Showing posts with label SAUDI ARABIA. Show all posts
Showing posts with label SAUDI ARABIA. Show all posts

23 Aug 2010


Riyadh,Saudia,April 16

Wafanyabiashara wa Saudi Arabia wameiomba Tanzania kama wanaweza kukodi hekta nusu milioni (500,000) za ardhi inayofaa kwa kilimo hususan cha mpunga na ngano kama sehemu ya mpango wa kujitosheleza kwa chakula kwa falme hiyo ya jangwani.

Maofisa waandamizi wa chemba ya biashara ya jiji la Riyadh walitoa ombi hilo wakati wa ziara ya Rais Jakaya Kikwete katika falme hiyo.

"Tanzania ipo tayari kufanya biashara nanyi.Kuna heka milioni 100 (hekta milioni 40.5)za ardhi nzuri yenye rutuba",Kikwete aliwaambia wafanyabiashara hao.

Samir Ali Kabbani,mkuu wa kamati ya kilimo ya chemba hiyo alisema kwamba wamepata majibu mazuri sana."Kikwete ametuambia kwamba Tanzania inaweza kutukodisha ploti ambazo kila moja ina ukubwa wa hadi hekta 10,000 kwa kipindi cha miaka 99",Kabbani alilieleza Shirika la Habari la Reuters baada ya mkutano huo na Kikwete.

Maofisa na wafanyabiashara wa Kisaudi walitrajiwa kuitembelea Tanzania wiki chache baada ya mkutano huo.

"Wanaweza kukodi ardhi kutoka serikalini",January Makamba,msaidizi wa Rais Kikwete,aliieleza Reuters."Lakini inabidi tuhakikishe kuwa hatuishii kwenye hali kama ile ya Nigeria:hifadhi kubwa ya mafuta lakini foleni kubwa kwenye vituo vya kuuzia mafuta",alisema Makamba.

Maafisa wa Saudia wanaiona Tanzania kama sehemu mwafaka kutokana na mazingira ya kijiografia,kisiasa na wingi wa maji na ardhi ya kilimo.Makampuni kadhaa ya nchi hiyo tayari yameanza kuwekeza katika miradi ya kilimo huko Indonesia na Ethiopia.

Agosti mwaka jana Indonesia ilisema kuwa mjumuiko wa makampuni ya Bin Ladin ya Saudi Arabia unatarajia kuwekeza dola bilioni 4.3 katika hekta 500,000 za kilimo cha mpunga.Mahitaji ya ngano kwa Saudia kwa mwaka yanakadiriwa kufikia tani milioni 2.5,na mwaka juzi nchi hiyo iliagiza kutoka nje karibu tani milioni 1 za mchele,kwa mujibu wa Idara ya Kilimo ya Marekani.

CHANZO: Reuters


5 May 2010

Je una ndoto za kupata shahada ya juu?Basi jaribu shahada ya uzamifu (doctorate) ya ndoto,jambo linalotarajiwa kuwa halisi nchini Saudi Arabia. 

Yusuph al-Harthy,Msaudia mahiri katika kutafsiri ndoto,ana mpango wa kuanzisha taasisi ya kitaaluma itakayotoa shahada ya kwanza na ya uzalimi,na hata shahada ya uzamifu (PhD) katika ndoto na maono,kwa mujibu wa gazeti la Al-Hayat.

"Kutafsiri ndoto ni kwa asili yake ni njia ya kutoa ushauri nasaha,alisema Harthy ambaye anaendesha tovuti ya kufundisha namna ya kukokotoa maana ya ndoto.Taasisi anayotarajia kuanzisha kitashirikiana na chuo kikuu kimoja cha Uarabuni ambacho bado hakijatajwa.

Dini ya Kiislam ina historia ndefu ya kutafsiri ndoto,huku mwananzuoni wa aliyezaliwa karne ya 7,Muhammad Ibn Sirin,mwenyeji wa Basra katika Iraki ya leo,akitambulika kwa mchango wake wa kuhariri daftari (catalogue) za tafsiri za ndoto.

Harthy,ambaye hujadili ndoto kwenye vituo vya radio na shoo za runinga,haafikiani na mtizamo wa Wizara ya Saudia inayoshughulikia masuala ya Uislamu kwamba tafsiri ya ndoto sio sayansi inayoweza kufundishwa bali ni jambo linalotokana na hamasa (inspiration).

Imetafsiriwa kutoka tovuti ya Shirika la Habari la AFP

22 Dec 2008


A Saudi court has rejected a plea to divorce an eight-year-old girl married off by her father to a man who is 58, saying the case should wait until the girl reaches puberty.

The divorce plea was filed in August by the girl's divorced mother with a court at Unayzah, 135 miles north of Riyadh just after the marriage contract was signed by the father and the groom.

Lawyer Abdullar Jtili said:"The judge has dismissed the plea, filed by the mother, because she does not have the right to file such a case, and ordered that the plea should be filed by the girl herself when she reaches puberty."

"She doesn't know yet that she has been married," Jtili said then of the girl who was about to begin her fourth year at primary school.

Relatives who did not wish to be named said that the marriage had not yet been consummated, and that the girl continued to live with her mother.

They said that the father had set a verbal condition by which the marriage is not consummated for another 10 years, when the girl turns 18.

The father had agreed to marry off his daughter for an advance dowry of £5,000, as he was apparently facing financial problems, they said.

The father was in court and he remained adamant in favour of the marriage, they added.

Mr Jtili said he was going to appeal the verdict at the court of cassation, the supreme court in the ultra-conservative kingdom which applies Islamic Sharia law in its courts.

Arranged marriages involving pre-adolescents are occasionally reported in the Arabian Peninsula, including in Saudi Arabia where the strict conservative Wahabi version of Sunni Islam holds sway and polygamy is common.

In Yemen in April, another girl aged eight was granted a divorce after her unemployed father forced her to marry a man of 28.

SOURCE: Daily Mail

18 Sept 2008

Ustaadh mmoja mwenye msimamo mkali huko Saudi Arabia ametoa fatwa dhidi ya kikatuni-kipanya Mickey Mouse,akidai kuwa "kipanya" huyo ni askari wa shetani.Huu sio utani,BONYEZA HAPA kusoma habari hiyo ya kuchekesha.

27 Dec 2007


Mwanasiasa mahiri na Waziri Mkuu wa zamani wa Pakistani,Benazir Bhutto ameuawa baada ya kupigwa risasi mjini Rawalpindi,karibu na mji mkuu wa nchi hiyo Islamabad.Mwanamama huyo ambaye alirejea nchini humo hivi karibuni akitokea kwenye hifadhi ya kisiasa,alipigwa risasi mbili,moja ya shingoni na nyingine ya kifuani,baada ya kumaliza kuhutubia mkutano wa hadhara.Aliyemuua alijilipua kwa bomu la kutoa mhanga baada ya shambulio hilo.Angalau watu 20 waliuawa pia katika shambulio hilo linalotarajiwa kuiingiza Pakistan katika machafuko.
-------------------------------------------------------------------
NANI ANAHUSIKA NA MAUAJI HAYO? (Uchambuzi wa kiuanafunzi)
Jibu jepesi ni YEYOTE.Kifo hicho kinaweza kuwa ni mkakati wa Al-Qaeda kuhakikisha Pakistan inaendelea kuwa "unstable" hivyo kuweka mazingira mazuri ya kustawi kwa "cells" za kikundi hicho cha kigaidi.Pia mauaji hayo yanaweza kuwa kazi ya kikundi chochote kile chenye msimamo mkali wa kidini (ambacho pengine hakina mahusiano na Al-Qaeda).Kwanini wamuue?Sababu kuu ni kwamba mwanamama huyo alikuwa akiwakilisha yale yote yanayopingwa na vikundi vyenye msimamo mkali:demokrasia,haki za akinamama,mahusiano mazuri na Marekani na nchi za Magharibi bila kusahau sapoti yake kwa vita dhidi ya ugaidi.Lakini pia,Bhutto anaweza kuwa ameuawa na "elements" flani ndani za mfumo wa siasa za nchi hiyo (majenerali walio madarakani na wastaafu,mashushushu,nk).Baadhi ya hawa wanaweza kuwa maadui aliowatengeneza kipindi cha utawala wake,lakini wengine wanaweza kuwa wale ambao hawakuwa radhi kumwona mwanamama huyo akirejea kwenye upeo wa kisiasa wa nchi hiyo.

Mmoja wa wasaidizi wa Bhutto anadai kuwa aliandikiwa barua na mwanasiasa huyo hivi karibuni ambapo aliwataja watu watatu walio kwenye serikali ya Rais Pervez Musharaf ambao alidai wana mpango wa kumkwamisha katika harakati zake za kisiasa.Lakini pia Oktoba 18 mwaka huu,Bhutto alinusurika kuuwawa katika shambulio lililogharimu maisha ya mamia ya wafuasi wake.Kwa mtazamo wa mbali zaidi,kidole kinaweza kuelekezwa kwa Ramzi Yousef (ambaye kwa sasa yuko gerezani nchini Marekani kwa kuhusika kwake na mashambulizi ya kigaidi ya Septemba 11,2001).Mwezi Julai mwaka 1993,Ramzi alijaribu kumuua Bhutto kwa bomu lakini hakufanikiwa.Ilifahamika baadae kwamba gaidi hiyo alikuwa akitekeleza mpango ulioandaliwa na "elements" flani ndani ya Pakistan,katika baadhi ya nchi za Ghuba na kamanda mmoja wa vikundi vya Afghanistan aliyekuwa na "connection" na Saudi Arabia.

Kama nilivyosema mwanzoni,YEYOTE kati ya makundi hayo niliyoyataja,anaweza kuwa mhusika.Ukweli unabaki kuwa uamuzi wa mwanamama huyo kurejea Pakistan kutoka kwenye hifadhi yake ya kisiasa ulikuwa ni sawa na kujiandikia hukumu ya kifo kwani alikuwa na maadui wengi,ndani na nje ya Pakistan.Bhutto mwenyewe alikiri kufahamu kwamba uamuzi wake wa kurejea Pakistan ulikuwa ukihatarisha maisha yake,na hilo linaweza kumfanya akumbukwe kwa ujasiri wa kutoogopa kuuawa (japo sasa ameuawa) kwa minajili ya kuwatumikia Wapakistani.

PS: Huu ni uchambuzi wangu binafsi kama mwanafunzi wa Siasa za Kimataifa,jisikie huru kunikosoa.

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.