Showing posts with label REGINALD MENGI. Show all posts
Showing posts with label REGINALD MENGI. Show all posts

11 May 2009


HIVI KARIBUNI,WAZIRI WA NCHI OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI NA UTUMISHI WA UMMA),USTAADHA HAWA GHASIA,ALITOA ONYO KALI DHIDI YA WATU WANAOJIHUSISHA NA KILE ALICHOKIITA "WIZI WA NYARAKA ZA SERIKALI".NISINGEPENDA KUREJEA REACTIONS MBALIMBALI ZILIZOTOKANA NA KAULI HIYO LAKINI MMOJA YA SAUTI ZILIZOPINGA VIKALI TAMK HILO LA GHASIA NI MBUNGE WA KARATU NA KATIBU MKUU WA CHADEMA,DR WILBROAD SLAA.MWANASIASA HUYO NGULI WA MAPAMBANO DHIDI YA UFISADI ALIELEZA WAZIWAZI KWAMBA NYARAKA ZINAZOFICHA UFISADI HAZIPASWI KUWEKWA KWENYE KUNDI LA NYARAKA ZA SIRI ZA SERIKALI.DR SLAA ALIELEZA BAYANA KWAMBA PINDI AKILETEWA NYARAKA ZA AINA HIYO ATAZIMIA PASI UOGA KWA VILE NI KWA NJIA HIYO NDIO TUMEFANIKIWA KUBAINI SKANDALI KAMA ZA EPA,RICHMOND NA NYINGINEZO.


NI DHAHIRI TAMKO LA WAZIRI GHASIA LILENGA KUWATISHA WATU KAMA DR SLAA.LAKINI PIA WAZIRI HUYO ALIFANYA HIVYO KWA VILE NI MIONGONI MWA VIONGOZI WA SERIKALI WENYE DHAMANA NA MASUALA YANAYOHUSU IDARA MBALIMBALI ZA SERIKALI.


BILA KUUMAUMA MANENO,HEBU TUJIULIZE: HIVI ROSTAM AZIZ ALIPOITISHA PRESS CONFERENCE YAKE NA KUTOA "USHAHIDI" MBALIMBALI KUPIGILIA MSUMARI HOJA YAKE KUWA REGINALD MENGI (MWENYEKITI MTENDAJI WA MAKAMPUNI YA IPP) NI FISADI NYANGUMI,ALIZIPATAJE NYARAKA MBALIMBALI ZINAZOPASWA KUWA KATIKA HIFADHI YA TAASISI HUSIKA ZA SERIKALI?

ROSTAM SI MTUMISHI WA MAMLAKA YA MAPATO AU MWAJIRIWA KATIKA WIZARA YA FEDHA KIASI CHA KUWA NA "DATA" ALIZOTOA KUHUSU MENGI.NA KWA VILE MAMLAKA HUSIKA ZIMEKUWA KIMYA KUHUSU WAPI MBUNGE HUYO WA IGUNGA ALIPATA NYARAKA HIZO NI WAZI KWAMBA ALIPATIWA KWA RIDHAA YA WAHUSIKA.

WATETEZI WA ROSTAM,KUANZIA WAZIRI SOPHIA SIMBA NA KAPTENI GEORGE MKUCHIKA WAMEKUWA KIMYA KABISA KUKEMEA "HUKUMU" ALIYOTOA ROSTAM DHIDI YA MENGI TOFAUTI NA WALIVYOKURUPUKA MARA BAADA YA KIPENZI CHAO KUTAJWA KUWA NA MENGI KUWA NI FISADI PAPA.BY THE WAY,MENGI SI MTU WA KWANZA KUMTUHUMU ROSTAM KUWA NI FISADI.HIYO NI OPEN SECRET,NA KINACHOKWAZA WATU HAWA KUCHUKULIWA HATUA NI NJAA TU ZA HAO WENYE WAJIBU WA KUFANYA HIVYO ZINAZOKIDHIWA NA JEURI YA FEDHA ZA MAFISADI HAO.

SASA,SIJUI WAZIRI GHASIA ANAWEZA KUTUELEZA NINI KUHUSU WIZI WA NYARAKA ZA SERIKALI ULIOFANYWA NA ROSTAM.NAUITA WIZI KWA VILE ROSTAM SIO TRA,DPP,MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI AU TAASISI YOYOTE YA SERIKALI YENYE DHAMANA YA KUWA NA NYARAKA ZILIZOTUMIWA NA MFANYABIASHARA HUYO KWENYE "KUJENGA KESI" YAKE DHIDI YA MENGI.

SASA NAELEWA KWANINI ROSTAM ANAWEZA KU-WISH ASINGEJIBU HOJA ZA MENGI KWANI WATAPOFIKA MAHAKAMANI ANAPASWA KUULIZWA YEYE ALIKUWA NA NYARAKA HIZO KAMA NANI?ALIZIPATAJE?NA JE KUWA NAZO SIO KOSA (KWA KUREJEA "MKWARA" WA WAZIRI GHASIA?

NA HIYO NI NJE YA TAARIFA ZA KUAMINIKA KUWA NYINGI YA DATA ALIZOTUMIA ROSTAM NI "MAKANJANJA" (FAKE DATA) AMBAPO WAJANJA WA MJINI WALIPOSIKIA KUNA TENDA YA FEDHA NYINGI YA KUWEZESHA KUPATIKANA KWA INCRIMINATING EVIDENCE DHIDI YA MENGI WAKACHANGAMKIA TENDA HIYO LAKINI KATIKA HALI YA UFISADI.WHY NOT,KUMFISADI FISADI NI SAWA KABISA NA KULIPA KWA NOTI BANDIA MANUNUZI YA CHENI ILIYOTENGENEZWA KWA DHAHABU FEKI.


MWISHO,NAPENDA KUSISITIZA KWAMBA SINA CHUKI NA ROSTAM AU MTANZANIA YEYOTE MWENYE ASILI YA NJE YA NCHI.ILA SIFICHI UKWELI KWAMBA NINA ZAIDI YA CHUKI,HASIRA,DUA BAYA (NA MENGINE NISIYOWEZA KUTAJA HAPA) DHIDI MAFISADI.UTETEZI WA KIPUUZI WA MAFISADI UMEKUWA KWENYE VITU KAMA RANGI,DINI,KABILA,NK.MTAKUMBUKA MKURUGENZI WA IPC,EMMANUEL OLE NAIKO ALIZONGWA KUHUSU KWANINI ALITOA KIBALI CHA UWEKEZAJI KWA KAMPUNI YA KITAPELI YA RCHMOND,KIMBILIO LAKE KUU LILIKUWA UKABILA.ETI "NAANDAMWA KWA VILE NATOKA ENEO MOJA NA LOWASSA"!

LEO HII AKINA ROSTAM,MANJI,SOMAIYA,JEETU NA SUBASH WANATAKA KUTUAMINISHA KUWA TUHUMA DHIDI YAO ZINACHANGIWA NA "UTANZANIA" WAO WENYE ASILI YA NJE YA NCHI.HUU NI UTETEZI MUFILIS NA NI WA KIFISADI KAMA WANAVYOTUHUMIWA.HIVI WANATAKA KUTUAMBIA KUWA TULIPOPAMBANA NA MKOLONI,MJERUMANI NA MWINGEREZA TULIKUWA WABAGUZI WA RANGI?

5 May 2009








CHANZO: Jamii Forums


4 May 2009

NA KUNA BOMU JINGINE LA ASKARI WASTAAFU.KILA NISOMAPO HABARI KUWA WASTAAFU WA JESHI WANAZUNGUSHWA KUHUSU MAFAO YAO,NAPATWA NA UOGA FLANI KWAMBA WASIJE KUAMUA KUTUMIA UJUZI WAO WA KIJESHI KUDAI HAKI ZAO.
NA NIPITAPO PALE MWENGE KWENYE FLATS ZA JESHI NA KUANA NAMNA "ZILIVYOCHOKA" NAPATWA NA HOFU NYINGINE SIKU WAUNGWANA HAWA WATAKAPOAMUA KUDAI KWA NGUVU MAISHA BORA KAMA YALE YA VIGOGO KULE MASAKI,MIKOCHENI,OYSTERBAY,NK.TALKING OF OYSTERBAY,NAPATA KUMBUKUMBU YA YALE MAHEMA WANAYOISHI ASKARI POLISI KATIKA "KAMBI" ILIYO JIRANI NA KITUO CHA POLISI OYSTERBAY.
BOMU JINGINE NI HAO MGAMBO AMBAO KULA NA ANASA ZAO ZINATEGEMEA KUVUNJA HAKI ZA BINADAMU ZA WAMACHINGA,WANAODIWA KODI ZA MANISPAA/HALMASHAURI NA WANYONGE WENGINE.MOST OF MGAMBO HAWA HAVE NO IDEA WHATSOEVER KUHUSU HUMAN RIGHTS.WANACHOJUA WAO NI PIGA,NYANG'ANYA,TAIFISHA!HAWA NI VIUMBE HATARI ZAIDI KWA VILE MAISHA YAO KWA KIASI KIKUBWA YANATEGEMEA UBABE WAO DHIDI YA WANYONGE WAO.KWA MFANO,MARA NYINGI LUNCH ZAO NI VYAKULA WANAVYOWAPORA MAMA NTILIE NA VITOWEO WANAVYORUDI NAVYO BAADA YA KUMALIZA KAZI NI VILEVILE WANAVYOWAPORA WANANCHI WANAOJITAFUTIA RIDHIKI ZAO HALALI.
KUNA MTU AMENINONG'ONEZA SOMETHING HE CALLED FACTS ETI HUO MLIPUKO WA MABOMU NI HUJUMA.I DIDNT TAKE HIM SERIOUS KWA VILE ALIKUWA AMEONJA KILEVI KIDOGO.HE WENT FURTHER TO ARGUE KWAMBA VIRUSI (VIRUS) WA HUJUMA WAMEANZA KUSAMBAA KUTOKA KWA MAFISADI KWENDA KWA PROFESSIONALS WALIOSAHAULIKA AU KUTELEKEZWA.REASONS HE CITED,KAMA MZEE WA VIJISENTI AMEJICHOTEA BILIONI ZAKE KADHAA NA BADO HAJAGUSWA,AU MAJAMBAZI WA RICHMOND BADO WANAPETA LICHA YA KUBAINISHWA NA KAMATI YA MWAKYEMBE,NA DOWANS NAO WANAENDELEA NA JEURI YA KUIPELEKA TANESCO MAHAKAMANI LICHA YA HIZO MILIONI MIA NA USHEE PER DAY WALIZOZAWADIWA,WAMILIKI WA KAGODA WAMEENDELEA KUWA GHOSTS WASIOTAJIKA,THEN MTU YEYOTE ANWEZA KUSHAWISHIKA KUWA FISADI,MHUJUMU WA UCHUMI AU USALAMA,AU MLIPUA MABOMU!DRUNK AS HE WAS BUT THIS KINDA MADE SENSE TO ME!
KUNA BOMU JINGINE KUBWA ZAIDI YA HAYO HAPO JUU,AU ZAIDI YA HAYO YALOKWISHALIPUKA.KWA UPANDE MMOJA NI RESERVE ARMY OF LABOUR,INAYOZALISHWA NA UBINAFSISHAJI,KUPUNGUZA MATUMIZI,"KEEP CITY/TOWN CLEAN OPERATIONS" (KAMA HIZO ZA MGAMBO ZINAZOISHIA KUWAFANYA WAMACHINGA WAJIULIZE "TUFANYE NINI ILI TUSIBUGHUDHIWE,AU TUWE WAPORAJI?"),WAKULIMA WALIOFIKIA HATUA YA KUTAFSIRI KUWA KILIMO NI SAWA NA KIFUNGO BCOZ CO-OPS HAZITAKI KULIPA MADENI HUKU WASSIRA NA WIZARA YAKE WAKIWA KWENYE SUINGIZI WA PONO KUHUSU KUTAFUTA MASOKO KWA WAKULIMA,NA MAKUNDI KAMA HAYO.KWA UPANDE MWINGINE NI WANANCHI WALALAHOI WANAOSIKIA NAMNA MAFISADI WANAVYOWADHIHAKI KWA PRESS CONFERENCES HUKU WAKITETEWA NA BAADHI YA VIONGOZI,WANANCHI WALIOCHOSHWA NA DANADANA ZA KUMWEKA WAZI MMILIKI WA KAGODA,WALIOKATISHWA TAMAA NA AHADI BAADA YA AHADI KUWA MAISHA BORA YAKO NJIANI (AS WE APPROACH THE GENERAL ELECTION,THEY WOULD KEEP ON REMINDING US THAT WE ARE NOW APPROACHING THE MAISHA BORA DESTINATION,EVERYBODY SHOULD REMAIN SEATED TILL WE ARRIVE i.e. BAADA YA GENERAL ELECTION,MEANING RETURNING THEM TO POWER AND GOING BACK TO SQUARE ONE.IF THEY BOTHER GIVING EXCUSES AS TO WHY IT'S FEBRUARY 2011 AND WE ARE YET TO ARRIVE AT MAISHA BORA,THEY WOULD PROBABLY SAY "OH,TUMEPOTEA NJIA.MSIHOFU TUTAFIKA MUDA SI MREFU...."
MABOMU HAYA NILIOBAINISHA KWENYE STORI HII NI HATARI ZAIDI KULIKO HAYO YANAYOLIPUKA HUKO MBAGALA.YATAKAPOLIPUKA,SI TUME YA MKUU WA MAJESHI WALA NGONJERA ZA "TUTALIPA FIDIA" ZITAKAZOWEZESHA KUREJESHA HALI KWENYE UTULIVU.THE TIME IN NOW.IT'S NOW OR NEVER!

ANYWAY,HEBU TUSIKIE HADITHI ZA ROSTAM KUHUSU TUHUMA ZILIZOTOLEWA (NA REGINALD MENGI) DHIDI YAKE NA WAHINDI WENZIE KWAMBA WAO NI MAFISADI PAPA.

Rostam amlipua Mengi, amwita nyangumi wa ufisadi


Ramadhan Semtawa na Salim Said


MFANYABIASHARA wa jijini Dar es salaam, Reginald Mengi aliwabatiza wafayabiashara wenzake watano jina la "mapapa wa ufisadi", na sasa mmoja wa waliotuhumiwa amejibu mapigo kwa kumbatiza jina la "nyangumi wa ufisadi".


Rostam Aziz, ambaye ni mmoja wa wafanyabiashara watano waliotuhumiwa na Mengi kuwa mapapa wa ufisadi, jana alitoa mlolongo wa tuhuma za ufisadi dhidi ya mwenyekiti huyo mtendaji wa makampuni ya IPP, na kueleza kuwa atawasilisha vielelezo kwa vyombo husika ndani ya saa 48 ili Mengi aanze kuchunguzwa.


Mapigo ya Rostam, ambayo yanazidi kupandisha joto la vita hiyo ya maneno, yametokana na tuhuma nzito ambazo Mengi alizitoa Aprili 23 wakati alipotaja wafanyabiashara watano akitaka wadhibitiwe mapema, akiwemo mbunge huyo wa
Igunga. Tofauti na Mengi ambaye hakutoa vielelezo na kusema yuko tayari kupandishwa kizimbani ili ukweli udhihirike, Rostam aliorodhesha tuhuma nyingi na kuahidi kuzikabidhi kwenye vyombo vya serikali ili hatua zichukuliwe. Huku akimtaja Mengi kwa majina yote matatu kila wakati, Rostam, aliwaambia waandishi jana akisema: "... nataka niweke wazi kwamba tuhuma zote zilizotolewa na Mengi dhidi yangu ni za uongo na ni upuuzi mtupu. Tuhuma hizo ni mwendelezo wa wimbo ule ule ambao amekuwa akiuimba kwa muda mrefu sasa na tayari nilikwishazitolea kauli huko nyuma.


"... nimeamua kuitisha mkutano huu ili kuwaeleza, na kupitia kwenu kuwaelimisha Watanzania, wamjue Reginald Abraham Mengi katika sura yake halisi na dhamira yake chafu na ovu, na kumtambua kwamba mtu huyu ni nyangumi wa ufisadi katika nchi hii," alisema Rostam katika moja ya aya zake za utangulizi. Nyangumi ni samaki wa baharini aliye mkubwa kuliko papa. Rostam alianza kwa kuorodhesha matukio 10 ya ugomvi ambayo anadai Mengi aliuanzisha dhidi ya watu mbalimbali, kuanzia maaskofu hadi kikundi cha uchekeshaji, wakati kwa mujibu wa Rostam maslahi ya Mengi ya kibiashara yalipoingiliwa na baadaye kuyageuza kuwa ni ugomvi wa nchi nzima.


"Sasa ameanzisha ugomvi na mimi baada ya kuona kwamba mimi nimekuwa mshindani wake mkubwa katika umiliki wa vyombo vya habari hapa nchini, anataka kuufanya ugomvi wa nchi nzima," anaeleza Rostam. Akiorodhesha tuhuma za ufisadi dhidi ya Mengi, Rostam alidai mwenyekiti huyo wa IPP alianza kuifilisi nchi kwa kushiriki kwenye vitendo vilivyochangia kuifilisi Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) na kusababishwa iuzwe "kwa bei poa".


Alidai kuwa Mengi, akitumia kampuni yake ya Anche Mwedu Ltd katika miaka ya themanini, alichukua mkopo wa fedha NBC na amegoma kulipa hadi leo, huku akilazimisha suala hilo lifikishwe mahakamani. Rostam alidai kuwa mkopo wa kwanza uliotolewa kupitia hati ya maandishi ya makubaliano, ulifikia jumla ya Sh3.2 bilioni na kwamba hadi Januari mwaka 1996 ulifikia riba ya Sh 1.7 bilioni.


Alidai mkopo wa pili chini ya kampuni hiyo ulikuwa wa mpango wa Loan Agreements na ulihusu jumla ya Sh386,746,631.06 hadi kufikia Januari 1996. Akiongeza kudai kuwa mkopo wa tatu ulikuwa chini ya utaratibu wa udhamini wa serikali (government guarantee) ambao ulikuwa wa jumla ya Sh1,803,137,210 hadi kufikia Januari 1996. Rostam alidai kupitia utaratibu mwingine, Mengi alichukua mkopo mwingine ambao ulihusu jumla ya Sh417.6 milioni hadi kufikia Januari 1996.


"Jumla ya fedha zote za NBC ambazo amekuwa akidaiwa Mengi kupitia kampuni yake ya Anche Mwedu Limited (AML) hadi kufikia Januari 1996 zilikuwa ni Sh 5.8 bilioni, fedha hizi hadi kufikia sasa 2009 pamoja na riba zinafika takriban Sh28 bilioni," alidai Rostam huku akitaka akaunti za benki ambazo mikopo hiyo ilipitia. "Hivi ndivyo Mengi alivyochangia kuifilisi NBC, benki ya wananchi masikini wa Tanzania. Fedha hizi zilizochukuliwa na Mengi Sh28 bilioni zinaweza kujenga shule za sekondari 100 ambazo zingeweza kuwanufaisha watoto wa kimaskini wa Tanzania." Rostam pia alidai kuwa Mengi aliteketeza Sh2.5 bilioni kwa kutumia kampuni ya uwekezaji ya wazalendo ya NICO, kwa kununua hisa za kiwanda cha Interchem Pharma Ltd kinachomilikiwa na familia yake ambacho Rostam alidai kuwa Mengi alijua kuwa kingekufa.


"Huku akijua hali mbaya ya kiwanda hicho alitumia nafasi yake kuziteketeza Sh2.5 bilioni fedha za Watanzania masikini wasiopungua 22,000 wenye hisa NICO kwa kuifanya inunue asilimia 51 ya hisa. Kiwanda hicho sasa kimewekwa kwenye orodha ya kufilisiwa baada ya kushindwa kujiendesha chini ya mwaka mmoja tokea Mengi kuizamisha NICO," alisema. Rostam, ambaye pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu na Kamati Kuu ya CCM, pia alidai Mengi kwa kutumia mpango wa Mfuko wa Kuagiza Bidhaa kutoka Nje (Commodity Import Support-CIS), alichukua fedha nyingi kupitia msaada wa nchi wafadhili, lakini hadi jana alikuwa hajazilipa.


Rostam alikiri kwamba wafanyabiashara wengi akiwemo yeye walikopa, lakini wamelipa na wanaendelea kulipa hadi sasa na kuongeza kwamba Mengi "anayejidai ana uchungu na Watanzania amekuwa akiwaongezea umasikini kwa kuchota fedha hizo baadaye kuruka na kukataa kuzilipa". Rostam pia alitoa mchanganuo huo wa fedha za CIS ambazo alidai Mengi alizipata na kutaja nchi zilizotoa, akianza na Norway ambayo alidai mwaka 1988 hadi 1989 iliisaidia kampuni ya IPP kupitia kampuni ya Anche Mwedu kupata Krona 6milioni, na baadaye kupitia kampuni hiyo hiyo ilipata Krona 4 milioni.


Alidai mwaka 1991/92, Japan ilisaidia Bonite Bottlers kuchukua Yen 160 milioni na baadaye ikasaidia Medicare kupata Yen 115 milioni na Canada mwaka 1988/89 ikasaidia Anche Mwedu dola za nchi hiyo 0.5milioni. Pia alidai mwaka 1988/89 Italia ilisaidia Anche Mwedu kupata Lira 1.7milioni, Japan 1997 ilisaidia Anche Mwedu Yen 20milioni na Japan tena 1994 ilisaidia Bonite Bottlers kupata Yen nyingine 160 milioni.


Pia alidai Tume ya Uchumi ya Ulaya (European Economic Commission-EEC), katika kipindi cha mwaka 1988/89 ilisaidia Bonite Bottlers kupata EEU 0.5199. "Fedha hizi zilizo katika sarafu tofauti za kigeni zikibadilishwa kwa shilingi za Tanzania na riba kwa miaka yote tokea zilipochukuliwa zinafikia mabilioni ya shilingi," alisema Rostam. "... badala ya kurejesha fedha hizi... Mengi alizitumia kujitajirisha."


Pia alidai kuwa Mengi aliingia ubia na serikali katika umiliki wa kiwanda cha Tanpack Industries Ltd, lakini bila ya kumjulisha mbia wake (serikali) alitumia dhamana ya kiwanda kukopa Sh600 (sic) kutoka benki ya NBC na "kuzitumia kwa njia anazozijua yeye". "Benki hiyo ilipochachamaa kutaka ilipwe fedha zake, Mengi alitaka Tanpack ilipe lakini serikali ikakataa kulitambua deni hilo... Matokeo ya ufisadi huo wa Mengi, Tanpack ikafilisiwa na kufa," alidai Rostam. Miongoni mwa matukio ambayo Rostam alidai Mengi alikorofishana na watu mbalimbali ni pamoja na zabuni ya ubinafsishaji hoteli ya Kilimanjaro (sasa Kempiski).


"Alianzisha ugomvi na aliyekuwa Waziri wa Utawala Bora Mheshimiwa Wilson Masilingi baada ya kushindwa zabuni ya ubinafsishaji wa hoteli ya Kilimanjaro, akataka kuufanya kuwa ugomvi wa nchi nzima," alidai Rostam. "Katika kudhihirisha jinsi alivyo na chuki na visasi kutokana na kuikosa tu hoteli hiyo, amekuwa hakanyagi na hata kushiriki shughuli yoyote inayofanyika katika hoteli hiyo." Kuhusu kutajwa kwenye ufisadi katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), Dowans na tuhuma nyingine, Rostam alisema "hizo zote nimekwishazitolea maelezo... ni porojo tu hakuna hata moja ninayohusika nayo".


Ni vema Watanzania wakafahamu kwamba kila anapokabiliwa na matatizo au anapotenda maovu, kimbilio lake la haraka la kujifichia limekuwa ni kusaka huruma kwa wananchi kwa kutaka aonekane ni sehemu yao na kwamba anaonewa kwa kuwatetea wao. Ukweli ni kwamba amekuwa akifanya hivyo ili kutafuta hifadhi na kinga akijua ana madhambi mengi."


Akijibu tuhuma chache kati ya hizo huku akikataa kuzungumza kwa kirefu, Mengi alisema "mafisadi papa wana uwezo mkubwa sana siyo tu kwa mali za umma bali hata kutunga uongo kama ilivyofanywa na Rostam Aziz leo (jana)".


"Naomba nimpe Rostam Aziz ushauri wa bure kama kweli anataka kujisafisha ama kuondokana na shutuma zinazomkabili za ufisadi aende mahakamani ikiwezekana kesho (leo) asubuhi," alisema Mengi.


"Hata baada ya kukutana na waandishi wa habari leo, hoja ya kushutumiwa kama fisadi papa inabakia pale pale. Watanzania wanasubiri kwa hamu kubwa kusikia kwamba Rostam Aziz ameenda mahakamani kwa sababu Watanzania wengi hasa wanyonge wana hasira nyingi dhidi ya ufisadi."

CHANZO: Mwananchi

LET'S HOPE SOPHIA SIMBA NA KAPTENI MKUCHIKA WATAMKOMALIA ROSTAM AS THEY DID TO MENGI ALIPOTOA TUHUMA DHIDI YA MAFISADI PAPA.I CANT SEE SOPHIA SIMBA SAYING "WATOTO WA MJINI WANASEMA ROSTAM AMECHEMKA" AS SHE DESCRIBED MENGI'S STATEMENT.

SOONER OR LATER HAWA MAFISADI WA KIASIA WATAINGIA IKULU KAMA RAIS KAMA WENYE UCHUNGU WA DHATI NA NCHI YETU HAWATAAMKA SASA.WAMESHAIFANYA NCHI HII KUWA IKO MIFUKONI MWAO,WANATUPUUZA NA KUONGEA CHOCHOTE WANACHOJISKIA KUSE,A,SIMPLY BECAUSE OF JEURI YA FEDHA ZAO ZA KIFISADI.COULD YOU EXPECT MHINDI MWENYE ASILI YA KITANZANIA KUFANYA HIVYO INDIA AU YEMEN,OR WHEREVER THESE FISADIs ORIGINATE FROM?


28 Apr 2009

NKWAZI MHANGO
St John’s NL, Canada


AT last names are openly named! When Hon. Harrison Mwakyembe named Rostam Aziz as a suspect behind Kagoda profligacy, many scratched their heads. Some thought it was just politics. Others said: there must be something truly fishy. Others thought the government would wake up and bring him to book. Mwakyembe is a lawyer and an MP who knows what he is doing.

Before long, Reginald Mengi, the Executive Chairman of IPP, massively and openly weighed in with more damning allegations. He minced no words. He averred: Rostam, Yusuf Manji, Jayantkumar Chandubhai Patel (Jeetu Patel) who is facing EPA charges, Tanil Somaiya, and Subash Patel are the most corrupt people in Tanzania.

Today I’ll specifically look at two -Rostam and Manji. They’ve been stealing thunder when it comes to corruption save the government has pretended not to hear or see!
No doubt. The two are CCM bigwigs just like Mengi himself.

What makes things worse is the fact that the duo has been mentioned, though not openly, in almost all multi-million scams. I still remember how Manji was alleged to have swindled wananchi’s money, thanks to his business connections with NSSF. Though this was swept under the carpet, we still have more questions than answers.

Manji also tried hand in politics when he vied for Kigamboni Constituency backed by Yusuf Makamba - CCM’s secretary general who is said to have thick but suspicious bond with the duo.

As for Rostam, it’s an open secret. �He has been cowering before allegations connecting him with EPA theft thanks to being the mind behind Kagoda. Refer to the recent revelations by Bhyidinka Michael Sanze, a lawyer who presided over EPA authorization by Benjamin Mkapa - former president engrossed in many scams.

Also Rostam was linked with Richmond, thanks to his Caspian Company’s address being used by Richmond. He too was named by Ibrahim Msabaha as PM Edward Lowassa’s Arab in Richmond scam.

What damns so as to create doubts is the fact that, the duo, despite being mentioned in many scandals, still has much influence in CCM. They are awarded many lucrative tenders and other projects. They, too, are CCM’s financiers or donors. And this is the reason that forced the Father of the Nation Mwl. Julius Nyerere to sarcastically aver that CCM has been taken by corrupt business people. Who can step in Nyerere’s shoes.
Given that the government has been dragging feet in dealing with the buggers behind Kagoda, now it is aware who those buggers are. Will it go on keeping mum and acting indifferently as it sits on the same.

Silence is gold. But sometimes, it is admission of guilt. When Rostam was confronted by the media to shed light onto Mengi’s allegations, he’s quoted as thus. ’’Mengi is full of jealousy, hatred and what not. There is no way I can help him except to pray God and ignore all, for it is enough a punishment for him. Due to how I was brought up, I cannot quarrel with an old man.’’

Do such gimmicks address the allegations really. Let’s call shorts to white washing and be serious especially when allegations are damningly serious like these.

Though it can be lightly and wrongly perceived as racism and hatred for Mengi to name five Tanzanians of Asian decent as the most corrupt in the country, there is truth in this. Why should it be racism or hatred to aver they are corrupt but not when it comes to owning our economy Why not when they’re given tenders and other preferential treatments.

As Rostam once said that those alleging he is corrupt are labouring under racism, petty jealousy and hatred, but again, is it racism really or corruption.

Suspects should mount reasonable defence in lieu of taking camouflage under the colour of their skin. For example, if someone says Indians own a big chunk of national housing, will this be referred to as racism? If one avers that Indians own over 75% of commerce in the country, will it be branded hatred. If one avers that Indian and Chinese illegal immigrants and hawkers are favoured by authorities, will this be jealousy.

Indians own almost every lucrative business. And now they’ve already penetrated into politics, thanks to rotten takrima law. They live in government houses whilst its workers make do on the outskirts of the city. They’ve remained holier than us since they were brought in by colonialists.

We well know. Indian business moguls are almost behind every stinking lucrative government tender. Refer to the radar, presidential jet purchase, NSSF, Richmond, EPA and what not.

Many will wonder why. It is simple. Corrupt government officials prefer to do dirty business with Indians. They can not divulge their secrets. They’re easy to intimidate and repatriate when things go wrong as it happened in Chavda scam. So indigenous ’fisadis’ are left out of the big picture.

And if you look at whom Tanzania prefers to award citizenship to, you’ll find that Indians outsmart others. They still do the same- being middlemen-the job for which colonialists brought them. When white colonialists left and black ones took over, the role of Indians remained the same almost everywhere in Africa. Go to Kenya, Malawi, South Africa and elsewhere. Indians are still doing the same job-weakening the indigenous for the good of corrupt rulers.

So to avert wasting time, if Kikwete could take a leaf from Mengi, our war on corruption would make more sense than it is today when it is but white washing.

In other words, corruption in Tanzania is like ’mduara’ dance. It’s conspiracy between venal rulers and their corrupt guests. It’s time to rally behind Mengi to see to it that those ’fisadis’ are not harming him. Shall they, Mtikila’s gabacholi era will be latched onto. And the government must stop its indifference. The ’isadis’ it has been asking for are now given pro bono.
FOR MORE,VISIT HIM AT freethinking unabii

27 Apr 2009


KUNA MAMBO YANAYOTOKEA HUKO NYUMBANI YANAKERA KUPITA MFANO.HIVI HAWA WATANZANIA WENZETU WALIOKABIDHIWA DHAMANA YA KUTUONGOZA (TUKIAMINI KABISA KUWA WANA UPEO MZURI TU WA KUTAFAKARI MAMBO) WANAWEZAJE KUONGEA MAMBO YA AJABU NAMNA HII?ANYWAY,HEBU SOMA KWANZA HABARI HUSIKA KISHA TUENDELEE KUJADILI



* Waziri Sophia Simba asema Mengi kachemsha
*Mkuchika naye asema wanamchunguza

Ramadhan Semtawa na Leon Bahati

MAWAZIRI wawili, Sophia Simba na George Mkuchika jana walimshambulia mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi ambaye wiki iliyopita alitangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia, akisema ni mafisadi waliokubuhu.

Simba, ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora) na Mkuchika, Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo walisema mfanyabiashara huyo wa jijini Dar es salaam "amechemsha".

Mengi alitangaza majina ya wafanyabiashara hao Alhamisi iliyopita akisema ni kati ya watu wasiozidi 10 ambao alidai wanaifilisi nchi na kutaka wadhibitiwe mapema kabla hawajaitingisha na kuiyumbisha nchi. Hata hivyo, Mengi, ambaye alidai katika taarifa yake kuwa juhudi za Rais Jakaya Kikwete zinakwamishwa na watu hao, hakueleza jinsi watano hao wanavyoitafuna nchi zaidi ya kusema kuwa wanatorosha fedha wanazozipata 'kifisadi'.

Jana, kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam mawaziri hao wawili walitoa kauli za kumshambulia mwenyekiti huyo mtendaji wa makampuni ya IPP, kauli ambazo zinadokeza mtazamo wa serikali katika mjadala unaoendelea wa vita dhidi ya ufisadi na vinara wake.

Waziri Simba, ambaye wizara yake pia inawajibika katika vita dhidi ya ufisadi, alisema: "Kakosea... watoto wa mjini wanasema kachemsha." Simba alitoa msimamo huo jijini Dar es Salaam jana muda mfupi baada ya kufungua semina ya wadau wa vyama vya siasa kuhusu namna ya kuiboresha Sheria ya Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma ya mwaka 1995.

Simba alisema Mengi hana mamlaka hayo ya kutaja watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Kabla ya kujibu swali kuhusu kitendo cha Mengi, ambaye anamiliki televisheni ya ITV na kituo cha redio cha Radio One Stereo, kutaja majina ya watu hao aliowaita
mafisadi papa, Simba alihoji: " Hapa kuna mtu wa ITV?." Baadaye alisema: "Sikilizeni, kwanza kitendo alichokifanya Mengi si sahihi, kakosea hawezi kuhukumu watu, mamlaka hayo anatoa wapi?"

Simba, huku akionekana kama mtu ambaye alikuwa akitafuta jukwaa kuzungumzia suala hilo, alisema Mengi amekosea kwa kuwa baadhi ya watu aliowataja wana kesi mahakamani."Anahukumu watu," alisema. "Kuna mtu kama Jeetu (Patel) ana kesi mahakamani (EPA), sasa unapokuja kusema ni fisadi wakati mahakama haijathibitisha, unakuwa na maana gani.

"Kwanza kwanini awatuhumu wafanyabiashara wenzake tu, ina maana si ana nia mbaya nao."

Alisema Mengi amechukua uamuzi huo kama vile serikali, wakati serikali ipo siku zote na imekuwa ikifanya kazi zake kwa umakini kwa kufuata misingi ya sheria.

"Serikali ipo na inafanya kazi kwa misingi ya sheria, sasa yeye kukaa na kutangaza watu nasema si sahihi kabisa. Mahakama pekee ndiyo inaweza kumtia mtu hatiani, lakini huwezi kuhukumu watu kama hakuna mamlaka."

Waziri Simba, ambaye pia ni mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), alisema Mengi hapaswi kutumia vyombo vyake vibaya. "Asitumie vyombo vyake kufanya atakavyo yeye. Huwezi kukaa katika chombo chako na kuanza kuhukumu watu. Kila mtu akifanya hivyo itakuaje," alihoji.

Akiongea na Mwananchi baada ya kupata taarifa za kauli ya Simba, Mengi alisema: "Namuombea kwa Mwenyezi Mungu na kwa maskini wa Tanzania ili wamsamehe kwa sababu hajui anenalo." Mengi hakutaka kuzungumza zaidi kuhusu hatua hiyo ya Mama Simba.

Naye Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali itamchukulia hatua za kisheria Mengi iwapo itabainika alikiuka taratibu na kanuni za nchi kwa kutangaza majina ya watu anaowatuhumu kwa ufisadi
.

Mkuchika alisema jijini Dar es Salaam jana kwa sasa serikali inafanya uchunguzi juu ya suala hilo na itatumia mikanda ya video pamoja na maelezo ya kimaandishi aliyoyatoa Mengi siku alipokutana na waandishi wa habari.

"Tumekusudia kupata ule mkanda wa video, pia tusome maelezo yake ya kimaandishi... tukigundua kuna mahala ambapo sheria haikuzingatiwa, (Mengi) atachukuliwa hatua," alisema Mkuchika.

Mkuchika alisema serikali imepokea malalamiko mengi kutoka kwa watu wengi, wakishutumu hatua iliyochukuliwa na Mengi, ambaye pia anamiliki viwanda vya vinywaji.

Bila kutaka kuwataja majina, Mkuchika alisema miongoni mwa walalamikaji, wapo walioeleza kuwa vyombo vya habari vya mfanyabiashara huyo havikuwatendea haki watuhumiwa waliotajwa kuwa ni mafisadi wakuu.

Alisema ni kutokana na vyombo hivyo kuwataja majina watuhumiwa bila ya kuwapa fursa ya kujibu madai dhidi yao. Waziri Mkuchika alipotakiwa kueleza siku ambayo uchunguzi huo utakamilika, alijibu wananchi wanapaswa kuwa watulivu kwa sababu serikali ikimaliza kuchunguza, itawatangazia yale waliyobaini.

Hii ni mara ya pili katika kipindi cha miezi takribani mitatu kwa Mengi kuingia katika mvutano na serikali baada ya kuvutana mapema mwaka huu na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha kutokana na kutangaza kuwa kuna mipango ya kumfilisi na kumuua.

Mengi pia amewahi kujikuta katika malumbano na watendaji wa serikali hasa na waziri wa zamani wa nchi, ofisi ya rais (utawala bora), Wilson Masilingi alipotoa tuhuma kuwa suala la utoaji zabuni ya ununuzi wa hoteli ya Kilimanjaro, hivi sasa inajulikana kama Kilimanjaro Kempiski, kulikuwa na kitu alichokiita "mchezo mchafu". Suala hilo liliamsha malumbano makali, lakini liliishia hewani.

Katika tuhuma za wiki iliyopita, Mengi aliwahusisha wafanyabiashara hao watano na kashfa za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), utoaji zabuni ya ufuaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development (LLC) na uuzwaji wa jengo la Mfuko wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii (NSSF).

Mengi, ambaye kituo chake cha televisheni cha ITV kiliwahi kuendesha mchezo mkubwa wa bahati nasibu ya Jackpot Bingo, pia aliitaja Bahati Nasibu kuwa katika tuhuma hizo, pamoja na mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma.


CHANZO: Mwananchi


HALAFU TUKISEMA UFISADI NI MIONGONI MWA SERA ZA CCM TUTAITWA WACHOCHEZI?CHADEMA WALIPOTOA LIST OF SHAME CCM,KAMA KAWAIDA YAKE,IKAJA JUU KUDAI HIZO NI POROJO ZA KISIASA.WENGINE WAKAENDA MBALI ZAIDI NA KUTISHIA KUWAPELEKA AKINA SLAA MAHAKAMANI KWA MADAI YA "KASHFA".HADI LEO HAKUNA HATA MMOJA WAO ALIYEKWENDA MAHAKAMANI,NA SANASANA BAADHI YA WATUHUMIWA HAO KWA SASA WAKO MAHAKAMANI WAKITUHUMIWA KUHUSU YALEYALE YALOTAJWA KWENYE LIST OF SHAME.


TATIZO LA MAWAZIRI WOTE WAWILI SIO MANJI AU THE PATELS.NI MR UNTOUCHABLE.HUYU AKIGUSWA BASI NDIO KAMA UMEPIGA LUMUMBA,HQ YA CCM.HAIHITAJI UPEO WA JUU KUBAINI KUWA WANACHOONGEA MAWAZIRI HAO WAWILI NI SAWA NA SELF-DENIAL.YAANI TUKIMJUA MWIZI TUSIMUITE MWIZI MPAKA AFIKISHWE MAHAKAMANI?TUTAMFIKISHAJE HUKO PASIPO KUMTUHUMU IN THE FIRST PLACE?


NA KWANINI ALALAMIKE WAZIRI SIMBA NA MKUCHIKA NA SIO HAO WALIOTAJWA NA MENGI?WAMETUMWA AU WANATUMIWA?WASITUFANYE WATOTO KUHUSU HABARI ZA HAO MAPAPA WA UFISADI KUFIKISHWA MAHAKAMANI KWA VILE HILO HALIWEZEKANI.KWANI KUNA SABABU NYINGINE INAYOSABABISHA KUSUASUA KUWATAJA WAMILIKI WA KAGODA ZAIDI YA UKWELI KUWA AMONG THE WAMILIKI NI MR UNTOUCHABLE?


AH,SIJUI MAMBO HAYA YATAENDELEA HADI LINI!

25 Apr 2009



MZALENDO MMOJA AMENITUMIA UJUMBE UFUATO KWENYE E-MAIL,NAMI NAOMBA KUUWASILISHA KAMA ULIVYO:


Kuna habari kwamba mmoja wa wafanyabiashara aliyetajwa na Mkurugenzi wa IPP Bwana Reginald Mengi amenunua hisa nyingi za umiliki wa kituo cha kurusha matangazo ya Television.

Mfanya biashara huyo inasemekana ni yule aliyetumia mtindo huohuo kununua hisa za kampuni iliyokuwa inatoa gazeti lilikuwa maarufu kabla ya mwaka 2005 na sasa si maarufu tena.

Mfanyabiashara huyo ambaye ana hisa kwenye kampuni moja ya simu za mikononi inasemekana ana mpango wa kutumia minara ya kampuni hiyo ya simu ili kusambaza matangazo ya kituo hicho nchi nzima kwa urahisi na bila gharama kubwa.

Kwa vile kampuni yake ndiyo yenye mtandao mkubwa hapa nchini basi itakuwa ni rahisi kwake kusikika nchi nzima kuzidi vyombo vyote vya habari.

Iwapo mpango huo utatekelezwa basi mfanyabiashara huyo atakuwa anaongoza kusikika eneo kubwa nchini.

Bwana Mengi ina ITV na Redio zake tabidi avute bidii ya kasi kwa sababu yeye hataweza kuwa na mtandao mkubwa kama hiyo TV.

Wenu mtafuta habari

24 Apr 2009

Boniface Meena na Mkinga Mkinga

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Reginald Mengi jana aliamua kujitoa muhanga alipotangaza majina ya wafanyabiashara watano wenye asili ya Kiasia ambao anadai kuwa ni mafisadi papa wanaoiba mabilioni ya fedha za wananchi na kutaka wachukuliwe hatua kwa madai kuwa wataiyumbisha na kuitingisha nchi.

Kati ya wafanyabiashara waliotajwa na Mengi, wawili wamefunguliwa mashtaka ya tuhuma za wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), wengine wakiwa wameshatajwa kwenye kashfa mbalimbali, zikiwemo za zabuni ya utoaji umeme wa dharura ya Richmond Development na uuzwaji wa jengo la Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Mengi, ambaye anamiliki kampuni ya IPP yenye kampuni mbalimbali zikiwemo za habari na vinywaji, alitaja wafanyabiashara hao watano akisema kuwa ndio papa kwa ufisadi lakini akasema idadi ya mafisadi wanaofilisi nchi hawazidi 10.

"Wanaotuhumiwa kuwa mafisadi papa wanahusishwa na karibu kila kashfa kubwa hapa nchini zikiwepo kashfa za Richmond, EPA, Dowans, helikopta na magari ya jeshi, ndege ya rais, rada, NSSF, Bahati Nasibu ya Taifa, mradi wa makaa ya mawe wa Mchuchuma na kadhalika," alidai Mengi katika mkutano wake na waandishi wa habari alioufanya kwenye ofisi yake jijini Dar es salaam.
>
Kati ya wafanyabiashara hao watano ambao Mengi alidai ni mapapa wa ufisadi, wamo Rostam Aziz, Yusuf Manji na Jayantkumar Chandubhai Patel (Jeetu Patel), ambao Mwananchi ilipata nafasi ya kuzungumza nao kuhusu tuhuma hizo za Mengi.

Hata hivyo, Mengi hakuwa tayari kutoa vielelezo kuthibitisha madai yake, lakini akasema iwapo watamshtaki mahakamani na wafanye hivyo kwa kuwa huko ndiko haki inakopatikana.

Mengi alirusha tuhuma nyingi kwa watu hao ambao alidai kuwa wamecharuka baada ya Rais Jakaya Kikwete kuamua kupambana nao na hivyo wameamua kupambana na yeyote anayemsaidia mkuu huyo wa nchi katika vita hiyo.

"Jitihada kubwa za Mhe. Rais za kuleta maendeleo na maisha bora kwa kila Mtanzania zinazoofishwa na wizi mkubwa wa rasilimali za taifa. Bado Watanzania wengi wanaandamwa na umaskini mkubwa; hawajui hata mlo mmoja kwa siku utatoka wapi," alidai Mengi ambaye pia alitoa taarifa ya maandishi aliyoisaini.

"Cha kusikitisha ni kuwa pale Mtanzania mwema mwenye uwezo anaposaidia jamii kuondokana na umasikini, mafisadi wanapiga kelele kuwa misaada ya aina hiyo ina agenda. Wanapinga kwa kuwa wanataka Watanzania wafe na njaa na matatizo mengine."

Mengi alikwenda mbali zaidi na kudai mafisadi anaowatuhumu wanaweza wakaunga mkono matatizo yanayotokana na Deci, taasisi inayoendesha mchezo wa kuchangisha fedha na kulipa maradufu na Watanzania kubakia "wakifukuzana na wachungaji bila ya kujiuliza ni kina nani hasa wanachochea vurugu".

Wakiongea na Mwananchi, watu hao wanaotuhumiwa kwa ufisadi hawakutaka kujibu kwa kirefu na badala yake walimtuhumu mwenyekiti huyo mtendaji wa IPP kuwa ana wivu, fitina chuki na ambaye ameshindwa kuendesha nyumba na biashara zake, huku mwingine akieleza kuwa anatumia haki yake ya kidemokrasia ya kutoa maoni yake.

"Mengi... (si mstaarabu)," alisema Manji ambaye anamiliki kampuni ya Quality Group. " Biashara zake zimemshinda ndio maana anazungumza ovyo." Rostam Aziz, ambaye ni mbunge wa Igunga anayejishughulisha na biashara mbalimbali za miradi mikubwa ya ujenzi, uchimbaji na habari, alimuelezea Mengi kama mtu ambaye analingana kwa umri na baba yake mzazi na hivyo hawezi kubishana naye.

Lakini akasema: "Mengi amejaa chuki, wivu na fitina. Sina cha kumsaidia isipokuwa kumuombea Mungu ili amsaidie kwa kumpuuzia hayo maana ni adhabu kwa nafsi yake mwenyewe. Kwa malezi niliyopata, siwezi kubishana na mzee."

Jeetu Patel naye alisema haoni busara kujibizana na Mengi na kwamba alichofanya mwenyekiti huyo wa Chama cha Wafanyabiashara Wenye Viwanda (CTI) ni kutumia haki yake ya kidemokrasia ya uhuru wa kuongea.

“Hayo ni matatizo yake," alisema Patel, ambaye anakabiliwa na kesi ya tuhuma za wizi wa fedha za EPA. "Amewaita waandishi kuzungumza nao... sikumsikia lakini ninachoweza kusema ni kwamba anatumia uhuru wake wa kujieleza.>
"Binafsi sijui chochote kuhusu hizo tuhuma za Mengi dhidi yangu, ila anayo haki ya kusema chochote. Nina mambo mengi ya kufanya hivyo sioni kama itanisaidia kwenye biashara zangu za kila siku kuanza majibizano na Mengi."

Katika mkutano wake na waandishi wa habari, Mengi alidai kuwa watu hao aliowataja si tu kwamba wanaiba rasilimali za Tanzania, bali pia wanaiba muda wa Watanzania.

"Badala ya kutumia muda katika shughuli za maendeleo, tunajikuta tukitumia muda mwingi kupambana nao na hawatingishiki," alidai Mengi. "Badala yake wanatumia fedha walizotuibia kuanzisha magazeti ya kujenga kiburi cha kutudharau, kututukana na kutunyanyasa. Inakuwa kesi ya mwizi kumkimbiza na kumpiga aliyeibiwa.

"Hata sasa hivi, mafisadi papa wanaendelea kutumia uwezo wao wa kiuchumi uliotokana na wizi wa rasilimali za nchi yetu kushawishi na kupata miradi mikubwa mikubwa kwa kutumia majina tofauti tofauti huku wakipuuza kabisa kelele za wananchi kuhusu ufisadi wao.

Alisema ni muhimu wananchi wakajiuliza hawa mafisadi wanapata wapi ujasiri wa majigambo, dharau na nguvu za kutukana na kunyanyasa watu.

Alisema mafisadi papa ni lazima wajue kwamba iwapo wapambanaji wa ufisadi watapata madhara kwa njia yoyote hapa nchini au nje ya nchi, wananchi wa Tanzania watawawajibisha.

"Ni lazima Watanzania wote tuone kwamba sasa tumefika mahali pa kusema imetosha," alidai Mengi.

CHANZO:Mwananchi

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.