Showing posts with label OPPOSITION POLITICS IN TANZANIA. Show all posts
Showing posts with label OPPOSITION POLITICS IN TANZANIA. Show all posts

4 Sept 2010

Kwa mujibu wa blogu ya Utakapojua Hujui Ndipo Utakapojua (mwanahabari mahiri Ansbert Ngurumo),Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa alionekana Ikulu siku ya Alhamisi majira ya saa 9 alasiri ambapo inaelezwa alikutana na Rais Jakaya Kikwete,mgombea wa CCM ambaye amelalamikiwa na Chadema kwa kukiuka Sheria y Gharama za Uchaguzi.Awali,Tendwa alisema kuwa angetoa "hukumu" keshokutwa (Jumatatu).

Kwa hakika,haihitaji utaalam wowote kuhusisha tukio hilo (la Tendwa kukutana na Kikwete) na pingamiz la Chadema.Na haihitaji ujuzi wa sheria kubashiri matokeo ya "hakimu kukutana faragha na mshtakiwa" siku chache kabla ya hukumu.

Wengi wetu tunafahamu Tendwa atasema nini hiyo Jumatatu.Most likely,ameshafanya maamuzi ila kinachoshughulikiwa sasa ni usanii wa lugha ya utoaji wa maamuzi hayo.Na ni katika hilo ndio maana inamlazimu awasiliane na JK ili "ajenge mazingira ya hukumu ya haki".Katika mazingira tuliyonayo ambapo Msajili wa vyama vya siasa ni kama kibaraka wa CCM,haiwezekani kabisa kiongozi huyo kutoa maamuzi ya haki yatakayokiathiri chama hicho.

Na dalili za "usanii" zimeonekana tangu Chadema wawasilishe malalamiko yao.Hivi Tendwa anaweza kuwaambia Watanzania kwanini imchukue takriban wiki nzima kutoa maamuzi kuhusu malalamiko ya Chadema?Je hiyo pekee sio dalili ya uzembe na kutowajibika ipasavyo?Awali aliwaeleza waandishi wa habari kuwa angetoa maamuzi Jumatatu lakini hakueleza kwanini itachukua muda wote huo kutoa maamuzi hayo muhimu kwa mustakabali wa demokrasia nchini mwetu.Jibu jepesi ni kwamba hana ubavu wa kutoa maamuzi kabla ya kupata ridhaa ya CCM.Na kwa vile CCM ndio watuhumiwa,ni dhahiri maamuzi ya Tendwa yataelemea kuipendelea CCM.

Nafahamu kuna wataosema "aah,sasa kelele za nini wakati maamuzi hayajatolewa?" Wana haki ya kusema hivyo lakini wanapaswa pia kutambua vema mapungufu ya Katiba yetu yanayomfanya mgombea wa chama tawala kuwa na advantage kubwa dhidi ya wagombea wengine kutokana na ukweli kwamba Katiba inampa rais nguvu kubwa mno.

Kikwete ameendelea kupuuza malalamiko ya Chadema kwa kuzidi kutoa rushwa ya ahadi katika mikutano yake ya kampeni.Sote tumemsikia akiwazuga wapigakura huko Mbagala kuhusu daraja la Kigamboni na ahadi nyingine hewa ya huduma ya uhakika kwa maji jijini Dar es Salaam.Huyu mtu hana aibu kwa sababu ahadi anazotoa sasa zinatoa picha ya mgombea anayeomba idhini ya kuingia madarakani kwa mara ya kwanza na sio aliyekuwa rais wetu kwa miaka mitano iliyopita.Kama tangu 2005 hadi leo ameshindwa kuwezesha ujenzi wa daraja hilo la Kigamboni,kwanini tumwamini kuwa ataweza katika mhula wake wa mwisho (2010-2015) hasa ikizingatiwa kuwa kipindi hicho cha pili kitatumika zaidi kwa yeye kujitengenezea mazingira ya "kustaafu kwa amani"?

Jeuri ya Kikwete inasababishwa na ufahamu kuwa Chadema,na vyama vingine vya upinzani,havina mahala pa kukimbilia pindi wasiporidhishwa na mwenendo wa kampeni za Kikwete na CCM kwa ujumla.Anafahamu kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi,Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa,Mahakama na taasisi nyingine za kusimamia uchaguzi na sheria nza nchi kwa ujumla,ziko mikononi mwa CCM.Hata hivyo,wapinzani hawapaswi kukata tamaa kwa vile nchi yetu kama masikini wa kutupwa inategemea sana misaada ya wafadhili.Japo kuwapigia magoti wafadhili kunaweza kutafsiriwa kama "kuegemea kwenye ukoloni" lakini tufanyeje kama nchi yetu inaendeshwa kiholela.Binafsi,nina matumaini makubwa kuwa nchi wafadhili zinafuatilia kwa karibu mwenendo wa kampeni za vyama vya siasa nchini na hazitasita kuchukua hatua mwafaka pale CCM itakapotumia ubabe wake kulazimisha ushindi.

Hata hivyo,wakati we keep on hoping for the best and expecting the worst,Tendwa afahamu kuwa he wont get away with this issue as easily as he might think.Blogu hii inaamini kuwa Chadema ni chama makini na chenye rekodi nzuri ya ufuatiliaji mambo.Ni katika mantiki hiyo basi blogu hii inatarajia kuwa Chadema hawatamruhusu Tendwa kufanya uhuni wa aina yoyote ile katika maamuzi yake.Ni heri uchaguzi uvurugike lakini haki ipatikane.Kutoa fursa ya sheria za nchi kupindishwa kwa namna watawala wanavyotaka ni hatari sana hasa tukizingatia ulevi wa madaraka unaowakabili viongozi wengi wa "dunia ya tatu".

Kama alivyoandika Ngurumo katika blogu yake,nami narejea kumkumbusha Tendwa kuwa HATUDANGANYIKI!

31 Mar 2010


Mwaka 1996 nikiwa mwanafunzi wa mwaka wa kwanza pale Mlimani nilipata 'somo' moja muhimu kuhusu wanasiasa wa Tanzania.Ilikuwa ni kwenye mhadhara (lecture) ya Dr (Profesa kwa sasa) Max Mmuya katika somo Siasa na Serikali Tanzania na Nchi Nyingine za Afrika Mashariki (PS 102),ambapo mhadhiri huyo alitupatia wasifu wa wagombea urais wanne walioshiriki Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995.Pasipo kuingia sana kiundani,wagombea hao wote walikuwa 'wawakilishi wa tabaka tawala'.Hakuna mmoja kati yao ambaye tungeweza kumtambua kama 'mlalahoi'.Ni katika minajili hiyo ndipo makala hii inajaribu kuangalia kama ujio wa CCJ utakuwa na lolote jipya kwa 'mlalahoi' (mtu wa kawaida mtaani)Binafsi,tafsiri yangu ya kwanza ya ujio wa CCJ katika kipindi hiki tunachoelekea uchaguzi mkuu hauna tofauti sana na wanasiasa wanaobadili vyama pindi wakiona hawana nafasi ya kupitishwa na vyama vyao kugombea nafasi flani au wale ambao hawakupitishwa na vyama hivyo.Japo hiyo ni haki yao ya kikatiba,jamii inapaswa kuwaangalia wanasiasa hao kwa jicho la shaka pia.Je wanafanya hivyo kwa minajili ya kupata fursa ya kuutumikia umma au ni maslahi binafsi?Historia inaweza kutusaidia katika kupata jibu la swali hili.Mara nyingi tumesikia wanasiasa wakipita huku na kule wakijaribu kutuaminisha kuwa bila wao hatuwezi kupata maendeleo.Cha kuchekesha ni kwamba baadhi ya wanaotueleza hivyo,wamekuwa madarakani miaka nenda miaka rudi na badala ya kusonga mbele maendeleo yetu yanazidi kudorora.

Ni vigumu kuamini kuwa CCJ italeta mabadiliko yoyote ya maana kwa vile kimsingi chama hicho hakina tofauti na CCM,Chadema,CUF au chama kingine cha siasa.Labda tofauti kubwa ni kuwa CCJ si chama tawala,lakini kama ni hilo basi hata Chadema au NCCR Mageuzi navyo si vyama tawala.Labda tofauti nyingine ni upya wake.Lakini historia pia inatuusia kuwa si kila kipya ni kinyemi.Upya wa chama si jambo la muhimu kwa wananchi bali ufanisi wake katika kuwatumikia.Je katika mazingira tuliyonayo,CCJ inaweza kweli kuwa mkombozi wa Watanzania?Jibu linaweza kupatikana kutoka kwa waasisi wa CCJ na sie wananchi wenyewe.Kwa viongozi wa chama hicho,so far hawajatuthibitishia kuwa ujio wa chama chao utaleta lolote jipya zaidi ya maneno mataaaamu just like ilivyo kwenye miongozo mbalimbali ya CCM.Kama nilivyowahi kuandika mara kadhaa,tatizo la Tanzania (na pengine Afrika kwa ujumla) halijawahi kuwa katika kuunda mawazo au mipango mizuri.Siku zote kikwazo chetu ni usimamizi na utekelezaji wa mawazo/mipango hiyo.

Ni katika minajili hiyo ndipo wananchi wanapaswa kuhoji kama CCJ sio CCM kwenye jezi nyingine.Yani mvinyo wa zamani kwenye chupa mpya.Na kibaya zaidi,kwa kuzingati tukio la jana ambapo mmoja wa wabunge wa CCM Fred Mpendazoe ametangaza kujiunga na CCJ,chama hicho kipya kina kila dalili ya kuwa CCM-B.Hilo halina ubaya iwapo wanaotoka CCM na kujiunga na CCJ watakuwa wanasiasa wenye uchungu wa dhati kwa nchi yetu na wenye nia ya kuutumikia umma kwa uadilifu.Lakini miaka arobaini na ushee ya uhuru wetu imeshatupa darasa zuri kuhusu wanasiasa wetu.Wengi wao wametawaliwa na ubinafsi huku wakiamini kuwa ni wao pekee ndio wenye ujuzi,nguvu,mamlaka na haki ya kutuongoza.Kibaya zaidi,kwa kiasi kikubwa wengi wao wamechangia mno kutufikisha hapa tulipo:hohehahe wa kutupwa huku raslimali za nchi yetu zikiibiwa kana kwamba hazina mwenyewe.

Pengine siitendei haki CCJ kwa kuiona kama shati chakavu lililopigwa pasi na kunyunyiziwa uturi.Lakini nina kila sababu ya kuhofia ujio wake.Japo natambua kuwa katika siasa timing is everything,lakini kwa muda huu mchache uliosalia kabla ya uchaguzi mkuu,yayumkinika kuamini kuwa chama hicho kitakuwa washiriki tu badala ya kuwa serious contenders.Hilo si baya sana iwapo matokeo mabaya kwenye uchaguzi ujao hayatopelekea hadithi kama za NCCR Mageuzi mwaka 1995.Tatizo la vyama vinavyofikiria uongozi tu badala ya utumishi kwa umma ni kwamba vikishindwa uchaguzi basi ndio inakuwa mwisho wa safari.Yani vinakuwa kama mapenzi ya pesa,ukiwa nazo utaonekana mfalme,'ukifulia' unabwagwa.

Nimalizie kwa hitimisho lisilopendeza kwa wale wanaotaka kuiona CCM ikidondoka kwenye uchaguzi mkuu ujao.Kinyume na fikra zinazoelekea kupata umaarufu kuwa ujio wa CCJ ni kilio kwa CCM,ukweli ni kwamba chama hicho kimekuja kugawa kura za wapinzani.Hilo linaweza tu kuepukika iwapo CCJ itaamua kushirikiana na chama kingine/vingine kwenye uchaguzi mkuu ujao.Lakini kinachokwaza ushirikiano wa vyama vyetu vya upinzani sio kutofautiana kwa sera zao bali ubinafsi.Wapinzani wataendelea kuwa wapinzani kwa muda mrefu huku CCM 'ikipeta' licha ya kulea ufisadi na kuipeleka nchi kusikoeleweka.Kwa wapiga kura,CCM inabaki kuwa the devil they know.Ni uamuzi mbovu lakini at the end of the day unaendelea kuiweka CM madarakani.

Na nisisahau.CCJ ina kazi ya ziada ya kukabiliana na 'nguvu za giza' zinazotumia pesa za walipa kodi kuhakikisha CCM inatawala milele.Na si ajabu miongoni mwa wanaopigia debe CCJ,au watakaojiunga hivi karibuni, ni wawakilishi wa nguvu hizo za giza.

8 Mar 2010


It's nearly less than seven months before Tanzanians go to poll to elect,among others, the 5th phase president,should all go well.However,none of the major opposition parties have so far come up with any names of their potential presidential candidates.Does this imply that they have indirectly endorsed a potential CCM candidate,the incumbent president Jakaya Kikwete?The Swahili word for it is 'kusuasua'.Arguably,that's how one could describe opposition politics in Tanzania.Nearly two decades after Tanzania embarked into multiparty politics,most,if not all,of the country's opposition parties have been a hughe disappointment.It could well be concluded that Tanzanians are yet to benefit from the considerably huge number of opposition parties.They are more popular for their seemingly incessant internal skirmishes than their polices or service to the society.Although the ruling party CCM has frequently been accused of meddling into the Opposition's affairs,the truth remains that they are either too weak or too disorganised to pose any serious challenge to the ruling party.

The first multiparty elections saw the perceived might of NCCR Mageuzi,a party that was seen as a serious contender for the ruling of the country.However,sooner after the party lost miserably to CCM,it embarked into a bitter power struggle that eventually led to its chairman,and one of the four 1995 presidential candidates,Augustine Mrema,to switch sides to join TLP.

The next two elections in 2000 and 2005 continued to be the same sad story as CUF and Chadema succeeded in pulling huge crowds during their campaign rallies but only for them to receive meagre number of votes.

Although Chadema emerged fairly stronger in the elections after winning a substantial number of seats in local elections,and has so far gained considerable support in its outspoken stance against economic sabotage (ufisadi) it has so far failed to project any personality that voters could take as a serious contender against Kikwete.And with election looming,the party seems more concerned with increasing their share of parliamentary votes than winning the presidential seat.

The opposition is well aware of how strong CCM remains despite its poor record in delivering its election promises.While opposition parties have an uphill task of convincing potential members and supporters to join them,the ruling party has a distinct advantage from the pre-political reform era where membership to the party was compulsory.That's on top of the current de-facto single-party political environment in which all the characteristics of a one party state prevail except for the legal and constitutional provisions making it official.

One would have expected that by now the opposition parties should have started the process of nominating their presidential candidates process if their participation in the coming election is to make any difference. Faced with acute financial and logical constraints,and with such limited time left before the election,it's fair to conclude that the opposition parties have 'informally' endorsed a CCM candidate even without making such a stance public.

While this blog has nothing personal against such an 'endorsement',it is disaapointed to see how 18 years of opposition politics have produced so little hope to Tanzanians and therefore leaving them with no other choice than continuing to vote for CCM,a party that is so out of touch with voters.Once they lose the election,which is becoming most likely,they (opposition parties) would certainly repeat same old excuses such as calling for an independent electoral commission and constitutional reforms,all of which would brand CCM as a culprit in sabotaging democratic development in Tanzania.However,unless the opposition parties clean up their act,they are doomed to continue to perform dismally in every election.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.