Showing posts with label SENEGAL. Show all posts
Showing posts with label SENEGAL. Show all posts

28 Jun 2011

Pichani ni jengo la "Tanesco ya Senegal",Senelec,lililoshambuliwa na waandamanaji wenye hasira kuhusu kukatika umeme mara kwa mara jijini Dakar.Akina sie tunashambulia kwa matusi,lawama,na manung'uniko huko Twitter na Facebook!!!

Sio siri kwamba upole wa Watanzania ni miongoni mwa sababu kuu za mabaya mengi yanayotokea huko nyumbani.Na kama kuna suala linalosikitisha kuhusu mwamko wa Watanzania kudai haki zao ni tatizo la mgao wa umeme sambamba na ubabaishaji wa hali ya juu wa serikali na Tanesco katika kushughulikia tatizo hilo.

Sasa hivi,mitandao ya jamii ya Twitter na Facebook imetawaliwa na malalamiko ya Watanzania wengi kuhusu mgao.Wengine wanaishiwa na uvumilivu na kuishia kuitukana Tanesco,kana kwamba matusi hayo yatarejesha umeme.Wengine wamekuwa wakipeana taarifa kuhusu maeneo ambayo "Tanesco wameshachukua umeme wao".Kwa kifupi,kinachosikika zaidi ni manung'uniko,lawama,vilio na hata matusi.Cha kusikitisha ni kwamba hakuna dalili yoyote kutafsiri malalamiko hayo into vitendo.

Sio kama nawasimanga ndugu zangu.I really feel you lakini ukweli mchungu ni kwamba kelele zenu haziwezi kumaliza tatizo hilo.Kinachohitajika ni kudai haki kwa nguvu.By "nguvu" simaanishi vurugu bali kuchukua hatua za makusudi kuhakikisha serikali na Tanesco wanawajibika.Mgao utaendelea milele iwapo Watanzania wataishia kulalamika tu.Hakuna miujiza katika kuleta mabadiliko.Either watu wajitoe muhanga kudai haki yao kama walipakodi au waendelee kuteswa na mgao.

Bahati nzuri,wenzetu nchini Senegal wanatuonyesha namna gani matatizo yanayoathiri nchi yanavyoshughulikiwa na umma.Nisieleze kwa maneno yangu bali naomba usome habari ifuatayo:

Associated Press

DAKAR,Senegal: Maelfu ya waandamanaji wameingia mitaani katika mji mkuu wa Senegal kupinga kukatika umeme mara kwa mara.Maandamano hayo ni tukio la tatu la vurugu nchini humo ndani ya wiki.

Wananchi wenye hasira walivamia ofisi za shirika la umeme la Senelec,jijini Dakar baada ya maandamano ya kupinga kukatika kwa umeme kwa muda mrefu.

Watu kadhaa walishambulia majengo ya serikali hapo jana.Wanadaia kuwa baadhi ya maeneo yamekuwa yakikosa umeme kwa masaa 24 au zaidi.

Kama ilivyo kawaida kwa vyombo vya dola barani Afrika,askari wa kikosi cha kutuliza ghasia walipambana na waandamanaji kwa kutumia maji na mabomu ya machozi.Msemaji wa polisi hakuweza kuthibitisha idadi ya waliojeruhiwa katika ghasia hizo.

Alhamisi iliyopita,vurugu kubwa ziliibuka kupinga mpango wa mabadiliko ya katiba ya nchi hiyo

Uchaguzi ni wenu Watanzania wenzangu.Mwendelee kulalama huku Serikali na Tanesco wakiendelea kuwasanifu (mgao wa umeme hauwagusi kwa vile aidha wana jenereta zinazojazwa mafuta na hela yako mlipakodi au maeneo wanayoishi hayakatwi umeme kutokana na unyeti wake) AU muige mfano wa wenzetu wa Senegal.Hakuna njia ya mkato katika kutatua matatizo sugu yanayosababishwa na watendaji wasiotimiza wajibu wao.It's now or never!

16 Oct 2010


Senegal welcomed 163 Haitian university students to Dakar Wednesday. Senegalese president Abdoulaye Wade, offered them free education after an earthquake devastated their island nation in January.

Sanogier Genevieve Julbertha arrived in Senegal Wednesday, less than a year after a catastrophic earthquake in her country killed about 200,000 people and caused widespread structural damage.

The 20-year-old law student is one of the more than 160 Haitians who will enroll in a Senegalese university this fall free of charge.

She says she does not have the words to describe how good it is to be in Senegal. She says we are the same people. We share the same roots. She says life is still difficult for many Haitians. Many universities collapsed, she says, and many families are still homeless.

The Senegalese government was swift to offer aid to Haiti in the earthquake's aftermath this January, committing $1 million in emergency relief as well as offering land to Haitians who wanted to relocate to Senegal.

Senegalese President Abdoulaye Wade addressed the students Wednesday at a ceremony at the foot of his recently-inaugurated Monument to the African Renaissance. He called the students' arrival an act of "panafrican solidarity."

Mr. Wade says today marks the return of young Haitians to the land of their ancestors and a resounding victory for Africa. Others before us have tried, he says, only to return to a land still dominated by outside forces, but these students are returning freely to an independent Africa in control of its destiny.

The students will attend one of three Senegalese universities on full scholarships from the Senegalese government.

Mardoche Fontilus, 20, says he will study psychology in Senegal. The opportunity is a "dream come true," he says, but it cannot erase the memories of this past year.

He says the earthquake impacted the lives of everyone in Haiti, and it was our brothers, sisters, aunts and cousins under the rubble. He says he is grateful for the international aid they have received, but January 12 was a sad day they will never be able to forget.

Fontilus said he hopes the education he receives in Senegal will allow him to return to Haiti and help rebuild his country.

SOURCE: VoA

Categories

Blog Archive

© Evarist Chahali 2006-2022

Search Engine Optimization SEO

Powered by Blogger.