFERENCE YAKE NA KUTOA "USHAHIDI" MBALIMBALI KUPIGILIA MSUMARI HOJA YAKE KUWA REGINALD MENGI (MWENYEKITI MTENDAJI WA MAKAMPUNI YA IPP) NI FISADI NYANGUMI,ALIZIPATAJE NYARAKA MBALIMBALI ZINAZOPASWA KUWA KATIKA HIFADHI YA TAASISI HUSIKA ZA SERIKALI?

ROSTAM SI MTUMISHI WA MAMLAKA YA MAPATO AU MWAJIRIWA KATIKA WIZARA YA FEDHA KIASI CHA KUWA NA "DATA" ALIZOTOA KUHUSU MENGI.NA KWA VILE MAMLAKA HUSIKA ZIMEKUWA KIMYA KUHUSU WAPI MBUNGE HUYO WA IGUNGA ALIPATA NYARAKA HIZO NI WAZI KWAMBA ALIPATIWA KWA RIDHAA YA WAHUSIKA.

WATETEZI WA ROSTAM,KUANZIA WAZIRI SOPHIA SIMBA NA KAPTENI GEORGE MKUCHIKA WAMEKUWA KIMYA KABISA KUKEMEA "HUKUMU" ALIYOTOA ROSTAM DHIDI YA MENGI TOFAUTI NA WALIVYOKURUPUKA MARA BAADA YA KIPENZI CHAO KUTAJWA KUWA NA MENGI KUWA NI FISADI PAPA.BY THE WAY,MENGI SI MTU WA KWANZA KUMTUHUMU ROSTAM KUWA NI FISADI.HIYO NI OPEN SECRET,NA KINACHOKWAZA WATU HAWA KUCHUKULIWA HATUA NI NJAA TU ZA HAO WENYE WAJIBU WA KUFANYA HIVYO ZINAZOKIDHIWA NA JEURI YA FEDHA ZA MAFISADI HAO.

SASA,SIJUI WAZIRI GHASIA ANAWEZA KUTUELEZA NINI KUHUSU WIZI WA NYARAKA ZA SERIKALI ULIOFANYWA NA ROSTAM.NAUITA WIZI KWA VILE ROSTAM SIO TRA,DPP,MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI AU TAASISI YOYOTE YA SERIKALI YENYE DHAMANA YA KUWA NA NYARAKA ZILIZOTUMIWA NA MFANYABIASHARA HUYO KWENYE "KUJENGA KESI" YAKE DHIDI YA MENGI.

SASA NAELEWA KWANINI ROSTAM ANAWEZA KU-WISH ASINGEJIBU HOJA ZA MENGI KWANI WATAPOFIKA MAHAKAMANI ANAPASWA KUULIZWA YEYE ALIKUWA NA NYARAKA HIZO KAMA NANI?ALIZIPATAJE?NA JE KUWA NAZO SIO KOSA (KWA KUREJEA "MKWARA" WA WAZIRI GHASIA?

NA HIYO NI NJE YA TAARIFA ZA KUAMINIKA KUWA NYINGI YA DATA ALIZOTUMIA ROSTAM NI "MAKANJANJA" (FAKE DATA) AMBAPO WAJANJA WA MJINI WALIPOSIKIA KUNA TENDA YA FEDHA NYINGI YA KUWEZESHA KUPATIKANA KWA INCRIMINATING EVIDENCE DHIDI YA MENGI WAKACHANGAMKIA TENDA HIYO LAKINI KATIKA HALI YA UFISADI.WHY NOT,KUMFISADI FISADI NI SAWA KABISA NA KULIPA KWA NOTI BANDIA MANUNUZI YA CHENI ILIYOTENGENEZWA KWA DHAHABU FEKI.


MWISHO,NAPENDA KUSISITIZA KWAMBA SINA CHUKI NA ROSTAM AU MTANZANIA YEYOTE MWENYE ASILI YA NJE YA NCHI.ILA SIFICHI UKWELI KWAMBA NINA ZAIDI YA CHUKI,HASIRA,DUA BAYA (NA MENGINE NISIYOWEZA KUTAJA HAPA) DHIDI MAFISADI.UTETEZI WA KIPUUZI WA MAFISADI UMEKUWA KWENYE VITU KAMA RANGI,DINI,KABILA,NK.MTAKUMBUKA MKURUGENZI WA IPC,EMMANUEL OLE NAIKO ALIZONGWA KUHUSU KWANINI ALITOA KIBALI CHA UWEKEZAJI KWA KAMPUNI YA KITAPELI YA RCHMOND,KIMBILIO LAKE KUU LILIKUWA UKABILA.ETI "NAANDAMWA KWA VILE NATOKA ENEO MOJA NA LOWASSA"!

LEO HII AKINA ROSTAM,MANJI,SOMAIYA,JEETU NA SUBASH WANATAKA KUTUAMINISHA KUWA TUHUMA DHIDI YAO ZINACHANGIWA NA "UTANZANIA" WAO WENYE ASILI YA NJE YA NCHI.HUU NI UTETEZI MUFILIS NA NI WA KIFISADI KAMA WANAVYOTUHUMIWA.HIVI WANATAKA KUTUAMBIA KUWA TULIPOPAMBANA NA MKOLONI,MJERUMANI NA MWINGEREZA TULIKUWA WABAGUZI WA RANGI?

4 May 2009


MWANASIASA MAKINI ANAPASWA KUCHUNGA ULIMI WAKE.ANAPASWA PIA KUELEWA KWAMBA LOLOTE LITOKALO MDOMONI MWAKE LAWEZA KUTAFSIRIWA KUWA NI KAULI YA SERIKALI.

KWA MAANA HIYO,KAULI ZA SOPHIA SIMBA NA GEORGE MKUCHIKA KUMTETEA ROSTAM AZIZ WAZIWAZI ZIMEWAFANYA WANANCHI WENGI KUWAONA MAWAZIRI HAO KAMA VIBARAKA WA ROSTAM,MFANYABIASHARA NA MWANASIASA ANAYEHUSISHWA NA TUHUMA LUKUKI ZA UFISADI.

SOPHIA SIMBA NA MWENZIE MKUCHIKA WALILIPUKA KUMTETEA ROSTAM PASIPO KUELEWA KWAMBA MHINDI HUYO NAE ALIKUWA ANA MPANGO WA KUJIBU SHUTUMA ZA MENGI.NA KATIKA KUJIBU SHUTUMA HIZO,ROSTAM AMEJIGAMBA KUWA MENGI AMEKEMEWA NA WAZIRI SIMBA NA MKUCHIKA.

HIVI WATU WAZIMA HAWA NA AKILI ZAO HAWAONI KUWA WAMEDHALILISHWA?YAANI INA-SOUND AS IF WALITUMWA NA ROSTAM IN THE FIRST PLACE KABLA YA MTUHUMIWA HUYO WA UFISADI KUITISHA PRESS CONFERENCE.MAWAZIRI WAZIMA WANA-ACT AS IF NI SPOKESPERSONS WA,SIO SERIKALI,BALI MHINDI FLANI MWENYE FEDHA?

BAADA YA PRESS CONFERENCE YA ROSTAM HAPO JANA,BAADHI YA WATU WANAULIZA "YUKO WAPI SOPHIA SIMBA?YUKO WAPI MKUCHIKA?" WAKITARAJIA MAWAZIRI HAO WATAMTENDEA HAKI MENGI KWA KUMKEMEA ROSTAM.HAWANA JEURI WALA UBAVU HUO.SIMPLY BECAUSE KAMA KUITWA FISADI PAPA KWA MHINDI HUYU KULIWAKURUPUA KUROPOKA WALIYOSEMA,NI DHAHIRI KUWA ROSTAM AKIKOHOA TU NA WAO WANALIPUKA.UJASIRI HUO WA KUMKEMEA WATOE WAPI.NA KATIKA SIASA HIZI ZA KIMAFIA ZILIZOLETWA NA WANAMTANDAO,MWANASIASA YEYOTE ATAKAYETHUBUTU KUMGUSA THE DON,MR UNTOUCHABLE,BASI NAYE ATACHAFULIWA.

YOTE HIYO NI TAMAA YA MADARAKA.WAKO RADHI KUUZA UTU WAO KWA AJILI YA KUMPIGIA MAGOTI FISADI FLANI AWASDAIDIE KUFIKIA MALENGO YAO.NA SI SOPHIA SIMBA NA MKUCHIKA PEKEE,KUNA WENGI TU WANAOWAOGOPA MAFISADI KWA VILE NDIO WALIOFADHILI HARAKATI ZAO ZA KISIASA.

HALAFU HAWA NDIO WA KUWATEGEMEA KUTULETEA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA?LABDA MAISHA BORA KWA MAFISADI NA VIBARAKA WAO!

SHAME ON THEM!


27 Apr 2009


KUNA MAMBO YANAYOTOKEA HUKO NYUMBANI YANAKERA KUPITA MFANO.HIVI HAWA WATANZANIA WENZETU WALIOKABIDHIWA DHAMANA YA KUTUONGOZA (TUKIAMINI KABISA KUWA WANA UPEO MZURI TU WA KUTAFAKARI MAMBO) WANAWEZAJE KUONGEA MAMBO YA AJABU NAMNA HII?ANYWAY,HEBU SOMA KWANZA HABARI HUSIKA KISHA TUENDELEE KUJADILI



* Waziri Sophia Simba asema Mengi kachemsha
*Mkuchika naye asema wanamchunguza

Ramadhan Semtawa na Leon Bahati

MAWAZIRI wawili, Sophia Simba na George Mkuchika jana walimshambulia mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi ambaye wiki iliyopita alitangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia, akisema ni mafisadi waliokubuhu.

Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na Mkuchika, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo walisema mfanyabiashara huyo wa jijini Dar es salaam "amechemsha".

Mengi alitangaza majina ya wafanyabiashara hao Alhamisi iliyopita akisema ni kati ya watu wasiozidi 10 ambao alidai wanaifilisi nchi na kutaka wadhibitiwe mapema kabla hawajaitingisha na kuiyumbisha nchi. Hata hivyo, Mengi, ambaye alidai katika taarifa yake kuwa juhudi za Rais Jakaya Kikwete zinakwamishwa na watu hao, hakueleza jinsi watano hao wanavyoitafuna nchi zaidi ya kusema kuwa wanatorosha fedha wanazozipata 'kifisadi'.

Jana, kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam mawaziri hao wawili walitoa kauli za kumshambulia mwenyekiti huyo mtendaji wa makampuni ya IPP, kauli ambazo zinadokeza mtazamo wa serikali katika mjadala unaoendelea wa vita dhidi ya ufisadi na vinara wake.

Waziri Simba, ambaye wizara yake pia inawajibika katika vita dhidi ya ufisadi, alisema: "Kakosea... watoto wa mjini wanasema kachemsha." Simba alitoa msimamo huo jijini Dar es Salaam jana muda mfupi baada ya kufungua semina ya wadau wa vyama vya siasa kuhusu namna ya kuiboresha Sheria ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995.

Simba alisema Mengi hana mamlaka hayo ya kutaja watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Kabla ya kujibu swali kuhusu kitendo cha Mengi, ambaye anamiliki televisheni ya ITV na kituo cha redio cha Radio One Stereo, kutaja majina ya watu hao aliowaita
mafisadi papa, Simba alihoji: " Hapa kuna mtu wa ITV?." Baadaye alisema: "Sikilizeni, kwanza kitendo alichokifanya Mengi si sahihi, kakosea hawezi kuhukumu watu, mamlaka hayo anatoa wapi?"

Simba, huku akionekana kama mtu ambaye alikuwa akitafuta jukwaa kuzungumzia suala hilo, alisema Mengi amekosea kwa kuwa baadhi ya watu aliowataja wana kesi mahakamani."Anahukumu watu," alisema. "Kuna mtu kama Jeetu (Patel) ana kesi mahakamani (EPA), sasa unapokuja kusema ni fisadi wakati mahakama haijathibitisha, unakuwa na maana gani.

"Kwanza kwanini awatuhumu wafanyabiashara wenzake tu, ina maana si ana nia mbaya nao."

Alisema Mengi amechukua uamuzi huo kama vile serikali, wakati serikali ipo siku zote na imekuwa ikifanya kazi zake kwa umakini kwa kufuata misingi ya sheria.

"Serikali ipo na inafanya kazi kwa misingi ya sheria, sasa yeye kukaa na kutangaza watu nasema si sahihi kabisa. Mahakama pekee ndiyo inaweza kumtia mtu hatiani, lakini huwezi kuhukumu watu kama hakuna mamlaka."

Waziri Simba, ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), alisema Mengi hapaswi kutumia vyombo vyake vibaya. "Asitumie vyombo vyake kufanya atakavyo yeye. Huwezi kukaa katika chombo chako na kuanza kuhukumu watu. Kila mtu akifanya hivyo itakuaje," alihoji.

Akiongea na Mwananchi baada ya kupata taarifa za kauli ya Simba, Mengi alisema: "Namuombea kwa Mwenyezi Mungu na kwa maskini wa Tanzania ili wamsamehe kwa sababu hajui anenalo." Mengi hakutaka kuzungumza zaidi kuhusu hatua hiyo ya Mama Simba.

Naye Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali itamchukulia hatua za kisheria Mengi iwapo itabainika alikiuka taratibu na kanuni za nchi kwa kutangaza majina ya watu anaowatuhumu kwa ufisadi
.

Mkuchika alisema jijini Dar es Salaam jana kwa sasa serikali inafanya uchunguzi juu ya suala hilo na itatumia mikanda ya video pamoja na maelezo ya kimaandishi aliyoyatoa Mengi siku alipokutana na waandishi wa habari.

"Tumekusudia kupata ule mkanda wa video, pia tusome maelezo yake ya kimaandishi... tukigundua kuna mahala ambapo sheria haikuzingatiwa, (Mengi) atachukuliwa hatua," alisema Mkuchika.

Mkuchika alisema serikali imepokea malalamiko mengi kutoka kwa watu wengi, wakishutumu hatua iliyochukuliwa na Mengi, ambaye pia anamiliki viwanda vya vinywaji.

Bila kutaka kuwataja majina, Mkuchika alisema miongoni mwa walalamikaji, wapo walioeleza kuwa vyombo vya habari vya mfanyabiashara huyo havikuwatendea haki watuhumiwa waliotajwa kuwa ni mafisadi wakuu.

Alisema ni kutokana na vyombo hivyo kuwataja majina watuhumiwa bila ya kuwapa fursa ya kujibu madai dhidi yao. Waziri Mkuchika alipotakiwa kueleza siku ambayo uchunguzi huo utakamilika, alijibu wananchi wanapaswa kuwa watulivu kwa sababu serikali ikimaliza kuchunguza, itawatangazia yale waliyobaini.

Hii ni mara ya pili katika kipindi cha miezi takribani mitatu kwa Mengi kuingia katika mvutano na serikali baada ya kuvutana mapema mwaka huu na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha kutokana na kutangaza kuwa kuna mipango ya kumfilisi na kumuua.

Mengi pia amewahi kujikuta katika malumbano na watendaji wa serikali hasa na waziri wa zamani wa nchi, ofisi ya rais (utawala bora), Wilson Masilingi alipotoa tuhuma kuwa suala la utoaji zabuni ya ununuzi wa hoteli ya Kilimanjaro, hivi sasa inajulikana kama Kilimanjaro Kempiski, kulikuwa na kitu alichokiita "mchezo mchafu". Suala hilo liliamsha malumbano makali, lakini liliishia hewani.

Katika tuhuma za wiki iliyopita, Mengi aliwahusisha wafanyabiashara hao watano na kashfa za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), utoaji zabuni ya ufuaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development (LLC) na uuzwaji wa jengo la Mfuko wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii (NSSF).

Mengi, ambaye kituo chake cha televisheni cha ITV kiliwahi kuendesha mchezo mkubwa wa bahati nasibu ya Jackpot Bingo, pia aliitaja Bahati Nasibu kuwa katika tuhuma hizo, pamoja na mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma.


CHANZO: Mwananchi


HALAFU TUKISEMA UFISADI NI MIONGONI MWA SERA ZA CCM TUTAITWA WACHOCHEZI?CHADEMA WALIPOTOA LIST OF SHAME CCM,KAMA KAWAIDA YAKE,IKAJA JUU KUDAI HIZO NI POROJO ZA KISIASA.WENGINE WAKAENDA MBALI ZAIDI NA KUTISHIA KUWAPELEKA AKINA SLAA MAHAKAMANI KWA MADAI YA "KASHFA".HADI LEO HAKUNA HATA MMOJA WAO ALIYEKWENDA MAHAKAMANI,NA SANASANA BAADHI YA WATUHUMIWA HAO KWA SASA WAKO MAHAKAMANI WAKITUHUMIWA KUHUSU YALEYALE YALOTAJWA KWENYE LIST OF SHAME.


TATIZO LA MAWAZIRI WOTE WAWILI SIO MANJI AU THE PATELS.NI MR UNTOUCHABLE.HUYU AKIGUSWA BASI NDIO KAMA UMEPIGA LUMUMBA,HQ YA CCM.HAIHITAJI UPEO WA JUU KUBAINI KUWA WANACHOONGEA MAWAZIRI HAO WAWILI NI SAWA NA SELF-DENIAL.YAANI TUKIMJUA MWIZI TUSIMUITE MWIZI MPAKA AFIKISHWE MAHAKAMANI?TUTAMFIKISHAJE HUKO PASIPO KUMTUHUMU IN THE FIRST PLACE?


NA KWANINI ALALAMIKE WAZIRI SIMBA NA MKUCHIKA NA SIO HAO WALIOTAJWA NA MENGI?WAMETUMWA AU WANATUMIWA?WASITUFANYE WATOTO KUHUSU HABARI ZA HAO MAPAPA WA UFISADI KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA VILE HILO HALIWEZEKANI.KWANI KUNA SABABU NYINGINE INAYOSABABISHA KUSUASUA KUWATAJA WAMILIKI WA KAGODA ZAIDI YA UKWELI KUWA AMONG THE WAMILIKI NI MR UNTOUCHABLE?


AH,SIJUI MAMBO HAYA YATAENDELEA HADI LINI!

13 Oct 2008


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimefanikiwa kulidhibiti jimbo la uchaguzi la Tarime katika uchaguzi mdogo uliofanyika jana kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo,Chacha Wangwe.Kwa mujibu wa taarifa za uhakika kutoka huko nyumbani,Chadema imepata kura34,545 wakati CCM imepata kura 28,996.Licha ya ushindi huo wa jimbo,pia Chadema imefanikiwa kushinda uchaguzi wa kiti cha udiwani.

Wakati huohuo,Serikali imelifungia gazeti la Mwanahalisi kwa miezi mitatu kwa tuhuma za uchochezi.Uamuzi huo wa Serikali umetangazwa na Waziri wa Habari,Utamaduni na Utangazaji,Kapteni George Mkuchika.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.