Showing posts with label Masahihisho. Show all posts
Showing posts with label Masahihisho. Show all posts

20 Sept 2011



Mdau mmoja mkubwa wa blogu hii amenitumia ujumbe ufuatao,nami naomba niuwasilishe kama ulivyo 


20/09/2011 09:00 kaka chahali.....naheshimu sana kazi zako za uandishi....ila kwahili nahisi umekosea

nikweli magamba wanafanya kila wawezalo huko igunga ila kutumia picha isiyo na uhalisia juu ya tukio hilo ni jambo la kudhalilisha taaluma yako ya uandishi.....

Picha ya kwanza ni imepigwa morogoro na si igunga na tena ilikuwa ni mashindano ya kula .....verify it here http://issamichuzi.blogspot.com/2011/07/mashindano-ya-kula-yafana-sana-mkoani.html

chonde ni heri kutoa habari bila picha kuliko kucopy and paste picha za matukio mawili tofauti....

ningefurahi kama utalitolea ufafanuzi jambo hili....

Regards,KM
mdau ninayefatilia kazizako twitter,facebook na kwenye hii blog yetu tuk


Baada ya kufuatilia kiungo (link) kilichobainishwa na mdau huyo nimegundua kuwa chanzo cha picha husika (ambacho ni jukwaa la mtandaoni la Jamii Forums) hakikuwasilisha picha husika kwa usahihi.

Naomba kutumia fursa hii kuomba radhi kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wote walioguswa na picha husika.Kuna nyakati waandishi hujikuta katika wakati mgumu kuthibitisha uhalisia wa kila habari,picha au chanzo cha habari/picha husika.

Lakini ni matumaini yangu makubwa kuwa kila msomaji wa blogu hii ataiga mfano wa mdau MK pindi kunapojitokeza mapungufu au makosa ya aina yoyote ile.Kwangu,kukosolewa ni miongoni mwa njia za kujifunza na kujirekebisha.Naomba kumshukuru sana mdau MK kwa ujumbe wake,na ninatumini tutazidi kushirikiana.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.